Pre GE2025 Brigedia Jenerali, Mndolwa: Wananchi kuongozwa na kiongozi mmoja, haimaanishi kwamba hawana akili, kiongozi bora anakubali ushauri wa wananchi

Pre GE2025 Brigedia Jenerali, Mndolwa: Wananchi kuongozwa na kiongozi mmoja, haimaanishi kwamba hawana akili, kiongozi bora anakubali ushauri wa wananchi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Brigedia Jenerali, Fransic Mndolwa alipofanya mahojiano na kituo cha Televisheni cha ITV kwenye kipindi cha dakika 45 Februari 10, 2025 alisema Wananchi kuongozwa haimaanishi hawana akili, kwani viongozi wanasaidia kusimamia kanuni ambazo zimekubalika, na kanuni hizo haziwezi kusimamiwa na watu wote kwani itakuwa ni fujo

"Wananchi kwa kuongozwa na kiongozi mmoja mfano mkuu wwa wilaya, mkuu wa mkoa hata Rais, Waziri sio kwamba wananchi hawana akili, hapana wana akili zao kila mmoja akipata nafasi anafikiria, huyu amepata nafasi ya uongozi hapa atafanya kazi za uongozi kuunganisha wenzake katika kuhakikisha kwamba mambo yanakwenda, lakini sio kwamba yeye ana akili kupita wengine wote sasa tatizo lipo hapo. Mtu mwingine anapoambiwa yeye ni mkuu wa wilaya, mkuu wa mkoa, anataka atakalosema yeye basi ni hilohilo hapana, lazima atambue wale anaowaongoza ni watanzania wenye hadhi sawa na yeye"

"Viongozi wanasaidia kusimamia kanuni ambazo tumekubaliana, kanuni haziwezi kusimamiwa na watu wote itakuwa ni fujo, lazima kuwa na mwenzenu mtaalamu anajua hiki kiko hivi anakumbusha ndo uongozi. Kuna watu wengine hawataki hata mawazo ya wananchi wa kawaida, kiongozi mzuri ni yule anayekubali kuongozwa, anapata ushauri wa wale anaowaongoza" alisema Brigedia Jenerali, Mndolwa

Soma pia: Pre GE2025 Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025


 
"Wananchi kuongozwa haimaanishi hawana akili, Viongozi wanasaidia kusimamia kanuni ambazo tumekubaliana, kanuni haziwezi kusimamiwa na watu wote itakuwa ni fujo"- Brigedia Jenerali, Fransic Mndolwa.

View attachment 3232795

Kuongoza ni kuonyesha njia.

Je, ni Kanuni zipi hizo ambazo Wananchi wa Tanzania tumekubaliana na Viongozi wa nchi hii ikiwa Mwongozo Mkuu kabisa wa kuendesha nchi, yaani Katiba ya nchi sisi Wananchi wenyewe hatukuwahi kushirikishwa katika mchakato wa utungwaji wake?

Hoja yake hii ingeweza kuwa ina mashiko endapo kama kweli Wananchi wengi zaidi waliopo kwenye nchi hii wangekuwa wameshirikishwa kikamilifu katika mchakato wa kufunga Katiba ya nchi kuanzia na hatua za awali kabisa, sambamba na michakato mingine yote kabisa ya utungaji wa Sheria za nchi.
 
Hahaha,
Na hicho ndo hutokea mara nyingi hasa kwenye tawala zetu.
Watawaliwa wanaona kabisa kuwa wanaongozwa kuelekea kutumbukia shimoni, lakini hawana uhuru wa kukosoa miungu watu (a.k.a watawala)
Haswaa tunaitikia mapambio ya viongozi bila hata kufikiria (tumeunda mfumo mbovu sana)...
 
Back
Top Bottom