Kesi ya Boniface AK Mwabukusi kupinga kukatwa kwenye Uchaguzi wa Rais wa Tanganyika Law Society kutolewa hukumu leo pale Mahakama kuu ya Tanzania
Jumaa Mubarak π
----
Your browser is not able to display this video.
Mahakama Kuu ya Tanzania kanda ya Dar es Salaam leo, Ijumaa Julai 26.2024 imetoa hukumu ya kesi iliyokuwa imefunguliwa na Wakili wa kujitegemea Boniface Mwabukusi dhidi ya TLS (Chama cha Mawakili Tanganyika) ambapo Wakili Mwabukusi alikuwa anapinga maamuzi ya kamati ya rufani kumuengua kugombea nafasi ya Rais wa chama hicho katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mapema mwezi ujao.
Baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili Mahakama imeridhika na hoja zilizotolewa na upande wa Mwabukusi ambapo sasa rasmi imetengua maamuzi ya kamati ya rufani ya TLS, hivyo kwa sasa Wakili Mwabukusi amerejeshwa kugombea nafasi ya Rais wa TLS.
Katika kesi yenye msisimuko mkubwa sana Jaji Butamo Kasuka Philip wa Mahakama Kuu (Masijala Ndogo ya Dar es Salaam) ametengua na kubatilisha uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya Rufaa ya TLS na kumfanya Mwabukusi kushinda kesi dhidi ya TLS.
Hivyo, basi Boniface Anyisile Kajunjumele Mwabukusi ni mgombea rasmi wa nafasi ya Rais wa TLS katika uchaguzi mkuu wa TLS wa mwaka 2024.
Katika kesi yenye msisimuko mkubwa sana Jaji Butamo Kasuka Philip wa Mahakama Kuu (Masijala Ndogo ya Dar es Salaam) ametengua na kubatilisha uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya Rufaa ya TLS na kumfanya Mwabukusi kushinda kesi dhidi ya TLS.
Hivyo, basi Boniface Anyisile Kajunjumele Mwabukusi ni mgombea rasmi wa nafasi ya Rais wa TLS katika uchaguzi mkuu wa TLS wa mwaka 2024.