Bunge Primary School, Uchafu mwingine city center unaofumbiwa macho na vigogo

Bunge Primary School, Uchafu mwingine city center unaofumbiwa macho na vigogo

Simao Latino

JF-Expert Member
Joined
Jan 11, 2025
Posts
477
Reaction score
608
Eti wakuu, kwa Karne ya sasa kuna umuhimu gani wa kuendelea kuwa na Primary Schools kama Bunge pale kati kati kabisa ya Mji?? Lengo ni nini?? Tena shule ya serikali, shule zinazofahamika kwa kuwa na wanafunzi wachafu wasio na maadili hakuna mfano.

Eneo potential la kuweka investments za maana, wewe unaweka shule ya msingi? Hata kama ilijengwa zamani, Je, bado kuna uhalali wa kuendelea kuwepo pale?

Ni mtoto yupi anayesoma primary ya Bunge ni mkazi wa eneo lile lililojaa ofisi za serikali?

Uwepo wa shule kama Bunge huleta msuguano tu wa kimaslahi kwa maana ikifika December, kila mzazi anayefanya kazi Posta, mwenye IST anataka mwanae akasome Bunge. What for.

Hata kama ni shule, basi mpeni muwekezaji binafsi atakayeweza kumaintain mazingira pamoja na usafi wa wanafunzi kama zilivyo shule zingine za private za English Medium lakini sio kuweka shule uchafu katika eneo potential kama Posta Mpya (A few kilometers from the state house)

Vp kuhusu usalama wa watoto wadogo?? Yale mazingira gani ya shule watoto wanachangamana na wababa watu wazima wanaenda kupata lunch pale. Wakibakwa je (Sexual Harassment)??

Kwa zile movements za Magari binafsi kwanza ni hatari hata kwa usalama wa wanafunzi wa Darasa la kwanza..

SHULE YA BUNGE CITY CENTER NI UCHAFU MWINGINE UNAOFUMBIWA MACHO NA VIGOGO..
 
Japo sio wengi kivile lakini Kuna watoto pale wa ocean road, Ohio,mitaa ya st Joseph n.k
Mkuu, hao ni wachache mno kuweza ku justify uwepo wa shule uchafu kama Bunge pale prime area kama Posta..

Vp kuhusu usalama wa watoto wadogo?? Yale mazingira gani ya shule watoto wanachangamana na wababa watu wazima wanaenda kupata lunch pale. Wakibakwa je (Sexual Harassment)??

Kwa zile movements za Magari kwanza ni hatari hata kwa usalama wa wanafunzi wa Darasa la kwanza..
 
Back
Top Bottom