Bunge laazimia Serikali inunue ndege nyingine kwa ajili ya kuhudumia viongozi

Bunge laazimia Serikali inunue ndege nyingine kwa ajili ya kuhudumia viongozi

Yaan wanunue Ndege wakati barabara ni mbovu au unamaanisha nini? Hivi kwanini wasitunge Sheria kiongozi akizingua alambwe Shaba? Unawaahidi wananchi mambo lukuki hautekelezi hata moja alafu unataka Pesa za wananchi mjinunulie Ndege kuna viongozi wanastahiri kulambwa Shaba za kichwa
Punguza Hasira dunia ya Africa ndivyo ilivyo.
 
Yaani hawa WATAWALA wetu hawashabiani na sisi kabisa,..wana dunia yao tofauti kabisa na sisi!!

Wakati sisi tunawaza UMEME wa uhakika,wao wanawaza maV8

Wakati sisi tunawaza na kuomba kuboreshewa usafiri wa barabarani na majinii kama DART na Kivuko ferry,wao wanawaza kuongeza NDEGE..dah
 
Serikali ina ndege tatu za viongozi kama tulivyoarifiwa; ndege ya Rais na ndege zingine mbili kwa ajili ya Makamu wa Rais na Waziri Mkuu.

Katika hali mbaya ya kiuchumi ambayo tunakabiliana nayo ikiwemo madeni ya Taifa, maisha magumu kwa wananchi,
Kama mtu anasema watoe pesa kwenye Vituo vya Afya Ili wanunue ndege unadhani kuna mwanasiasa ana maana kumtetea mtu wa chini? 👇
Screenshot_20240214-012543.jpg
 
Serikali ina ndege tatu za viongozi kama tulivyoarifiwa; ndege ya Rais na ndege zingine mbili kwa ajili ya Makamu wa Rais na Waziri Mkuu.

Katika hali mbaya ya kiuchumi ambayo tunakabiliana nayo ikiwemo madeni ya Taifa, maisha magumu kwa wananchi, ukosefu wa ajira kwa vijana, uhaba wa vyakula kama sukari na mafuta ya kupikia, nauli kupanda kwa sababu ya ughali wa mafuta, ukosefu wa fedha za kutosha kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi elimu ya juu, madawa na vifaa tiba hospitali za umma, pembejeo za kilimo kwa wakulima nk inakuwaje Bunge kuazimia kununua ndege mpya kwa viongozi?

Si wabunge hawa hawa kila siku wanalalamikia uduni wa huduma za jamii kwa wananchi wao? Si wabunge hawa hawa wanalilia serikali itoe fedha za maafa ya mafuriko, barabara mbovu, upungufu wa chakula na maradhi yanayowakumba wananchi.

Ina maana shida zote hizi wabunge wamezisahau mara hii?

Inashangaza Bunge kupitisha azimio la kununua ndege ya viongozi wakihesabiwa Rais wa Zanzibar na Makamu wake wawili, ina maana Serikali ya Zanzibar haiwezi kununua ndege kwa ajili ya viongozi wake? Ina maana hata magari ya viongozi wa Zanzibar yananunuliwa na Serikali ya Tanganyika? Mapato ya serikali ya Zanzibar ni kwa ajili ya nini kama hayawezi kuhudumia viongozi wake.

Napata wasiwasi huenda hata mishahara ya viongozi wa Zanzibar inalipwa na Serikali ya Tanganyika. Huu ni unyonyaji hauwezi kuvumilika hata kidogo! Yaani kwa Wazanzibari chao ni chao lakini chetu Watanganyika ni chao pia Wazanzibari! Huu si uungwana hata kidogo.

Hakika serikali tatu ni muhimu hivyo katiba mpya ni sasa!

Haikande Hichilema aliuza hata hIyo moja iliyokuwa imenunuliwa na watangulizi wake.

Kwetu, kazi iendelee; vipaumbele hamna!

Tutakapo wafurusha madarakani tutapiga mnada majumba hadi magari wanayopeana.
 
Piga kura ya kuwaondoa wahuni. Pigania kipatikane chama kipya cha kuwatetea Wananchi.


Huoni kwamba wakati umefika kwa wananchi kujitetea mwenyewe? Huyu Mwananchi amekua akitetewa enzi na enzi, hakuna matokeo chanya.


“Aliebebwa mgongoni haujui urefu wa safari.
 
Hapa inabidi tuwapongeze wawakilishi wetu,tabu waliokuwa wanapata Viongozi wetu kwa kuwa na ndege chache siyo jambo zuri.Zinunuliwe hata tatu za Kuanzia alafu zingine mwakani ili Viongozi waweze kutuhudimia vizuri.


Nakuunga mkono.

Ikiwezekana kila jimbo nchi nzima lipate ndege yake na kila Wizara nao wapate za kwao.
 
Waafrika tuna matatizo lakini Watanzania tuna matatizo makubwa sana

Nchi zinazotuletea misaada husikii mambo ya kipuuzi namna hii.
Katika nchi hizo, Waziri anapewa 'credit card' ya kampuni kutumia kwa ticket na accommodation

Majuzi viongozi wa Bunge hili wamepitisha sheria ya kulipa 'watu wanaopendana' kwa kisingizio cha Wenza.
Kwamba hata wakiacha utumishi 'Wenza ' wanaendelea kulipwa. Wakifariki tayari wana 'insurance' ya familia zao

Wakati hayo yakiendelea kuna Walimu, Wauguzi, madktari, wahasibu, Wahandisi wastaafu hawajapata hata kikotoo cha kuanzia maisha. Kuna Polisi anasema miaka 30 ya utumishi amepewa milioni 18 yaani mshahara wa mwezi mmoja wa hao Wabunge wanaotunga sheria.

Tunaomba Bunge lipitishe haya
Bunge la JMT lipiisha sheria ya kuhakikisha kila mzazi anapewa kitanda na godoro kabla ya kujifungua
Bunge Lipitishe sheria ya kununua magari yatakayopeleka mishahara kwa Walimu vijijini
Bunge linunue 'Coaster' za kuharakisha mabwana shamba kufika mashambani haraka
Bunge lipitishe sheria Wahasibu wote wapewe magari maalumu kwa kusafirisha pesa na 'cheki'
Bunge lihakikishe kila Mwalimu ana Noah ili kuwahi darasani.
Bunge lipitishe sheria ya kila jimbo kuwa na Helicopter ya Wagonjwa

Mwisho, Wananchi wajilaumu kwasababu Katiba hii ndiyo inawapa uwezo wa kufanya upuuzi tunaouona

Kama wewe ni mwananchi na unasema siasa haikuhusu, Katiba mpya haikuhusu ni vema lakini gharama za hizo ndege zinakuhusu 100%

Afrika ina umasikini wa Viongozi si rasilimali.

JokaKuu Pascal Mayalla


Huwezi kuwalaumu viongozi kana kwamba wameshushwa kutoka mawinguni.

Viongozi wetu wanaakisi uhalisia wa sisi wananchi na aina ya maisha tuliyoyachagua.
 
Waafrika tuna matatizo lakini Watanzania tuna matatizo makubwa sana

Nchi zinazotuletea misaada husikii mambo ya kipuuzi namna hii.
Katika nchi hizo, Waziri anapewa 'credit card' ya kampuni kutumia kwa ticket na accommodation

Majuzi viongozi wa Bunge hili wamepitisha sheria ya kulipa 'watu wanaopendana' kwa kisingizio cha Wenza.
Kwamba hata wakiacha utumishi 'Wenza ' wanaendelea kulipwa. Wakifariki tayari wana 'insurance' ya familia zao

Wakati hayo yakiendelea kuna Walimu, Wauguzi, madktari, wahasibu, Wahandisi wastaafu hawajapata hata kikotoo cha kuanzia maisha. Kuna Polisi anasema miaka 30 ya utumishi amepewa milioni 18 yaani mshahara wa mwezi mmoja wa hao Wabunge wanaotunga sheria.

Tunaomba Bunge lipitishe haya
Bunge la JMT lipiisha sheria ya kuhakikisha kila mzazi anapewa kitanda na godoro kabla ya kujifungua
Bunge Lipitishe sheria ya kununua magari yatakayopeleka mishahara kwa Walimu vijijini
Bunge linunue 'Coaster' za kuharakisha mabwana shamba kufika mashambani haraka
Bunge lipitishe sheria Wahasibu wote wapewe magari maalumu kwa kusafirisha pesa na 'cheki'
Bunge lihakikishe kila Mwalimu ana Noah ili kuwahi darasani.
Bunge lipitishe sheria ya kila jimbo kuwa na Helicopter ya Wagonjwa

Mwisho, Wananchi wajilaumu kwasababu Katiba hii ndiyo inawapa uwezo wa kufanya upuuzi tunaouona

Kama wewe ni mwananchi na unasema siasa haikuhusu, Katiba mpya haikuhusu ni vema lakini gharama za hizo ndege zinakuhusu 100%

Afrika ina umasikini wa Viongozi si rasilimali.

JokaKuu Pascal Mayalla
Yaani unashindwa hata kuendana na mada
Hii inaonyesha wewe kweli ni mhenga aliyepitwa na wakati
Yaani unakuja kuliomba bunge ndani JF 😳
Hebu tufatilie wa kileo tunavyoipelemba mada, na inaenda kwa mtiririko unaotakiwa
Sio kutoa nasaha za kizeezee kama malenga
At least hujatumbikizia kuhusu Muungano, ambao unakusosesha usingizi.
 
Huoni kwamba wakati umefika kwa wananchi kujitetea mwenyewe? Huyu Mwananchi amekua akitetewa enzi na enzi, hakuna matokeo chanya.


“Aliebebwa mgongoni haujui urefu wa safari.

Mwananchi mwenyewe bado hajapewa elimu ya kutosha hajui tatizo lake kubwa ni nini, hana biashara, kazi, mlo mmoja kwa siku, ana watoto saba.

Inabidi kumsaidia asimame. Baada ya hapo atajitetea mwenyewe.
 
Back
Top Bottom