Bukoba: Ndege ya Precision Air yapata ajali Ziwa Victoria, watu 19 wafariki dunia

Bukoba: Ndege ya Precision Air yapata ajali Ziwa Victoria, watu 19 wafariki dunia

Komandoo kipensi wa majini walikua wana ogopa kulowesha nguo zao kwenye maji
647884082.jpg
 
Ndege huwa inaruka angani japo ikitua ziwani inavyo vifaa vyake vya uokoaji yaani fulana na maboya ila inahitaji wahudumu wake walio makini na jasiri. Ndege ina milango na boya kubwa ambalo hutumika kuwatoa abiria ndani tayari wakiwa wamevaa fulana za kuelea japo haziwazuii samaki na mamba kutafuna miguu.
Mamba anakaa ziwani?
 
Hii serikali kazi kukopa tu na mijitu kwenda nje ya nchi kila kukicha lkn hakuna hata mwenye akili timamu alosema kuhusu ununuzi wa vifaa vya uokoaji Wala askari kutrainiwa jinsi ya kuokoa watu kweny majanga
Kabla ya kuilaumi Serikali jilaumu wewe na watanzania wenzako kwa kutoiwajibidha Serikali I'll iyimize mnachokihitaji.
 
Wanaosema ndege ingeenda Mwanza je wanajua sababu ya kushindwa kutua? Kama tayari kulikua kuna hali ya hewa mbaya/hitilifu wangeendaje Mwanza na hali/hitilafu hiyo, tushukuru waliotoka hai the rest tuwaachie wataalamu na baada ya hapo hatua zichukuliwe kwa uzembe wote utakaobainishwa kuanzia kwenye airline operator mwenyewe mpaka kwa mamlaka za uokozi.
 
Hakuna wa kumlaumu; hakuna anayepanga ajali, na chombo chochote cha moto kinakuwa na mifumo yake, pale mfumo mmoja wapo unapofeli kunaweza kusababisha majanga.
 
Ndugu msiamini sana Serikali yetu Magufuli aliiharibu sana hao abiria 26 waliokolewa labda wakionekana ndio nitaamini.

Ndege kama ninavyoijua mimi plus huduma mbovu za uokoaji tulizonazo ikite ndani ya ziwa-halafu uniambie watu wameokolewa? Hii ni fanganya Toto na uongo wa mchana.
 
Vifo vinafika 19
Kuna upuuzi mkubwa umefanyika eti wanaazima vifaa vya uokoaji kutoka Kagera Sugar nimeumia Sana kiukweli
Waliopona na wangapi kwanza tuanzie hapo maana mpaka mda huu naona kuna Kama kificho ficho flani , Serikali hakusababisha ajali ,ila tumeona mapungufu katika vitendea kazi vya huokoaji, plus na akili ndogo wa viongozi wa Mkoa.

Na Kama ndivyo hakuna sababu ya kuficha ukweli
 
Ndugu msiamini sana Serikali yetu Magufuli aliiharibu sana hao abiria 26 waliokolewa labda wakionekana ndio nitaamini.
Ndege kama ninavyoijua mimi plus huduma mbovu za uokoaji tulizonazo ikite ndani ya ziwa-halafu uniambie watu wameokolewa???.hii ni fanganya Toto na uongo wa mchana.
Facts!
 
Mikutano kama hii inasaidia nini wakati kazi ya uokozi inaendelea????
dodoma_zone_~p~CkoBfhlq27l~4.jpg

dodoma_zone_~p~CkoBfhlq27l~3.jpg

Screenshot_20221106-194907_Instagram.jpg
 
Kikosi cha zima moto na uokoaji , kinatakiwa kutafakari katika haya hivi karibuni moto uliwaka kule mlina Kilimanjaro lakini jitihada za kuuzima moto zilikuwa siyo effective sana ikichangizwa na vifaa vilivyokuwa vikitumika, leo tena Ndege imedondoka lakini pia tumeendelea kushuhudia bado kikosi hiki hakijajipanga kisawasawa kukabiliana na matukio ya dharula katika maeneo tofauti tofauti.

Serikali ione umuhimu wa kukiwezesha kikosi hiki ili kifanye wajibu wake kisheria kikamilifu... Roho za watu hazina spare...Mlima Kilimanjaro unaiingiza serikali fedha nyingii sanaaa. Basi upewe kipaumbele maalumu.

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom