Buriani Mzee Ruksa: Ni Deng Xiaoping Wetu wa Mageuzi ya Kiuchumi, Demokrasia, Haki za Binadamu na Uhuru wa Habari. Asante kwa Ruksa Zako, Pumzika!

Baba yako alitetewa na Lakha na akasalimika, sasa kwa nini wewe unashindwa kumuiga Lakha uwatetee watanzania wote wakiwemo wa Chadema ili nawe uwe Lakha mpya, hata hivyo ni Mwinyi pekee ndiye aliyejiuzulu, hao wengine mamlaka iliwaondoa.
Lowasa hakuwa waziri mkuu mstaafu, alijiuzulu, Mrema pia alijiuzulu hakustaafu.
 
Ha haa,eti kale ka copy kaje huku..THUBUTU..muulize Sungura wa MCT kilichomkuta, baada ya wahuni wa Magazeti ya Chama kumchomekea kwa kuandika front page " Mh Samia asema hatogombea 2025"

Asante kwa ANDIKO zuri legend!
Mkuu Muhumba wa Mukinyaa, issues ya kale ka copy kuja huku sio issue ya yeye kuamua bali ni circumstances za 2025 kufuatia hoja HII
P
 
Maisha yalikuwa magumu sana kipindi cha awamu ya kwanza , mzee Ruksa aliyapooza maumivu.
Awamu ya Tatu pia maisha yalikuwa magumu sana ikaja awamu ya nne ikayayapooza maumivu.
awamu ya tano ...........
Sasa tupo awamu ya sita......
 
Mtu kuwa kama Murtaza Lakha ni kipaji adimu na uwezo mkubwa sijabahatika kuona wakili hata anayemkaribia.
P
 
Mtu kuwa kama Murtaza Lakha ni kipaji adimu na uwezo mkubwa sijabahatika kuona wakili hata anayemkaribia.
P
Uwezo unaweza kupatikana kwa juhudi zako ukiamua, siamini uamuzi wa kuwatetea watu wote bila ubaguzi kunahitaji darasa ni utashi tu unatakiwa.
Mwambie Mungu akuondolee roho ya chuki akujaze roho ya upendo ili uishi milele.
 
Aliishi maisha ambayo kurasa zake zimejaa mifano mizuri kwa sisi na vizazi vijavyo..

Nimewaza sana sana, hakuna binadamu aliyekamilika lakini mzee Mwinyi alijaa bashasha na hekima kubwa inayofaa kuigwa na wastaafu wote. Hakuwa mchoyo wa elimu lakini alikuwa mchoyo wa chuki. Hakuwa mchoyo wa elimu lakini alikuwa mchoyo wa uzembe.

Tuendelee kutafakari mema na mambo yote aliyoifanyia Tanzania. Tuendelee kujenga kwenye misingi waliyotuachia waasisi wetu akiwemo mzee Mwinyi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…