Mpigania uhuru wa pili
JF-Expert Member
- Apr 12, 2023
- 3,380
- 6,376
Miaka 20By the time Mwinyi anachukua nchi, how old were you?.
P
Sii wote!, nimesoma na Dr. Mwinyi shule moja Primary na sekondari, ,( japo sio darasa moja), Huyu jamaa ni kichwa!, sio kilaza!Familia yake ina bahati sana ya Uongozi ila ni vilaza.
Huyo member anaitwa stroke ni mropokaji maarufu hajui kitu ila anajifanya mjuajiSii wote!, nimesoma na Dr. Mwinyi shule moja Primary na sekondari, ,( japo sio darasa moja), Huyu jamaa ni kichwa!, sio kilaza!
P
Baba yako alitetewa na Lakha na akasalimika, sasa kwa nini wewe unashindwa kumuiga Lakha uwatetee watanzania wote wakiwemo wa Chadema ili nawe uwe Lakha mpya, hata hivyo ni Mwinyi pekee ndiye aliyejiuzulu, hao wengine mamlaka iliwaondoa.Wanabodi
View attachment 2923058Siku ya leo, tunampunzisha Mzee wetu, Rais Mtaafu wa Tanzania, Mzee Ali Hassan Mwinyi, kwa jina maarufu la Mzee Rukhsa, kwenye nyumba yake ya malalo ya makao ya milele.
Mara ya Kwanza Kulisikia Jina la Ali Hassan Mwinyi.
Kwa mara ya kwanza jina la Ali Hassan Mwinyi, nililisikia mwaka 1977 nikiwa darasa la 3 shule ya msingi, wakati huo akiwa ni Waziri wa Mambo ya Ndani wa serikali ya Nyerere, alipolazimika kujiuzulu kutokana na kashfa ya vifo vya watuhumiwa wawili wa mauaji ya vikongwe, huko Mwanza mwaka 1976.
Mwinyi hakuwa peke yake aliyejiuzulu kutokana na kashfa hiyo, bali Makamo wa pili wa rais na Waziri Mkuu, Rashidi Mfaume Kawawa, pia aliondolewa!, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, anyeshughulikia Usalama wa Taifa, Peter Siyovelwa aliondolewa!. Wakafuatiwa na watendaji wakuu wa vyombo vya usalama Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Emelio Mzena, akastaafishwa kwa manufaa ya umma!, Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Samweli Pundugu akastaafishwa kwa manufaa ya umma, na Kamishna Mkuu wa Jeshi la Magereza pia akapumzishwa.
Mwalimu Nyerere alikuwa sio mtu wa mchezo hata kidogo!, kwani baada ya kuwafagia kule juu, fagio la chuma, likatua mjini Mwanza, likaanzia kumfagia Mkuu wa Mkoa Peter Kisumo, akaenda na maji, RPC wa Mwanza, RSO, OCD, na DSO wa Mwanza, kwanza wote wakafutwa kazi, kisha wakarejeshwa vijijini kwao, kwa kusombwa na Land rover 109 usiku usiku na kurudishwa kwenye their places of domicile na mwisho wa siku walikuwa kushitakiwa kwenye ile kesi maarufu, "Kesi ya Mauaji Mwanza" ya mwaka 1976. Mtu pekee aliyesalimika kati ya hao washtakiwa ni mtu mmoja tuu, aliyeitwa Andrew Mayalla, na salama yake, mdogo wake anayetwa Mathew Kasanga, kumuwekea wakili mahiri wa wakati huo, Wakili Murtaza Lakha, kumtetea kaka yake, lakini wengine wote, walikwenda na maji na walikula mvua za kutosha!. Ni kupitia tukio hilo ndipo nilipoanza kulisikia jina la Ali Hassan Mwinyi. Hiki kisa cha Kesi ya Mauaji Mwanza pia nilikihadithia kwenye bandiko hili TISS Ikanushe tuhuma za uvamizi, utekaji, utesaji na mauaji!. Wasijadiliwe na Bunge kwa uwazi bali wachunguzwe, wakithibitika wafumuliwe!
Sijui uwajibikaji wa aina hii ya enzi za Nyerere, ulikuja kupotelea wapi, siku hizi watuhumiwa wanakufa mikononi mwa polisi, and no body cares!.
Tukio hilo lilileta mageuzi makubwa nchini mwetu, kwanza Idara ya Usalama wa Taifa, ilifumuliwa na kusukwa upya kwa kufanyiwa mabadiliko makubwa, ikaletwa sheria ya usalama wa Taifa, ya 1976, Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976 na katiba mpya ya mwaka 1977.
Jina la Ali Hassan Mwinyi, nikaja kukutana nalo tena shule ya msingi, jijini Dar es Salaam, tukisoma na mtoto wake Hussen Mwinyi (Dr)aliyenitangulia madarasa mawili. Baada ya shule ya Msingi nikajiunga shule ya sekondari ya Tambaza, ile mwaka 1985 Rais Mwinyi anakuwa Rais wa Tanzania, yule mtoto wake Hussein Mwinyi alikuwa anasoma PCB Tambaza! alikuwa darasa moja na mtoto wa Malecela, Seche. Kitendo cha mtoto wa rais na mtoto wa Makamo wa Pili wa Rais na Waziri Mkuu John Malecela kusoma shule moja, na halikuwa jambo dogo!, sasa ndio nikazidi kumfahamu Ali Hassan Mwinyi kwa karibu, wakati huo hapo Tambaza pia tuko na mtoto wa Nyerere na Mtoto wa Mkapa, darasa moja.
Mwanzo wa Mwinyi Kutwa Mzee Ruksa.
Wakati Mwinyi anachukua urais ile 1985, hali yetu ya Uchumi ili dhollfu bin taaban, baada ya vitavya Kager ana Mwalimu Nyerere kutangaza miezi 18 ya kufunga mikanda, mambo kiukweli yalikuwa magumu, tumekula unga wa Yanga, kutoka Marekani ambao kule kwao ni chakula cha mifugo!, Watu wamevaa magunia, sandarusi hadi sisi wanafunzi nchi nzima tumevaa uniforma ya kitambaa cha madurufu, ambacho nip amba chafu ya kutupa!.
Mahitaji muhimu yote ni kwa resheni kupitia maduka ya kaya, tulikuwa tunapanga foleni siku nzima kusubiria kuuziwa kilo mbili mbili za sukari, hivyo Watoto wote mnatumwa, ili kuwahi foleni, watu walidamka asubuhi na kupanga mawe, gari linaweza kuja saa 10 jioni au siku nyingine kutoka bila bila, haliji kabisa.
Nchi za mabeberu zilimpa Mwalimu Nyerere masherti magumu ya kutupa misaada, ndipo Mwalimu akaamua kuliko kukubali misaada ya masherti na kugeuka nyuma akageuka jiwe, bora aachie ngazi, kwa mtindo wa kung’atuka na kumpisha Ali Hassan Mwinyi. Hivyo Mwinyi aliipokea nchi ikiwa kwenye dhiki kubwa!.
Baada ya ya kuingia rais Muislamu, kukaibuka vikundi vya Waislamu wenye siasa kali, kwanza waligomea Nguruwe wasichinjiwe mahali pamoja, na wanyama wengine kwasababu nguruwe ni haramu kwa Waislamu,
na isiuzwe bucha zile zile za nyama ya kawaida.
Vikundi hivyo vikaleta vurugu za kulazimisha nyama ya nguruwe ipigwe marufuku kwasababu ni haramu, na kuanzishwa mihadhara ya kashfa, kwa wanazuoni wa Kiislamu kuikosoa Biblia na kusema nguruwe hata kwenye Biblia ni Haramu. Vurugu hizo zikapelekea kuvamia mabucha ya nguruwe na kuvunja kisha kukimbilia kujificha misikitini kulikopelekea vurugu za Msikiti wa Mwembecha miaka kadhaa baadae.
Rais Mwinyi akatangaza rukhsa mtu yoyote kula kitu chochote, hakuna ruhusa ya mtu mwingine yeyote kuingilia uhuru wa mtu wa dini nyingine yoyote kula chochote, “Ruksa” na huo ukawa ndio mwanzo wa kuitwa Mzee wa Ruksa, wale wahuni kwa kisingizio cha dini walishughulikiwa kikamilifu, ikiwemo Msikiti wa Mwembechai Kuvamiwa, tena ikatokea mmoja wa wana vuguvugu hawa ni mshikaji wangu sana wa deski moja sekondari ya Tambaza, akiitwa Hassan.
Baada ya kuzifungulia hizo ruksa, alikuja kufungulia ruksa nyingine nyingi za biashara, Uchumi, akaruhusu mitumba, akaruhusu Chai Maharage, akalipindua Azimio la Arusha lililoweka miiko ya uongozi na kuleta Azimio la Zanzibar ambalo liliruhusu viongozi kufanya biashara na kumiliki mali na hapa sasa ndio viongozi wa umma wakaanza kuwa matajiri na kuupindua uchumi wetu kutoka uchumi wa kijamaa na kuingia kwenye uchumi wa kibepari wa nguvu ya soko, market economy.
Ruksa nyingine kubwa Rais Mwinyi aliyotuachia ni ruksa ya mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini Tanzania kiasi kwamba sifa ya Baba wa demokrasia Tanzania inamstahili kabisa!, Mwinyi ndie Deng Xioping wetu!.
Japo Rais Mstaafu, Ali Haasan Mwinyi, Mzee wa Rukhsa, ametutoka kwa kutangulia mbele ya haki, huku nyuma Watanzania tunaendelea kuzifaidi rukhsa zake, tutanzienzi milele, na tena sio tuu ametuachia Rukhsa, pia ametuachia na kale ka copy pale Zanzibar!, cha mtu rahimu kama yeye!.
Akina sisi, tayari tumeisha mshauri Mama, kama hoja Hivyo kama HII sauti ni sauti ya kweli, na kama vipi 2025, ataona ni parefu, hakuna ubaya, akikapisha kale ka Copy kule kaje huku kutufungulia ruksa nyingine zote zilizobakia!.
Buriani Ali Hassan Mwinyi, Mwendo Umeumaliza.
inna lillahi wa inna ilayhi rajiun
(إِنَّا لِلَّهِ وَإِنَّ إِلَيْهِ رَاجِعُونَ)
Paskali.
Tanzania tunaishi kwa viwango vya chini sana vya TBS, ukweli ni kwamba chini ya CCM kila mtu anaweza kuwa rais na akasifiwa sana.Mambo mengi yalianza kuharibika kwake.
Mzee wa kila kitu Ruksa alivurunda.
Mkuu Muhumba wa Mukinyaa, issues ya kale ka copy kuja huku sio issue ya yeye kuamua bali ni circumstances za 2025 kufuatia hoja HIIHa haa,eti kale ka copy kaje huku..THUBUTU..muulize Sungura wa MCT kilichomkuta, baada ya wahuni wa Magazeti ya Chama kumchomekea kwa kuandika front page " Mh Samia asema hatogombea 2025"
Asante kwa ANDIKO zuri legend!
Then ulikuwepo ile miezi 18 ya kukaza mikanda. Nchi alipoipokea Mwinyi kutoka kwa Nyerere na aliyoyafanya yana tofauti gani na Deng alipoipokea China kutoka kwa Chairman Mao?.Miaka 20
Moja ya vitu vya hovyo kupata kufanyika nchini.Sherehe zikiangukia weekend zinalipiwa siku za kazi. Nchi ilikua ya wote
Hayafanani hata kidogo tuache kujifarijiThen ulikuwepo ile miezi 18 ya kukaza mikanda. Nchi alipoipokea Mwinyi kutoka kwa Nyerere na aliyoyafanya yana tofauti gani na Deng alipoipokea China kutoka kwa Chairman Mao?.
P
Mtu kuwa kama Murtaza Lakha ni kipaji adimu na uwezo mkubwa sijabahatika kuona wakili hata anayemkaribia.Baba yako alitetewa na Lakha na akasalimika, sasa kwa nini wewe unashindwa kumuiga Lakha uwatetee watanzania wote wakiwemo wa Chadema ili nawe uwe Lakha mpya, hata hivyo ni Mwinyi pekee ndiye aliyejiuzulu, hao wengine mamlaka iliwaondoa.
Lowasa hakuwa waziri mkuu mstaafu, alijiuzulu, Mrema pia alijiuzulu hakustaafu.
Uwezo unaweza kupatikana kwa juhudi zako ukiamua, siamini uamuzi wa kuwatetea watu wote bila ubaguzi kunahitaji darasa ni utashi tu unatakiwa.Mtu kuwa kama Murtaza Lakha ni kipaji adimu na uwezo mkubwa sijabahatika kuona wakili hata anayemkaribia.
P
AmenUwezo unaweza kupatikana kwa juhudi zako ukiamua, siamini uamuzi wa kuwatetea watu wote bila ubaguzi kunahitaji darasa ni utashi tu unatakiwa.
Mwambie Mungu akuondolee roho ya chuki akujaze roho ya upendo ili uishi milele.
Aliishi maisha ambayo kurasa zake zimejaa mifano mizuri kwa sisi na vizazi vijavyo..Wanabodi
View attachment 2923058Siku ya leo, tunampunzisha Mzee wetu, Rais Mtaafu wa Tanzania, Mzee Ali Hassan Mwinyi, kwa jina maarufu la Mzee Rukhsa, kwenye nyumba yake ya malalo ya makao ya milele.
Mara ya Kwanza Kulisikia Jina la Ali Hassan Mwinyi.
Kwa mara ya kwanza jina la Ali Hassan Mwinyi, nililisikia mwaka 1977 nikiwa darasa la 3 shule ya msingi, wakati huo akiwa ni Waziri wa Mambo ya Ndani wa serikali ya Nyerere, alipolazimika kujiuzulu kutokana na kashfa ya vifo vya watuhumiwa wawili wa mauaji ya vikongwe, huko Mwanza mwaka 1976.
Mwinyi hakuwa peke yake aliyejiuzulu kutokana na kashfa hiyo, bali Makamo wa pili wa rais na Waziri Mkuu, Rashidi Mfaume Kawawa, pia aliondolewa!, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, anyeshughulikia Usalama wa Taifa, Peter Siyovelwa aliondolewa!. Wakafuatiwa na watendaji wakuu wa vyombo vya usalama Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Emelio Mzena, akastaafishwa kwa manufaa ya umma!, Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Samweli Pundugu akastaafishwa kwa manufaa ya umma, na Kamishna Mkuu wa Jeshi la Magereza pia akapumzishwa.
Mwalimu Nyerere alikuwa sio mtu wa mchezo hata kidogo!, kwani baada ya kuwafagia kule juu, fagio la chuma, likatua mjini Mwanza, likaanzia kumfagia Mkuu wa Mkoa Peter Kisumo, akaenda na maji, RPC wa Mwanza, RSO, OCD, na DSO wa Mwanza, kwanza wote wakafutwa kazi, kisha wakarejeshwa vijijini kwao, kwa kusombwa na Land rover 109 usiku usiku na kurudishwa kwenye their places of domicile na mwisho wa siku walikuwa kushitakiwa kwenye ile kesi maarufu, "Kesi ya Mauaji Mwanza" ya mwaka 1976. Mtu pekee aliyesalimika kati ya hao washtakiwa ni mtu mmoja tuu, aliyeitwa Andrew Mayalla, na salama yake, mdogo wake anayetwa Mathew Kasanga, kumuwekea wakili mahiri wa wakati huo, Wakili Murtaza Lakha, kumtetea kaka yake, lakini wengine wote, walikwenda na maji na walikula mvua za kutosha!. Ni kupitia tukio hilo ndipo nilipoanza kulisikia jina la Ali Hassan Mwinyi. Hiki kisa cha Kesi ya Mauaji Mwanza pia nilikihadithia kwenye bandiko hili TISS Ikanushe tuhuma za uvamizi, utekaji, utesaji na mauaji!. Wasijadiliwe na Bunge kwa uwazi bali wachunguzwe, wakithibitika wafumuliwe!
Sijui uwajibikaji wa aina hii ya enzi za Nyerere, ulikuja kupotelea wapi, siku hizi watuhumiwa wanakufa mikononi mwa polisi, and no body cares!.
Tukio hilo lilileta mageuzi makubwa nchini mwetu, kwanza Idara ya Usalama wa Taifa, ilifumuliwa na kusukwa upya kwa kufanyiwa mabadiliko makubwa, ikaletwa sheria ya usalama wa Taifa, ya 1976, Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976 na katiba mpya ya mwaka 1977.
Jina la Ali Hassan Mwinyi, nikaja kukutana nalo tena shule ya msingi, jijini Dar es Salaam, tukisoma na mtoto wake Hussen Mwinyi (Dr)aliyenitangulia madarasa mawili. Baada ya shule ya Msingi nikajiunga shule ya sekondari ya Tambaza, ile mwaka 1985 Rais Mwinyi anakuwa Rais wa Tanzania, yule mtoto wake Hussein Mwinyi alikuwa anasoma PCB Tambaza! alikuwa darasa moja na mtoto wa Malecela, Seche. Kitendo cha mtoto wa rais na mtoto wa Makamo wa Pili wa Rais na Waziri Mkuu John Malecela kusoma shule moja, na halikuwa jambo dogo!, sasa ndio nikazidi kumfahamu Ali Hassan Mwinyi kwa karibu, wakati huo hapo Tambaza pia tuko na mtoto wa Nyerere na Mtoto wa Mkapa, darasa moja.
Mwanzo wa Mwinyi Kutwa Mzee Ruksa.
Wakati Mwinyi anachukua urais ile 1985, hali yetu ya Uchumi ili dhollfu bin taaban, baada ya vitavya Kager ana Mwalimu Nyerere kutangaza miezi 18 ya kufunga mikanda, mambo kiukweli yalikuwa magumu, tumekula unga wa Yanga, kutoka Marekani ambao kule kwao ni chakula cha mifugo!, Watu wamevaa magunia, sandarusi hadi sisi wanafunzi nchi nzima tumevaa uniforma ya kitambaa cha madurufu, ambacho nip amba chafu ya kutupa!.
Mahitaji muhimu yote ni kwa resheni kupitia maduka ya kaya, tulikuwa tunapanga foleni siku nzima kusubiria kuuziwa kilo mbili mbili za sukari, hivyo Watoto wote mnatumwa, ili kuwahi foleni, watu walidamka asubuhi na kupanga mawe, gari linaweza kuja saa 10 jioni au siku nyingine kutoka bila bila, haliji kabisa.
Nchi za mabeberu zilimpa Mwalimu Nyerere masherti magumu ya kutupa misaada, ndipo Mwalimu akaamua kuliko kukubali misaada ya masherti na kugeuka nyuma akageuka jiwe, bora aachie ngazi, kwa mtindo wa kung’atuka na kumpisha Ali Hassan Mwinyi. Hivyo Mwinyi aliipokea nchi ikiwa kwenye dhiki kubwa!.
Baada ya ya kuingia rais Muislamu, kukaibuka vikundi vya Waislamu wenye siasa kali, kwanza waligomea Nguruwe wasichinjiwe mahali pamoja, na wanyama wengine kwasababu nguruwe ni haramu kwa Waislamu,
na isiuzwe bucha zile zile za nyama ya kawaida.
Vikundi hivyo vikaleta vurugu za kulazimisha nyama ya nguruwe ipigwe marufuku kwasababu ni haramu, na kuanzishwa mihadhara ya kashfa, kwa wanazuoni wa Kiislamu kuikosoa Biblia na kusema nguruwe hata kwenye Biblia ni Haramu. Vurugu hizo zikapelekea kuvamia mabucha ya nguruwe na kuvunja kisha kukimbilia kujificha misikitini kulikopelekea vurugu za Msikiti wa Mwembecha miaka kadhaa baadae.
Rais Mwinyi akatangaza rukhsa mtu yoyote kula kitu chochote, hakuna ruhusa ya mtu mwingine yeyote kuingilia uhuru wa mtu wa dini nyingine yoyote kula chochote, “Ruksa” na huo ukawa ndio mwanzo wa kuitwa Mzee wa Ruksa, wale wahuni kwa kisingizio cha dini walishughulikiwa kikamilifu, ikiwemo Msikiti wa Mwembechai Kuvamiwa, tena ikatokea mmoja wa wana vuguvugu hawa ni mshikaji wangu sana wa deski moja sekondari ya Tambaza, akiitwa Hassan.
Baada ya kuzifungulia hizo ruksa, alikuja kufungulia ruksa nyingine nyingi za biashara, Uchumi, akaruhusu mitumba, akaruhusu Chai Maharage, akalipindua Azimio la Arusha lililoweka miiko ya uongozi na kuleta Azimio la Zanzibar ambalo liliruhusu viongozi kufanya biashara na kumiliki mali na hapa sasa ndio viongozi wa umma wakaanza kuwa matajiri na kuupindua uchumi wetu kutoka uchumi wa kijamaa na kuingia kwenye uchumi wa kibepari wa nguvu ya soko, market economy.
Ruksa nyingine kubwa Rais Mwinyi aliyotuachia ni ruksa ya mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini Tanzania kiasi kwamba sifa ya Baba wa demokrasia Tanzania inamstahili kabisa!, Mwinyi ndie Deng Xioping wetu!.
Japo Rais Mstaafu, Ali Haasan Mwinyi, Mzee wa Rukhsa, ametutoka kwa kutangulia mbele ya haki, huku nyuma Watanzania tunaendelea kuzifaidi rukhsa zake, tutanzienzi milele, na tena sio tuu ametuachia Rukhsa, pia ametuachia na kale ka copy pale Zanzibar!, cha mtu rahimu kama yeye!.
Akina sisi, tayari tumeisha mshauri Mama, kama hoja Hivyo kama HII sauti ni sauti ya kweli, na kama vipi 2025, ataona ni parefu, hakuna ubaya, akikapisha kale ka Copy kule kaje huku kutufungulia ruksa nyingine zote zilizobakia!.
Buriani Ali Hassan Mwinyi, Mwendo Umeumaliza.
inna lillahi wa inna ilayhi rajiun
(إِنَّا لِلَّهِ وَإِنَّ إِلَيْهِ رَاجِعُونَ)
Paskali.
Nimekuambia mwambie Mungu, wewe unasema Amen!Amen
P
Jambo lolote la Mungu hujibiwa na Amen.Nimekuambia mwambie Mungu, wewe unasema Amen!
Anza kulitoa hilo jambo kisha sema Amen.Jambo lolote la Mungu hujibiwa na Amen.
P