"Boys 2 Men", kwanini msiiache Tanzania ipumue?

"Boys 2 Men", kwanini msiiache Tanzania ipumue?

Safi. Ngoja tuone Tanzania inapoelekea.
 
Mimi nikisema huwa nachukiwa na kuonekana mwendawazimu, lakini niwaambieni ndugu zangu: Hawa wazee wa Cold-War na Ujamaa ni watu hatari mno kwa mustabali na ustawi wa taifa letu. Hiki kizazi kimerivuruga sana hili taifa na kitaendelea kufanya wanachokitaka mpaka tutapoamua kuwatoa kinguvu. Bila hivyo tutapiga mbizi kwenye lami....

Ukiwatoa utawaweka akina nani? Unahisi wakitoka hao Boys 2 men watakaoingia hawatakuwa na hizo tabia? Kwa hizi nchi zetu za Afrika especially kusini mwa jangwa la Sahara tutapata tabu sana. Hata ukiingia wewe ktk huo uongozi nakuhakikishia utakuwa kama haohao tu, alosema “hakuna mkate mgumu mbele ya chai” hakuwa mjinga.
 
Habari Wana JF,
Naomba kuuliza swali,
Je, "Boys 2 Men" ndio wazalendo wakubwa wa nchi hii?

Je, ni kwamba "Boys 2 Men" wanaipenda sana Tanzania?

Najenga hoja. Mnaoipenda nchi hii. Tuache u_CCM , u_CHADEMA. Tuulizane.
Je, "Boys 2 Men" ndio mwarobaini wa matatizo ya nchi hii?!

Je, Kuna uhusiano gani kati "Boys 2 Men", na "CCM INA WENYEWE"?

Naomba tuongee kama Taifa la watanzania. Je, nchi hii inamilikiwa?

Tafadhali sana, tuweke makundi ya kisiasa pembeni.

Binafsi nilimponda sana JK, nikamponda sana JPM, na Sasa najiuliza nianze kumponda na Samia? Au kuna tatizo sehemu Mimi sijajua? Nitaponda wangapi?

Nchi hii ni maskini sana. Je, "Boys 2 Men" ndio watakaoipeleka mbele nchi yetu?

Naomba kuwasilisha.

Karibuni tujadili Tanzania yetu ipone na kupaa kimaendeleo.
TANZANIA INA LAANA MKUU

Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
 
Bora boys 2 men kuliko Sukuma gang
Boys 2 men tuliishi vizuri watoto Shule za mana tulijenga tulinujua V8 kwa pesa zetu
Lini bro,mi nakumbuka maisha Bora kwa Kila mtanzania ambayo tukisubiri Sana baadae nikashuhudia watu wanagawana fedha kwenye viroba na hizo ndio zilitapakaa mitaani,serikali wakati huo inakopa fedha za kulipa mishahara.
Nakumbuka makusanyo ya Kodi kwa mwezi ilikuwa sh 7b mishahara 6b ya ziada bakuli lilitembea dunia nzima saidia masikini saidia masikini mi sijui wewe ulikuwa umetega wapi mrija wako sikubishii huenda wewe ulikuwa mswano inategemea ulitega wapi.
 
Lini bro,mi nakumbuka maisha Bora kwa Kila mtanzania ambayo tukisubiri Sana baadae nikashuhudia watu wanagawana fedha kwenye viroba na hizo ndio zilitapakaa mitaani,serikali wakati huo inakopa fedha za kulipa mishahara.
Nakumbuka makusanyo ya Kodi kwa mwezi ilikuwa sh 7b mishahara 6b ya ziada bakuli lilitembea dunia nzima saidia masikini saidia masikini mi sijui wewe ulikuwa umetega wapi mrija wako sikubishii huenda wewe ulikuwa mswano inategemea ulitega wapi.
Labda kamba yake ilikuwa ndefu

Sent from my Infinix X658E using JamiiForums mobile app
 
Huu mtandao wa wahuni ulioasisiwa na jk ndio umeifikisha nchi kwenye huu umaskini na bado wanataka kuendelea kutuibia.

Nchi hii haiwezekani kupata maendeleo mpaka awa wahuni wote wafeHatuwezi
In short hauwezi kuisha kwa sababu hawa watu wanapandikiza vimelea ambavyo vimeanza kuchipua kwenye utawala wa Huyu mama .vishapandikizwa na sasa vinamwagiliwa maji ila natamani opposition upae turudi ka uchaguzi wa 2015 uliokuwa umesababishwa na Huyu mkwere
 
Lini bro,mi nakumbuka maisha Bora kwa Kila mtanzania ambayo tukisubiri Sana baadae nikashuhudia watu wanagawana fedha kwenye viroba na hizo ndio zilitapakaa mitaani,serikali wakati huo inakopa fedha za kulipa mishahara.
Nakumbuka makusanyo ya Kodi kwa mwezi ilikuwa sh 7b mishahara 6b ya ziada bakuli lilitembea dunia nzima saidia masikini saidia masikini mi sijui wewe ulikuwa umetega wapi mrija wako sikubishii huenda wewe ulikuwa mswano inategemea ulitega wapi.
Duuu nakumbuka kuna gazeti moja uingereza lilimnanga huyo ombaomba kwa kutembeza bakuli mpaka watanzania kwa ujumla tukabeba aibu yake
 
Mkuu matatizo ya Tanzania hayakuanza na Raisi Jakaya wala Raisi Magufuli, yana mzizi mrefu sana. Pia hatuwezi kudharau kabisa mchango wa hawa wazee wala ushauri wao, japo mimi naamini kwamba wao wananufaika na huu mfumo hivyo ni nadra kwa wao kufanya maamuzi magumu yenye maslahi kitaifa. Wengi wao ni wahafidhina huku wengine wakiwa ni walafi mno. Sasa hilo la tutapataje fikra mpya ni jingine ambalo ukilizungumzia hadharani huwezi kukosa kuitwa mhaini, mchochezi au gaidi.......
Ni juzi bingwa mmoja amekiri kuwa mitandao inayo nguvu kubwa so mi nashauri kwa hili taasisi CCM lililojigeuza joka kuu ,tuandamane humu humu watatusikia .sisi siyo visiki Mkuu , wasiposikia lazima tutapata njia mbadala ya kuwajulisha watusikie.
 
Huu ni uchochezi wa chuki dhidi ya "kizazi" fulani.

Tafadhali ndugu kumbuka wanaoongoza nchi ni CCM na si kizazi fulani.

Angalia vijana walioaminiwa jinsi walivyofanya.
Hustahili kuwa humu Jf kwa kuwa unachochea mauaji ya halaiki kwa kudhahania tu.
Mimi nikisema huwa nachukiwa na kuonekana mwendawazimu, lakini niwaambieni ndugu zangu: Hawa wazee wa Cold-War na Ujamaa ni watu hatari mno kwa mustabali na ustawi wa taifa letu. Hiki kizazi kimerivuruga sana hili taifa na kitaendelea kufanya wanachokitaka mpaka tutapoamua kuwatoa kinguvu. Bila hivyo tutapiga mbizi kwenye lami....
 
Bora boys 2 men kuliko Sukuma gang
Boys 2 men tuliishi vizuri watoto Shule za mana tulijenga tulinujua V8 kwa pesa zetu
Upumbavu wa kusomesha peke yako kwa damu na jasho LA masikini , Unajenga huku jirani yako analala kwenye tope huo uchumi ?
Huo ni upumbavu
 
Dawa ni kuipiga chini CCM, miaka zaidi ya 60 kila siku ni porojo tu! Tuwape wengine nao wakizingua wapigwe chini! Ccm wamejipa hatikiliki ya nchi hii kwa hiyo wanafanya watakavyo! Ndio mana wanafunga watu kwa ajili ya kutetea katiba mpya!
Na ajabu tunakopa ili kujenga vyoo na madarasa yasiyozalisha !!! Too much kwa kweli
 
Huu mtandao wa wahuni ulioasisiwa na jk ndio umeifikisha nchi kwenye huu umaskini na bado wanataka kuendelea kutuibia.

Nchi hii haiwezekani kupata maendeleo mpaka awa wahuni wote wafe.
Hao wahuni wote wakifa kwani hawana watoto wao? Mwingine kashapewa na Unaibu.
 
Back
Top Bottom