BUKAVU: M23 yakuta mlango wa mji wazi

BUKAVU: M23 yakuta mlango wa mji wazi

Isue
Waache wapeleke. Kilichozuia ndege kutua Goma, hata huko kitakuwepo. M23 ya sasa, ni tofauti na ya zamani. Angalizo: vitani kila upande unapoteza. Kama wanaoingia mijini ni maelfu, wengine wanabaki kulinda maeneo waliyoyapata, nani anajua ni wangapi? South Africa iliwahi kupigana vita wapi ikashinda!? Kama inawatakia matatizo mateka wake, basi ijichanganye.

Japo mpaka sasa wapo, na wengine bado wapo Burundi hawajajoin wenzao huko kibaruani.
Isue nikwamba congo yenyew iko fragmented na mbaya zaid watu wamechoka vita. Kwahiyo hata waambiwe tunawauza kwa mkopo ila mtaishi bil vita watakubali.
Hivyo SA atajkuta katika mazingira magumu hasa kuleak kwa taarifa zao kwa maadui.
Hiyo risk inatakiwa waichukue wacongo wao kwanza then ndo outsiderz wawaboost , badala yake wanatimua mbio.
 
Rwanda ni land locked country vikwazo vinaweza kuiumiza sana kuliko.
Haiwezi kuwa sababu hiyo. Hata nchi zenye bandari zinaweza kuwekewa vikwazo.Issue ni wanakabiliana vipi na vikwazo hivyo. Dunia ya sasa imejaa unafiki. Anzia UN hiyo unayoisikia. Utamnyima hiki, mwenzie atampa. Kwani unadhani anaingia vitani kichwa kichwa? Hivyo vikwazo vinaweza vikawepo kimaandishi tu. Nani analinda mali ya mfaransa Mozambique? Yeye mfaransa huyo influence yake kwa watu wake wa karibu, ni kubwa kucover gap. Tall alisema haogopi vikwazo. Hujaelewa kitu hapo?
 
Ndo ilivyo.

Miaka 30 sasa, watu wa mashariki mwa DRC hawajui amani. Walipo leo,kesho wapo kwingine.Wanawake kubakwa,ni kugusa. Mali za watu kuibiwa, kawaida. Mwanajeshi alikuwa mtu wa kuogopa. M23 ilipolianzisha Goma,watu walijua ni yale yale. Kadri siku zinavozidi kwenda, wakaona hali ni tofauti. Watu wakaanza kukesha wanafanya biashara,wengine wakitembea, mharifu akikamatwa, wanamalizana nae. Kila walipofika,hawajawahi kumdhuru raia. Ndo wameanza kuonekana kumbe ni watu wema. Ikawa sasa imefikia hatua hiyo unayoiona, risasi zinalindima nje, watu wanajifungia ndani, wakiwaona tu, shangwe. Jiulize, nchi ipi iliwahi tokea dunia hii,kwenye vita watu wakawasindikiza wanaoitwa waasi. Kifupi, ni dalili za kwamba watu wamechoka uongozi uliyopo.
Asante mkuu Kwa ufafanuzi mzuri,

Nahisi Kivu kusini, Kivu kaskazini, na katanga Kuna nchi inakuja kuundwa hapo
 
Haiwezi kuwa sababu hiyo. Hata nchi zenye bandari zinaweza kuwekewa vikwazo.Issue ni wanakabiliana vipi na vikwazo hivyo.
Nchi za Afrika ya Mashariki zikiweka vikwazo haswa Kenya na Tanzania sijui kama unakumbuka vikwazo alivyowekewa Buyoya wa Burundi hadi akasalimu amri.
Ilifikia wakati mimi na wenzangu tukaanza kusmuggle fuel Petrol na Diesel nadhani ulikuwa mdogo sana.
 
Nchi za Afrika ya Mashariki zikiweka vikwazo haswa Kenya na Tanzania sijui kama unakumbuka vikwazo alivyowekewa Buyoya wa Burundi hadi akasalimu amri.
Ilifikia wakati mimi na wenzangu tukaanza kusmuggle fuel Petrol na Diesel nadhani ulikuwa mdogo sana.
Burundi sasa hivi vikwazo amewekewa na nani?! Hiyo fuel issue yake unaielewa?

Uelewa sana juu ya hilo sina. Lakini,mfano Tanzania, hiyo bandari yake akimuwekea vikwazo mnyaRwanda, hasara kubwa anapata nani!? Maana hapo hata DRC, akibaniwa na Rwanda, huo mlolongo unautafakari!? Japo kidiplomasia haiwezekani.
Kenya inaanzaje!? Uganda inaanzaje! Siasa waachie wahusika, sisi tujilie ubwabwa wetu na tunywe castle, basi. Hilo si jepesi kama unavyofikilia.
 
Asante mkuu Kwa ufafanuzi mzuri,

Nahisi Kivu kusini, Kivu kaskazini, na katanga Kuna nchi inakuja kuundwa hapo
Kwa nini mkuu! Kumbuka, mpaka ufike Kasai, lazima upite mkoa wa Maniema. Na tukiacha vita vya kwenye karatasi, huko kote kuna watu. Wenye hela zao. M23 haiwezi kushikilia maeneo na kufukuza watu. Hasa nguzo za taifa. Kwa hiyo, mtutu wa bunduki lazima uende sambamba na diplomasia. Japokua, kuna mawili: DRC uongozi uachie ngazi, kwa maana yote iwe na influence ya M23, au kipande cha mashariki kimegwe. Si jambo jepesi. Kwa sababu, hilo linaweza kusababisha hata eneo lililobaki, wazee wa mkwanja wakinukishe, kupata nchi zao. Nani asiekipenda kile kiti!!!! Inaweza ikawa kama kuchimba zege kwa kijiko, lakini mambo yatakaa sawa tu.
 
Burundi sasa hivi cikwazo amewekewa na nani?! Hiyo fuel issue yake unaielewa?

Uelewa sana juu ya hilo sina. Lakini,mfano Tanzania, hiyo bandari yake akimuwekea vikwazo mnyaRwanda, hasara kubwa anapata nani!? Maana hapo hata DRC, akibaniwa na Rwanda, huo mlolongo unautafakari!? Japo kidiplomasia haiwezekani.
Kenya inaanzaje!? Uganda inaanzaje! Siasa waachie wahusika, sisi tujilie ubwabwa wetu na tunywe castle, basi. Hilo si jepesi kama unavyofikilia.
Tatizo watutsi wanapenda sana vita wakimalizana na Congo wataingia Burundi zeni Tanzania tukae mkao wa kula
 
Tatizo watutsi wanapenda sana vita wakimalizana na Congo wataingia Burundi zeni Tanzania tukae mkao wa kula
Hayo ni maoni yako. Japo kwa ushauli wangu, ungepunguza nyege. Nani anapenda vita? Kuna aliekwambia vita ni mechi ya kirafiki eh! Mbona Tanzania huko huo ujinga ujinga wa kubagua watu hamna? Bro, miaka 30 ni muda mfupi sana, laiti ungeweza kufuatilia kwanza au kuomba ueleweshwe haya yote yalitokana na nini.

Huko Burundi, ulizia watu wanaitwa IMBONERAKURE wana kazi gani?
Leo hii, CCM inaweza ikaenda shule za msingi kupigisha watoto paledi za kisiasa na kuwafundisha wachukie kabila furani? Kama haiwezi, kwa nini wanaofanya hivo waonewe huruma?

Iko hivi, mwaka 1994, Warundi waliokuwa wamekimbilia Rwanda, walijiunga na wahutu wenzao kuuwa watu.
Badae, wakarudi kwao. Wameondoka na imani ya kwamba mtutsi hastahili kuishi. Hilo hilo ndo waliloliendekeza.
Majuzi, katibu mkuu wa chama tawala Burundi alisema, haitakaa itokee hilo kabila litawale tena. Yuko wapi kwanza yeye?

Rwanda haina shida ya kupigana na Tanzania, mambo yao yakienda kombo, wanayamaliza kisiasa. Hata Tanzania ikiishinda Rwanda, unadhani itakuwa haijapoteza chochote? Ukianzia rekodi ya kuwa ndo nchi ya amani ukanda huu kama si Afrika nzima!!!
 
DRC wanaweza kupitishia Mizigo yao Kigoma na Burundi na hata Lubumbashi.
Vitu vingine uwe unatumia akili bro. Kwani, wanapopitisha Rusumo, hiyo Kigoma hawaijui? Mfanyabiashara yeyote anaangalia na faida. Hiyo barabara unaijua wewe au unaongea tu! Wakifika Kigoma wanafanyaje!!! Karibu ni Kalemie. Wanaokwenda Goma? Je, una uhakika Burundi itaruhusu mizigo iendayo katika maeneo ya M23!!!!
 
Vitu vingine uwe unatumia akili bro. Kwani, wanapopitisha Rusumo, hiyo Kigoma hawaijui? Mfanyabiashara yeyote anaangalia na faida. Hiyo barabara unaijua wewe au unaongea tu! Wakifika Kigoma wanafanyaje!!! Karibu ni Kalemie. Wanaokwenda Goma? Je, una uhakika Burundi itaruhusu mizigo iendayo katika maeneo ya M23!!!!
Elewa ninachosema iwapo Nchi za Afrika ya Mashariki zitakapoamua kuiwekea vikwazo Rwanda.
Naona wewe ndiye hunielewi tena umaongea na mtu ambaye alikuwa ni smuggler wakati wa vikwazo vya Serikali ya Kijeshi ya Buyoya.
 
Elewa ninachosema iwapo Nchi za Afrika ya Mashariki zitakapoamua kuiwekea vikwazo Rwanda.
Naona wewe ndiye hunielewi tena umaongea na mtu ambaye alikuwa ni smuggler wakati wa vikwazo vya Serikali ya Kijeshi ya Buyoya.
We simuggle sikuzuii. Ila hilo wazo, haliwezekani. Sahau kabisaaaaa.
 
Back
Top Bottom