Buriani Amina Chifupa!

Buriani Amina Chifupa!

Status
Not open for further replies.
Naona mmejibu maswali yangu mawili. Moja ni hilo la kutoa heshima za mwisho, hivyo Waislamu hawana nafasi hiyo. La pili ni kuwa inawezekana mwili wa marehemu kuangaliwa na wataalamu na kufanyiwa uchunguzi (jambo ambalo haliwezekani kwa sasa kinadharia). Vipi kuhusu kufukua maiti kwa ajili ya uchunguzi, inaruhusiwa katika dini ya Kiislam?
 
Yeah,
Inaruhusiwa kabisa kwani wapo watu waliozikwa ktk makaburi ya muda kisha wakahamishiwa sehemu nyingine!..

Itakuwa ujinga mkubwa kukataa hivyo wakati kuna makaburi kibao ya waislaam yamechukuliwa ktk development na sijui hiyo mifupa imetupwa wapi!
 
Hivi, katika dini ya Kiislamu, watu wakishatalikiana bado wanabakia kuwa mume na mke?
 
Nooo!....
Labda jamaa walirudiana bila sisi kujua! kuna kila dalili ilitokea hivyo maanake ndoa kama hiyo sio lazima kuwepo na sherehe.
 
kwa hiyo bado itaendelea kuaminika kwamba cause of death ya marehemu ni malaria + kisukari au inakuwaje hapa ?
 
KadaMpnzani,
Ndio imeshatoka hiyo yaani sasa ni Udaku mtupu... Huyo Nchimbi, Mpakanjia na Zitto watakuwa na wakati mgumu sana ktk maisha yao kwa sababu kila mmoja wao atahukumiwa kuhusika ama kusababisha kifo huko mitaani. Na kibaya ni kwamba wao wenyewe watakuwa kila siku wakijiuliza swali hilo hilo kuwa kuhusika kwao kunaweza kuwa ndio sababu?..hata kama Zitto hakutembea na marehemu!
Na vigumu sana watu kuamini maneno yao 100% kwa sababu shahidi ndio kisha ondoka!...
 
Mkandara,hiyo haijatoka...ninaandika kitu ambacho kitawashtua Tanzania na kusema kile kilichomo ndani ya mawazo ya watu wengi.
 
Hivi humu katika wachangiaji wa JF hakuna madaktari wa binadamu humu? Kuna hali inayoitwa Depression, sijui tafsiri yake kwa kiswahili, hali inayomfanya muathirika kuvuruga mfumo mzima wa kemikali katika mwili wake hivyo kusababisha kupanda kwa Msukumo wa damu (BP), ambayo nayo inasababisha kupanda na kushuka bila mpangilio kwa kiwango cha sukari mwilini!... Depression inasababishwa haswa iwapo muathirika hakupata nafasi ya kutatua msongamano wa mawazo yalokuwa yanamkabili!

Kwa mtizamo wangu naona machungu ya kuvunjika ndoa yake na kunyimwa nafasi ya kujitetea/kujielezea ndiyo chanzo kikuu cha Depression, (kama hiyo ndiyo hali iliyomsibu). Hali hiyo ikimpata mtu mwenye roho ndogo na kutopata msaada wa kitaalamu kwa wakati muafaka, kila gonjwa lilokuwemo na lisokuwemo litafumka, na ndiyo maana wengine huishia kujitundika kitanzi kama sio kunywa dawa ya panya!

Katika nchi zinazokubali dubwana hili "Depression", wamefikia hatua hata ya kuwa na trained psychologists, psychitrists, na Counsellors, wenye mafunzo maalum kuwasaidia watu wenye matatizo hayo!

Kwa wenye Imani, tukumbuke; Kila mtu anazaliwa kwa siku yake, na atakufa kwa siku yake Mw'mungu alomjaalia, kwani hakuna liwezekanalo ila kwa kuwezeshwa na mwenyezi Mungu! Kifo ni kifo tu, ila sababu ya kufa ndiyo inayozua maswali na majibu mengi! Tusiwape kichwa sana hao wanaojitia madaktari wa nguvu za giza, mpaka ikafikia "kunguru kuogopa ubawa wake"! Mwenyezi Mungu ndio mjuzi wa yote, yaliyo dhahiri na yaliyojificha.

Mwenyezi Mungu Ailaze pema peponi Roho ya ndugu yetu Amina Chifupa, Yeye ametangulia, nasi tunafuatia.

Poleni wafiwa, na wote wenye uchungu katika hili, ila mwenyezi mungu anapotupatia kifo ni sawa tu anatukumbusha sote tumo safarini, na aliyemchukua kwanza ndiye aliyempenda zaidi, Kazi ya mwenyezi Mungu haina makosa, tuwe na subira, yeye ndiye hakimu mkuu!
 
mbona mnaogopa kulisema hili? Mnajidai mko mbele kutoa rambi rambi huku mnajua wazi kuwa MUUWAJI hapa ni NCHIMBI

wana JAMBO FORUMS acheni unafiki

bbc.jpg
 
Kuna taarifa kuwa waislam wamekuja juu baada ya waGALA kuingilia shunguli nzima ya kumzika Amina ambaye leo ni siku ya Pili hajazikwa. Kuna taarifa kuwa kulikuwa na mipango ya kuipeleka MAITI Dodoma kisha ikazikwe kijijini kwao

ac13.jpg


Lawama zaidi zimepelewa kwa Baba yakle Amina ambaye anaonyesha kila dalili za ku CAPITALISE msiba wa mwanae kwa ajili ya Political ambitions zake kwa kukubali kuburuzwa na mijitu ya serikali.Huyu mzee japo ni Muislam lakini ajabu ni kwamba anakubali kupelekwa pelekwa ili kuwafurahisha waGALA ambao wanaongoza huu msiba kupitia magazeti,ma TV na kadhalika
 
ndiyo sikatai lakini baada ya kuuona huu UNAFIKI nimeona bora niseme kwani hii ni nyumba yetu wote na kama kuna UNAFIKI unaendelea basi mie ntasema tuu
 
KadaMpnzani,
Ndio imeshatoka hiyo yaani sasa ni Udaku mtupu... Huyo Nchimbi, Mpakanjia na Zitto watakuwa na wakati mgumu sana ktk maisha yao kwa sababu kila mmoja wao atahukumiwa kuhusika ama kusababisha kifo huko mitaani. Na kibaya ni kwamba wao wenyewe watakuwa kila siku wakijiuliza swali hilo hilo kuwa kuhusika kwao kunaweza kuwa ndio sababu?..hata kama Zitto hakutembea na marehemu!
Na vigumu sana watu kuamini maneno yao 100% kwa sababu shahidi ndio kisha ondoka!...


Labda wangejitokeza hadharani na kukanusha maneno yaliyokuwa yamesemwa, wasingebebeshwa hii lawama. Hatuwezi kuwatenganisha na kadhia hii kwa sababu hawakutaka kujitokeza hadharani kusema ukweli ni upi. Walijua kitakachotokea na ndiyo maana wakawa wanasubiri saa tu itimie, mauti imkute halafu wajitokeze eti wanalia kwa uchungu na blah blah kibao.
 
Kuna taarifa kuwa waislam wamekuja juu baada ya waGALA kuingilia shunguli nzima ya kumzika Amina ambaye leo ni siku ya Pili hajazikwa. Kuna taarifa kuwa kulikuwa na mipango ya kuipeleka MAITI Dodoma kisha ikazikwe kijijini kwao

Lawama zaidi zimepelewa kwa Baba yakle Amina ambaye anaonyehs kila dalili za ku CAPITALISE msiba wa mwanae kwa ajili ya Political ambitions zake kwa kukubali kuburuzwa na mijitu ya serikali

alipolazwa Lugalo walimsaidia kitu gani? Yaani ameshakuwa maiti ndiyo wanataka kuingilia mipango ya familia.
 
halafu huyu alieandika hii mada kwa nini asema waislamu na siyo mzee wake amina chifupa !! plz moderator ebu angalia hili suala bana, sio akikosea mtu mmoja mnasema generalize the whole thingy, thats some sh!t now !! hata hivyo mzee chifupa hajakosea
 
halafu mtu mwenyewe aliyeandika hana hata source wala nini sijui kapata wapi hizo info
 
mbona mnaogopa kulisema hili? Mnajidai mko mbele kutoa rambi rambi huku mnajua wazi kuwa MUUWAJI hapa ni NCHIMBI

wana JAMBO FORUMS acheni unafiki
bbc.jpg


kwa hiyo na wewe ni MNAFIKI si ndio !?! haya kijana wee tukana mamba tu kabla huja..............
 
Mchongoma
Mimi sio daktari. Ila hilo la depression ondoa kabisa. Tanzania tatizo hilo lipo tena kwa wengi.....kwani watu wanaishi katika dimbwi la matatizo yasiyotatulika....lakini matokeo sio kama yaliyomkuta AC.

Mimi pia ni mhanga wa Depp miaka kama 3 iliyopita(mpaka nililazwa)....is more of psychic problem.....suicidal thoughts...likely to emerge among the alternative solutions to whatever problems.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom