Bunda: Mwili wa Samson Josiah, mmiliki wa mabasi ya Super Sami waokotwa mto Ndabaga kwenye Kiroba

Maskini,naimagine jinsi alivyoteseka kuchinjwa bila nganzi,Binadamu ni zaidi ya mnyama.Babu yangu aliniambia zamani ukiona Binadamu unapata moyo,siku hizi ni bora ukutane na Simba kuliko Binadamu mwenzako.
Ccta mie naogopa sana lifestyle iliyopo sasa Tanzania. Hebu angalia ujasiri walionao hao wauaji!! Najiuliza je inamaana tangu wazaliwe hawajawahia kufundishwa uwepo wa mungu!? Nimechoka kabisa heri kufa kwa Ukimwi lkn si kwa style hii. Nchi imelaaniwa
 
Labda anataka aunganishe doti,mauaji ya Diwani wa CDM Kule Moro, Mwenyekiti wa NCCR MAGEUZI kule Kasulu na hili LA huyu tajiri ili ahitimishe kuwa mauaji ya sasa yamewalenga wapinzani.
Tungoje atakuja kuyajibu maswali yako yeye mwenyewe.
Sio kila kitu mnakiweka kwenye siasa wafanyabiashara yaweza kuwa alikua na mkwaruzano na matajiri wenzake ,,,msiingize siasa kila tukio
 
Kuna mambo pia tunafanya nyuma na kusahau kabisa,, tunaacha vidonda mioyoni kwa watu ,, hujui mtu anawaza nn mwishoe ndio huwa hivyo,,,, unaweza kuta ni kisas hata cha miaka 15 iliyoisha ,,

Hatuwez jua pia,,
Kisasi gani,mambo yko wazi tusimeze maneno wasiojulikana wanafanya mambo kwa baraka za mkuu,huo mto kwa upande wa serengeti unamamba wengi sana ukipita utafikiria mijusi imejianika juani.
Wamechoma gari serengeti halafu wakaja kumtupia upande wa mto kilawira ambapo hakuna mamba angeuawa serengeti maiti isingefika hpo ilipookotwa mamba wangeshafanya yao
 
Hapo ndipo tunaona mambo ya ukweli yalivyo, kapotea mtu, mke, watoto, jamaa na marafiki wametoa taarifa marehemu kapatikana...
Sasa haya ya mitandaoni kwamba maiti zaokotwa baharini halafu ndugu kutokulalamika haingii akilini kabisa..
Mkuu kama hilo furushi lingekwama mahali huko mtoni ni dhahiri marehemu asingejulikana alipo. Nina mashaka hilo furushi ilidhamiriwa lionekane.
 
Mgeni... sawa labda mgeni muuaji.
 
Huyu alikuwa chama gani kwani? Wanaomfahamu watueleze alikuwa anataka ubunge au nafasi ya kisiasa? Na je anahistoria gani nyuma ya utajiri wake?
hajawahi kujihusisha Na siasa, pombe hanywi. Ila hakuwa mnoko kuwakopesha fedha wahitaji.
 
Duuuh...! Na walofanya hio kitu wakifika kwa WANENE wao wanasema deal done!! Aiseeee Tanzania haiko Salama
 
Jamani acheni siasa kwenye mambo kama haya. Ni vizuri vyombo vya ulinzi na usalama vikafanya kazi yake. Tukiendelea kuilaumu serikali/watawala mwisho wetu hautakuwa salama. Tutaanza kuuana kwa ajili ya ugomvi wa mashamba, ardhi, mirathi, mapenzi, dhuluma, nk, huku tukijua kwamba tutaibebesha mzigo serikali kwamba ndiyo imehusika. Tukifika huko, ni hatari sana kwa mustakabli wa taifa letu.
 
Mungu ailaze roho yake mahala pema peponi.
 
Fanya busara kidogo kwa kuigiza kama nawewe ni mtu timamu.

Unaharibu upepelezi kwa kuingiza siasa. Au wewe ndio muhusika hapa unafanya hivi kuwapotosha wapelelezi?

Inahitaji upelelzi gani hapo mkuu?
Style yao ya mauaji ni ileile , namini huko kanda ya ziwa kutakuwa n amauaji mengi sana yakiendelea kimyakimya.
 
Huyu alikuwa chama gani kwani? Wanaomfahamu watueleze alikuwa anataka ubunge au nafasi ya kisiasa? Na je anahistoria gani nyuma ya utajiri wake?

Mkuu ni wachama gani ufa na kufugwa kwenye sandarusi na mawe?
hivi huoni haya mambo yanafanana?
 
kaka mbona unabagua umesahau polisi wetu kibiti na raia wa eneo hilo?
 
Sijameza maneno,, nimewaza upande wa pili ,, siku zote dhambi yoyote ifanyikao ni vuno la shetan" na analaumiwa sawa ila kumbuka kuna mengine shetan hukana na kusema sijamtuma ni akil zake tu,,,

Kuna kikundi cha watu wanachukulia faida ya kufanya yao kwa hali hii iliyopo sasa mpka inamfrustrate mkuu wetu wa nchi
 
Hiviii wale wanaotoaga uhai wa binadamu wenzao ikitokeaga nao wakafaa huwaa wanakutana na wale waliowakatisha uhai wao? Huwa wanajiskiajee aibu huruma au?

Usalama wetuu umezid kuwa salamaa na shwarii kabisaa aman mpaka imejaaa pomon
 
Huyu alikuwa chama gani kwani? Wanaomfahamu watueleze alikuwa anataka ubunge au nafasi ya kisiasa? Na je anahistoria gani nyuma ya utajiri wake?

Ukishatajiwa hayo yote utachukua hatua gani? Tunakoelekea huko hata mtu akiwa na upungufu wa nguvu za kiume tutaingiza siasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…