TANZIA Buriani Mama Tumaini Kakuyu Mlewa, Mpambanaji hodari, mwasisi wa shughuli za usafi maofisini na upambaji wa kumbi za mikutano, sherehe nk

TANZIA Buriani Mama Tumaini Kakuyu Mlewa, Mpambanaji hodari, mwasisi wa shughuli za usafi maofisini na upambaji wa kumbi za mikutano, sherehe nk

Screenshot_20210809-075207~2.png
 
Laana aliyotuachia mwendakuzimu yani tangu aondoke ndugu zetu na wapendwa wetu wanapoteza maisha sana. Its not fair at all!

JF Member
 
Ametimiza kusudi la Mungu sote ni wapangaji,kabla ujaondoka duniani,fanya kitu cha faida ukumbwe hata usipokuwepo Ili uje umkumbushe Mungu akupunguzie adhabu.
Nilijenga msikiti, kanisa,kisima,shule,daraja,nk.
 
Nimefanya kazi kwenye kampuni yake kwa zaidi ya miaka kumi, hatukuwa na mahusiano ya damu. Wala hakuwa ndugu yangu kabisa, lakini huyu Mama hakuwahi kumuacha mtu aangamie.

Mishahara haikuwa mikubwa, pia mishahara haikuwa kidogo, kampuni yake ilikuwa kioo kwa malipo mazuri kwa kampuni za usafi.
Nilianza kazi kwake nikiwa nimemaliza form four na div 4 ya point 26 mwaka 1998.

Akanishauri nijiendeleze kielimu, nikamwambia Mimi nasomesha wadogo zangu.

Akanipeleka Mwenge Mzumbe QT, kwa gharama zake nikarisiti na kupata div 2.

Kwangu ilikuwa nu furaha kubwa na huzuni pia, nikijiuliza wadogo zangu wawili watasomaje?

Huyu Mama hakuwajua ndugu zangu, lakini alitusomesha wote watatu.

Tunaposema huyu Mama ni mfano muwe mnaelewa.

Hajabadilisha maisha yangu tu, ila ya watu wengi pia.

Zaidi ya wamiliki 85% wa makampuni ya usafi amewasaidia kwa namna Moja ama nyingine
Niko kanisani, kanisa limezizima
 
View attachment 1885747

Tumaini Kakuyu Mlewa alikuwa ndiye mtu wa Kwanza kuwa na kampuni professional ya usafi akichukua tenda kwenye ofisi za makampuni mbalimbali, mahospitali viwanda nk kupitia kampuni yake ya Fame Consolidated Services LTD.

Pia aliasisi shughuli za upambaji wa kumbi za starehe, mikutano etc.

Huyu Mama hakuwa mwanasiasa, ila wajasiriamali tunamlilia sana.

Mungu mpokee

Apumzike kwa amani mja wake mola huyu.

Acha tuwasaidie wale wanaojiona ni wazalendo zaidi:

"Aroo! Siyo Corona hiyo. Ni magonjwa mengine. Kama malaria, kisukari, pressure, pumu, seli mundu na saratani."

Kwanza mtu hawezi kuishi milele.
 
Back
Top Bottom