Buguruni, Dar: Mtoto wa miaka 10 akutwa amejinyonga chumbani kwake

Buguruni, Dar: Mtoto wa miaka 10 akutwa amejinyonga chumbani kwake

aise

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2018
Posts
5,175
Reaction score
16,488
Habari za usiku wakuu! Kuna mtoto wa miaka 10 amekutwa amejinyonga chumbani kwake hapa Buguruni.

Maelezo ya kina hayajapatikana ila kwa maelezo ya awali ni kwamba mtoto katoka shule mida ya saa tisa jioni na baada ya kufika nyumbani amefanya shughuli ndogo ndogo na baada ya muda umeingia chumbani na kujifungia humo.

Dada wa kazi baada ya kuona huyu mtoto kajifungia ndani kwa muda mrefu akaanza kupiga hodi ili mtoto afungue mlango.

Amepiga hodi sana baada ya kuona kimya na tayari hapo ni jioni kama saa 11 ikabidi atafutwe fundi avunje kitasa waingie ndani.
Baada ya kuingia ndani ndipo wakamkuta mtoto amejinyonya kwa kufunga kamba kwenye dirisha.

Polisi wamekuja wameuchukua mwili wa mtoto, dada wa kazi, kaka wa marehemu na fundi aliyevunja kitasa cha mlango.
Maelezo zaidi watakuwa nayo polisi baada ya kufanya uchunguzi wao
 
Zipo za chini chini
Wengine wameshaingiza imani za kishirikina maana hawa wazazi ni Wakinga kwahiyo kwamba huenda ni kafara wazazi wametoa 🤔 Kwamba itakuwaje mtoto wa miaka 10 ajinyonge?
Au kauliwa halafu kawekwa pale kwenye kitanzi kama geresha.

Bila shaka polisi watakuja na majibu ya yenye kueleweka
 
Habari za usiku wakuu! Kuna mtoto wa miaka 10 amekutwa amejinyonga chumbani kwake hapa Buguruni.

Maelezo ya kina hayajapatikana ila kwa maelezo ya awali ni kwamba mtoto katoka shule mida ya saa tisa jioni na baada ya kufika nyumbani amefanya shughuli ndogo ndogo na baada ya muda umeingia chumbani na kujifungia humo.

Dada wa kazi baada ya kuona huyu mtoto kajifungia ndani kwa muda mrefu akaanza kupiga hodi ili mtoto afungue mlango.

Amepiga hodi sana baada ya kuona kimya na tayari hapo ni jioni kama saa 11 ikabidi atafutwe fundi avunje kitasa waingie ndani.
Baada ya kuingia ndani ndipo wakamkuta mtoto amejinyonya kwa kufunga kamba kwenye dirisha.

Polisi wamekuja wameuchukua mwili wa mtoto, dada wa kazi, kaka wa marehemu na fundi aliyevunja kitasa cha mlango.
Maelezo zaidi watakuwa nayo polisi baada ya kufanya uchunguzi wao
Fundi kaingia kanunua kesi ya mauuwaji bila kujua leo analala lockup
 
Fundi kaingia kanunua kesi ya mauuwaji bila kujua leo analala lockup
Wamechukuliwa na Difenda usiku huu huu.
Lakini dogo kaacha maswali mengi sana.
Maana ametoka shule vizuri, hapa mtaani kuna mama anauza sambusa dogo amenunua sambusa vizuri, kaenda nyumbani kafua sare zake za shure vizuri, baada ya hapo kaingia chumbani ikawa mwisho wake
 
Tujifunze kutenga muda wa kuongea na watoto wetu
Siku hizi wanapitia mengi sana huko shuleni. Huenda kuna mwl anamnyima Amani, au kuna wenzie wanamfanyia bullying hana pa kushtaki maskini. R.I.P mtoto mzuri
 
Watoto nao wanapata sonona,

Nakumbuka niliwahi shuhudia mtoto wa miaka 13 alidakwa akijaribu kujinyonga

Alikuwa kiranja wa bweni, akidaka wenzake wanaingia na chakula bwenini anawasemea kwa walimu.

Wenzake wakawa wanamtenga, hawaongei nae kabisa.

Ndo akafikia huko....
 
Back
Top Bottom