A
Anonymous
Guest
Barabara ya ‘Mnara wa Vodacom’ inayochepuka kutoka barabara mpya iendayo Butiama-Nyamuswa-Ukerewe imekuwa kero kwa wakazi wa Ligamba mtaa wa Ligamba ‘A’—Wilaya ya Bunda, Mara.
Barabara hii, licha ya kuelekea kwenye minara ya Vodacom na ofisi za TBC pamoja na minara ya TBC, haijawahi kufanyiwa marekebisho tangu kipindi cha uchimbaji moramu uliokuwa unaendelea mtaa huo wakati wa ujenzi wa barabara kuu ya lami ya Ukerewe-Butiama.
Katika barabara hii, Vodacom wamepitisha nyaya za Fibre kuelekea kwenye mtandao wao na kusababisha mmonyoko wa ardhi huku nyaya zikibaki nje baada ya mvua za miezi hii.
Mnamo nusu ya kwanza ya mwaka huu, kwenye ufunguzi wa minara ya TBC Mkoani Mara, Waziri wa Ujenzi akiwa mgeni rasmi alitoa ahadi ya kujenga barabara hiyo lakini hadi sasa haijawahi hata kufanyiwa ukarabati.
Licha ya mashirika makubwa kutumia barabara hiyo, bado hali yake si nzuri huku madaraja na barabara vikiharibika vibaya kwa kukosa miundombinu kama mitaro.
Nitoe wito kwa serikali kuliangalia hilo na kushughulikia barabara hiyo inayotumiwa na wafanyabiashara wadogo wadogo wanaoelekea Bunda mjini kwa ajili ya biashara zao za mazao na mifugo. Lakini pia shule ya Msingi Kilimahewa iliyopo katika njia hiyo.
Barabara hii, licha ya kuelekea kwenye minara ya Vodacom na ofisi za TBC pamoja na minara ya TBC, haijawahi kufanyiwa marekebisho tangu kipindi cha uchimbaji moramu uliokuwa unaendelea mtaa huo wakati wa ujenzi wa barabara kuu ya lami ya Ukerewe-Butiama.
Katika barabara hii, Vodacom wamepitisha nyaya za Fibre kuelekea kwenye mtandao wao na kusababisha mmonyoko wa ardhi huku nyaya zikibaki nje baada ya mvua za miezi hii.
Mnamo nusu ya kwanza ya mwaka huu, kwenye ufunguzi wa minara ya TBC Mkoani Mara, Waziri wa Ujenzi akiwa mgeni rasmi alitoa ahadi ya kujenga barabara hiyo lakini hadi sasa haijawahi hata kufanyiwa ukarabati.
Licha ya mashirika makubwa kutumia barabara hiyo, bado hali yake si nzuri huku madaraja na barabara vikiharibika vibaya kwa kukosa miundombinu kama mitaro.
Nitoe wito kwa serikali kuliangalia hilo na kushughulikia barabara hiyo inayotumiwa na wafanyabiashara wadogo wadogo wanaoelekea Bunda mjini kwa ajili ya biashara zao za mazao na mifugo. Lakini pia shule ya Msingi Kilimahewa iliyopo katika njia hiyo.