Bunda: Mwili wa Samson Josiah, mmiliki wa mabasi ya Super Sami waokotwa mto Ndabaga kwenye Kiroba

Bunda: Mwili wa Samson Josiah, mmiliki wa mabasi ya Super Sami waokotwa mto Ndabaga kwenye Kiroba

Kwa jinsi alivyofungwa fungwa inaonekana alitupwa akiwa mzima mzima kama anavyoonekana hapo na kutoswa mtoni.

Eeh Mungu Baba ,Mwenye kila uweza na nguvu, Naomba ukakomeshe haya mauaji yanayofanyika dhidi ya watu mbali mbali, Nakemea pepo LA mauaji lililowaingia wahalifu hao. Naomba Mungu ukawabadilishe Roho za wauaji hawa wakawe na Roho iliyojaa Amani,upendo na unyenyekevu kwa wenzao ili Tanzania irudi katika hali Yake ya kuwa Mahali salama pa kuishi kwa kila RAIA.

Ee Mungu Baba mwenye enzi, naiombea na hii familia ya marehemu iliyoachwa katika taharuki na ukiwa, Ukawape nguvu na ujasiri wa moyo katika kipindi hili walichonacho cha huzuni kuu katika familia yao. Ukaiwezeshe familia hii istahimili msiba huu mzito kwao.

Naomba hayo kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo anayeishi na kutawala daima na milele

Amina.

Raha ya milele umpe ee Bwana
Na mwanga wa milele umwangazie
Apumzike kwa Amani.

Amina.

Hivi ni kweli Polisi wamezidiwa maarifa na hawa wauaji?

Tulipofikia sasa, yamfaa Rais aingilie kati mauaji haya yanayoendelea kwa kufanyia mabadiliko ya kiutawala hii Wizara ili waje wengine wenye mbinu mpya kuwadhibiti hawa wahalifu.

Haya mauaji yanayoendelea sasa mwisho wake ni UPI?
 
Achana na siasa kwenye kila jambo mtoto. Mtu kafa we unaulizia alikuwa chama gani. Unataka ukampe kadi ya chama chako au?

Labda anataka aunganishe doti,mauaji ya Diwani wa CDM Kule Moro, Mwenyekiti wa NCCR MAGEUZI kule Kasulu na hili LA huyu tajiri ili ahitimishe kuwa mauaji ya sasa yamewalenga wapinzani.
Tungoje atakuja kuyajibu maswali yako yeye mwenyewe.
 
Nchi si salama tena, hali hii haikubaliki iote mizizi ktk jamii yetu ya Ki-Tanzania.
 
Sijui hata niandike nini.,

Nimetamani kutukana.. Nikaona sio busara.

Nimetamani kulaani… nikagundua sio kaz yangu. Ni kaz ya Muumba.

Nimetamani kulumu… pia haitasaidia.

Ngoja niishie hapa.

R. I. P marehemu SamsonJosiah.

Umeuwawa kikatili sana.
 
Fanya busara kidogo kwa kuigiza kama nawewe ni mtu timamu.

Unaharibu upepelezi kwa kuingiza siasa. Au wewe ndio muhusika hapa unafanya hivi kuwapotosha wapelelezi?
Yaani huwa nasikitika sana nikisoma comments Za watu Kama hao. Inashangaza Sana kila mauaji ni wao,Yaani watanzania tumeshaingizwa kwenye michezo ya wanasiasa,kulaumu bila kuwa na ushahidi
 
Huyu alikuwa chama gani kwani? Wanaomfahamu watueleze alikuwa anataka ubunge au nafasi ya kisiasa? Na je anahistoria gani nyuma ya utajiri wake?
Hakuna añayejua ni mfuasi was chama gani, lakini Habari zilizopo alichangia vizuri tuu matibabu ya Lissu kama ambavyo wapo wa Chadema,CCM na vyama vingine walivyo changia
 
Kuna watu walipatikana katika mtindo huo huo tukaambiwa ni wahamiaji haramu!
sasa huyu ana jina tusubiri kuambiwa kama kajiua iki kuketa taharuki au wauaji wa ndanu wamekopi mtindo wa disposal wa wale wanaowatelekeza wahamiaji haramu waluokufa ili kuketa taharuki,ama wasiojulikana kwa ujumla wake wanaendeleza wimbi la mauaji?
Na sijui katika pelelezi zao wamepata kugundua kama kesi zote zinawatendaji wa aina moja au ni isolated na hapo tuanze mbali ,mauaji ya Mawazo yule wa morogoro ,mvungi nk na kwenye utekaji
Kibanda ,roma,nondo ,masheikh nk.
Na waliopotea kote iangaliwe kama wahusika wanahusiana.
 
Yaani huwa nasikitika sana nikisoma comments Za watu Kama hao. Inashangaza Sana kila mauaji ni wao,Yaani watanzania tumeshaingizwa kwenye michezo ya wanasiasa,kulaumu bila kuwa na ushahidi
Ila nawe pia usifanye kila kesi mpya ,kuwa na historia kidogo.
Waziri mwenye dhamana ya mambo ya ndani alitamka .
1.watu waliokutwa katika hali hiyo ni wahamiaji haramu
2.Roma alitekwa ukafanyika uchunguzikuna lolote unalolifahamu zaidi ya hisia kubwa tu kuwa kaambiwa asimnong'oneze hata mkewe kilichomtokea
3.Kwa sababu hz hz za sanaa za kiuharakati akakamatwa nay wa mitego -this time ikaonekan itaback fire akaachiwa kwa kauli ya mkuu wetu.
4.Kuna Masheikh wamekamtwa wakashikiliwa pasipojulikana baadae wakapatikana na walipotoka wao "walishukuru" kuwa wako hai na wakamatiaji wao "hawakuwa na nia mbaya" bali walikuwa wanatekeleza majukumu yao ya kiusalama!
Ni hawa masheik tu pekee ndio waliotoa hints nani anawakamata.
Hitimisho
Ukiangalia kesi pale ambapo wahanga wakonhai unatishika sana na yanayoendelea nchi hii japo kuwa kimsing pia tunakubaliana kywa kuna matatizo ya kiusalama na lazima walinzi wetu wawe makini hasa ukizingatia yale ya kibiti anbapo serikali pamoja na kuahidi kukimaliza na kulitolea maelezo mpaka leo hatuna maelezo nn kilikuwa kinaendelea kibiti -ujambazi au ugaidi!
 
Huyu alikuwa chama gani kwani? Wanaomfahamu watueleze alikuwa anataka ubunge au nafasi ya kisiasa? Na je anahistoria gani nyuma ya utajiri wake?
Maswali y ingi hayo ,siijui historia ya huyo jamaa ila utajiri mwingi siku hizi umekiwa mashaka matupu.
 
IMG_20180315_063046_451.jpg
 
Back
Top Bottom