Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ujamaa...
20:80 ni mgawo wa fursa.
Mimi naleta taarifa nyingi hapa si kwa nia ya kubishana na kufanya malumbano ni kutoa taarifa ambazo zimefanyiwa utafiti wa Waislam na kuziweka hadharani ili zijulikane.
Hiyo 20:80 iangalie hapo chini:
Uchaguzi 2020 - Waraka wa Uchaguzi wa Shura ya Maimamu Tanzania
Bismillahir Rahmanir Rahiim SHURA YA MAIMAMU TANZANIA WARAKA [MWONGOZO] UCHAGUZI MKUU WA TAIFA OKTOBA 2020 TANZANIA Umetolewa leo Tarehe 09. 07. 2020. UTANGULIZI Ugonjwa wa Korona – COVID-19 Sote Tunafahamu kuwa nchini mwetu na Dunia kwa ujumla kumekuwepo na taharuki kubwa ya Ugonjwa wa...www.jamiiforums.com
Ujamaa...Maelezo yangu ni marefu sana umeyasoma na kuyaelewa vizuri sana na huo ndio ukweli huenda nimekufungua kimawazo leo hii. nimeelezea mzizi wa wewe unaloona ni tatizo nisome vizuri na unipongeza kwa uchambuzi mahiri wa kukufufua kifikra. Yote hayo yanakurudisha kwene jumbe yangu tangu Lini dunia hii kukawa na 50/50 au 100/100 hilo swala halipo mkuu Mbona mambo yapo wazi na nimekuchambulia hapo juu dunia ya leo hakuna mgawanyo sawa wa fursa na rasilimali ila juhudi zako ndio zitakazokufanya ufike pale unapotaka kua. Kilimanjaro tu ina shule 319 na population yake haizi 3 million people ila dar Ina shule chache kinamba kuliko Kilimanjaro ila population yake ni more than 6 million people. Hapo bado kagera, mwanza, iringa, mbeya hata mavyuoni dar waliofurika ni wakristu. Unaweza chukua idadi ya shule private lindi, mtwara, tanga, pwani kwa pamoja ukagundua namba zao hazizidi mikoa miwili ya mbeya na bukoba hata kwa idadi ya wanafunzi pia. Mambo yapo wazi nimechambua vyema huko juu. Shura ya maimamu isiyo na wasomi itanishari nn mm niisome iwashauli nyinyi nini cha kufanya. chukua message yangu hapo juu muifanyie kazi ikiwezekana nitafuteni inbox niwape ushauri wa wapi muanzie. mapadre wote wa kanisa katoliki elimu yao ni kuanzia degree kwenda mbele hakuna padri asie msomi kwene professional ya aina yoyote nchi hii huwezi mkosa padre kwene hio professional, elimu za mashekhe walio wengi zikoje? Jibu unalo, sasa uwezo wao wa kufikili na utendaji Uwe sawa na wakina ponda kina kipozeo na wengine wengi kweli?. Sijawazarau ila hata wewe fananisha elimu, maamuzi, mfumo wa uongozi, taasisi hekina na busala za viongozi wa kanisa na hao nduguzo. Mtu hana kitu anaowa wake 3,4 hao watoto watasoma kweli angalia wanavyouza maeneo dar mengine ni potential area ufukweni mwa bahari wanaamia rufiji ikwilili mkuranga na kibiti wanaongeza na wake. Acheni masihara mzee mafanikio yanatafutwa hayaji kwa maandamano au kuyasubili au kusomeana hadithi. akina hussein Mwinyi leo hii ni maraisi wadogo zao ni mawaziri akila lizzy ni manaibu kwasababu shuke ipo kichwani afu unaibuka na 20/80 za kina ponda kutoka likoma na mchikichini. Hao sio wasomi mtu mda wote anakariri hadithi hana maarifa na elimu ya kuchambua mzizi wa tatizo afu anitupie lawama mimi msomi wa degree 3 ntakuona mjinga tu yaani lasaba unikaripie kwa maandamano. Someni.
Ujamaa...
Waislam wanajua kuwa serikali inajua.
Waislam tegemeo letu ni kuwaelimisha wananchi wote wajua tatizo linaloikabili nchi yetu.
Serikali ndiyo ya kuwapa Waislam majibu si yule ambae ananufaika na dhulma iliyopo.
Mradi wewe ushatufahamu sisi tumetosheka.
''Hawashauli,'' ''Kufikili,'' ''Ikwilili,'' ''busala...''
Ujamaa...Serikali ipi hio. Yaani serikali ijibu hoja za kina ponda kweli?. Mbona mnaizadharau serikali namna hio!!. Ukweli nimeshakwambia mzee wangu lawama hazijengi chukueni ushauri muufanyie kazi umeelimisha je umechukua hatua gani. Waislam kibao ni matajiri ila wengi wao hawajajenga mashule au mavyuo ila wanazo biashara za mabilion Kwanini msianze na hao. Nchi hii kuna watu wanashule kuzizidi jumuiya za kiislam napo serikali itoe jibu kweli. Mda huu tunaongea kuna maelfu ya matajiri wa kiislam wakisema wawekeze kwene mashule mavyuo na taasisi kubwa za afya huoni kama nchi tutapiga hatua.Eti waislam wanajua aya wamejua je juhudi zipi zimefanyika wewe mwenyewe kutwa unachapa vitabu na kuzunguka duniani umesita nini kuanza kuandika project za mshule mahospital ma vyuo na utafute wadau wakutusaidia ila kutwa vitabu vya sykes mala Nyerere mala 20:80 wapiii mzee miaka yote hujajenga hata darasa kama juhudi binafsi au mfano nini maana yake. Waendelee kujua tu namimi newajurisha pia huko mkoani Rukwa dayosisi ya mtowisa wanafungua chuo cha ufundi na afya, kesho Uwe macho TBC na hio ni Rukwa.
Yani unaleta hoja nyengine hata haina mashiko na unachoongea, so kukiwa na kijana aliacha shule inahusiana nini na tunachoongea hapa?Hawakuwa wakichanganya nyama, bucha la nguruwe liliuza nguruwe tu. Nakumbuka kulikuaa na bucha la kitimoto hapo ubungo mataa lilikiwa linauza kitimoto tu, tena kwa siku maalumu.
Kwa hali ilivyo sasa nadhani ndio muda bora zaidi wa kuvunja bar zilizotapakaa kila mahali nchi nzima zikiuza kitimoto.
Wakati ule mkivunja mabucha na kuandama mliamini Rais Mwinyi atawalinda, akawatosa, nakumbuka pia Mkapa alivyowanyoosha pale Mwembe Chai, kwa kifupi waislamu mna shida sana, nakumbuka kuna kijana tulikuwa tunasoma naye primary Liacha shule kwa ajili ya madrasa.
Huyo muisilamu anaekula kitimoto ameamua mwenyewe kwa Hiari yake, hivyo hakuna mtu atakae muingilia.Kosa lilikuwa ni la kijana aliyetumwa nyama pamoja na familia yake, alitakiwa aongozwe asiende kwenye bucha za kitimoto, bali aende kwenye bucha wanzauza nyama ya ng'ombe, maana kitimoto kilikuwa na bucha zake special.
Hiyo shida ilikuja kuwa kubwa kutoka na kukuzwa na waisalamu wenyewe,.
Na kama tatizo ni nguruwe nadhami kwa sasa hampaswi kabisa kukaa kwenye mabaa mengi, maana mabaa mengi yanauza kiyimoto, lakini ukienda utawakuta waisalmu kibao wanakunywa na wengine kula mdudu
Waisilamu walipigwa pini sana kwenye Elimu hio ni fact, huku Tanga kuna waisilamu wanaitwa John, Janeth na Majina kibao ya kikristo ni wazee sasa ilibidi wabadili majina wakati wa Nyerere ili waweze kufaulu.Serikali ipi hio. Yaani serikali ijibu hoja za kina ponda kweli?. Mbona mnaizadharau serikali namna hio!!. Ukweli nimeshakwambia mzee wangu lawama hazijengi chukueni ushauri muufanyie kazi umeelimisha je umechukua hatua gani. Waislam kibao ni matajiri ila wengi wao hawajajenga mashule au mavyuo ila wanazo biashara za mabilion Kwanini msianze na hao. Nchi hii kuna watu wanashule kuzizidi jumuiya za kiislam napo serikali itoe jibu kweli. Mda huu tunaongea kuna maelfu ya matajiri wa kiislam wakisema wawekeze kwene mashule mavyuo na taasisi kubwa za afya huoni kama nchi tutapiga hatua.Eti waislam wanajua aya wamejua je juhudi zipi zimefanyika wewe mwenyewe kutwa unachapa vitabu na kuzunguka duniani umesita nini kuanza kuandika project za mshule mahospital ma vyuo na utafute wadau wakutusaidia ila kutwa vitabu vya sykes mala Nyerere mala 20:80 wapiii mzee miaka yote hujajenga hata darasa kama juhudi binafsi au mfano nini maana yake. Waendelee kujua tu namimi newajurisha pia huko mkoani Rukwa dayosisi ya mtowisa wanafungua chuo cha ufundi na afya, kesho Uwe macho TBC na hio ni Rukwa.
Uhakika,Mbona nanusa viashiria vya upotoshaji na kupandikiza chuki fulani.... Mtu akuonee katika elimu wakati anachoona ni namba tu ya mtihani? Utatetea labda kwa shule za kiislamu tupu eeh
Umeleta taarifa isiyo na muunganiko katikati ni kwamba umelitaja tatizo, ukaruka njia, uchunguzi, majadiliano..... ukarukia kusema hitimisho kuwa ni hujuma. Kisayansi hauna mmlaka ya kutoa jibu wakati umekiri hauna data yoyote - Appeal to ignorance.
Hii sio sawa, kama umeona utumie silaha zozote kisa upo vitani kutetea imani jikumbushe kuwa midomo isemayo uongo ni chukizo kwa Mungu, msema kweli mpenzi wa Mungu. Mungu/dini gani hiyo itakayotetewa kwa uongo?
Hivi kweli hata mimi ambaye sijaunda tume kuchunguza huko kufeli kumetokanaje mbona majibu ya kuanzia[factors] baadhi yapo mfano suala la kukosekana kwa 'mchujo mkali' baadhi ya shule za kiislamu hazichuji kabisa wanafunzi wao zinaona ni ubaguzi flani na eti kufaulu ni majaaliwa tu muache aende atafaulu kwa kudra. Mwishoni ukileta wanafunzi mia wakafeli sabini utashangaa tena???? Utahitaji tume!?
Unapotengeneza mazingira ya kama mnaonewa ni kujaribu tu kujustify nanyi kuwaonea wasio na hatia baadae, bad, very bad. Haujengi. Nimeangalia muvi ya morbius nimeona madhara ya mtu kuishi katika jamii anayoamini inamuonea siku akipata nguvu anakuwa hafai kitu badala ya kuwaza kujenga anageuka mnyama. Mbaya sana.
Ujamaa...
Huenda kibri kimeziba uwezo wako wa kufikiri unashindwa kuona mabadiiko yaliyoko nchini.
Waislam walifutiwa historia yao na historia ya mashujaa wao.
Historia imeandikwa upya na inasomwa.
Waislam wanajenga shule bila kuzuiliwa na Wizara ya Elimu na BAKWATA kwa visingizio hivi au vile.
Jiulize iliwezekaneje kwa Sheikh Ilunga Kapungu kutembea nchi nzima akiwa na kibali akieleza hatari ya Mfumo Kristo?
Jiulize.
Kanisa lilikuwa kimya.
Umejiuliza kwa nini?
Waislam wa wanajua kila kitu na historia yao wanaijua na mashujaa wao wanawajua na serikali imetambua ukweli, mbivu na mbichi.
Mzee Waikela.
Nadhani unaijua historia yake.
Serikali iligharamia matibabu yake na ilikuwapo katika maziko yake.
Huyu alikuwa kiongozi wa Waislam na mpigania uhuru bega kwa bega na Julius Nyerere.
Angalia matokeo ya mitihani hakuna tena hujuma.
Shule za Kiislam zinafanya vizuri.
Baraza la Mitihani limepata somo na wametambua hatari iliyopo.
Waislam ni watu wenye subira.
Serikali imetambua tatizo lililopo.
Sisi tuko na serikali na tunaipa nafasi ya kutenda haki pasi na vurugu.
Mabango haya yalikuwapo katika maandamano ya kuipinga NECTA na hujuma zake.
Ripoti ya hujuma Waislam tunayo na iliwasilishwa serikalini.
Ndipo nakueleza kuwa wakutoa majibu si wewe kwani wewe huusiki na lolote.
Haya yalikuwa mwaka wa 2012.
Leo hakuna serikali itataka haya.
Serikali haitaki na Waislam pia hatutaki haya.
Sote tunaitakia amani na salama nchi yetu.
Huu ndiyo mchango wetu Waislam kwa nchi yetu na viongozi wetu.
View attachment 2311565View attachment 2311567View attachment 2311569
Waisilamu walipigwa pini sana kwenye Elimu hio ni fact, huku Tanga kuna waisilamu wanaitwa John, Janeth na Majina kibao ya kikristo ni wazee sasa ilibidi wabadili majina wakati wa Nyerere ili waweze kufaulu.
Institution nyingi za kiisilamu za kimataifa kama Al haramain, African Muslim na nyenginezo zilikuwa banned na kukatazwa kuleta Elimu, waliambiwa tu walete majengo ambayo Bakwata na vibaraka yao wanayageuza kuwa fremu za Biashara kila kukicha.
Hivi karibuni nchi imekuwa open taasisi nyingi za kiisilamu za kimataifa zina invest kwenye Elimu ya Tanzania, Feza na Istiqama ni mifano tosha kwa shule za kiisilamu zinazofanya Vizuri.
It doesn't matter mi nimetolea TU mfano Huku, ila zamani ni jambo la kawaida muisilamu kubadili jina ili asome, inawezekana hata hao wamebadili Kwa sababu hio hio.Mbona mbeya wakina imma, james , issa, magreth, lili wapo wengi ni waislam napo tusemaje?. Watu wanafungua taasisi nyingi tu kila kukicha sikuhizi watu kibao na taasisi kibao zinajenga mashule, vyuo sio muslim tu wapo wengi sana. Tusidanganyane hapa mifano ipo hai
Ujamaa...Mzee acha uongo. Kibri kimezidi uwezo wako wa kupokea ushauri. Who is ilunga kapungu. Nani kafuta historia, mashujaa wapi hao. Kanisa liwajibu wapumbavu wasio na elimu wala vigezo eti leo hii kadinari wa kanisa takatifu katoliki la mitume awajibu akina ilunga, ponda?? Uwezo wako wa kufikiri umepungua sana kwanza ni utomvu wa nidhamu na mmomonyoko wa maadili kutaka kanisa liwajibu wapuuzi katika jamii. Bakwata unayoisema vibaya toka zamani leo hii ndo unaona umuhimu wao kujenga mashule na kuwaendeleza nyinyi!!! tangu lini walizuiliwa kujenga mashule eti nacte wanajua kwani hakuna akina abdalllah kule, chukiiii ni donda la roho. Inferiority complex inawachanganya. Mabadiliko yamekuja baada ya jamii kufunguka na kuchukua hatua za kupeleka watoto shule sio kibinti kinafikisha miaka 16 kinaozwa wajanja kwene vitabu vya kale mfumo huo wametoka. Wala usitudanganye humu jukwaani kusoma ushindwe wewe uje uwalalamikie wenzio huwa unaongea mengi ila jipya hakuna ni upupu tu. Eti waislam!!!. Pigisheni watoto shule. Kutwa kuongea humu ila mada ni zilezile wala huna jipya.
Ujamaa...
Tofauti baina yetu ni kuwa mwenzangu umeghadhibika ilhali kila kitu unacho wewe.
Mimi ndiye nisiye na lolote lakini naeleza yangu kwa utulivu.
Ingekuwaje kama wewe ungekuwa kwenye nafasi yangu?
Bila shaka vita vingewaka.
Nimeandika historia ya wazee wangu na jamii yangu.
Historia hii sasa imehifadhika na wale waliofutwa leo wanazungumzwa hadharani kuwa walipigania uhuru wa Tanganyika.
Hii ndiyo tofauti iliyopo baina yetu.
Picha ya kwanza Azam TV ''Morning Trumpet'' 2015.
Picha ya pili kulia Bi. Chiku bint Said Kisusa, Bi. Titi Mohamed, kushoto Bi. Tatu bint Mzee na Mwalimu Nyerere ni huyo katikati akisindkizwa na akina mama hawa safari ya kwanza UNO, 1955.
View attachment 2312486View attachment 2312488
Dubai na abudhabi sio nchi ni miji iko UAETanzania ina Waislamu wa ajabu sana. Nakiri mimi ni Mkristu ila nimebahatika kutembea vya kutosha kwenye nchi za Kiislamu kama Malaysia, Indonesia, Dubai, Iran, Abu Dhabi, Sudan na Turkey.
Nakiri kuwa nimewahi kula nyama ya nguruwe kwenye hoteli za 5 Star nchini Dubai, Malaysia na Turkey. Ni aibu kwa Waislamu wa Tanzania kuanzisha vurugu sababu ya mboga.
Sasa huyu marehemu Hassan Chikusa pengine kwa kupoteza kazi NBC sababu ya ujinga wa kuvunja mabucha kunaweza kukawa kulimuathiri kwa kipato na akashindwa kulea familia yake vizuri including kiwapa elimu wanae.
Lesson Learnt:
Muislamu usile nyama ya nguruwe kwa vile ni haramu period, lakini usihangaike na Wala nguruwe na mali zao.
Upo sahihi, nimekuja kujua mwaka juzi..nikijua Dubai ni nchi, kumbe ni UAE...na Mji mkuu sio hata Dubai.Dubai na abudhabi sio nchi ni miji iko UAE
Vitu vingine ni ujinga unaumizwa bure kisa walaji wa nguruwe kama we huli si uacheDaah moyo wangu huumia sana napopata historia juu ya maonevu wanayoyapitia waislamu hapa nchini.Ndani ya Tanzania waislamu ndiyo jamii pekeee iliyoumizwa Mara nyingi zaidi huku wakiwa dhariri na hakuna wa kuwatetea.
Ujamaa...Sikupingi kuelezea historia za hao nduguzo ila habari za kuhusisha kanisa na ujinga ujinga iwe mwisho huo ni utomvu wa nidhamu na kipimo cha mmomonyoko wa maadili kutuhumu kanisa kwa maneno ya vijiwe vya likona, ndanda street,manyema pili kubali kusikiliza hoja za wenzio sio ukikabwa na hoja unakimbilia kusema mtu kaghadhabika. Jamii imebadilika sana kila mtu ni msomi sasa vizazi vipya vyote ni wasomi huko zamani jamii za wasomi ilikua ni wachaga, wahaya, wanyakyusa, kwa wingi huku jamii nyingine zikiwa nyuma kwene fursa na ajira selikalini leo ni 2022 maelfu ya watu ni wasomi toka makabila yote kila kabila lina wasomi sasa sio kama zamani. Hata jamii za kiislam zilizokua zinaoza vibinti vya miaka 15,13,16 kwa asilimia kubwa wameacha na watoto wanapelekwa shule vilevile usukumani na jamii kubwa za kikristu zilizokua zinaoza watoto kwa kubadilishana na n’gombe hali hio imepungua sana wote wanapiga shule. Hakuna hujuma za nacte wala bakwata wala ponda wala ilunga wala kanisa wala msikiti bali jamii imebadilika sana hata mashule yanaelemewa na wanafunzi huku kila mwaka maelfu ya watahiniwa wakimiminika mitaani. Piga makofi tafadhali!!!
Ninajuwa nchi ni UAE na Makao Makuu ni Abu Dhabi pamoja na Emirates zingine 6 including Dubai, Sharjah nkDubai na abudhabi sio nchi ni miji iko UAE