Bukoba: Ndege ya Precision Air yapata ajali Ziwa Victoria, watu 19 wafariki dunia

Mkuu usimshangae huyo kwani ni emotion tu kwa mtu na mtu, kuna watu hata movie tu wanalia

Ila baada ya siku kadhaa tutajua tabia zake kwenye mitandao hata ndugu na watu wa karibu wakitueleza alivyo who are we to judge a man
 
Hawa wanaleta siasa but believe me hali si kama watu wa ....wanavyo push agenda zao humu,kukaa tu 20 minutes hapo unaponaje,hizi siri siri sijui faida ni ipi ,africans puuuh!
Hapo BP hata kama huna inaanza hapo hapo.
 
 
Labda walifungua mlango wakatoka wakawafungia waliobaki
Mbona najibu hivi?
Wanakera sana yaani waokoajia wanashindwa na wavuvi

Ni mda sasa wa na vetting ya uhakika kwa wafanyakazi hawa kuanzia wa juu akipewa kwa kubebwa hawezi kujua wa chini wanafanya nini wala haijui kazi yake ni nini na usimamizi ukoje
 
Watu 19 wamethibitika kufariki dunia katika ajali ya ndege inayomilikiwa na Shirika la Ndege la Precision, iliyotokea mapema hii leo mkoani Kagera.

Ndege hiyo ilikuwa ikisafiri kutoka Dar es kwenda Bukoba mkoani Kagera, na ilipata ajali hiyo ikiwa na watu 43 ndani.

Ajali hiyo imetokea katika ziwa Victoria, takribani mita 100 kabla ya ndege hiyo kutua katika uwanja wa ndege wa Bukoba.
 
Niwakumbushe Rais na Makamu wake wako nje ya nchi wakitafuta misada ili wajanja waje waile! Nchi ya mazombi hii twendeni tu!
Ushawahi kujiuliza uwanja uko karibu na ziwa lakini hakuna vifaa vya ukoaji! Our leader they do not think out of the box!
 
Yaani maisha sijui hata yana maana gani, inauma na kuumiza sana!
Tunaweza kuilaumu serikali na watendaji wote wanaohusika na ukoaji kwa kutokuwajibika kwa namna moja au nyingine lakini ajali haina kinga, ajali haitangulizi taarifa kwamba itakuja. Kwa sababu hio kila tahadhari inabidi ichukuliwe kwa wote wenye kuhusika vinginevyo sauti za lawama zitakua nyingi baala ya pongezi.

Yote ya yote maisha yetu hapa duniani tumedhaminiwa tu , wakati fulani huyo mwenye dhamana akiamua vinginevyo inatupasa tusilaumu bali kushukuru.

Tunamshukuru Mungu kwa ajili ya maisha ya ndugu zetu hao walio fariki, tunaomba wajaliwe pumziko la milele.
 
Mkorea uliona Jerusalem hii hapa..hilo eneo mwaka 2013.nilipanda bus maarufu la Moro rangi ya Simba, tulipoanza mteremko kutoka ilula bus likafeli break...mule ndani hakuna alioeonekana mpagani ...zilipgwa sala hatari..Mungu alituifikisha comfort..salama. ila wengi tulihama bus.na kuendelea na safari
 
Inamaana kwa taarifa hii Rubani hajajumuisha katika watu waliopoteza maisha? Lakini mkuu wa mkoa Chalamila alikuwa naongea watu 26 kuokolewa mbona namba imeanza kuleta mkanganyiko!
Ndege ilikuwa na jumla ya watu 43
waliookolewa 26
waliofariki 19
Hapo kuna walakini ngoja tuvumuilie tutapata taarifa zote kwa usahihi! Polen sana nyote!
 
Niwakumbushe Rais na Makamu wake wako nje ya nchi wakitafuta misada ili wajanja waje waile! Nchi ya mazombi hii twendeni tu!
Ushawahi kujiuliza uwanja uko karibu na ziwa lakini hakuna vifaa vya ukoaji! Our leader they do not think out of the box!
Makamu wa Rais tu mwenyewe sijawai mjua sura wala kichwa chake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…