BoT: Kipato cha kila mkazi wa Dar chaongezeka kwa shilingi Laki 5, wa mikoani kwa Laki 1

BoT: Kipato cha kila mkazi wa Dar chaongezeka kwa shilingi Laki 5, wa mikoani kwa Laki 1

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687
Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na BoT kwenye ripoti yake ya Consolidated Report ya mwaka 2022 inaonesha Pato la Kila Mkazi wa Dar limeongezeka Kwa Shilingi Laki 5 wakati wastani wa Pato la Kila Mtanzania likiongezeka kutoka sh.2.7 mln Hadi sh 2.8 mln (Laki Moja) Kwa mwaka 2022.

My Take: Kila mtu aangalie account yake na mapato yake kama yameongezeka au hapana 😁😁

IMG_0574.jpeg


=====

Kipato cha kila mkazi wa Dar chaongezeka kwa laki 5 - SwahiliTimes​


Takwimu zilizotolewa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) zinaonesha ongezeko la asilimia 5 katika wastani wa kipato cha Mtanzania kwa mwaka ambao umechagiwa na na kukua kwa uchumi wa Kanda ya Dar es Salaam, Kanda ya Kaskazini na Kanda ya Ziwa.

Takwimu zinaonesha kuwa wastani wa kipato cha Mtanzania (GDP per Capita) cha mmoja mmoja kimeongezeka zaidi kutoka wastani wa TZS milioni 2.7 hadi Shilingi milioni 2.8.

Wastani wa kipato cha wakazi wa Dar es Salaam kimeongezeka zaidi kuliko maeneo megine nchini kutoka Shilingi milioni 4.81 hadi shilingi milioni 5.39 kwa mwaka 2022 sawa na ukuaji wa asilimia 12 ikilinganishwa na mwaka uliopita ambapo kila mkazi wa Dar es Salaam aliongeza TZS 500,000 katika mapato yake ya mwaka .

Hata hivyo, hesabu ya pato la mtu mmoja mmoja inapatikana kwa kugawa pato la Taifa au eneo fulani (GDP) kwa idadi ya watu waishio humo.

Shirikia la Fedha Duniani (IMF) linasema GDP hupimwa kwa kuangalia thamani ya bidhaa na huduma zilizozalishwa katika kipindi husika na pia si zote ambazo zinajumuishwa.
 
Hii ndio Taarifa Mpya kutoka BOT , kwamba watu wa Dar wameongeza utajiri wao kwa 12% kutoka mil 4.8 mwaka uliopita hadi mil 5 mwaka huu .

Screenshot_2023-10-11-16-30-19-1.png


Toa maoni yako .
 
Nakumbuka miaka Ile ya 1992 - 1998 hapa DAR hapakuwa na familia inashindia chai na mihogo asubuhi lakini sikuhizi mihogo imekuwa BURGER kuanzia mitaa ya Kariakoo, Mnazi mmoja, Upanga Hadi Posta
 
Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na BoT kwenye ripoti yake ya Consolidated Report ya mwaka 2022 inaonesha Pato la Kila Mkazi wa Dar limeongezeka Kwa Shilingi Laki 5 wakati wastani wa Pato la Kila Mtanzania likiongezeka kutoka sh.2.7 mln Hadi sh 2.8 mln (Laki Moja) Kwa mwaka 2022.

My Take: Kila mtu aangalie account yake na mapato yake kama yameongezeka au hapana [emoji16][emoji16]

=====

Kipato cha kila mkazi wa Dar chaongezeka kwa laki 5 - SwahiliTimes​


Takwimu zilizotolewa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) zinaonesha ongezeko la asilimia 5 katika wastani wa kipato cha Mtanzania kwa mwaka ambao umechagiwa na na kukua kwa uchumi wa Kanda ya Dar es Salaam, Kanda ya Kaskazini na Kanda ya Ziwa.

Takwimu zinaonesha kuwa wastani wa kipato cha Mtanzania (GDP per Capita) cha mmoja mmoja kimeongezeka zaidi kutoka wastani wa TZS milioni 2.7 hadi Shilingi milioni 2.8.

Wastani wa kipato cha wakazi wa Dar es Salaam kimeongezeka zaidi kuliko maeneo megine nchini kutoka Shilingi milioni 4.81 hadi shilingi milioni 5.39 kwa mwaka 2022 sawa na ukuaji wa asilimia 12 ikilinganishwa na mwaka uliopita ambapo kila mkazi wa Dar es Salaam aliongeza TZS 500,000 katika mapato yake ya mwaka .

Hata hivyo, hesabu ya pato la mtu mmoja mmoja inapatikana kwa kugawa pato la Taifa au eneo fulani (GDP) kwa idadi ya watu waishio humo.

Shirikia la Fedha Duniani (IMF) linasema GDP hupimwa kwa kuangalia thamani ya bidhaa na huduma zilizozalishwa katika kipindi husika na pia si zote ambazo zinajumuishwa.
Huo ni unafiki mweupe ,2021 kurudi nyuma mama ntilie alikuwa akiuza 60,000 faida ilikuwa kama 25 hadi 30 .leo hii ukiuza 60000 fidi ni kama 8 mpaka 12 hicho kipato kinaongezeka vip
 
Huo ni unafiki mweupe ,2021 kurudi nyuma mama ntilie alikuwa akiuza 60,000 faida ilikuwa kama 25 hadi 30 .leo hii ukiuza 60000 fidi ni kama 8 mpaka 12 hicho kipato kinaongezeka vip
Kwa nini?
 
 
Nakumbuka miaka Ile ya 1992 - 1998 hapa DAR hapakuwa na familia inashindia chai na mihogo asubuhi lakini sikuhizi mihogo imekuwa BURGER kuanzia mitaa ya Kariakoo, Mnazi mmoja, Upanga Hadi Posta
Kwani burger na mihogo wewe unachagua nini?
 
Nakumbuka miaka Ile ya 1992 - 1998 hapa DAR hapakuwa na familia inashindia chai na mihogo asubuhi lakini sikuhizi mihogo imekuwa BURGER kuanzia mitaa ya Kariakoo, Mnazi mmoja, Upanga Hadi Posta

Nkaula mhogo wa kuchemsha na chai ya rangi mara nyingi asubuhi, havina mahusiano na kutokuwa na hela, ni aina ya chakula napenda.
 
Back
Top Bottom