Kuna mtu @sunk ameniita Monkey kwa kupinga ongezeko la hii bei.

Sasa namuuliza kama hao wabunge nao ni monkeys?
 
Tuliambiwa tuna zaidi ya sijui lita ngapi huko na kiparangoto; matumizi ya mafuta kwa nchi nzima kwa siku ni kiasi gani ili tu-kalikuleti kuona kama kweli bei mpya inapaswa kuanza!

Pili, kile kilichokuwa kinaifanya bei ya mafuta kwa TZ iwe juu kuliko nchi karibia zote ziliyoizunguka ni nini? Kwanini wasianze na hiyo kwanza?

Tatu, wale waTz wachache walioifadhili movie ya Royo Tua, kwanini wasishawishiwe kuleta shehena yao kizalendo kabisa kuisaidia nchi?

Nne, zile tozo zimefikia wapi? Zinafanya nini? Madarasa 15,000 bado hayajakamilika? Kule kwa Nape kuna shule ya udongo, inatisha, hawajaiona? Tozo za simu ziende ku-subsdize huko.

Tano, hii biashara ya mafuta hawamo?

Sita, Jambo letu ni lini na kwa kiasi gani? Tumeshaona wenzetu walivyofanya, sisi je?
 
Labda atachaguliwa na mumeo
Hata ukinidhihaki ila ukweli ni kwamba uchaguzi wa mwaka 2025, umeshaisha tunakwenda kuchaguwa wabunge tu.

Wenye akili timamu wote wanalijuwa hili hakuna mwenyewe jeuri ya kumuondowa sitting president huku vyombo vyote vya ulinzi na usalama viko chini yake na vinamtii.

 
Baki na mawazo yako ya kijinga, wenye nchi ni wananchi wakiamua hana la kufanya
 
Hoja ya msingi aliyoitoa huyo Mbunge, ni kuwa ni kwanini Serikali yetu inaendelea kuweka makodi kibao kwenye mafuta hayo ya Petroli

Mbona nchi za wenzetu, ikiwemo Kenya imeshachukua hatua za dharura, ikiwemo ku-subsidize bei za mafuta
 
Watunga sera ndiyo hao hao wafanyabiashara wakubwa wa mafuta
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…