Brazil to play Tanzania in a friendly

Brazil to play Tanzania in a friendly

Jamani hizi lawama nyingine hazina kichwa wala miguu. Manji kweli anaweza kuwa fisadi ,llakini yanga wao eamemuomba awasaidie amekubali na ameongeza zaidi kwa kuwalipia viingilio, sasa tatizo nini? ulitaka akatae?. hivi kuna mafisadi wangapi wazawa nchi hii hawajui kutoa hata senti angalau kwa watoto yatima? kama lawama basi walaumu yanga na si manji kwaswala la msaada, na mlaumu manji kama manji kwa ufisadi

Wanaomba wasaidiwe kununuliwa pipi?? What a joke!! kwa nini hajawajengea uwanja wao.? Njaa tu hizi na kutokuwa na mawazo endelevu.
 
Wanaomba wasaidiwe kununuliwa pipi?? Wah a joke!! kwa nini hajawajengea uwanja wao.? Njaa tu hizi na kutokuwa na mawazo endelevu.

Mkuu umeisoma vizuri post no1? swala la uwanja ni jingine na swala la kuombwa kugharamia mkutano ni lingine. na pia swala la asaidie katika lipi lipo mikononi mwake,.kwamujibu wa maelezo yako basi wa kulaumiwa ni yanga si manji
 
natanguliza:kwa maoni yangu.
wajameni inaniuma sana nikifikiria kuwa wapo ndugu zangu kule kijijini hawana maji, umeme, madawa na hata vifaa vya shule ila serikali inadiliki kugharamia ujio wa timu ya brazil kwa tsh 3 bilion,pia inauma kuona hata malimbikizo yetu ya mishahara hatulipi ili tuwasidie hao ndugu zetu.mbaya zaidi kiingilio cha mchezo huo ni tsh 200,000 hadi tsh 50,000 ambacho ni zaidi ya kima cha chini cha mshahara wa mfanyakazi au hata akitoa hio tsh 50,000 mwezi huu atakula matembele mpaka yaote tumboni.kwa hio ni mechi ya walionazo tu, sisi walala puu tulie, kweli

kwa upande wangu sijaona faidi ya ujio wa timu hii kiuchumi kwani wabrazili hawajagi kutalii kwetu, watalii wengi wanatoka europe na si hivyo tu bali tunatakiwa kujitangaza kimataifa kwa kutumia tuvuti(website) na maonyesho kwenye balozi zetu wala sio kwa mpira ambao hata dstv inayoonekana dunia nzima hawaonyeshi hii maechi.

Haya ni matumizi mabaya ya hela za serikali kwa kupenda misifa ya kijinga, hata hao wanaotupa misaada watashangaa na kutuona mapopopo.

Tumechoka na udhalimu huu,mwaka huu lazima tuing'oe serikali ya ccm jamani

mfurukutwa
 
brazil iko janja sana iko naona haina kitu kuze sauz sasa nataka kutafuta pesa kwa vibonde
 
Nina mpango wa kuitisha harambee mpwa niende nikanunue hiyo ticket 200,000! Nasikia jukwaani watakuwa wanagawa kofia, Tshirt na kadi za CCM

Duh mpwa utachangiwa tu haina neno siku hiyo kubali kufunga kunywa chuma chakavu.
 
Hii inadhihirisha wabongo tulivyo ishiwa na akili ya kufikiria mambo ya msingi na ya maendeleo. Huyu manji amefanya ufisadi pale NSSF na katuibia pesa kibao za matrekta ya kuzoa taka manispaa kinondoni kwa sababu anavaa tisheti ya kijani/njano. Leo anawalipia kiingilio ktk mechi, anatumia pesa alizokwiba kwetu anatununulia pipi na peremende....alafu hapo utakuta vizee vya dar es salaam meno 32 nje.......pambafu kabisa.
Angalizo hapo kwekundu ni meno 32 nje au meno 12 nje, au mapengo nje kabisaa :confused3:
 
Nina mpango wa kuitisha harambee mpwa niende nikanunue hiyo ticket 200,000! Nasikia jukwaani watakuwa wanagawa kofia, Tshirt na kadi za CCM

30000 + 200,000 = 230,000/=

230,000 (divide by 2) = 115,000/=

115,000 (times) 60,000 = 6,900,000,000 (6.9bn Tshs)

In whatever the case pesa yakuileta Timu ya Socccer ya Brazil ni around 6bn! (taka usitake)!

Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu blah blah ya Bunge alinukuriwa hivi:

"...Tanapa spent 1.07bn/- for the CNN adverts in 2007/2008 "

Leo hii tunaspend 7bn kuitangaza Tanzania ndani ya MASAA MAWILI? Hivi mbona tuko hivi?
 
haa mie nikajua utanipa offer kumbe tena nifanye harambee mmh!

Ofa sister noma, kama mfuko hautoshi bora iangalie kwenye luninga kama mimi.. kwa jinsi miundombinu ilivyo fake watakaoenda watajuta .. kumbuka JK lazima aende, hivyo kutoka lazima kwanza atoke na barabara zote zitafungwa (baada ya mechi kama nusu saa hivi)... kama mechi ikiisha saa nne ujue kama unakaa Bunju kufika ni alfajiri!
 
Watanzania mna lawama sana....mpaka mnatia aibu!!

Jamaa kajitolea kuwasaidia wana Yanga, kuna tatizo gani katika hili???

nani nchi hii ambaye hajawahi kusaidiwa???
 
Sioni problem ya hivyo viingilio. Mbona kwenye mamiss watuwanalipa elfu 50 hadi laki
 
Nimejiuliza sana nikaishia kuamini kuwa hili nayo ni dili! Mambo yamefanywa kimya kimya kama EPA na RICHMOND hatimaye Brazil hii hapa. Balozi wa Brazil anawapeleka akina Mkwasa mafunzo ya ukocha kwao, mara anatangaza kuwaleta nyota wao bongo, hatimaye TFF wanakuja na viingilio vya kutisha. Wizara husika kimyaaaaa!!! Tafakari! Chukua hatua!
 
Hivi Manji katununulia za Tshs. ngapi?
 
ofa sister noma, kama mfuko hautoshi bora iangalie kwenye luninga kama mimi.. Kwa jinsi miundombinu ilivyo fake watakaoenda watajuta .. Kumbuka jk lazima aende, hivyo kutoka lazima kwanza atoke na barabara zote zitafungwa (baada ya mechi kama nusu saa hivi)... Kama mechi ikiisha saa nne ujue kama unakaa bunju kufika ni alfajiri!


asante kwa ushauri kakaangu
 
Wazee wa mujini najua hili linawezekana kabisa. Natafuta ticket za dili nione mechi ya Brazil na Taifa Stairs, nilikuwa disappointed last time walipokuja Ivory coast, nilinunua ticket za 60,000 mbili na Mzenj wangu! Wakati nanunua ticket pale karibu Steers kule mjini kuna vijana walinifata brother nina ticket za dili nipe hiyo 60,000 nakupa mbili tickets. Nikawa na wasi wasi ila niliambiwa inawezekana ni ticket zenyewe mzee Chilla Tenga huwa anashirikiana na akina Mwakalebela kuwa na ticket za ziada. Niliignore wale vijana kuogopa kupigwa fake.

Tuliingia uwanjani nikiwa nimeshikana mkono na Mzenji. Tukaelekezwa kwenye lile jukwaa husika, nilitegemea kutakuwa na watu wastaarabu maana hata raisi alikuwa hapo kwa VIP. Chakushangaza kulikuwa na jamaa wanakula mahindi ya kuchoma, wachafu chafu hivi, wanaongea hovyo hovyo nadhani pia walikuwa wamelewa pombe za kiasili.

Katika uliza uliza nikaambiwa ujanja wa mjini hizo ticket zao za dili huenda wamenunua ticket za 60,000 kwa buku 10. Na kweli baada ya kuulizia siku ya pili nikaambiwa mjini hapo wajinga ndio wanaoliwa. Kila tukio kubwa huwa kuna mambo ya dili.

Zis time nimeamua nioneka wa mujini nami, nitapata wapi ticket za dili naambiwa kila kitu dili hapo mjini hata ukitaka mega selebriti kuna watu wakuongea nao...

Nataka ticket ya dili siwezi lipia 400,000 hahahaha usawa huu mimi na mzenj

Ticket ya dili


Masa K
 
Back
Top Bottom