Buriani

Buriani

Unene unaficha mambo mengi ikiwemo cholesterol inayopunguza damu kupita vizuri kwenye mishipa.

Sasa mapafu yakijaa mucus kutokana na Corona, kiasi cha hewa inayosafishwa inakupungua sana na hivyo kusababisha kiasi cha oxygen kwenye damu kuwa kidogo. Ukiwa mnene uwezo wa damu safi kuzunguka mwilini unazidi kupungua. Hivyo kuharakisha ogani za mwili kudhoofika kwa kukosa oxygen.

Kingine ni kuwa mafuta mwilini yanazuia uwezo wa diaphragm (msuli wa kusukuma mapafu) kufanya kazi yake ya kusukuma mapafu ili hewa iingie na kutoka, ndiyo maana watu wanene wanapatashida kupumua.

Hivyo utaona mlolongo wa matatizo unaosababishwa na unene kwenye Corona ni mrefu.
Mkuu safi saana kwa maelezo mazuri endeleeni kutoa elimu wenye utaalamu mtaokoa wengi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa mara nyingine bandugu bapenzi, itakuwa kutojitendea haki kutojitendea haki uzi huu.

Hali si hali:

Akaja baba mmoja, toka safari ya mbali,
Kavimba yote mapaja, na kutetemeka mwili,
Watoto wake wakaja, ili kumtaka yake kauli,
Xxxxxxxxxxxxxxxxx, yyyyyyyyyyyyyyy.


buriani.
 
Kwa mara nyingine bandugu bapenzi, itakuwa kutojitendea haki kutojitendea haki uzi huu.

Hali si hali:

Akaja baba mmoja, toka safari ya mbali,
Kavimba yote mapaja, na kutetemeka mwili,
Watoto wake wakaja, ili kumtaka yake kauli,
Xxxxxxxxxxxxxxxxx, yyyyyyyyyyyyyyy.


buriani
Huu uzi wa mwaka 2020. Nataka kukwambia, kama Mungu alivyowaaibisha maadui mliosema tutakufa kuliko Italy, ATAWAAIBISHA NA MWAKA HUU 2021ili ajitwalie UTUKUFU!

Maneno yenu na unabii hasi tunayafuta kwa DAMU TAKATIFU YA YESU KRISTO.

Zaburi 35Z na aburi 109
 
Huu uzi wa mwaka 2020. Nataka kukwambia, kama Mungu alivyowaaibisha maadui mliosema tutakufa kuliko Italy, ATAWAAIBISHA NA MWAKA HUU 2021ili ajitwalie UTUKUFU!

Maneno yenu na unabii hasi tunayafuta kwa DAMU TAKATIFU YA YESU KRISTO.

Zaburi 35Z na aburi 109

Uzi wa 2020 unaishi huo. Mwulize mzee baba.

Kumbuka jitihada zote hizi ni kwa kuwa tungependa kuishi, sisi na wewe.

Tuvae barakoa, tunawe maji tiririka, tuweke social distance. Tuwahami walioko Hatarini kwa nguvu zote.

Huna sababu ya kudhani Mungu atatuabisha sisi wenye nia za dhati kama hizi.

Kwa vile wala si mashindano tunaendelea kuwakumbusha kutokumjaribu bwana Mungu wetu. Hii ikiwa kama ilivyo kwenye waraka wa TEC na hata pia ule wa maaskofu wa Moravian.

Eeh mola wetu hebu ukatusamehe sisi waja wako tusiojua hata tuyasemayo.
 
Huu uzi wa mwaka 2020. Nataka kukwambia, kama Mungu alivyowaaibisha maadui mliosema tutakufa kuliko Italy, ATAWAAIBISHA NA MWAKA HUU 2021ili ajitwalie UTUKUFU!

Maneno yenu na unabii hasi tunayafuta kwa DAMU TAKATIFU YA YESU KRISTO.

Zaburi 35Z na aburi 109
Hivi nyinyi viherehere wa kijani kibichi mna akili timamu kabisaaa ? Kuchezea roho za watanzania kisa mliyemsukumiza Ni mgonjwa wa bipolar disorder na saikatriki kesi na nyie mnafuata njia yake .
 
😭😢😤😡🥵🤒😷🤧😪😓😰🤬
 
Mungu atunusuru, wengine tuligomaga kufa Hadi tuwe matrilionea, tukaacha pombe, tukaacha kula nyama nyekundu, tukaacha papuchi gongaring, tukaacha vyote ili turefushe maisha. Sasa dude vurugavunja limeingia
Ukikaribia kufa niite nije nikuongoze sara ya toba, nitakuzika mwenyewe
 
Nyakati za nyingi hofu



Winner Chimba




Nyakati za nyingi hofu, hizi zimetufikia

Kirusi kama siafu, vile kinanyemelea

Twajiona wote wafu, japo bado twatembea

Nani tumgeukie, Isipokuwa Rabana



Kifo kinatuvizia, kila tunapotembea

Hakitaki kuachia, kambi kimejiwekea

Sana kinatunukia, woga kinatuachia

Nani tumtegemee Isipokuwa Rabana?



Niwawazapo wazazi, woga unanivamia

Yakiwapata maradhi, kipi kitachotokea

Magonjwa ya nyemelezi, wanayo nakumbukia

Nani atusaidie, kama sio mwenye enzi?



Wangu binti na kijana, sana ninawawazia

Shuleni wanapokwenda, bila hata barakoa

Vipi wakiambukizwa, hofu inanivamia

Sina wa kumgeukia, isipokuwa Rabana



Mtandaoni kiingia, mawazo nipunguzie

Nakutana na tanzia, mara huyu mara yule

Wazee watangulia, nani tumkimbilie?

Nani atatufariji, Isipokuwa Rabana?



Wanaanguka magwiji, walosheheni hekima

Wajuzi na wabobezi, ya maarifa hazina

Wetu wazazi na walezi, walotulea vijana

Nani tutamlilia, isipokuwa Manani



Wenye nguvu vijana, nao wajiondokea

Madaktari sanasana, kazini wanajifia

Nguvu kazi ya taifa, bure inapotelea

Nani atusaidie, Isipokuwa Mwenyezi?

Ka mshumaa wanazima, bila hata kutuaga

Nyoyo zimetuzizima, waondoka ghafla ghafla

Na tulie kimyakimya, wanasema wa siasa

Hawataki kusikia, vilio vikizidia



Hawataki kusikia, amani twaichafua

Eti tukiomboleza, taharuki tunazua

Tanzia hawazitaki, eti zinawachefua

Nani tumkimbilie, Isipokuwa Rabana?



Viongozi wa taifa, wale tulowachagua

Wasomi walobobea, nao pia wamefyata

Tafiti wameziacha, wafata ya kusikia

Wamegeuka vioja, sinema kutufanyia



Wote wamejificha, hawana la kutwambia

Wale tulowategemea, sasa wametukimbia

Wametuacha wakiwa, nani atatutetea?

Nani atatutetea, Isipokuwa Rabana?



Nani atutegemeze, isipokuwa Rabana

Hofu tumuelezee, asiyechoshwa na waja

Machozi tummwagikie, kwake mwingi wa faraja

Hayupo mwingine tena, Isipokuwa Rabana



Azielewa simanzi, kamwe hatatukataa

Tukumbate kifuani, machozi atayafuta

Tumwelezee huzuni, yeye anategemeka

Ndiyo yeye tumaini, Hakuna mwingine tena



Tusiache tahadhari, bora sana kujikinga

Wasiwasi ni akili, hata wakitusimanga

Wengine kuwafikiri, huo ndio uungwana

Hayo yote tukifanya, Mola atatusitiri.
 
Ngoja nijichagulie wimbo kabisa, kama ikitokea nimewatoka mnipigie wimbo wa kamanda wa daz nundaz na parapanda.
Wosia uheshimiwe.
Parapanda zipo mbili, ile ya kidini na ile ya Roma na Stamina, eleza bila kuacha gap
 
Back
Top Bottom