Salary Slip
Platinum Member
- Apr 3, 2012
- 49,390
- 152,301
Nchi hii kuna sheria ambazo hutungwa halafu huwa zipo tu kwenye makaratasi na mojawapo inaweza kuwa ni Microfinanc ACT ya Mwaka 2018 na kanuni zake.
Sheria hii, pamoja na mambo mengine, inapiga marufuku watu kufanya biashara ya kukopesha bila kusajaliwa na kuwa na leseni na inatoa adhabu kali kwa wanaovunja hii sheria.
Hata hivyo, kinachoendelea mitaani ni kama vile hii sheria haipo, na watu wanafanya hii biashara kiholela baadhi kwa kutoza riba kubwa tena kwa kunyanyasa wakopojaji wakati wao hata kodi hawalpi na hata leseni hawana.
Hata kwa walio na leseni na ni tatizo kwanini mtu akikwama, basi mkopaji hutamani hata kukimbia nyumbani au eneo lake la biashara kuogopa fedheha ya kudhalilishwa au kudaiwa mbele za watu.
Ni kweli wakopojaji wanapaswa kulipa, ila mtu anapokwama, sheria inamlinda dhidi ya unyanyasaji au uzalilishaji na hata mikataba wanayotoa inapaswa kuzingatia sheria na kanuni zake.
Hivyo, nashauri BoT watoe matangazo kwenye vyombo vya habar kukumbusha kuwa ni kosa la jinai kufanya hii biashaara kama hujasajiliwa na huna leseni.
Pia, wenye leseni wazingatie mashariti ya leseni zao ikiwa ni pamoja na kutoa mikataba na kutonyanyasa wateja wao.
Halikadhalika, wakopojaji nao wakumbushwe kuwa wana wajibu wa kulipa madeni yao kukingana wa mikataba yao.
Kilichonisukuma kuandika haya ni hii mikopo ambayo marejesho yake ni ya kila siku bila kujali mtu siku hiyo umeuza au hujauza na umepata faida au hujapata ila rejesho ni lazima.
Wahanga wakubwa huku mitaani ni kina Mama ambao unaweza hata kuwaonea huruma wanapohangaika na haya marejesho ya kila siku.
Mwisho, nashauri serikali kupitia BOT, ikiwezekana wapige marufuku marejesho ya kila siku na iwe ni option ya mteja kutaka kurejesha kila siku.
Siamini kama kuna biashaara ya kutengeneza faida kila siku ya Mungu na hata kama ipo, Siamini kama kila siku hutopata dharau ukashindwa kufanya biashaara mfano kuugua au kuguliwa, n.k.
BoT chukueni hatua kunusura watu hasa kina Mama ambao wengi wao mitaji yao ni midogo. Ikiwezekana, pia mje na utaratibu sheria au kanuni kudhibiti riba kwenye hii biashaara ambayo kwa kiasi kikubwa inafanywa kiholela na wahusika hata kodi hawalipi.
Sheria hii, pamoja na mambo mengine, inapiga marufuku watu kufanya biashara ya kukopesha bila kusajaliwa na kuwa na leseni na inatoa adhabu kali kwa wanaovunja hii sheria.
Hata hivyo, kinachoendelea mitaani ni kama vile hii sheria haipo, na watu wanafanya hii biashara kiholela baadhi kwa kutoza riba kubwa tena kwa kunyanyasa wakopojaji wakati wao hata kodi hawalpi na hata leseni hawana.
Hata kwa walio na leseni na ni tatizo kwanini mtu akikwama, basi mkopaji hutamani hata kukimbia nyumbani au eneo lake la biashara kuogopa fedheha ya kudhalilishwa au kudaiwa mbele za watu.
Ni kweli wakopojaji wanapaswa kulipa, ila mtu anapokwama, sheria inamlinda dhidi ya unyanyasaji au uzalilishaji na hata mikataba wanayotoa inapaswa kuzingatia sheria na kanuni zake.
Hivyo, nashauri BoT watoe matangazo kwenye vyombo vya habar kukumbusha kuwa ni kosa la jinai kufanya hii biashaara kama hujasajiliwa na huna leseni.
Pia, wenye leseni wazingatie mashariti ya leseni zao ikiwa ni pamoja na kutoa mikataba na kutonyanyasa wateja wao.
Halikadhalika, wakopojaji nao wakumbushwe kuwa wana wajibu wa kulipa madeni yao kukingana wa mikataba yao.
Kilichonisukuma kuandika haya ni hii mikopo ambayo marejesho yake ni ya kila siku bila kujali mtu siku hiyo umeuza au hujauza na umepata faida au hujapata ila rejesho ni lazima.
Wahanga wakubwa huku mitaani ni kina Mama ambao unaweza hata kuwaonea huruma wanapohangaika na haya marejesho ya kila siku.
Mwisho, nashauri serikali kupitia BOT, ikiwezekana wapige marufuku marejesho ya kila siku na iwe ni option ya mteja kutaka kurejesha kila siku.
Siamini kama kuna biashaara ya kutengeneza faida kila siku ya Mungu na hata kama ipo, Siamini kama kila siku hutopata dharau ukashindwa kufanya biashaara mfano kuugua au kuguliwa, n.k.
BoT chukueni hatua kunusura watu hasa kina Mama ambao wengi wao mitaji yao ni midogo. Ikiwezekana, pia mje na utaratibu sheria au kanuni kudhibiti riba kwenye hii biashaara ambayo kwa kiasi kikubwa inafanywa kiholela na wahusika hata kodi hawalipi.