Bunge na ubinafsishaji wa Bandari ya Dar es Salaam, huu ni ufisadi mkubwa

Bunge na ubinafsishaji wa Bandari ya Dar es Salaam, huu ni ufisadi mkubwa

Serikali yetu imejaa wezi na wapigaji wa kila aina pale Bandari. Kama suala la NBC lilikuja na majibu tofauti na matarajio yetu sio kigezo cha kuwanyima hawa jamaa wa Dubai wakaendesha bandari yetu.

Huko USA bandari nyingi tu zinaendeshwa na makampuni ya kukodisha, sisi tuna kipi chenye kuwazidi hao wamarekani kiuchumi na katika suala zima la tija itakayopatikana hapo bandarini?.

Kama mleta mada hatumiwi bila ya kujijua basi hana uwezo wa kutazama hasara tunayopata kama Taifa kwa bandari kuendelea kuendeshwa na kundi la wapigaji.

Maana uhalisia ni kwamba wapigaji huwa wanabadilishwa kadri ya awamu mpya ya uongozi inapoingia madarakani, madudu ni yale yale ya miaka yote.
Unalinganisha nchi ya wanaojielewa na Tanzania huku ambako wizo na ufisadi ukitokea adhavu yake ni kuitwa stupid? US wanafanya hayo kwa kuwa wapo vizuri kila eneo na sheria zao ni ngumu kwa mtu kuhujumu au kuiba
 
Marehemu JPM alikuja na mkwara wa kuweka kamera pale bandarini na kutangaza makontena zaidi ya elfu moja yaliyopiita bila ya kulipiwa ushuru, hakuna kipya cha maana alichoweza kukibadilisha mpaka anaaga dunia.

SSH ameona utumbo wetu wa uendeshaji na hivyo ni maamuzi sahihi kuja kivingine kuliko kujitetea kwa kete ya uzalendo wakati tija hailingani na rasilimali iliyopo.
Utumbo wa uendeshaji? Mbona walisema sasa hivi kipindi Cha mama bandari Ina ufanisi wa Hali ya juu sana na mapato yameongezeka sana
 
Sisi Watanzania hatuwezi kujisimamia wenyewe ni WEZI, WABINAFSI, ROHO MBAYA na TUNAPENDA MILOLONGO MIREFU BILA SABABU.

Dunia ya sasa inakwenda spidi sana na bandari ni sehemu muhimu sana ya kuharakisha maendeleo, sasa sisi tunafikiria kujinufaisha binafsi.

Mimi naunga mkono wazo la Serikali la kubinafsisha bandari.
Ikibinafsishwa ndio kila kitu kitakua poa? Mashirika mengi tuliyobinafsisha hakuna lililofanya vizuri zaidi yalianza kufa
 

Attachments

  • D74A33FD-0D93-440C-BD08-6A78EA897608.jpeg
    D74A33FD-0D93-440C-BD08-6A78EA897608.jpeg
    23 KB · Views: 3
Kama Tanzania tutabinafsisha bandari wakati huu ambao imeongeza makusanyo, volume ya mizigo imeongezeka, trilioni za fedha tumekopa na zitalipwa na walipa Kodi basi tukubali Kwamba Mwenyenzi Mungu aishiye asipotuadhibu atawaadhibu watoto na wajukuu zetu Kwa kuwarejesha utumwani

TUMEUZA MIGODI NA MADINI YOTE
TUMEUZA MBUGA ZA WANYAMA
TUMEKOPA TRILIONS
TUMEUZA VISIWA
LEO TUNAUZA BANDAR

NA HAYA YOTE YANAFANYIKA BILA UWAZI WALA USHIRIKISHAJI WANANCHI

KULIKUWA NA UMUHIMU GANI MAHUFULI KUWEKEZA TRILIONS BANDARI
Nchi yangu Tanzania na chama cha mapinduzi hapa mmekosea
Una wazimu sio bure.
 
Umeandika huku umepaniki, lakin pale bandarin kwakweli Mimi naona Bora wabinafishe tu maana tumekuwa tukisikia kila siku Kuna hujuma Mara makontena yamevushwa bila Kodi, Mara mifumo ya bandari na TRA haisomani, Mara mtu kapenyeza bomba la mafuta, na hayo Mambo kila kiongozi akienda bandarini lazima atoe/aone mapungufu, serikali inapoteza hela nyingi Sana kutokana na mismanagement ya watumishi wasio waminifu. Naona muwekazaji akiingia hata zile nafas za ajira zitatolewa kwa uwazi. Na mapato yataongezeka
 
Umeandika huku umepaniki, lakin pale bandarin kwakweli Mimi naona Bora wabinafishe tu maana tumekuwa tukisikia kila siku Kuna hujuma Mara makontena yamevushwa bila Kodi, Mara mifumo ya bandari na TRA haisomani, Mara mtu kapenyeza bomba la mafuta, na hayo Mambo kila kiongozi akienda bandarini lazima atoe/aone mapungufu, serikali inapoteza hela nyingi Sana kutokana na mismanagement ya watumishi wasio waminifu. Naona muwekazaji akiingia hata zile nafas za ajira zitatolewa kwa uwazi. Na mapato yataongezeka
Hakuna shirika la umma lilibinafsisgmhwa tukafanya vizuri, zaidi ndio hufa. Kwenye migodi tuliwaps watu kwa assumptions hizo lakini hadi leo hakuna nchi ilichopata zaidi
 
Hakuna shirika la umma lilibinafsisgmhwa tukafanya vizuri, zaidi ndio hufa. Kwenye migodi tuliwaps watu kwa assumptions hizo lakini hadi leo hakuna nchi ilichopata zaidi
Nitajie shirika moja wapo ambalo lilibinafishwa na wageni likafa....Kuna viwanda kibao vimekufa kwasabu ya uhujum, sahz ishu za ajira isingekuwa shida..hebu angalia operation za private sector zilivyo strong chukulia mfano wa mitandao ya simu ndo utajua
 
Nitajie shirika moja wapo ambalo lilibinafishwa na wageni likafa....Kuna viwanda kibao vimekufa kwasabu ya uhujum, sahz ishu za ajira isingekuwa shida..hebu angalia operation za private sector zilivyo strong chukulia mfano wa mitandao ya simu ndo utajua
ATCL, TTCL et al
 
Nitajie shirika moja wapo ambalo lilibinafishwa na wageni likafa....Kuna viwanda kibao vimekufa kwasabu ya uhujum, sahz ishu za ajira isingekuwa shida..hebu angalia operation za private sector zilivyo strong chukulia mfano wa mitandao ya simu ndo utajua
Umesema viwanda vilibinafsishwa vikafa, alafu hapo hapo unaniambia nikutajie shirika lililobinafsishwa likafa?

Tulibinafsisha trc, unajua kilichotokea?
Tulibinafsisha atcl unajua kilichotokea?
Tanesco tuliwapa wale wasouth Africa, nini kilitokea?
TTCL tuliwapa wale waholanzi, nadhani unakumbuka kilichotokea
UDA?
THB?
Hapo kweyewe TPA, tuliwapa ticts kuendesha hizo ghati je ufanisi uliongezeka? Mapato? Ikawaje tena tukaona bora hizo operations zirudi kuwa chini ya tpa?
 
Waarabu skills walizo nazo kuuza na kununua sasa hii ya kuendesha mitambo sidhani kama wanayo wao wenyewe kampuni zao zinaendeshwa na wataalamu wa kichina,wazungu.Hapo usikute ni TICS Huyo kwa mlango wa nyuma
 
Umesema viwanda vilibinafsishwa vikafa, alafu hapo hapo unaniambia nikutajie shirika lililobinafsishwa likafa?

Tulibinafsisha trc, unajua kilichotokea?
Tulibinafsisha atcl unajua kilichotokea?
Tanesco tuliwapa wale wasouth Africa, nini kilitokea?
TTCL tuliwapa wale waholanzi, nadhani unakumbuka kilichotokea
UDA?
THB?
Hapo kweyewe TPA, tuliwapa ticts kuendesha hizo ghati je ufanisi uliongezeka? Mapato? Ikawaje tena tukaona bora hizo operations zirudi kuwa chini ya tpa?
Hayo mashirika sahz yapo chini yetu Nini kinaendelea....Yale matangazo ya posta na simu yalipotea baada ya kutoka muwekazaji
 
Huu mkataba utakuja vunjwa huko mbeleni na mmojwapo wa watawala.
 
Kama Tanzania tutabinafsisha bandari wakati huu ambao imeongeza makusanyo, volume ya mizigo imeongezeka, trilioni za fedha tumekopa na zitalipwa na walipa Kodi basi tukubali Kwamba Mwenyenzi Mungu aishiye asipotuadhibu atawaadhibu watoto na wajukuu zetu Kwa kuwarejesha utumwani

TUMEUZA MIGODI NA MADINI YOTE
TUMEUZA MBUGA ZA WANYAMA
TUMEKOPA TRILIONS
TUMEUZA VISIWA
LEO TUNAUZA BANDAR

NA HAYA YOTE YANAFANYIKA BILA UWAZI WALA USHIRIKISHAJI WANANCHI

KULIKUWA NA UMUHIMU GANI MAHUFULI KUWEKEZA TRILIONS BANDARI
Nchi yangu Tanzania na chama cha mapinduzi hapa mmekosea
Ni nani ameshauri jambo la ajabu kama hili?!
Twafa, masikini Tanzania.
 
Kwani watanzania hatuwezi kuendesha taasisi zetu hadi tumpe mwarabu, baada ya hapo tumpe na shirika la ndege halafu sisi tukae kijiweni kunywa gahawa na kashata, siyo?
Umasikini upo katika hali mbili, wa fikra na ule mali.
Mbaya zaidi ni ule wa fikra kwa kuwa unapoteza hata Ile mali ndogo iliyokuwepo.
Wahenga walisema, "Cha mlevi huliwa na mgema."
Kuna tatizo kubwa la tafsiri ya maendeleo katika nchi yetu. Kwa mfano tukiwapa wachina kandarasi ya kujenga barababa, tunaita maendeleo, ambapo ukweli tumeendeleza wachina sisi tukirudi nyuma.
 
Bunge letu ni taasisi na muhimili wa kidola usiopaswa kuegemea mihimili mingine ya kidola katika taifa.

Kwa nini Bunge la JMT lielekezwe kubariki badala ya kusimamia (dhibiti) na kutoa mwongozo (rule of procedure) kuhusu namna ya serikali kuingia mikataba kama huu wa TPA?

Wadau tunaamini Bunge halipaswi kuwa reduced to that level of a government department endorsing the latter's contracts deals already entered by parties.

We would rather have seen the parliament pushing for disclosure of the said contracts, not the contrary.

Kama mkataba haupo Bungeni/hadharani, Bunge linaridhia nini?

Pili, ni jambo la kushangaza kuona Tanzania inaendelea kuwa taifa lisilojifunza. Kama ilivyokuwa wakati wa ghiliba za ABSA kurubuni serikali (na watanzania kwa ujumla) kisha kupewa NBC (1997) bure, mtindo huu umejirudia miaka 26 baadaye, ukitumiwa na Falme (Emirate) ya Dubai ikishirikiana na Kampuni ya DP World (DPW) kuchukua mamlaka ya Bandari ya Tanzania (TPA) kwa njia ya kuingia Hati ya Makubaliano (Memorandum of Understanding/MoU).

Tujuavyo sisi, ni kwa njia hii ya MoU, kama ilivyokuwa kwa NBC, TPA inaondoka pasipo waarabu hawa kulipa hata senti moja.

Wengi wa watanzania waliolilia NBC, wakiongozwa na Mwl. Nyerere, wamekwishafariki, TPA italiliwa na nani yarabi?

Ushauri kwa Wabunge Utaalam na teknolojia ni variables zinazonunuliwa sokoni. Core economic value ya TPA ni proximity ya nchi (geoeconomic advantage) katika bahari ya Hindi na maziwa Makuu ya Afrika. Hiyo advantage ndio inaitofautisha Tanzania na nchi nyingine. Tukiisha kuipoteza thamani hii we are worthless.

Option bora ya kuimarisha ufanisi TPA inatakiwa kwanza, kubadirisha management recruitment approach ili key management positions zote zijazwe kwa kuzingatia vigezo vya umahiri na matokeo ya ushindani katika soko la kazi, bila kujali iwapo mtendaji mkuu na team yake ya menejimenti ni raia wa watanzania au wageni, provided wameshindana na kudhihirisha mahiri wa kusimamia uendeshaji wa kazi za TPA.

Pili, mfumo na muundo wa TPA uwekwe bayana kuwa CEO na team yake wawe na mamlaka ya kupendekeza, kwa mujibu wa sheria ya manunuzi, kununua na kutumia teknolojia na vifaa (machinery & equipment) vya kuendesha bandari kwa ufanisi pasipo kuingiliwa na mamlaka za serikali.

Aidha, kama serikali inaona kuna umuhimu wa kubinafsisha TPA basi iweke na kutangaza utaratibu wa kuuza hisa za TPA kwenye soko la mitaji la Dar es Salaam (DSE) - hata cross-floating of shares - ambapo serikali inaweza ku-retain 51% ya hisa, kisha 49% ya hisa za mtaji wa TPA zikawa floated through IPO.

We need transparency in the governance of our national assets, properties and resources not otherwise.
Walianza na Ngorongoro na sasa ni Bandari yetu macho.
 
Marehemu JPM alikuja na mkwara wa kuweka kamera pale bandarini na kutangaza makontena zaidi ya elfu moja yaliyopiita bila ya kulipiwa ushuru, hakuna kipya cha maana alichoweza kukibadilisha mpaka anaaga dunia.

SSH ameona utumbo wetu wa uendeshaji na hivyo ni maamuzi sahihi kuja kivingine kuliko kujitetea kwa kete ya uzalendo wakati tija hailingani na rasilimali iliyopo.
Mpaka mtakapotawaliwa na hao Waarabu ndipo mtapata akili.
 
Back
Top Bottom