Bunge jipya lina hali mbaya! Serikali itafanaje kuliokoa Bunge ili kuwa na Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni?

Bunge jipya lina hali mbaya! Serikali itafanaje kuliokoa Bunge ili kuwa na Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni?

Kwa taarifa yenu serikali inakwenda kufanya kazi kwa kasi mpya na wananchi wategemee maendeleo yenye tija.Tunapigania kuwa taifa lenye uchumi wa kati WA JUU.Tunatarajia kuwa taifa lenye uchumi wenye nguvu katika ukanda wa Afrika Mashariki kati na kusini. Upinzani utatuchelewrsha bana, mbona CHINA hana upinzani na mambo yake ni super.
 
Magufuli hajashinda Urais kwa haki kwanza ulijue hilo! La pili Wabunge wa Upunzani wameibiwa kura zao na kulikuwa na kura fake nyingi tu! La tatu usijifanye msamaria mwema kwa Wapinzani wewe ni moja ya watu WANAFKI SANA HAPA DUNIANI!
 
Baada ya JPM kuwaambia wakurugenzi kuwa hatawalipa mishahara iwapo watatangaza wapinzani kushinda ndio hili limetokea sasa.

Uchaguzi ulikuwa wa upendeleo na udanganyifu.NEC imetufikisha hapo.Hakuna mwwnye furaha
 
shutuma za Lisu kuwa kibaraka wa Wazungu hazina mshiko
Unasema hivyo kwa kuwa huna unachokijua juu ya hili. Sikulaumu!
Yeye aende zake huko Belgium akaishi kwa amani, sisi tunaendelea kujenga nchi yetu. Tumechelewa mno, tumepigwa sana, tumeliwa kwa muda mrefu; sasa tumepata mtu aliye serious kutuongoza tutoke kwenye hiyo hali, tutamuunga mkono na kumpa support kila iwezekanavyo oli tutoke kwenye hii hali. Sasa hivi hatuhitaji distractions zozote za kizembe.
 
Upuuzi wa aina yake huo. Msingi wa uchaguzi ni kuwapa wananchi fursa na mamlaka ya namna wanavyotaka kuongozwa hili halijafanyika. Wametangazwa kwa matakwa mtu mmoja. Basi aendelee kuteua wanaomuunga mkono na mauaji, mateso na kukanyaga katiba.
Ateue viti maalum toka CCM itakidhi matakwa ya kisheria.
 
Wanabodi,

Hili ni bandiko la swali, Bunge letu jipya linalokwenda kuundwa hivi karibuni baada ya uchaguzi Mkuu, lina hali mbaya sana ya kuwa liko kwenye hati hati ya kutokuwepo kwa kambi rasmi ya upinzani Bungeni.

Swali ni Jee NEC, Rais Dr. Mwinyi na Rais Dr. Magufuli wataingia huruma na kuokoa jahazi kwa kuliokoa Bunge letu la JMT ili liweze kuwa na kambi rasmi ya upinzani Bungeni?.

Declaration of Interest

Japo mimi ni kada wa chama cha siasa, na uchaguzi umekwisha, sasa narejea kwenye zile safu zangu za " Kwa Maslahi ya Taifa", ambazo zinatanguliza uzalendo kwa maslahi ya taifa letu Tanzania, hivyo nakuomba unisome with clear conscious kama mnamsoma Mtanzania mwingine yoyote, lakini kama tayari umeisha ni lebo mimi ni kada na kujiambia kila ninachoandika ni kwa maslahi ya chama changu na sio maslahi ya taifa, nakushauri uishie hapa, maana hata ukiendelea kunisoma with pre conceived opinion, hautaweza kuiona rationale ya bandiko hili.

Na kwa vile hili ndilo bandiko langu la kwanza Jukwaa la Siasa baada ya Uchaguzi, naomba kuchukua fursa hii kumpongeza Rais, Dr. John Pombe Joseph Magufuli kwa ushindi wa kishindo, nakipongeza Chama changu CCM, na kupongeza wote waliodhinda.

Japo ni lengo la kila mwana CCM, kuona chama chake kinashinda viti vyote na kata zote, ila pia kuna baadhi ya wana CCM, ambao ni makada wazalendo zaidi, wamefurahishwa na ushindi wa kishindo wa CCM, ila pia ni wazalendo zaidi kwa nchi kuliko chama, tungependa kuona wapinzani makini wachache wakiingia Bungeni ili kujenga ile dhana ya Bunge la vyama vingi. Hivyo kushindwa kwa mtu kama Zitto ni masikitiko kwa wana CCM wazalendo wengi wa type yangu!. Tunapenda Bunge la CCM, lakini pia lenye mwamko na msisimko wa challenges za upinzani.

Hivyo kwenye kushangilia ushindi, nawasihi viongozi wetu na wana CCM wazalendo wenzangu, tushangilie kwa kiasi, tusiwatambie upinzani, tusiwakejeli, kuwatukana wala kuwabeza, kwasababu nao ni Watanzania wenzetu na wamechaguliwa na Watanzania, hivyo kwenye hotuba zetu, tupunguze kujimwambafy na badala yake tuongeze humility na kuhutubia hotuba za ku heal na sio za ku hurts.

Wapinzani

Asiyekubali kushindwa sio mshindani, uchaguzi umekwisha, aliyeshinda ameshinda kwa haki na kihalali, aliyeshindwa ameshindwa kwa haki na kihalali, tukubali matokeo, kazi sasa ibaki ni moja tuu, kuijenga nchi yetu kwa kutoa kila aina ya ushirikiano kwa washindi.

Vitabu vya dini zote vinafundisha Wananchi kutii mamlaka halali. Baada ya uchaguzi kumalizika na rais kupatikana na kuapishwa, kile kitendo cha kuapishwa ni kumhalalisha rasmi hivyo baada ya rais Magufuli kuapishwa, sasa yeye ni mamlaka halali, ndiye rais wa JMT, ni rais wa Watanzania wote, waliomchagua, wasio mchagua, hata ambao hawakupiga kura, rais Magufuli ndiye rais wa nchi, tutii mamlaka halali.

Baada ya kuapishwa na kuanza kazi, hakuna kitu kinachoitwa kususa, kutokubali matokeo au kutomtambua rais, huko ni kujifurahisha tuu, kwa sababu tayari rais yupo na ana exist, umtambue, usimtambue, yeye ndio rais wako na yupo kwa ajili yako. Unaweza usimpende, unaweza usimkubali, lakini huwezi kutomtambua!. Hivyo viongozi wa upinzani acheni hadaa za kuwahadaa wafuasi wenu kuwa hamumtambui rais. Rais ni mtu mwenye status of duality.

1. Rais Magufuli ni mtu, ni binadamu, unaweza usimpende, usimkubali na ukakataa kutambua ushindi wake, that is human, kama humpendi mtu, hakuna anayeweza kukulazimisha umpende au umkubali, hilo una uhuru nalo.

2. Rais Magufuli ni Taasisi ya urais, president institution, hii ni mamlaka, hakuna choice ya kuipenda, kuikubali au kuitambua, ipo kisheria hivyo ni lazima uiheshimu, na kuitii mamlaka hii, it's not a matter of choice, its an obligation, ni lazima kuitii mamlaka na usipotii, mamlaka inakushughulikia, ndio maana hata sheria, kutokujua jambo fulani ni kosa kisheria, is not an excuse sheria isi act on you, hivyo hakuna kitu kinachoitwa kutokumtambua rais.

Huo ulikuwa ni utangulizi tuu kuwekana sawa, mada ya leo ni hii.
Kufuatia poor performance ya vyama vya upinzani kwenye uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, kwa Watanzania kuvikataa na badala yake kukichagua CCM pekee, but 4!, idadi hiyo haiwezi kutimiza akidi inayotakiwa kuweza kuunda kambi rasmi ya upinzani Bungeni.

Ibara ya 14 ya Kanuni za Bunge zinaeleza
2) Wabunge wote wa Upinzani wanaweza kuunda Kambi Rasmi ya Upinzani iwapo idadi yao itakuwa si chini ya asilimia kumi na mbili na nusu ya Wabunge wote.
(3) Chama cha Upinzani hakitakuwa na haki ya kuchagua Kiongozi wa Upinzani Bungeni, isipokuwa tu kama kina idadi ya Wabunge wasiopungua asilimia kumi na mbili na nusu ya Wabunge wote.

Idadi ya Wabunge wote wa Bunge la JMT ni 357, hivyo asilimia 12.5% ni wabunge 28.

Kwa matokeo ya uchaguzi huu, hata baada ya allocation ya wabunge wa viti maalum, idadi hiyo haiwezi kufikiwa, hivyo Bunge lijalo, lina hati hati ya kutokuwa na kambi ya upinzani Bungeni, kambi hii ikikosekana, maana yake, hakutakuwa na serikali kivuli, hivyo bajeti za serikali tuu zitawasilishwa bila maoni ya kambi ya upinzani, jambo ambalo is not healthy kwa Bunge la vyama vingi.

Watu watatu pekee wenye uwezo wa kuokoa jahazi hili, ni
1. Tume ya Taifa ya Uchaguzi, ikubali kutoa nafasi ya upendeleo kwa viti maalum vya upinzani hata kama hawakukidhi vingezo.
Mfano, maadam sifa ya kupata viti maalum ni chama kupata asilimia 10 ya kura zote, then Tume inaweza kuamua, wale wagombea urais wote waliopata kura zaidi ya asilimia 10%, wote waingie Bungeni.

2. Rais wa Zanzibar, anazo nafasi 10 za uteuzi wa wawakilishi, katika nafasi hizo zote 10, ateue wawakilishi 10 wa vyama vya upinzani, kati ya hao 10, wawakilishi 5, waingie kwenye GNU, na wawakilishi 5 waingie kwenye Bunge la JMT toka Baraza la Wawakilishi. This is a very big sacrifice to make.

3. Rais wa JMT, Dr. John Pombe Joseph Magufuli, na yeye ana nafasi zake za uteuzi wa wabunge 10. Usually lengo la uteuzi huu ni ili rais aweze kupata watu wa kutosha kumsaidia, kwa kuwa mawaziri, lakini kwa line up ya walioshinda CCM, kuna line up ya kushibisha mawaziri wote, na bado akabakiwa na reserve team inayoweza kuunda Baraza la Mawaziri la akiba.

Hivyo kama rais Magufuli akiingia huruma, akaamua kuliokoa Bunge letu tukufu, then na yeye ateue angalau wabunge 6 wa upinzani kuingia Bungeni kwenda kuimarisha upinzani, na rais Magufuli anaweza kuitumia kete hii kupiga ndege wawili kwa jiwe moja.
1. Kuuokoa Upinzani 2. To heal the nation from the election wounds ambazo to some ni very painful na kuna watu wako very bitter!.

Kwa ushauri wangu, napendekeza rais Magufuli awateue hawa wafuatao
1. Tundu Lissu- aligombea nae
2. Zitto Kabwe - Most Interactive MP
3. James Mbatia- Very Compromising
4. Prof Haruna Lipumba - Good Puppeteer
5. JJ.MNYIKA- Mjengaji hoja mzuri

Hili likifanyika, litatibu makovu ya uchaguzi Mkuu huu, na kuingiza vichwa vya upinzani ambavyo vitalichangamsha Bunge letu na kuliongezea msisimko.

Hili lusipofanyika, Bunge la chama kimoja, bila any challenges, japo litaharakisha maendeleo bila upinzani, litakosa msisimko na lita bore!.

Kwa kumalizia, namalizia kwa lile swali la msingi, kuwa Bunge jipya lina hali mbaya liko kwenye hati hati ya kutokuwepo kambi rasmi ya upinzani Bungeni.

Swali ni Jee NEC, Rais Dr. Mwinyi na Rais Dr. Magufuli wataingia huruma kuliokoa Bunge letu la JMT ili liweze kuwa na kambi rasmi ya upinzani Bungeni?.

Jibu la swali hili, litapatikana ndani ya kipindi cha wiki moja kuanzia Jumatatu Ijayo.

Nawatakia Jumamosi Njema

Paskali
Rejea za Bunge la Chama Kimoja


...
IMG_20201106_142408.jpg
 
Nipende kuwashukuru wote mliotoa michango yenu bila unafiki na kumshushua Pascal kwa unafiki aliouonyesha , anaouonyesha wote waliompa za uso bila huruma big up , Kati ya uliowataja ni nani alimwambia anashida na ubunge wa kuokotwa barabarani .

Nyinyi kaeni bungeni peke yenu muigeuze Tanzania kama ulaya . Muda sio mrefu mtajua madhara ya kumsukumiza wagonjwa wa bipolar disorder . Labda Kuna kitu watu hawakijui hii situation itawatesa CCM kuliko upinzani , usifikiri Wana CCM wanaipenda CCM kwa sababu ya rangi yake ya kijani au alama ya jembe na nyundo , walikuwa wanaipenda CCM kwa sababu ya maslahi , hivi una fikiri kwa uchache Nape , January , Kinana ,Makamba , Kikwete na wengine wengi bado wanaipenda CCM ?

Hata kuisikia hawataki ila hawawezi kujionyesha hadharani maana watakolimbwa .Jiwe hataki mtu yoyote yule apate hela anataka hela zote achukue yeye mpaka kodi za milango ya ofisi na viwanja vya CCM vinalipiwa kwenye akaunti hela zinaenda moja kwa moja kwa Jiwe na zamani ilikuwaje ? Unafikiri wanafurahi ?
Screenshot_20201101-195743.png
 
Nilichojifunza kwenye hii post yako ni kwamba kumbe hamkujipanga kabisa na hili bao la mkono. Unapocheza draft lazima uwe unajua unavyotoa kete 2 uliwe una lengo la kula kete 5... Sasa wakati mnapora mkasahau kuacha angalau majimbo 30 ya upinzani, hata kwa Mbatia na Lipumba kama mlikuwa mmewakamia CHADEMA na ACT Wazalendo??? Sasa majuto ni mjukuu na kwa jinsi wananchi wanavyowajua wabunge wa chama chenu bungeni wanavyoboa, hata kama mkianzisha bunge live, mmeanza kujishtukia wenyewe.
 
Mimi ningeshauri hao wabunge wa upinzani walioshinda wajiunge tu na CCM na wapitishwe bila kupingwa!
Yule wa Chadema kule Nkasi naona ameshaanza kuota mapembe na kuanza kuvutana na viongozi wake, yanaweza kujirudia yale ya Sesil Mwembe ya kukingiwa kifua na viongozi wa bunge, let's wait and see.
 
Ni kweli kwani maisha hayataenda? Mwl.nyerere alituongoza kupitia mfumo huo na maisha yakaenda.Inaumiza sana kuwa na upinzani umaolifanyia udalali nchi yetu, upinzani uliotayari kupiga bei nchi.Hatuhotaji bora mfumo wa chama kimoja na rasilimali zetu xikabaki salama
Ukikosa akili kichwani kwako ujiandae kujazwa kila aina ya ujinga na upumbavu... Tumepata uhuru 1961 upinzani umeanza 1995 sasa jiulize kabla ya huo upinzani nini kilitufanya tusipige hatua za maendeleo?

Haya tokea 1961 mpaka leo nchi imeongozwa na Tanu/ccm lakini eti lawama ni wapinzani. Yaani ukiwa na majitu yasiyo na akili kama wewe ndiyo furaha ya watawala, na watakutawala huku wakipeana vyeo mpaka ushike adabu huku ukisugua matako.
 
Mpaka Leo una mawazo ya mtu kuuza inchi

Karne ya 21 bado unawaza kuuzwa

Ndio maana slogan ya lowasa ilikuwa ni ELIMU ELIMU ELIMU
Yaani mkuu mpaka naona aibu... Ila ukweli ni kwamba hawa ndiyo majority huko lumumba na ndiyo wanayoifanya kazi ya akina Bashiru na Pole pole kuwa rahisi.
 
Nimesoma na kushangaa. Malengo ya ccm yametimia sasa kwanini ihangaike na walioshindwa kihalali. Meko alisema wapinzani wanachelewesha maendeleo sijui kama unalijua hilo.
Huruma hii ya ccm inatoka wapi. Pascal uwe mkweli ccm na Meko hawajawahi kuwa na busara hizo na hawatakuwa nazo.
Mkuu ukiona huyu bwana kaja na post kama hii jua kwamba huko ndani kwao linawatafuna maana hawakuwa wameangalia mbele kwenye mchakato wao wa bao la mkono... Wameanza kuona image mbaya itakayoonekana huko bungeni kwa outsiders na wadau wengine.
 
Tundu Lisu yupi? Huyu ambaye sio raia wa Tanzania? Kesha ukana uraia kwa nini abembelezwe? Hawa wapumbavu wakae huko huko ndiko size yao.

Zito Kabwe yupi? Huyo mnafiki mwenye chama cha mfukoni? Kama umeshindwa kumwelewa huyu mnafiki toka atishiwe maisha yake kule Kenya hutamwelewa kamwe.

CCM ipo imara haina haja ya upinzani Bungeni. Watanzania sio wajinga, watu ambao kila uchwao wanatusengenya tena kwa makuwadi ati ushoga ndio kitu muhimu hapa duniani. P usipotoke.

[emoji23] [emoji23] [emoji23] Anglia mbumbumbu lingine hili
 
CDM na ACT msidanganyike na kutudanganya kuwa mkikubali hiyo offer eti wakapatikane watu wa kupush ajenda ya kutaka/kuleta reforms kupitia mle bungeni, wote tunajua maamuzi ya bungeni huwa yanafikiwa kwa kupiga kura (Mara zote zikipingwa kwa ushabiki wa vyama, CCM vs vingine) Tangu kuanzishwa kwa vyama vingi tz hakuna jambo ambalo serikali ya ccm italipeka bungeni likakwama au likapita kwa sababu kulikuwa na wabunge kadhaa wa upinzani, and vice versa (yaani upinzani tz tangu kuanzishwa kwako haijawahi kushinikiza Jambo lolote ile kubwa ambalo ccm wanilipinga/hawakubalini nalo likafanikiwa kupita bungeni)..

OTHERWISE kupata nafasi kadhaaa bungeni kwa ajili ya mshahara,posho na ruzuku ndio huwa lengo lenu japo mnajificha kwenye kutetea watz kwa kutaka reforms.

Nafasi hii CDM na ACT wanayopewa kufanya maridhio wanatakiwa waitumie vizuri kutokubali kugawiwa TU vyeo kama posho kwa yaliyo fanyika kwenye uchaguzi... Hakika hapa itadhihilisha upinzani tz Ni wasaka tonge kama ccm tu.

Badala yake waandae list ya demands kushikiza ccm na serikali kuitekeleza ili kufika maridhio na muafaka wa kitaifa wenye manufaaa ya muda mrefu kwa zaidi mtu mmoja mmoja au ya chama kimoja kimoja. Pia kukomesha haya yaliyotokea kwenye uchaguzi huu..

Demand list
1- kuvunjwa kwa NEC hii mara moja, ifanyiwe reforms ya muundo kuifanya iwe huru.

2- Polisi tz, ifanyiwe mabadiriko makubwa ya kuifunga isiweze kutumika kisiasa kunufaisha chama chochote.

3- Matokeo ya Rais tz yarusiwe kupigwa mahakamani,

4- Kufanyia marekebisho katiba haraka kunguza mamlaka ya Rais kuteua majaji ili kuongeza Uhuru wa mahakama,

5- Kupanga muda wa kumalizia mchato wa katiba mpya toka pale kwa rasimu ya Warioba... NB mchakato undelea Bila kuhodhiwa na wanasiasa Kama ilivyokuwa Hadi kupelekea ukakwama,

6- Ongezeaeni au kuboeesha haya.

Kukubali kupata viti kadhaa vya hisani bungeni itakuwa ni kujisaliti kwa msimo wenu kuwa mna hubiri mabadiriko/reforms.
Hakuna kipindi kizuri Cha kushinikiza ajenda/demand za upinzani Kama hiki ambacho mmeitwa mezani kujadiri kufikia mwafaka wa maridhiano,
 
Back
Top Bottom