Bunge la Kenya laamua nchi kujitoa katika mahakama ya ICC.

Bunge la Kenya laamua nchi kujitoa katika mahakama ya ICC.

Kesho , alhamisi tarehe 5/09/2013 BUNGE LA KENYA litakutana kwa dharura kujadili uwezekano wa nchi hiyo kujitoa kuwa mwanachama wa mahakama ya kimataifa, INTERNATIONAL CRIMINAL COURT(ICC) .

Hatua hiyo ya kwenye Kenya inakuja wakati Wiki ijayo, Makamu wa Rais William Ruto anatakiwa kwenda the Hague kwenye kesi yake kutokna na vurugu zilizopeleka watu kufa katika uchaguzi wa mwaka 2007 huku Rais Uhuru Kenyatta akitakiwa kwenda kwenye kesi hiyo mwezi novemba mwaka huu.

Endapo Kenya itafanikiwa kujitoa kwenye mahakama hiyo , itakuwa ni nchi ya kwanza kufanya hivyo.
Hata hivyo wakuu wa Icc wamesema wakuu hao wa KENYA wataendelea na kesi hata kama nchi yao itajitoa kwenye mahakama hiyo iliyoanzishwa mnamo mwaka 2002.

Mwezi may mwaka huu, umoja wa Afrika(AU) uliishutumu ICC kuisakama Afrika kutokana na rangi yao madai ambayo yalikanushwa vikali na viongozi wa ICC na kudai kuwa wanapigania haki za wahanga wa Kiafrika.

Mahakama ya ICC inaundwa na nchi 121 zikiwemo 34 kutoka Afrika.
SOURCE:BBC
 
ICC ni mahakama ya kushughulikia waafrika,ni nzuri kwa sababu waafrika hatuna adabu ya uongozi.
Hata wakijitoa washitakiwe tu.
 
Hiyo ndio nchi inayoongozwa na watu wenye akili

safi sana

sio sisi tunaburuzwa tuu na wabunge wetu wa CCM na UPINZANI wote wanakubali tuuuu

Hiyo unaiita akili?
Kweli kabisaaaaa?????????
Hamia Kenya basi mkuu na we ukawe na akili.
 
Ni kama hakuna tena anayewajali hao wahanga wa hizo vurugu.

Wanaojaliwa sasa ni Uhuru na mwenzake tu.

Inasikitisha.

Halafu kuna mtu anacomment anasema hiyo ndio akili. Eti Kenya wana akili kutaaka kujitoa ICC.
Haitabadilisha udhalimu uliofanywa na hawa majangili.
 
Kesho , alhamisi tarehe 5/09/2013 BUNGE LA KENYA litakutana kwa dharura kujadili uwezekano wa nchi hiyo kujitoa kuwa mwanachama wa mahakama ya kimataifa, INTERNATIONAL CRIMINAL COURT(ICC) .

Hatua hiyo ya kwenye Kenya inakuja wakati Wiki ijayo, Makamu wa Rais William Ruto anatakiwa kwenda the Hague kwenye kesi yake kutokna na vurugu zilizopeleka watu kufa katika uchaguzi wa mwaka 2007 huku Rais Uhuru Kenyatta akitakiwa kwenda kwenye kesi hiyo mwezi novemba mwaka huu.

Endapo Kenya itafanikiwa kujitoa kwenye mahakama hiyo , itakuwa ni nchi ya kwanza kufanya hivyo.
Hata hivyo wakuu wa Icc wamesema wakuu hao wa KENYA wataendelea na kesi hata kama nchi yao itajitoa kwenye mahakama hiyo iliyoanzishwa mnamo mwaka 2002.

Mwezi may mwaka huu, umoja wa Afrika(AU) uliishutumu ICC kuisakama Afrika kutokana na rangi yao madai ambayo yalikanushwa vikali na viongozi wa ICC na kudai kuwa wanapigania haki za wahanga wa Kiafrika.

Mahakama ya ICC inaundwa na nchi 121 zikiwemo 34 kutoka Afrika.
SOURCE:BBC

.............Hatua hiyo ya kwenye Kenya inakuja wakati Wiki ijayo, Makamu wa Rais William Ruto anatakiwa kwenda the Hague kwenye kesi yake kutokna na vurugu zilizopeleka watu kufa katika uchaguzi wa mwaka 2007 huku Rais Uhuru Kenyatta akitakiwa kwenda kwenye kesi hiyo mwezi novemba mwaka huu............
 
Duh sasa nimebaini kwanini JK aka Vasco anatengwa na Uganda,Kenya na Rwanda.
 
Bunge la Kenya limeitisha kikao cha dharura kujadili kujiondoa kwa nchi hiyo kama mwanachama wa Mahakama ya kimataifa ya Uhalifu ICC.

Naibu wa Rais wa Kenya William Ruto alikuwa amepangiwa kufika mbele ya mahakama hiyo ya ICC wiki ijayo kujibu mashtaka ya uhalifu dhidi ya binadamu. Naye rais Uhuru Kenyatta anatarajiwa kufika mbele ya mahakama hiyo mwezi Novemba.
Uamuzi huu umechukuliwa kutokana na shinikizo kutoka kwa wabunge na wanachama wa chama kinachotawala cha Jubilee kutaka kuondolewa mashtaka yanayowakabili viongozi Uhuru Kenyatta na William Ruto.
Naibu wa Spika Joyce Laboso amepanga kikao hicho kufanyika Siku ya Alhamisi. Hata hivyo hata ikiwa bunge hilo litapitisha hoja hiyo, kujiondoa kama mwanachama wa ICC, ni uamuzi ambao lazima ufikishwe kwa wananchi katika kura ya maoni.

Baada ya kupita hapo ndipo itawasilishwa kwa baraza la Usalama la Umoja wa mataifa kupata idhini na kueleza sababu kamili za kutaka kuchukua hatua hiyo, pamoja na kuwa wananchi wenyewe wameamua.
Hata hivyo kwa mujibu wa sheria za mahakama hiyo ya ICC, hata kama nchi itajiondoa kama mwanachama, kesi ambazo zilikuwa tayari zimeshawasilishwa katika mahakama hiyo kuwahusu raia wa nchi hiyo, lazima zitaendelea kusikizwa hadi mwisho na hukumu kutolewa.
Kwa hiyo hata ikiwa Kenya itajiondoa sasa, viongozi wao Uhuru Kenyatta na William Ruto bado wanayo mashtaka ya kujibu mbele ya mahakama ya ICC.



lakini kesi iliyo mbele ya mahakama ya ICC kuhusu Kenyatta na Ruto iko pale pale. Si hayo tu, sasa wanataka mahakama ya Kenya iamuru eti, nasema eti wasinde kuhudhuria kwenye kesi yao Uholanzi. Wanaota mchana hawa.
 
Hiyo ndio nchi inayoongozwa na watu wenye akili

safi sana

sio sisi tunaburuzwa tuu na wabunge wetu wa CCM na UPINZANI wote wanakubali tuuuu

kuingia mkataba wa roma nchi hailazimishwi inaingia kwa hiari. na masharti ya kutoka si rahisi kihivyo....wakipeleka ombi uwezekano wa kujitoa ni baada ya mwaka baada ya ombi kupokelewa na lazima theluthi mbili ya wanachama wakubali.

Lakini kesi haziwezi kukoma kwa sababu wametenda makosa wakiwa wanachama wa ICC.

Ikiwa wanajitoa kwa sababu ya Uhuruto, wanapoteza muda, uamuzi huo hawezi kufuta kesi zinazowakabili.
 
lakini kesi iliyo mbele ya mahakama ya ICC kuhusu Kenyatta na Ruto iko pale pale. Si hayo tu, sasa wanataka mahakama ya Kenya iamuru eti, nasema eti wasinde kuhudhuria kwenye kesi yao Uholanzi. Wanaota mchana hawa.

si mchana mkuu, ni saa mbili au tatu asubuhi wakati watu tumeshaamka.

kama hawana hatia ya kuua kwa nini wanahaha hivi. Si waende tu kuthibitisha kutokuhusika kwao na mauaji?
 
Ulimpatia nani aniletee huo ujumbe we dogo? Na kwani kapatikana?

Halafu kwa nini umebadili jina?

nilikutumia humu humu siku nilipomuona, hajabadilika aisee - kama uko bongo nenda maeneo yale yale utaonana naye
 
Eti leo tena kuna shahidi mwingine tena kajitoa kwenye mojawapo ya kesi zinazowakabili hao majamaa (Uhuruto).

This is almost unheard of!

Hawajitoi kwa bure tu hawa. Ni lazima kuna witness tampering, witness intimidation, na kadhalika.

Na takeaway hapo (at least kwangu) ni kwamba hao Uhuruto look more and more guilty as charged.
 
Wakati Mhe. Ruto akijiandaa kwenda The Hague ICC kusikiliza kesi yake Wabunge wapatao 166 wameomba viza (90 WAMEPATA VIZA TAYARI) ubalozi wa Uholanzi kwenda kusindikiza Mheshimiwa wakati akihudhuria kesi yake pale ICC. Imekaaje hii wadau? ni unafiki, urafiki, uzalendo au? Gharama za kwenda huko NAULI, MALAZI nani anawajibika kuwalipia?
 
sasa hv wakijitoa mashahidi wote kuna kesi hapo?
 
Ha ha ha,,,,,,kama mlikua mmengoja kuona Kenya ikiadhibiwa,,kimataifa,,
bado mtaendelea na hizo ndoto zenu.

Hii Kesi,,,is going to nowhere,,and that is why Uhuru and Ruto decided
to cooperate with that damning ICC,,sijui nini,,unlike the president
of Sudan.

See how the number of withdrawal of witnesses,,,before the start
of this thing,,,witnesses against Uhuru were 40 something,,have now
dropped to 5.

The same with Ruto where the last one,,,,, withdrew,,just yesterday.

Angalieni sana,,enyi nyinyi ambao mnashangilia,,,msiachwe na aibu.

You are the same people,,who were expecting Kenyans to butcher each
other,,just before the last general elections.

Ndio,,leo alasiri iko mjadala katika mbunge,,,kuiondoa Kenya katika hiyo
minyororo ya ubepari.


Hiyo ni haki yetu kama vile umarekani na ndugu zao wanahaki ya kuto
kua memba wa hiyo,,ICC.

ICC is just nothing,,zero,,,do not expect us to go sleepless because of
these non sence
.

All those things,,are made up charges,,we can even select to tell the
president and deputy to ignore them and nobody can do anything
about it.

The president do not have to travel to Tanzania or anywhere,,
if things go bad,,to do what ,, buy gold or diamonds?????,,,,
wacheni,,,,,hizo zenu.

President Jomo Kenyatta never went outside this country other than
to Addis Ababa,,through out his time as president of this country.

So,,wacheni hizo vitisho hafifu na mutuwache na shida zetu.

Shughulikeni na zenu,,kama,,kuunda katiba mpya,,,kwani zenu ndizo
nyingi lakini mwaona wengine tuu.

Kama tuliweza kufanya uchanguzi na tukapita huo wakati,,,,aaaaahh
ICC is just a walk over.

I can,,once again,,,swear this,,,,,with my life.

Lakini,,,mna haki ya kuota ndoto,,vyovyote mpendavyo
lakini wembe ni ule ule kwamba,,,

Kenya iko ngangari,,,na bado,,,,,,mta shangaa na kupendaaaa
🙂:smile-big:🙂

Sisi ni,,,walewale na,,,,, hatubanduki.

So,,,ICC is just a passing glance,,,do not waste your energy on
this,,,nonsense.


 
For three years,,Syrians have been dying,,kama kunguni.

Where is that useless UN??????

Why is only Kenya and Africans.

What about Americans,,British, French,,and the rest,,
who facilitated Killings and inhumanity,,,,around the
world?????

Try to arrest an American and take him to ICC,,,,you will
see American special forces landing there and taking
him or her home,,by force???????


Then hear this useless Obama telling our people to cooperate will
that stupid ICC thing.

Wana tuchukua sisi,,kama,,,------- sana.

Thanks that the current government, in Kenya, is enjoying
massive support in the parliament and around the country that
we can easily undo what was done by Kibaki after
being mislead by Raila Odinga,,to sell Kenya to our
enemies.

We have zero political detainees,,in our country where all
those around us,,,have people in jails for going against
their governments.

Mmmmm,,,,,Kisha,,,eti,,,,mtatuambia nini????????????

If America and their brothers were god,,,China will never
be what they are,,today,,,but they are not gods,,simple
humans,,just like us.

Today's headlines,,around the world,,is about that
motion in the parliament about Kenya getting out
of ICC.

Days when Africans were nobodies is behind and
those who want to remain chained,,,,,


Shauri yenu,,,lakini sisi Kenya tutafanya tofauti
na nyinyi.

Hatutapigia watu,,,mangoti,,,eti sababu ni,,,weupe.

Waende wale huo,,,weupe wao.

Jinga sana.
 
Wakati Mhe. Ruto akijiandaa kwenda The Hague ICC kusikiliza kesi yake Wabunge wapatao 166 wameomba viza (90 WAMEPATA VIZA TAYARI) ubalozi wa Uholanzi kwenda kusindikiza Mheshimiwa wakati akihudhuria kesi yake pale ICC. Imekaaje hii wadau? ni unafiki, urafiki, uzalendo au? Gharama za kwenda huko NAULI, MALAZI nani anawajibika kuwalipia?

Hawa jamaa inaonekana kesi hii imewakalia vibaya kiasi kwamba kila mbinu inakwama. Sasa kama hata kesi yenyewe haijaanza ndiyo hivi; itakuwaje wakati wa hukumu. Sijui kama wanaelewa huu mpira wanaucheza na nani upande wa pili? Waliambiwa choices have consequences. Wabunge hawa wa Jubilee hawana maono kwa sababu wanaangalia upande mmoja tu wa Uhuruto lakini hawaangalii upande wa waathirika ambao ndiyo wapiga kura waliowapeleka bungeni ambao jamaa wakiwatumia kupindua kibao wao wabunge wa Jubilee ndiyo watapoteza kura. Uhuruto ni watu wawilitu lakini waathirika na jamaa zao pamoja na waona huruma ni mamilioni. Hawa jamaa wabunge wa Jubilee watawaingiza Uhuruto katika shimo refu la kisiasa ambalo hawataweza kujitoa. Political immaturity is at play here. Sisi yetu ni macho. Lakini wasisahau kwamba mfichaficha maradhi kilio kitamuumbua. Kule the Hague ni ushahidi wa mauaji na matukio ndiyo itaamua aina ya hukumu.
 
Duu hapo ni issue kwelikweli

Sasa hawa mabwana nd'o Ruto anashtakiwa kua aliwapanga na kuwaongoza kwa mchango wa fedha
na venginevyo. Wote hawa ni wa kabila la kwao.Kwake itakua ngumu kuchomoa pale ICC maana ushahidi
dhidi yake ulotokana kwa sana na vyombo vya dola ikiweno polisi na CID.

Afu pia kulikua na wengine wenye bunduki havi wakati wa kipindi cha hili zogo wengi wakiwa
ex-military wa tangu siku za rais Moi na kwa sasa ni raia wa kawaida.

Ruto ana kazi ngumu sana ya kuchomoa hii kitu kamanda.
 
Duh sasa nimebaini kwanini JK aka Vasco anatengwa na Uganda,Kenya na Rwanda.
Nd'o hapo sasa.

Unajua mimi nilishangaa sana kuona namna gani vipi hawa mabwana wanamchunia JK ambapo wanajua wazi
Tanzania ni asset kubwa sana ya EAC. Kisha nikaambiwa nitazame nyuma ya pazia hususan zile trip za
hawa mabwana kule Arusha na Dar.

ARUSHA.jpg


UK+1.jpg



dnuhuru2804tt.jpg
 
hawa UHURUTO wasichokijua ni kwamba mashahidi wengi walishatoroshwa kuja TZ na baada kusafirishwa kwenda ULAYA kusubiri siku ya kesi wamwage ushahidi hao mashahidi wachache wanaojitoa ni wale waliobaki Kenya tena ama unaahidiwa PESA ukileta ubishi wanakuua. Hawa jamaa ni MAFIA. tena Uganda & Rwanda wana-wa support kwa uMAFIA wao waliofanya 2007 but soon wataumbuka
 
Wabunge wa CORD wametoka nje nakuwaita wa Jubilee wezi, wanataka kujito ICC ili waendelee kuwaibia wakenya!
Wabunge wanaounga mkono kujitoa ICC wamecheza mchezo rough kama wa CCM na wabunge wa upinzani wamenasa kwenye mtego na wameamua kutoka nje kususia mjadala.

Kenya itakuwa nchi ya kwanza Duniani kujitoa kutoka Mahakama ya Kimataifa (ICC)!
 
Back
Top Bottom