Bunge halina mamlaka kumhoji Askofu Gwajima alichoongea na waumini wake

Bunge halina mamlaka kumhoji Askofu Gwajima alichoongea na waumini wake

MdogoWenu

JF-Expert Member
Joined
Dec 23, 2009
Posts
554
Reaction score
916
Askofu Gwajima,

Kwanza sikubaliani na wewe katika suala la kukataa chanjo ya Corona kwa kadiri unavyowahubiria waumini wako. Binafsi nimeshachanjwa na ninahimiza watanzania wote wachanje tofauti na unavyohubiri katika kanisa lako.

Hivyo, dawa pekee ya mimi kukupinga ni kwenda kuchanja na hivyo tayari nimeshachanjwa na sitarajii kupata madhara unayohubiri. Hivyo mimi ni mpinzani wako halisi katika mahubiri yako.

Lakini pamoja na kukupinga kwa staili yangu ninalipinga Bunge hatua linazochukua dhidi yako.

Umeitwa kwenye kamati ya Bunge kwamba umesema uongo na kushusha heshima ya bunge. Hapa mimi nakutetea kwa hoja zifuatazo.

Ulichokitoa kanisa kwako ni mahubiri kwa waumini wako. Waliandamana kutoka nyumbani wakakufuata kanisani kukusikiliza.

Ulisema vizuri kwamba unazungumza kama mtu wa Mungu na si kama mbunge wa Kawe.

Hivyo, ukifika kwenye kamati ya bunge kwanza waulize wanakutuhumu kwa kauli uliyoitoa wapi. Wakisema ni yale ya kanisani kwako kataa katakata kujibu lolote, waeleze mipaka yao kwamba dola ya Tanzania haina mamlaka ya kukuchagulia mahubiri na haina mamlaka na jambo la kidini.

Waambie wasome ibara ya 19(2) ya katiba inayosema kazi ya kutangaza dini siyo ya dola ni yako na wenzako mnaotangaza dini. Hivyo, usijibu chochote waache waamue wanachokitaka.

Kama wabunge wanakupinga waende kwenye makanisa yao na misikiti yao wafanye tofauti kama nilivyofanya. Mimi nimekupinga kwa kwenda kuchanjwa na ninahamasisha wengi kuchanjwa.

Hivyo, fanya kadiri ya maelekezo yangu, ukiwaacha kesho watafanya kwenye kanisa jingine kwa hoja tofauti.
 
Waumini wake ni wajinga.

Mtu kaiba kura mchana kweupe lakini mazombi bado yanamsikiliza.

Kuhusu chanjo anatakiwa achague kati ya ccm au kanisa la kitapeli,aache kimoja.

Mimi siamini siku ile kuwa yule Samia alichanjwa kweli,imekaa kisanii sana jinsi alivyochanjwa.

Gwajima ni tapeli lao walilolisaidia kuingia bungeni.

.Kawe wana bahati mbaya,gwajiboy na mzee mdee wote ni makalio
 
Waumini wake ni wajinga
Mtu kaiba kura mchana kweupe lakini mazomni bado yanamsikiliza
Kuhusu chanjo anatakiwa achague kati ya ccm au kanisa la kitapeli,aache kimoja..
Mimi siamini siku ile kuwa yule Samia alichanjwa kweli,imekaa kisanii sana jinsi alivyochanjwa..
Gwajima ni tapeli lao walilolisaidia kuingia bungeni
.Kawe wana bahati mbaya,gwajiboy na mzee mdee wote ni makalio
Ni kama kawaloga jmn
 
Waumini wake ni wajinga
Mtu kaiba kura mchana kweupe lakini mazombi bado yanamsikiliza
Kuhusu chanjo anatakiwa achague kati ya ccm au kanisa la kitapeli,aache kimoja..
Mimi siamini siku ile kuwa yule Samia alichanjwa kweli,imekaa kisanii sana jinsi alivyochanjwa..
Gwajima ni tapeli lao walilolisaidia kuingia bungeni
.Kawe wana bahati mbaya,gwajiboy na mzee mdee wote ni makalio
Usizoelee kutukana watu kienyeji hivyo! Ubawa wa mahubiri ya Gwajiboy ni nini?
Kuchanja ni hiari si ndio? Mnataka ndio mzee tu...mkikutana na resistance mnatumia miguvu badala ya akili! Waacheni watz waamue bila kuwalaghai na kuwagiribu kwa misinformation!
Mwanasiasa akikuambia nje giza kitu cha hekima kufanya ni kwenda kuchungulia mwenyewe ujiridhishe😜!
 
Alikosea mwenyewe kuingia kwenye Siasa. Kwanza, alijiunga na chama cha siasa cha CCMkwa hiari yake. Hivyo anapaswa kutii msimamo wa CCM.

Pili, akagombea ubunge kupitia chama cha siasa cha CCM na chama kikampigania hadi akapata ubunge. Bunge la CCM likapitisha Azimio la kumpongeza Salimia Rais wa Tanzania Kupitia CCM.

Hivyo ili awe huru kufanya atakayo kama kiongozi wa kiroho aanze kwanza kujiuzulu uanachama wake wa CCM na hivyo kupoteza ubunge.

Vinginevyo awe tayari kuunga mkono sias za CCM ikiwemo hayo anayoshitakiwa nayo. Hakuna namna. Kwanza, mambo ya kupinga utaalamu siyo kazi ya dini. Yeye mwenyewe aliamini katika utaalamu ndio maana alienda shule akajua kusoma na kuandika kwa Kiswahili na Kiingereza.

Aliamini katika utaalamu ndio maana alijenga nyumba na kuezeka mabati, anatumia vipaza sauti, gari, simu, viatu, nguo, n.k. vyote hivyo ni matokeo ya utaalamu. Ni ujinga kupingana na wanataaluma kwa mambo ya kitaalamu. aache kutumia hata hizo mic kanisani kwake.
 
Huongelei ibara yoyote ya katiba unalera ngonjera zisizo na kichwa wala miguu.

Alikosea mwenyewe kuingia kwenye Siasa. Kwanza, alijiunga na chama cha siasa cha CCMkwa hiari yake. Hivyo anapaswa kutii msimamo wa CCM. Pili, akagombea ubunge kupitia chama cha siasa cha CCM na chama kikampigania hadi akapata ubunge. Bunge la CCM likapitisha Azimio la kumpongeza Salimia Rais wa Tanzania Kupitia CCM. Hivyo ili awe huru kufanya atakayo kama kiongozi wa kiroho aanze kwanza kujiuzulu uanachama wake wa CCM na hivyo kupoteza ubunge. Vinginevyo awe tayari kuunga mkono sias za CCM ikiwemo hayo anayoshitakiwa nayo. Hakuna namna. Kwanza, mambo ya kupinga utaalamu siyo kazi ya dini. Yeye mwenyewe aliamini katika utaalamu ndio maana alienda shule akajua kusoma na kuandika kwa Kiswahili na Kiingereza. Aliamini katika utaalamu ndio maana alijenga nyumba na kuezeka mabati, anatumia vipaza sauti, gari, simu, viatu, nguo, n.k. vyote hivyo ni matokeo ya utaalamu. Ni ujinga kupingana na wanataaluma kwa mambo ya kitaalamu. aache kutumia hata hizo mic kanisani kwake.
 
Waumini wake ni wajinga
Mtu kaiba kura mchana kweupe lakini mazombi bado yanamsikiliza
Kuhusu chanjo anatakiwa achague kati ya ccm au kanisa la kitapeli,aache kimoja..
Mimi siamini siku ile kuwa yule Samia alichanjwa kweli,imekaa kisanii sana jinsi alivyochanjwa..
Gwajima ni tapeli lao walilolisaidia kuingia bungeni
.Kawe wana bahati mbaya,gwajiboy na mzee mdee wote ni makalio
Umetumia lugha ngum mkuu wangu
 
Askofu Gwajima,

Kwanza sikubaliani na wewe katika suala la kukataa chanjo ya Corona kwa kadiri unavyowahubiria waumini wako. Binafsi nimeshachanjwa na ninahimiza watanzania wote wachanje tofauti na unavyohubiri katika kanisa lako.
🤣 🤣 🤣 🤣 🤣Acheni kukwepa mzizi wa tatizo na kushughulikia matawi yake. Tatizo lipo kwenye kiongozi wa umma kuwa pia kiongozi wa dini! Hapa ndipo lilipo tatizo hasa. Kuna mgongano wa maslahi. Ama angejiuzulu uongozi wa kanisa na abaki kama muumini wa kawaida au ajiuzulu ubunge na abaki kuongoza kanisa.

Ndiyo maana huwa wanasema hata kama mtu ni mkurugunzi wa kampuni na anataka kugombea uongozi wa umma kama ubunge, inabidi ajiuzulu kwanza ule ukurugenzi ili akipata ubunge kusiwepo na mgongano wa maslahi. Gwajima angekuwa ameachia ngazi ya kuongoza kanisa lake na kuwa muumini wa kawaida haya yote yasingetokea.
 
Huongelei ibara yoyote ya katiba unalera ngonjera zisizo na kichwa wala miguu.
Aliyekudanganya kwamba CCM inaongoza kwa hizo ibara za katiba ni nani? Chama chake cha Siasa cha Askofu Gwajima kinajulikana tabia zake. Sasa anashangaa nini? Kwani hakujua anajiunga na chama cha aina gani? Na bado. Kuna siku hicho chama chake kitamtuma kwenda kupoteza watu, kuwapiga risasi watu, na hicho chama kina haki ya kuwatumia wanachama wake kufanya kazi zake zikiwemo za kuwaweka watu kwenye viroba.
 
Uganda haijaanza na Kibwetere watu kufia dini, walianza akina Karoli Lwanga kama hujui.

Hata kibwetere alikuwa na wajinga kama nyie, kwahiyo hata akikaa na nyie misukule yake mathalan akavunja sheria za nchi aachwe kisa kaongea na waumini duh
 
Back
Top Bottom