Brother amepata likizo anakuja kagua mashamba na mtaji nilishakula sijui nifanyeje

Brother amepata likizo anakuja kagua mashamba na mtaji nilishakula sijui nifanyeje

Chris wood

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2020
Posts
1,667
Reaction score
5,043
Asee Christmas kwangu imekuwa ya hovyo balaa, naona kama imekuja niumbua.

Kwanza kabisa mimi ni kijana wa miaka 33 ni degree holder lakini mpaka sasa sina kazi ya kueleweka, jambo ambalo limefanya nishindwe kuwa na familia.

Maisha Dar yalinitandika haswa ikabidi nirudi kwa mama ndio mpaka sasa nilipo,.. Niliwahi bahatisha kazi kwenye berau de change Dar lakini 2018 December tulivamiwa ofisini na askari wakatukamata japo baadae tuliachiwa lakini kibarua kikaota majani .

Baada ya hapo nilitafuta kazi bila mafanikio nikashindwa lipa pango ikabidi niendee kukaa kwa sista aka kwa shemeji nimekaa pale sana bila mishe yoyote kama miezi 6, kumbe shemeji, alikuwa anachukia ikabidi wanitengenezee zengwe pamoja na sista.

Siku hiyo asubuhi mimi sina hili wala lile nasikia ugonvi kati ya sista na shemeji, baadae sista akakasirika sana akachukua mabegi akaondoka. Mimi nikabaki najiuliza nimfate sista au niendele kukaa kwa shemeji? Nikasema wee mjinga usinitanie hapa siondoki,

Baada ya siku mbili sista kaniambia ameshafika nyumbani, shemeji nae siku hiyohiyo akaniambia kesho inabidi uondoke ninasafari ya kikazi nashukuru alinipatia kiasi kidogo nikachukua vyangu nikasepa kurudi kwa mama maana nilikuwa sina jinsi

Nimerudi home haikupita hata wiki mbili sista huyo akarudi kwa mumewe, nilimuuliza sista kama naweza rudi akasema nitulie kwanza.... hali iwe shwali.

Bahati nzuri mwaka huu brother kapata dili kwenye kampuni kubwa hapo Dar es salaam, ikabidi nitumie fursa ya kilimo kupata mtaji kutoka kwake kwa makubaliano kuwa tutakacho pata faida nusu kwa nusu mtaji wake ubaki pale pale

Mpaka naandika hapa sijawahi pokea hata shilingi kumi jamaa hatujamuona baada ya danadana kibao juzi hapa tunasikia kakamatwa sijui hata nianzie wapi.

Brother nae kila muda anataka nimtumie picha za mazao juzi nilisikia anaongea na mother kwenye simu kuwa anaumwa hawezi kuja kula Christmas jana usiku akapiga tena kuwa kapata nafuu ameshakata tiketi ya kuja asee nilivyosikia nimechanganyikiwa.

Leo asubuhi nimetoka njee nikakuta mbwa wanafanya mapenzi wamenasiana asee hasira zangu zote nimemaliza kwao nimewatandika bakora za kiwango cha stieglas gorge
hadi raia wakaingila kati, toka asubuh sijarudi nyumbani napiga hesabu sijui nitamwambieje brother
 
Last edited:
1608835696810.png
😀😀😀😀😀😀😀😀
 
Daah sasa hao mbwa wamekukosea nini wewe jamaaa

Hiyo hela bora hata ungehonga tu sasa wewe umeshindwa hata kujiongeza kuwa huyo jamaa ni tapeli

Na wewe utakua umejiunga q net wale wazee wa good morning
 
Kuna simulizi zipo humu jamiiforums watu walivyopoteza mitaji yao mikubwakubwa pamoja na midogo kwa njia hii ya kuwaamini ndugu wasio waaminifu kama wewe.

Dah! Ni hela ndogo ila itakuabisha vibaya huku ukiwa huna mbele wala nyuma
 
Sio kosa lako..

Kuna principle ndogo sana tunakosea pale tunapotaka kusaidia watu wetu wa karibu..

Hatuwaulizi wanataka nini ,wanataka kufanya nini sasa unamkabidhi mtu wazo lamo alifanyie kazi mwisho wa siku ni kuharibu tu...


Sema vijana hamsaidiki
 
Daaah... Pole sana mwamba ukipaniki maisha in magumu sana... Nakumbuka kidogo ningemuua mbuzi wa bibi kutokana stress nilimpiga jiwe akagalagala chini kama nyoka aliyemwagiwa mafuta ya taa... Cha muhimu mwambie tu ukweli bro wako
 
Huu Uzi unanifundisha kutokufanya biashara na Ndugu.

Kaka ako Tayari keshakula hasara,
na Cha kukufanya Hana.

Mtakaa vikao vya familia,
mtayamaliza na maisha yataendelea.

Aisee,
Ndo maana SIFANYAGI KABISA BIASHARA zangu na Ndugu.
 
Asee Christmas kwangu imekuwa ya hovyo balaa, naona kama imekuja niumbua.

Kwanza kabisa mimi ni kijana wa miaka 33 ni degree holder lakini mpaka sasa sina kazi ya kueleweka, jambo ambalo limefanya nishindwe kuwa na familia.

Maisha dar yalinitandika haswa ikabidi nirudi kwa mama ndio mpaka sasa nilipo,.. Niliwahi bahatisha kazi kwenye berau de change dar lakini 2018 December tulivamiwa ofisini na askari wakatukamata japo baadae tuliachiwa lakini kibarua kikaota majani .

Baada ya hapo nilitafuta kazi bila mafanikio nikashindwa lipa pango ikabidi niendee kukaa kwa sista aka kwa shemeji nimekaa pale sana bila mishe yoyote kama miezi 6, kumbe shemeji, alikuwa anachukia ikabidi wanitengenezee zengwe pamoja na sista.

Siku hiyo asubuhi mimi sina hili wala lile nasikia ugonvi kati ya sista na shemeji, baadae sista akakasirika sana akachukua mabegi akaondoka. Mimi nikabaki najiuliza nimfate sista au niendele kukaa kwa shemeji? Nikasema wee mjinga usinitanie hapa siondoki,

baada ya siku mbili sista kaniambia ameshafika nyumbani, shemeji nae siku hiyohiyo akaniambia kesho inabidi uondoke ninasafari ya kikazi nashukuru alinipatia kiasi kidogo nikachukua vyangu nikasepa kurudi kwa mama maana nilikuwa sina jinsi

Nimerudi home haikupita hata wiki mbili sista huyo akarudi kwa mumewe, nilimuuliza sista kama naweza rudi akasema nitulie kwanza.... hali iwe shwali.

Bahati nzuri mwaka huu brother kapata dili kwenye kampuni kubwa hapo dar es salaam, ikabidi nitumie fursa ya kilimo kupata mtaji kutoka kwake kwa makubaliano kuwa tutakacho pata faida nusu kwa nusu mtaji wake ubaki pale pale

Mpaka sasa ameshanitumia kama millioni 4.5 pia alinunua pikipiki kutoka kwa rafiki yale alikuwa kafulia akanikabidhi kuwa niwe nafanyia patrol kwenye shughuli za shamba.

Nifupishe tu pesa yote kuna jamaa alikuja akatushauri kwenye kikundi kuwa tukiwekeza kwenye kampuni yao kiasi cha 4.5m tutakuwa tunapata dola kati ya 100 na 200 kila mwezi, akatuonesha document yeye anavyolipwa nikaona hii ndio shortcut. Pia katuambia mtaji kwa mtu mmoja mmoja ni 5m hiyo 4.5m ni mkiwa kikundi kuanzia watu 4

Mpaka naandika hapa sijawahi pokea hata shilingi kumi jamaa hatujamuona baada ya danadana kibao juzi hapa tunasikia kakamatwa sijui hata nianzie wapi.

Brother nae kila muda anataka nimtumie picha za mazao juzi nilisikia anaongea na mother kwenye simu kuwa anaumwa hawezi kuja kula Christmas jana usiku akapiga tena kuwa kapata nafuu ameshakata tiketi ya kuja asee nilivyosikia nimechanganyikiwa.

Leo asubuhi nimetoka njee nikakuta mbwa wanafanya mapenzi wamenasiana asee hasira zangu zote nimemaliza kwao nimewatandika bakora za kiwango cha stieglas gorge
hadi raia wakaingila kati, toka asubuh sijarudi nyumbani napiga hesabu sijui nitamwambieje brother
Pandisha mashetani mwanzo mwisho, ongea kimasai,kichina na kihindi huku ukicheka na kulia kwa wakati mmoja
 
Back
Top Bottom