Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
-
- #21
NJIA PANDA ZA KUZIMU - 3
Siku ninayopata taarifa hiyo ndipo ikawa pia siku yangu ya mwisho kuwa katika nyumba ile nikarejea kule kambini.
Sikujua nini kilikuwa kinaendelea huku lakini kumbe kuna jambo moja baya sana lilikuwa linaendelea chinichini.
Kwanza nilimkuta yule msanii kule akiwa anateseka sana, niliogopa kumtazama machoni kwa sababu nilishiriki kumfikisha hapo.
Ukiachana na hili, jambo ambalo lilinishangaza na kisha kuniweka katika wakati mgumu zaidi katika maisha ya huko. Ni suala la Malkia na Adella kugombana, kisa kikuu ni baada ya malikia kusikia kuwa Adella ameshika mimba.
Vilikuwa ni vita baridi ambavyo vilikuwa vinanisubiri nifike ili viwake rasmi.
Wote walikuwa wamejipanga, wanasema kuwa wapiganapo mafahari ziumiazo nyika.
Niligeuka nyika katika hili.
Wa kwanza kuzungumza na mimi alikuwa ni Adella punde tu baada ya kurejea, alinieleza kuwa kuna vita inaibuka hivyo nijiandae lengo lake ni kunitorosha ilimradi tu nitoweke wakose wote.
‘’mkose wote, unamaanisha nini’’ nilimuuliza.
‘’malikia anakuhitaji na mimi nakupenda martin, malikia anataka kukupeleka njia panda ya kuzimu na mimi sihitaji uende huko..’’
‘’Mamaa weee njia panda ya kuzimu ni wapi kwani, Adella nisaidie nisaidie sitaki kwenda huko…’’ nilimsihi wakati hata sijapajua njia panda ya kuzimu.
Alipotaka kunieleza mara upepo ulivuma akanyamaza kimya.
Upepo ulipopita akanieleza kuwa malikia amejipitisha pale ili aweze kusikia ni kitu gani walikuwa wanazungumza.
Ile adella anataka kuendelea kuzungumza tena, mara wakafika watu watatu na kunieleza kuwa nilikuwa ninaitwa na malikia, hawakuwa na subira wakanivuta na kunipeleka nilipohitaji. Wakanisukuma ndani nikajikuta mbele yangu nikitrazamana na yule mwanamke anayeitwa malikia.
‘’acha kuwa mpumbavu kijana, yule binti anataka akupeleke njia panda ya kuzimu, epuka tamaa za muda mfupi ukiingia huko hautoki. Lengo langu nataka uishi vizuri hapa.. maana huko njia panda ya kuzimu, utakatwa ulimi nab ado utalazimishwa kuongea, utatobolewa macho yako na utalazimishwa kutambua rangi, hautapewa chakula nab ado utalazimishwa kufanya kazi. Ikiwa upo tayari muendekeze yule binti na hapatakuwa na muda wa kujuta’’ alimaliza kisha akanisukuma nikajikuta nipo nje.
Nilikuwa nimechanganyikiwa vibaya sana jamani, hasahasa maneno ya malkia yalinifanya nipagawe maradufu.
Kutobolewa macho, kukatwa ulimi…. Ama kweli hapo ndo palikuwa njia panda ya kuzimu…..
Sikujua ni kitu gani nifanye kwa wakati ule…..
Nikiwa bado palepale chini nilianza kuusikia mwili wangu ukiwa mzito na giza likaanza kutanda, wakati nazidiwa na usingizi ule niliwaona watu wawili wakiwa na ghadhabu kuu wakinikaribia, upandfe mmoja alikuwa ni malikia na upande mwingine akiwa ni adella.
Waliponifikia nikamwona adella akimkaripia malikia, malikia naye akamjibu adella sikuweza kusikia walichokuwa wakisema lakini kila mmoja alikuwa akijiamini nkuwa yeye ni mbabe kuliko mwenzake.
Mara wakatimua mbio na kunifikia, hapa sasa nikayasikia maneno yao machache.
‘’kama ni hivyo basi kila mmoja achukue nusu’’
Malikia akanishika miguu yote miwili na adella akanishika mikono, kila mmoja akaanza kuvuta kuelekea upande wake, walinivuta nikawa napiga makelele, lakini wao hawakujali waliendelea kunivuta, na baada ya muda kila upande ukaongeza wavutaji, hapa sasa niliipata joto ya jiwe.
Sauti haikutoka tena tumbo likawa linaniuma sana na upande wa uti wa mgongo pia.
Nikaanza kuhisi ngozi yangu ikianza kuachana, hapa sasa sauti haikutoka tena na nilikuwa naumia sana, waliendelea kuvuta hadi nikaliona tumbo langu likifunguka.
Nilitamani kusema neno lakini sikuweza kusema.
Nilitambua kuwa muda wowote ule kuwa mwili wangu unatengana nusu kwa nusu na hapo historia ya maisha yangu inafika ukomo.
Nikajaribu kupambania uhai wake katika dakika ya mwisho…. Nikajigeuza kwa nguvu sana huku nikiwasihi wasiniue.
Mara wakaniachia, na hapo nikaweza kufumbua macho yangu. Nilikuwa nipo pale chini nikigalagala huku tumbo likiniuma vibaya sana. Jasho lilikuwa linanitoka, lakini tumbo halikuwa limechanika kama nilivyoona katika maluweluwe yale.
Nilijaribu kusimama nikaanguka chini.
Nikasikia sauti ya kicheko kikali, nikageuka na kukutanisha macho yangu na malikia, nilipogeuka upande mwingine nikakutanisha macho na adella.
Kisha wote wakapotea….
Huo haukuwa mwisho bali mwanzo wa kuteseka.
Usiku mnene ulinikuta katika mtihani mwingine.
Nimesema ni usiku japokuwa sina uhakika, awali niliwaeleza kuwa huku usiku ulikuwa wa kufikia tu, akiamua malkia kuleta giza analeta, akiamua iwe mwanga analeta pia.
Nilishtuka kutoka gizani nikataka kuuliza ni nani anayenitikisa lakinmi nilishtukia nikiwa nimezibwa mdomo.
‘’nifuate Martin’’ sauti tulivu ya kike ilinisihi. Nikaitambua kuwa ilikuwa sauti ya Adella, akanivuta na kunisogeza pembeni.
‘’Martin, unatakiwa kuchukua maamuzi magumu sana ama la sivyo kuna jambo baya sana linaenda kutokea. Nilidhani ni mimi na malkia pekee tunaokuwania lakini kuna watu duniani wanakupigania urudi huko. Hii sasa ni vita, sikuangalia kwa makini sana lakini kuna mwanamke nimemuona kama anafanana na wewe sijui iwapo ni dada mama ama mama mdogo’’ alisita, sasa niliweza kuiona sura yako kwa mbali macho yalikuwa yamelizoea giza.
Maneno aliyozungumza sikuwa nikiyaelewa bayana, akanivuta karibu yake akachukua vitu fulani nisivyovitambua akavitafuna na kisha akanipaka chini ya macho yangu na kisha akanizaba kibao kikali usoni, nilitaka kupiga kelele kwa maumivu niliyopata lakini aliwahi kuniziba mdomo na hapo sasa akaniwekea mkono wake, mkono wake ukaanza kutanuka na hapo nikaiona sura ya mama yangu nikamuona Nasra yule mwanadada ambaye naweza kusema alikuwa daraja la mimi kufikia pale nilipo na pia nikamuona mwanaume fulani ambaye sikuwa namtambua sura.
‘’wote hao wanatakiwa kuuwawa mara moja kuna ambao wanafanya maombi lakini ni dhaifu katika imani, wapo wanaojaribu kwenda kwa waganga lakini bado hawajatimiza masharti ya waganga. Hawa wote ni maadui wa ufalme huu, kanuni ya ufalme huu ni kwamba tunakuleta sisi na sisi tutaamua wewe kurudi huko… sasa Martin ikiwqa ningeamua kukaa kimya basi hawa watu watatu wote wangeuwawa na siku ungeletewa miili yao hapa ili uwale nyama wasije wakaonekana tena duniani, maana bila wewe kula nyama yao watakuwa wakionekanba mara kwa mara na kuzua utata….’’ Alinizungumza kwa sauti ya chini huku akiwa amenikazia macho yake.
‘’sasa Martin ni kitu gani wahitaji zaidi nifanye ujue kuwa ninakupenda. Nimeamua kufanya jambo la hatari kama hili kwa manufaa yako lakini bado hauamini kuwa nahitaji kuwa mke wako…’’ alizungumza Adella kwa masikitiko.
‘’Adella, naomba unisaidie sana wasimuue mama yangu… mimi nitawapa chochote wanachotaka ilimradi wamuache mama yangu…’’ nilimsihi Adella.
Akacheka kidogo kisha akaniambia, ‘’hakuna wanachohitaji kwako zaidi ya roho yako, na hii sio kwamba wewe ndo unaamua la, wakiamua wanaichukua tu….. jambo la kufanya sasa Martin simama kama mwanaume, simama upigane….’’ Alinisihi huku akionekana kunitia ujasiri.
‘’mimi nipigane na malkia…’’ nilimuhoji huku nikiwa katika mshangao.
‘’kama haupo tayari kupambana basi uwe tayari kumla mama yako nyama…’’ alinijibu kwa hasira.
Jibu lile likaniingiza katika mtihani mgumu sana.
‘’sikia Martin nimemua kusimama kwenye upoande wako moja kwa moja… na wewe uwe upande wangu hasa… nahitaji ufanye jambo moja tu ili tuweze kuingia katika hii vita na kuokoa watu wasiokuwa na makosa……’’
‘’niambie lolote na nitafanya Adella niambie…’’
‘’nahitaji unywele walau mmoja tu wa malkia… utajua jinsi ya kuupata najua roho itaniuma lakini nakuruhusu kama ni kulala naye fanya hivyo lakini uje na uywele wake walau mmoja …..’’ alinieleza na hakungoja jibu, akapotelea gizani akiniacha nimeketi bila msaada wowote.
Sijui yalipita masaa ama dakika ngapi mwanga ukachukua nafasi yake, wale misukule wakaingia mashamabani wakisaidiwa na wafanyakazi wapya ambao walikuwa wakipatikana kwa kunyweshwa yale maji ambayo kwa macho yao waliona ni maji lakini ilikuwa ni damu.
Mashamba yalilimwa na kwa bahati nzuri mimi nilikuwa napewa nafasi ya kusimamia hii ilikuwa ni kwa sababu ya ukaribu wangu na malkia kimahusiano.
Siku hii nilishtuka na kumuona malkia mwenyewe akiwa anasimamia yale mashamba, nikakumbuka kuwa Adella alinieleza kuwa ninatakiwa kuupata unywele wa malikia, nilimuona jinsi alivyokuwa amejitanda kichwa chake hakuonekana nywele zake hata kidogo.
Nikasimama kutoka pale nilipokuwa na kujongea hadi alipokuwa amesimama.
‘’shkamoo mama.. malkia..’’ nilimsalimia huku nikiwa natetemeka, mwanamama yule alinigeukia na kunitazama jicho kali sana, jicho lake ni kama lilikuwa lina miale fulani ya moto.
Nilitishika sana.
‘’hiyo shkamoo hapa si mahali pake…..’’ alinijibu kwa kiburi.
Nikataka kuondoka akaniita, safari hii jicho lake halikuwa kali kama mwanzo. Alikuwa akinitazama tu na kisha kana kwamba ana umri sawa na mimi akaanza kuniomba msamahga ikiwa amezungumza vibaya.
Nikatumia fursa ile kujaribu kumlalamikia malkia kuwa hanitendei haki hata kidogo.
Mtego ukaenda sawa, akaniambia ni kweli hanitendei haki kwa sababu mimi namtesa.
Nikaduwaa, yaani hapo na hapo ninamtesa mama huyu.
Lakini sikutaka iwe mshangao wa muda mrefu nikamwambia nahitaji kuzungumza naye.
Akaniambia kuwa ataniita nyumbani kwake tutaketi na kuzungumza.
Akaendelea kusimamia shamba lile ambalo sijui lilitarajiwa kupandwa zao gani.
Nikajiweka kando kidogo hadi pale kilipovuma kimbunga cha ajabu, kimbunga kile kilivuma kuja upande wangu, nikajaribu kukikwepa kikawa kinanifukuza kwa nguvu, na kisha kikanipiga gwala nikaanguka chini, kikaendelea kuvuma huku kikininyanyua.
Kilipokuja kutulia nilikuwa ndani ya nyumba ile ya kifahari nba nilikuwa nikitazama na mwanamke mrembo wa kiarabu.
‘’karibu sana laazizi wangu…’’ sauti nyororo kabisa ilisema nami.
‘’wewe ni nani..na hapa ni wapi’’ nilihoji huku natweta kwa hofu.
‘’umehitaji kufanya mazungumzo na mimi…. Nipo hapa Martin sema nami kipenzi changu…’’ alizungumza binti yule mrembo katika maana halisi ya urembo.
Nilijisahau kabisa kuwa pale sikuwa katika dunia ya kawaida, nikajikuta nazipata zile hisia za kimatamanio kabisa ya waziwazi.
Nikajisahau kabisa kuwa nilikuwa nimeagizwa unywele wa malkia. Binti yule akanisogelea akinyata hadi akanifikia katika kochi ambalo nilikuwa nimetulizwa pale na kile kimbunga, akanishika mkono na kunivuta kuelekea nisipopajua.
Aliniingiza katika chumba kikubwa kilichokuwa na godoro kubwa sana akanisihi nilale pale. Nikatii amri yake na kujilaza pale.
‘’nahitaji kukupeleka katika dunia yap eke yako, nahitaji ukitoka hapa usimguse mwanamke mwingine bali mimi tu malkia wako’’ alizungumza kwa sauti nyororo sana iliyojaa mahaba tamanishi.
Nilipolala yeye akasogea kando na kisha akapiga makofi mawili.
Mama yangu wee….. lile godoro likaanza kubonyea na kisha taratibu likaanza kupotea na sehemu ile pakawa maji.
Kama hiyo haitoshi nilipojaribu kupiga mbizi nikahisi mguso fulani mgumu katika mbavu zangu.
Nikageuka kutazama ni kitu gani kilikuwa kimeniguza ni hapo nikakutana na domo kubwa la mamba…..
Hakuwa mmoja bali huo ukawa mwanzo wa kuwaona mamba wengi katika godoro lile la kimauzauza lililogeuka kuwa majki tena maji yenye mamba.
Nilipiga mayowe jamani, nililia sana huku nikiomba msamaha.
Nikimkwepa mamba huyu ninakutana na mamba mwingine……
Mara nikasikia kitu laini kabisa kikipenya katika mapaja yangu nikaingiza mkono na kukitoa.
Lahaula alikuwa ni nyoka mrefu mweusi.
Kitendo cha kumshika akavimba vipasa kisha akarusha kichwa chake kunifuata mimi…
Kifo nikakiona kikiwa katika mdomo wangu…..
Nyoka yule akanigonga katika mikono yangu, na hapo kimya kikatanda na matone ya damu yakaanza kuvuja kutoka katika dari pale ndani, damu ile ikawa inanimwagikia mimi.
Mamba wakaanza kunilamba kwa fuko…
Mamba ana ulimi mgumu jamani.
Hivi ni sayansi inasema kuwa mamba hawezi kutoa ulimi nje, mbona hawa mamba walikuwa wanbanilamba kwa fujo vile sasa……
Nguvu zikawa zinaniishia kadiri walivyokuwa wakinishambulia…
Kicheko cha yule malkia kiliendelea kutawala…..
UTATA…….
Kitu cha kushangaza ni kwamba licha ya wale mamba kuwa na sura za kutisha lakini nilijikuta nikifurahia namna ndimi zao zilivyokuwa zikiulamba mwili wangu, hapo awali nilikuwa nahisi kuumia lakini sasa ilikuwa ni raha ya ajabu sana. Nilitamani waendelee kunilamba vilevile, kweli wakaendelea hadi nilipofumba macho yangu.
Nilipofumba macho yangu nikawa katika ulimwengu mwingine kabisa nikiwa na yule malkia ambaye alikuwa amejiweka katika umbile la binti mrembo wa kiarabu.
Nikisema mrembo namaanisha haikuwa rahisi kumtoa kasoro, hata kile kicheko chake kikubwa kilikuwa kinasisimua bado.
Nilikuwa naye kitandani na ni yeye aliyekuwa akinilamba huku na kule.
Baadaye akaanza kuchojoa nguo zake.
Hatimaye akabaki mtupu na hapo nikaziona nywele zake jinsi zilivyomwagika mgongoni, palepale ikanijia ile kumbukumbu kuwa adell alaikuwa ameniagiza unywel wa malkia yule.
Nikatii alichotaka nifanye binti yule nikiwa katika mahaba mazito nikazifikia nywle zake na kukata kiasi cha nywele kwa kutumia meno yangu, nikaziacha mdomoni huku nikijipa tahadhari kubwa sana nisije nikazimeza.
Kweli mahaba yakachukua nafasi yake huku akinipa ahadi nzuri nzuri ambazo kwa mwenye tamaa angeweza kuingia mkenge, lakini mimi nilitaka kurejea duniani tu huku nikiwahi lisije likamkuta baya lolote mama yangu.
Baadaye akapotea yule malkia, kisha nikajikuta nipo katika kukimbizana na mamba. Nilikimbia kwa kasi hadi nikawa mbali na upeo wa wale mamba, na hapo fahamu zikanikaa sawa tena.
Nilikuwa nje ya kile chumba, nikiwa hata sijavuta pumzi zangu vizuri nikamsikia adella, alikuwa pembeni yangu na aliniuliza iwapo nilifanikiwa.
Hapo ndipo nikakumbuka kuwa niliagizwa nywele, nikakumbuka nilifanikiwa kuzihifadhi mdomoni.
Ila katika kukimbia ile dhahama ya mamba nahisi kuna kitu kilitokea.
Nilizimeza zile nywele bila kufahamu kama nilikuwa nazimeza.
Nilimueleza adella, akanieleza mara mbilimbili niseme ukweli nisimdanganye akajihangaisha bure.
Nilimsisitiza kuwa hakuna hata chembe moja ya uongo katika maelezo yangu.
Sikujua ni kitu gani alichokuwa anamaanisha dada yule.
‘’haya nikija unikaribishe usifunge mlango wako sawa…….’’ Aliniambia kauli tatanishi nikabaki kujiuliza huyu dada ana matatizo gani.
Hata kabla sijahoji zaidi akaondoka na kilichotokea baada ya dakika chache kila nikikumbuka huwa nasisimka na kusema kuwa duniani kuna vimambo vidogovidogo tu ila huko nilipokuwa ndio kuna mambo katika maana halisi ya mambo.
Nikiwa nimesimama pale mara alikuja nje usoni kwangu, ilikuwa mara ya kwanza kukutana na nzi kule lakini sikujali nikatumia mkono wangu kumpunga ili akae mbali nami, yule nzi akaondoka na kurudi tena usoni kwangu, nikampunga tena akaenda akarudi. Alikuwa anaunguruma kwa sauti iliyokuwa inanikwaza sana.
Nilipompunga kwa mara ya tatu alinigeuzia kibao nzi yule sasa akahamia upande wa masikio. Alilazimisha kupenya katika masikio yangu, nikaendelea kumpunga huku sasa hofu ikiongezeka.
Nikipunga sikio hili mara anahamia sikio la huku, nikipunga huku anakuja upende aliotoka awali.
Baadaye akatoweka zake nikajua ndio mwisho wa karaha ile, nikamngoja adell arejee nimuulize alikuwa ana maana gani aliposema kuwa akija nisiache kufungua mlango.
Nikiwa katika kuwaza vile nikamsahau yule nzi.
Hilo likawa kosa, nikashtukia ghafla katika sikio langu yule nzikapenya.
Ebwana eeh akatambaa upesi hadi kweli ngoma ya sikio huku akiendelea kuunguruma, nilikimbia jamani, usiombe kutokea na jambo kama hili. Kuingiliwa na mdudu sikioni. Hata akiwa mdogo hisia zinakuja kuwa ni mkubwa sana… mimi nilikimbia lakini sasa nikamsikia kabisa akipenya shingoni akawa anashuka chini huku akiunguruma. Niligalagala huku napiga mayowe. Nzi anazidi tu kupenya.
Ninasisimka mpaka leo nikikumbuka tukio lile, hakuna aliyekuja kunipa msaada nilikuwa mimi mwenyewe kwa asilimia zote.
Nilitapataba, hatimaye nikamsikia akitawala tumboni nzi yule.
Na baadaye akanza kupanda juu tena. Nilihisi kufa….
Safari hii hakupita sikioni bali alitokea mdomoni, upesi nikaachia mdomo akatoka.
Nikabaki nahema juu juu nisijue hata ni kitu gani hiki kimenitokea.
Nikiwa katika hali ile mara adella akafika, nilianza kumwelezea mkasa ulionikuta.
Adella akatabasamu kisha akaniambia.
‘’wewe nilikueleza kuwa uache mlango wazi ukaziba, nikaona nipitie mlango wa dharula..’’ alisema huku anatabasamu.
‘’adella… una unamaanisha nini wewe…..’’ nilimuuliza.
‘’niliingia kuchukua nywele, nilidhani umenidanganya, dah ulichukua nyingi zitatufaa sana…..’’ aliniambia. Sikutilia maanani kauli ya mwisho, nilitilia maanani kauli kuwa ni yeye alikuwa katika tumbo langu na ni yeye aliyepita sikioni kwangu.
Ilitisha sana kuamini katika tukio lile, lakiniu lilitokea na mimi ndiye mtokewa mwenyewe na hapa nafanya kukusimulia tu.
Usiombe ukakutwa na tukio kama hili.
‘’kesho tunaanza safari ya kuondoka, unatakiwa kuwa jasiri sana martin, tena jasiri sio kidogo yaani…. Kuna mambo magumu ukilemaa tu unakuwa katika mwisho mbaya. Utaishi njia panda ya kuzimu kwa mateso sana hadi kufa kwako…’’ alinieleza adella huku kwa mara ya kwanza kabisa nikiona ametawaliwa na hofu kuu.
‘’najua unawaza kuhusu yule nzi…. Hizo njia tunazitumia mara nyingi sana huku katika ulimwengu wetu.. sema mara nyingi tunaingia mwanadamu akiwa amelala, lazima tu ataacha masikio wazi lakini wale wanaolala midomo wazi tunawapenda zaidi maana ni rahisi sana kupitia mdomoni kuliko sikioni. Huwa tunaingia kwa akina mama kwa ajili ya kuzinyofoa mimba zao na kuzipachika mimba zetu feki, tunaingia kwa akina baba na kuvunja vizazi vyao….. huwa tunaingia katika namna hii martin. Ni njia hatari sana mfano mimi nilipokuwa napita mdomoni, ungesema unitafune tu basi kwisha habari yangu, na wewe pia ungekufa…. Ndo maana huwa tunaingia usiku wakiwa wamelala midomo wazi…..’’
Adella alinisimulia jambo lile kana kwamba ni jambo la kawaida sana katika maisha.
Kwangu mimi lilikuwa jambo linalosisimua na kutetemesha sana.
‘’kwa hiyo huwa mnaingia kwa yeyote mnayemtaka…..’’ nilimuuliza.
‘’mh hapana sio popote kuna watu wanazo kinga kali sana, ukimsogelea umekwisha, kwenye kinga hapa wapo ambao wametibiwa na kuwekewa kinga na mchawi ambaye anao utaalamu kupita sisi, na kuna wale wanaolindwa na Mungu…..’’
‘’hata nyie mnamjua Mungu kwani…’’ nilimuuliza nikiwa nimestaajabu.
‘’ni nani asiyemjua Mungu martin wangu, natambua kuwa haya tunayofanya sio sahihi nataka mimi na wewe twende duniani tukaombe radhi dunia na kisha tumtegemee Mungu…. Sasa hawa wanaolindwa na Mungu wapo katika madaraja tofauti, wale dhaifu kiimani huwa tunaingia bila wasiwasi, wale moto hatugusi hata nyumba yake, wale vuguvugu wasioelewa wapi pa kuegemea yaani wanategemea Mungu pamoja na waganga hawa ndo wepesi kupita wote katika kuwaingia….. maana wanaowategemea kila mmoja anategea kwa sababu hawapi imani wanayotaka….. unamtegemea Mungu na umefungwa hirizi nne….. hauna kitu wewe…’’ aliendelea kusema nami adella.
Na baadaye akaachana na mada hiyo, akanieleza kama nipo tayari kwa safari. Nikamjibu kuwa nipo tayari sana na ninamtegemea yeye kwa asilimia zote.
‘’twende kwa kutegemeana martin, usinitegemee mimi tu maana itafikia hatua hata mimi nitakutegemea wewe…’’ adella alizungumza kwa sauti ya chini iliyokuwa katika kitetemeshi cha wasiwasi….
‘’nitakuja kukushtua tuanze safari….’’ Aliniambia kisha akaondoka huku akiniachia pale chakula ambacho alikitoa katika mizunguko yake alipoagizwa duniani.
Kilikuwa chakula kizuri japokuwa kilikuwa kimepoa sana.
MWISHO???
Siku ninayopata taarifa hiyo ndipo ikawa pia siku yangu ya mwisho kuwa katika nyumba ile nikarejea kule kambini.
Sikujua nini kilikuwa kinaendelea huku lakini kumbe kuna jambo moja baya sana lilikuwa linaendelea chinichini.
Kwanza nilimkuta yule msanii kule akiwa anateseka sana, niliogopa kumtazama machoni kwa sababu nilishiriki kumfikisha hapo.
Ukiachana na hili, jambo ambalo lilinishangaza na kisha kuniweka katika wakati mgumu zaidi katika maisha ya huko. Ni suala la Malkia na Adella kugombana, kisa kikuu ni baada ya malikia kusikia kuwa Adella ameshika mimba.
Vilikuwa ni vita baridi ambavyo vilikuwa vinanisubiri nifike ili viwake rasmi.
Wote walikuwa wamejipanga, wanasema kuwa wapiganapo mafahari ziumiazo nyika.
Niligeuka nyika katika hili.
Wa kwanza kuzungumza na mimi alikuwa ni Adella punde tu baada ya kurejea, alinieleza kuwa kuna vita inaibuka hivyo nijiandae lengo lake ni kunitorosha ilimradi tu nitoweke wakose wote.
‘’mkose wote, unamaanisha nini’’ nilimuuliza.
‘’malikia anakuhitaji na mimi nakupenda martin, malikia anataka kukupeleka njia panda ya kuzimu na mimi sihitaji uende huko..’’
‘’Mamaa weee njia panda ya kuzimu ni wapi kwani, Adella nisaidie nisaidie sitaki kwenda huko…’’ nilimsihi wakati hata sijapajua njia panda ya kuzimu.
Alipotaka kunieleza mara upepo ulivuma akanyamaza kimya.
Upepo ulipopita akanieleza kuwa malikia amejipitisha pale ili aweze kusikia ni kitu gani walikuwa wanazungumza.
Ile adella anataka kuendelea kuzungumza tena, mara wakafika watu watatu na kunieleza kuwa nilikuwa ninaitwa na malikia, hawakuwa na subira wakanivuta na kunipeleka nilipohitaji. Wakanisukuma ndani nikajikuta mbele yangu nikitrazamana na yule mwanamke anayeitwa malikia.
‘’acha kuwa mpumbavu kijana, yule binti anataka akupeleke njia panda ya kuzimu, epuka tamaa za muda mfupi ukiingia huko hautoki. Lengo langu nataka uishi vizuri hapa.. maana huko njia panda ya kuzimu, utakatwa ulimi nab ado utalazimishwa kuongea, utatobolewa macho yako na utalazimishwa kutambua rangi, hautapewa chakula nab ado utalazimishwa kufanya kazi. Ikiwa upo tayari muendekeze yule binti na hapatakuwa na muda wa kujuta’’ alimaliza kisha akanisukuma nikajikuta nipo nje.
Nilikuwa nimechanganyikiwa vibaya sana jamani, hasahasa maneno ya malkia yalinifanya nipagawe maradufu.
Kutobolewa macho, kukatwa ulimi…. Ama kweli hapo ndo palikuwa njia panda ya kuzimu…..
Sikujua ni kitu gani nifanye kwa wakati ule…..
Nikiwa bado palepale chini nilianza kuusikia mwili wangu ukiwa mzito na giza likaanza kutanda, wakati nazidiwa na usingizi ule niliwaona watu wawili wakiwa na ghadhabu kuu wakinikaribia, upandfe mmoja alikuwa ni malikia na upande mwingine akiwa ni adella.
Waliponifikia nikamwona adella akimkaripia malikia, malikia naye akamjibu adella sikuweza kusikia walichokuwa wakisema lakini kila mmoja alikuwa akijiamini nkuwa yeye ni mbabe kuliko mwenzake.
Mara wakatimua mbio na kunifikia, hapa sasa nikayasikia maneno yao machache.
‘’kama ni hivyo basi kila mmoja achukue nusu’’
Malikia akanishika miguu yote miwili na adella akanishika mikono, kila mmoja akaanza kuvuta kuelekea upande wake, walinivuta nikawa napiga makelele, lakini wao hawakujali waliendelea kunivuta, na baada ya muda kila upande ukaongeza wavutaji, hapa sasa niliipata joto ya jiwe.
Sauti haikutoka tena tumbo likawa linaniuma sana na upande wa uti wa mgongo pia.
Nikaanza kuhisi ngozi yangu ikianza kuachana, hapa sasa sauti haikutoka tena na nilikuwa naumia sana, waliendelea kuvuta hadi nikaliona tumbo langu likifunguka.
Nilitamani kusema neno lakini sikuweza kusema.
Nilitambua kuwa muda wowote ule kuwa mwili wangu unatengana nusu kwa nusu na hapo historia ya maisha yangu inafika ukomo.
Nikajaribu kupambania uhai wake katika dakika ya mwisho…. Nikajigeuza kwa nguvu sana huku nikiwasihi wasiniue.
Mara wakaniachia, na hapo nikaweza kufumbua macho yangu. Nilikuwa nipo pale chini nikigalagala huku tumbo likiniuma vibaya sana. Jasho lilikuwa linanitoka, lakini tumbo halikuwa limechanika kama nilivyoona katika maluweluwe yale.
Nilijaribu kusimama nikaanguka chini.
Nikasikia sauti ya kicheko kikali, nikageuka na kukutanisha macho yangu na malikia, nilipogeuka upande mwingine nikakutanisha macho na adella.
Kisha wote wakapotea….
Huo haukuwa mwisho bali mwanzo wa kuteseka.
Usiku mnene ulinikuta katika mtihani mwingine.
Nimesema ni usiku japokuwa sina uhakika, awali niliwaeleza kuwa huku usiku ulikuwa wa kufikia tu, akiamua malkia kuleta giza analeta, akiamua iwe mwanga analeta pia.
Nilishtuka kutoka gizani nikataka kuuliza ni nani anayenitikisa lakinmi nilishtukia nikiwa nimezibwa mdomo.
‘’nifuate Martin’’ sauti tulivu ya kike ilinisihi. Nikaitambua kuwa ilikuwa sauti ya Adella, akanivuta na kunisogeza pembeni.
‘’Martin, unatakiwa kuchukua maamuzi magumu sana ama la sivyo kuna jambo baya sana linaenda kutokea. Nilidhani ni mimi na malkia pekee tunaokuwania lakini kuna watu duniani wanakupigania urudi huko. Hii sasa ni vita, sikuangalia kwa makini sana lakini kuna mwanamke nimemuona kama anafanana na wewe sijui iwapo ni dada mama ama mama mdogo’’ alisita, sasa niliweza kuiona sura yako kwa mbali macho yalikuwa yamelizoea giza.
Maneno aliyozungumza sikuwa nikiyaelewa bayana, akanivuta karibu yake akachukua vitu fulani nisivyovitambua akavitafuna na kisha akanipaka chini ya macho yangu na kisha akanizaba kibao kikali usoni, nilitaka kupiga kelele kwa maumivu niliyopata lakini aliwahi kuniziba mdomo na hapo sasa akaniwekea mkono wake, mkono wake ukaanza kutanuka na hapo nikaiona sura ya mama yangu nikamuona Nasra yule mwanadada ambaye naweza kusema alikuwa daraja la mimi kufikia pale nilipo na pia nikamuona mwanaume fulani ambaye sikuwa namtambua sura.
‘’wote hao wanatakiwa kuuwawa mara moja kuna ambao wanafanya maombi lakini ni dhaifu katika imani, wapo wanaojaribu kwenda kwa waganga lakini bado hawajatimiza masharti ya waganga. Hawa wote ni maadui wa ufalme huu, kanuni ya ufalme huu ni kwamba tunakuleta sisi na sisi tutaamua wewe kurudi huko… sasa Martin ikiwqa ningeamua kukaa kimya basi hawa watu watatu wote wangeuwawa na siku ungeletewa miili yao hapa ili uwale nyama wasije wakaonekana tena duniani, maana bila wewe kula nyama yao watakuwa wakionekanba mara kwa mara na kuzua utata….’’ Alinizungumza kwa sauti ya chini huku akiwa amenikazia macho yake.
‘’sasa Martin ni kitu gani wahitaji zaidi nifanye ujue kuwa ninakupenda. Nimeamua kufanya jambo la hatari kama hili kwa manufaa yako lakini bado hauamini kuwa nahitaji kuwa mke wako…’’ alizungumza Adella kwa masikitiko.
‘’Adella, naomba unisaidie sana wasimuue mama yangu… mimi nitawapa chochote wanachotaka ilimradi wamuache mama yangu…’’ nilimsihi Adella.
Akacheka kidogo kisha akaniambia, ‘’hakuna wanachohitaji kwako zaidi ya roho yako, na hii sio kwamba wewe ndo unaamua la, wakiamua wanaichukua tu….. jambo la kufanya sasa Martin simama kama mwanaume, simama upigane….’’ Alinisihi huku akionekana kunitia ujasiri.
‘’mimi nipigane na malkia…’’ nilimuhoji huku nikiwa katika mshangao.
‘’kama haupo tayari kupambana basi uwe tayari kumla mama yako nyama…’’ alinijibu kwa hasira.
Jibu lile likaniingiza katika mtihani mgumu sana.
‘’sikia Martin nimemua kusimama kwenye upoande wako moja kwa moja… na wewe uwe upande wangu hasa… nahitaji ufanye jambo moja tu ili tuweze kuingia katika hii vita na kuokoa watu wasiokuwa na makosa……’’
‘’niambie lolote na nitafanya Adella niambie…’’
‘’nahitaji unywele walau mmoja tu wa malkia… utajua jinsi ya kuupata najua roho itaniuma lakini nakuruhusu kama ni kulala naye fanya hivyo lakini uje na uywele wake walau mmoja …..’’ alinieleza na hakungoja jibu, akapotelea gizani akiniacha nimeketi bila msaada wowote.
Sijui yalipita masaa ama dakika ngapi mwanga ukachukua nafasi yake, wale misukule wakaingia mashamabani wakisaidiwa na wafanyakazi wapya ambao walikuwa wakipatikana kwa kunyweshwa yale maji ambayo kwa macho yao waliona ni maji lakini ilikuwa ni damu.
Mashamba yalilimwa na kwa bahati nzuri mimi nilikuwa napewa nafasi ya kusimamia hii ilikuwa ni kwa sababu ya ukaribu wangu na malkia kimahusiano.
Siku hii nilishtuka na kumuona malkia mwenyewe akiwa anasimamia yale mashamba, nikakumbuka kuwa Adella alinieleza kuwa ninatakiwa kuupata unywele wa malikia, nilimuona jinsi alivyokuwa amejitanda kichwa chake hakuonekana nywele zake hata kidogo.
Nikasimama kutoka pale nilipokuwa na kujongea hadi alipokuwa amesimama.
‘’shkamoo mama.. malkia..’’ nilimsalimia huku nikiwa natetemeka, mwanamama yule alinigeukia na kunitazama jicho kali sana, jicho lake ni kama lilikuwa lina miale fulani ya moto.
Nilitishika sana.
‘’hiyo shkamoo hapa si mahali pake…..’’ alinijibu kwa kiburi.
Nikataka kuondoka akaniita, safari hii jicho lake halikuwa kali kama mwanzo. Alikuwa akinitazama tu na kisha kana kwamba ana umri sawa na mimi akaanza kuniomba msamahga ikiwa amezungumza vibaya.
Nikatumia fursa ile kujaribu kumlalamikia malkia kuwa hanitendei haki hata kidogo.
Mtego ukaenda sawa, akaniambia ni kweli hanitendei haki kwa sababu mimi namtesa.
Nikaduwaa, yaani hapo na hapo ninamtesa mama huyu.
Lakini sikutaka iwe mshangao wa muda mrefu nikamwambia nahitaji kuzungumza naye.
Akaniambia kuwa ataniita nyumbani kwake tutaketi na kuzungumza.
Akaendelea kusimamia shamba lile ambalo sijui lilitarajiwa kupandwa zao gani.
Nikajiweka kando kidogo hadi pale kilipovuma kimbunga cha ajabu, kimbunga kile kilivuma kuja upande wangu, nikajaribu kukikwepa kikawa kinanifukuza kwa nguvu, na kisha kikanipiga gwala nikaanguka chini, kikaendelea kuvuma huku kikininyanyua.
Kilipokuja kutulia nilikuwa ndani ya nyumba ile ya kifahari nba nilikuwa nikitazama na mwanamke mrembo wa kiarabu.
‘’karibu sana laazizi wangu…’’ sauti nyororo kabisa ilisema nami.
‘’wewe ni nani..na hapa ni wapi’’ nilihoji huku natweta kwa hofu.
‘’umehitaji kufanya mazungumzo na mimi…. Nipo hapa Martin sema nami kipenzi changu…’’ alizungumza binti yule mrembo katika maana halisi ya urembo.
Nilijisahau kabisa kuwa pale sikuwa katika dunia ya kawaida, nikajikuta nazipata zile hisia za kimatamanio kabisa ya waziwazi.
Nikajisahau kabisa kuwa nilikuwa nimeagizwa unywele wa malkia. Binti yule akanisogelea akinyata hadi akanifikia katika kochi ambalo nilikuwa nimetulizwa pale na kile kimbunga, akanishika mkono na kunivuta kuelekea nisipopajua.
Aliniingiza katika chumba kikubwa kilichokuwa na godoro kubwa sana akanisihi nilale pale. Nikatii amri yake na kujilaza pale.
‘’nahitaji kukupeleka katika dunia yap eke yako, nahitaji ukitoka hapa usimguse mwanamke mwingine bali mimi tu malkia wako’’ alizungumza kwa sauti nyororo sana iliyojaa mahaba tamanishi.
Nilipolala yeye akasogea kando na kisha akapiga makofi mawili.
Mama yangu wee….. lile godoro likaanza kubonyea na kisha taratibu likaanza kupotea na sehemu ile pakawa maji.
Kama hiyo haitoshi nilipojaribu kupiga mbizi nikahisi mguso fulani mgumu katika mbavu zangu.
Nikageuka kutazama ni kitu gani kilikuwa kimeniguza ni hapo nikakutana na domo kubwa la mamba…..
Hakuwa mmoja bali huo ukawa mwanzo wa kuwaona mamba wengi katika godoro lile la kimauzauza lililogeuka kuwa majki tena maji yenye mamba.
Nilipiga mayowe jamani, nililia sana huku nikiomba msamaha.
Nikimkwepa mamba huyu ninakutana na mamba mwingine……
Mara nikasikia kitu laini kabisa kikipenya katika mapaja yangu nikaingiza mkono na kukitoa.
Lahaula alikuwa ni nyoka mrefu mweusi.
Kitendo cha kumshika akavimba vipasa kisha akarusha kichwa chake kunifuata mimi…
Kifo nikakiona kikiwa katika mdomo wangu…..
Nyoka yule akanigonga katika mikono yangu, na hapo kimya kikatanda na matone ya damu yakaanza kuvuja kutoka katika dari pale ndani, damu ile ikawa inanimwagikia mimi.
Mamba wakaanza kunilamba kwa fuko…
Mamba ana ulimi mgumu jamani.
Hivi ni sayansi inasema kuwa mamba hawezi kutoa ulimi nje, mbona hawa mamba walikuwa wanbanilamba kwa fujo vile sasa……
Nguvu zikawa zinaniishia kadiri walivyokuwa wakinishambulia…
Kicheko cha yule malkia kiliendelea kutawala…..
UTATA…….
Kitu cha kushangaza ni kwamba licha ya wale mamba kuwa na sura za kutisha lakini nilijikuta nikifurahia namna ndimi zao zilivyokuwa zikiulamba mwili wangu, hapo awali nilikuwa nahisi kuumia lakini sasa ilikuwa ni raha ya ajabu sana. Nilitamani waendelee kunilamba vilevile, kweli wakaendelea hadi nilipofumba macho yangu.
Nilipofumba macho yangu nikawa katika ulimwengu mwingine kabisa nikiwa na yule malkia ambaye alikuwa amejiweka katika umbile la binti mrembo wa kiarabu.
Nikisema mrembo namaanisha haikuwa rahisi kumtoa kasoro, hata kile kicheko chake kikubwa kilikuwa kinasisimua bado.
Nilikuwa naye kitandani na ni yeye aliyekuwa akinilamba huku na kule.
Baadaye akaanza kuchojoa nguo zake.
Hatimaye akabaki mtupu na hapo nikaziona nywele zake jinsi zilivyomwagika mgongoni, palepale ikanijia ile kumbukumbu kuwa adell alaikuwa ameniagiza unywel wa malkia yule.
Nikatii alichotaka nifanye binti yule nikiwa katika mahaba mazito nikazifikia nywle zake na kukata kiasi cha nywele kwa kutumia meno yangu, nikaziacha mdomoni huku nikijipa tahadhari kubwa sana nisije nikazimeza.
Kweli mahaba yakachukua nafasi yake huku akinipa ahadi nzuri nzuri ambazo kwa mwenye tamaa angeweza kuingia mkenge, lakini mimi nilitaka kurejea duniani tu huku nikiwahi lisije likamkuta baya lolote mama yangu.
Baadaye akapotea yule malkia, kisha nikajikuta nipo katika kukimbizana na mamba. Nilikimbia kwa kasi hadi nikawa mbali na upeo wa wale mamba, na hapo fahamu zikanikaa sawa tena.
Nilikuwa nje ya kile chumba, nikiwa hata sijavuta pumzi zangu vizuri nikamsikia adella, alikuwa pembeni yangu na aliniuliza iwapo nilifanikiwa.
Hapo ndipo nikakumbuka kuwa niliagizwa nywele, nikakumbuka nilifanikiwa kuzihifadhi mdomoni.
Ila katika kukimbia ile dhahama ya mamba nahisi kuna kitu kilitokea.
Nilizimeza zile nywele bila kufahamu kama nilikuwa nazimeza.
Nilimueleza adella, akanieleza mara mbilimbili niseme ukweli nisimdanganye akajihangaisha bure.
Nilimsisitiza kuwa hakuna hata chembe moja ya uongo katika maelezo yangu.
Sikujua ni kitu gani alichokuwa anamaanisha dada yule.
‘’haya nikija unikaribishe usifunge mlango wako sawa…….’’ Aliniambia kauli tatanishi nikabaki kujiuliza huyu dada ana matatizo gani.
Hata kabla sijahoji zaidi akaondoka na kilichotokea baada ya dakika chache kila nikikumbuka huwa nasisimka na kusema kuwa duniani kuna vimambo vidogovidogo tu ila huko nilipokuwa ndio kuna mambo katika maana halisi ya mambo.
Nikiwa nimesimama pale mara alikuja nje usoni kwangu, ilikuwa mara ya kwanza kukutana na nzi kule lakini sikujali nikatumia mkono wangu kumpunga ili akae mbali nami, yule nzi akaondoka na kurudi tena usoni kwangu, nikampunga tena akaenda akarudi. Alikuwa anaunguruma kwa sauti iliyokuwa inanikwaza sana.
Nilipompunga kwa mara ya tatu alinigeuzia kibao nzi yule sasa akahamia upande wa masikio. Alilazimisha kupenya katika masikio yangu, nikaendelea kumpunga huku sasa hofu ikiongezeka.
Nikipunga sikio hili mara anahamia sikio la huku, nikipunga huku anakuja upende aliotoka awali.
Baadaye akatoweka zake nikajua ndio mwisho wa karaha ile, nikamngoja adell arejee nimuulize alikuwa ana maana gani aliposema kuwa akija nisiache kufungua mlango.
Nikiwa katika kuwaza vile nikamsahau yule nzi.
Hilo likawa kosa, nikashtukia ghafla katika sikio langu yule nzikapenya.
Ebwana eeh akatambaa upesi hadi kweli ngoma ya sikio huku akiendelea kuunguruma, nilikimbia jamani, usiombe kutokea na jambo kama hili. Kuingiliwa na mdudu sikioni. Hata akiwa mdogo hisia zinakuja kuwa ni mkubwa sana… mimi nilikimbia lakini sasa nikamsikia kabisa akipenya shingoni akawa anashuka chini huku akiunguruma. Niligalagala huku napiga mayowe. Nzi anazidi tu kupenya.
Ninasisimka mpaka leo nikikumbuka tukio lile, hakuna aliyekuja kunipa msaada nilikuwa mimi mwenyewe kwa asilimia zote.
Nilitapataba, hatimaye nikamsikia akitawala tumboni nzi yule.
Na baadaye akanza kupanda juu tena. Nilihisi kufa….
Safari hii hakupita sikioni bali alitokea mdomoni, upesi nikaachia mdomo akatoka.
Nikabaki nahema juu juu nisijue hata ni kitu gani hiki kimenitokea.
Nikiwa katika hali ile mara adella akafika, nilianza kumwelezea mkasa ulionikuta.
Adella akatabasamu kisha akaniambia.
‘’wewe nilikueleza kuwa uache mlango wazi ukaziba, nikaona nipitie mlango wa dharula..’’ alisema huku anatabasamu.
‘’adella… una unamaanisha nini wewe…..’’ nilimuuliza.
‘’niliingia kuchukua nywele, nilidhani umenidanganya, dah ulichukua nyingi zitatufaa sana…..’’ aliniambia. Sikutilia maanani kauli ya mwisho, nilitilia maanani kauli kuwa ni yeye alikuwa katika tumbo langu na ni yeye aliyepita sikioni kwangu.
Ilitisha sana kuamini katika tukio lile, lakiniu lilitokea na mimi ndiye mtokewa mwenyewe na hapa nafanya kukusimulia tu.
Usiombe ukakutwa na tukio kama hili.
‘’kesho tunaanza safari ya kuondoka, unatakiwa kuwa jasiri sana martin, tena jasiri sio kidogo yaani…. Kuna mambo magumu ukilemaa tu unakuwa katika mwisho mbaya. Utaishi njia panda ya kuzimu kwa mateso sana hadi kufa kwako…’’ alinieleza adella huku kwa mara ya kwanza kabisa nikiona ametawaliwa na hofu kuu.
‘’najua unawaza kuhusu yule nzi…. Hizo njia tunazitumia mara nyingi sana huku katika ulimwengu wetu.. sema mara nyingi tunaingia mwanadamu akiwa amelala, lazima tu ataacha masikio wazi lakini wale wanaolala midomo wazi tunawapenda zaidi maana ni rahisi sana kupitia mdomoni kuliko sikioni. Huwa tunaingia kwa akina mama kwa ajili ya kuzinyofoa mimba zao na kuzipachika mimba zetu feki, tunaingia kwa akina baba na kuvunja vizazi vyao….. huwa tunaingia katika namna hii martin. Ni njia hatari sana mfano mimi nilipokuwa napita mdomoni, ungesema unitafune tu basi kwisha habari yangu, na wewe pia ungekufa…. Ndo maana huwa tunaingia usiku wakiwa wamelala midomo wazi…..’’
Adella alinisimulia jambo lile kana kwamba ni jambo la kawaida sana katika maisha.
Kwangu mimi lilikuwa jambo linalosisimua na kutetemesha sana.
‘’kwa hiyo huwa mnaingia kwa yeyote mnayemtaka…..’’ nilimuuliza.
‘’mh hapana sio popote kuna watu wanazo kinga kali sana, ukimsogelea umekwisha, kwenye kinga hapa wapo ambao wametibiwa na kuwekewa kinga na mchawi ambaye anao utaalamu kupita sisi, na kuna wale wanaolindwa na Mungu…..’’
‘’hata nyie mnamjua Mungu kwani…’’ nilimuuliza nikiwa nimestaajabu.
‘’ni nani asiyemjua Mungu martin wangu, natambua kuwa haya tunayofanya sio sahihi nataka mimi na wewe twende duniani tukaombe radhi dunia na kisha tumtegemee Mungu…. Sasa hawa wanaolindwa na Mungu wapo katika madaraja tofauti, wale dhaifu kiimani huwa tunaingia bila wasiwasi, wale moto hatugusi hata nyumba yake, wale vuguvugu wasioelewa wapi pa kuegemea yaani wanategemea Mungu pamoja na waganga hawa ndo wepesi kupita wote katika kuwaingia….. maana wanaowategemea kila mmoja anategea kwa sababu hawapi imani wanayotaka….. unamtegemea Mungu na umefungwa hirizi nne….. hauna kitu wewe…’’ aliendelea kusema nami adella.
Na baadaye akaachana na mada hiyo, akanieleza kama nipo tayari kwa safari. Nikamjibu kuwa nipo tayari sana na ninamtegemea yeye kwa asilimia zote.
‘’twende kwa kutegemeana martin, usinitegemee mimi tu maana itafikia hatua hata mimi nitakutegemea wewe…’’ adella alizungumza kwa sauti ya chini iliyokuwa katika kitetemeshi cha wasiwasi….
‘’nitakuja kukushtua tuanze safari….’’ Aliniambia kisha akaondoka huku akiniachia pale chakula ambacho alikitoa katika mizunguko yake alipoagizwa duniani.
Kilikuwa chakula kizuri japokuwa kilikuwa kimepoa sana.
MWISHO???