Tuna rais hasiyejua impact ya matamko yake kwenye eneo zima la uchumi.
 
Badala ya kukopa fedha ili watoe ruzuku kwenye mafuta,ni heri matumizi ya zile fedha za tozo za miamala ya simu zisitishwe matumizi yaliyokusudiwa ( Kama bado zinatumika huko lakini) ndiyo ziende kutoa hiyo ruzuku ya mafuta.
Nasema hivyo kwa sababu tozo za miamala ya simu ni tozo zilizoletwa kufanya kazi ambazo Kodi zetu tulizokuwa tunatozwa za kawaida zilikuwa zinafanya..mfano walisema tozo ni kwa ajiri ya ujenzi wa barabara,madarasa nk, kazi ambazo zimekuwa zikifanywa na Kodi zetu za kawaida.

Basi fedha ya tozo ifanye kazi hizo za dharura Kama kuweka ruzuku kwenye mafuta badala ya kuchukua mikopo mingine..Hali ya Ukraine na urusi ikitulia Bei za mafuta zikirudi katika Hali ya kawaida,tozo zitarudi kufanya kazi yake iliyokusudiwa
 
Taifa linakosa kauli ya .mwisho yenye mamlaka.

Watu wanakaa wanajadili tu bila kufikia muafaka wa lolote.
 
jamiiforuma tuwekeeni dislikes pia kusiwe na likes and quotes only
 
Hizo tozo haziondolewi moja kwa moja...Zinaondolewa kwa muda tu mpaka hali itakapokaa sawa sawa.
 
Tumelalamikia vifurushi siku mbili tumesahau. Hata hili nalo litapita
 
Keep Watching Bunge Live

na Kazi iendelee!

Braza Pascal Mayalla tunakutofautishaje na u-sisiemu wako...

Tunatenganisha vipi mabandiko yako na ukada wa chama cha mapinduzi,, Je tutumie historia yako ya nyuma au tuzingatie lipi hasa kujua hili andiko halina ukada ndani yake na hili lina ukada ndani yake....!! Ni wakati gani unafanya kazi za kichama na wakati gani unakuwa kitaifa...

Nauliza kwa vile 93% ya wana sisiemu wao huwa wanasifia almost everything cha mwenyekiti...Mna njaa NDIO, Mmekula NDIO, tunafuta tozo NDIO, tunarudisha tozo NDIO, tunafuta Bunge Live NDIO, tunarudisha Live NDIO...

Hii ni nje ya mada kidogo....
 

Kuitetea idara ni misimamo yako kama hii kuhakikisha CCM, hata ikifanya makosa unaitetea.
 
Mkuu Nas Jr , kwanza nakiri, the dividing line btn Pasco Kada wa Chama cha Mapinduzi, CCM, na Pasco Mzalendo wa kweli wa taifa hili, is very thin.
Tumia tuu kipimo cha objectivity kupima kama utetezi wangu ni wa kikada au kizalendo.
P
 
Mbunge wa Geita vijijini Msukuma asema mafuta yaliyopanda yalinunuliwa mwezi wa February 2022 kwa bei ya chini na yamepanda yakiwa ndani ya meli.

Hii ni harufu ya ufisadi ambayo inahitaji kuchunguzwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nilichojifunza hapa kuna watu wana elimu ya kawaida sana lakini michango yao ktk taifa ni zaidi ya maprofesa. Msukuma yuko vizuri ktk michango isiyohusisha ushindani wa siasa.
 
Japo huku Unguja tunapeta nilitaka kujua huko bara tozo 22 zilizopo kila unaponunua Lita 1 ya mafuta (petrol, diesel, kerosene) Tanzania bara ni zipi? Binafsi najua Ile "Road fund" tu. Karibuni Zanzibar.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…