Burundi yaongeza wanajeshi Kivu Kusini

sasa kama rwanda inaitesa congo, unataka kusema burundi nayo inaweza kuitesa rwanda? Rwanda inaona burundi si lolote si chochote kama tu imeweza kuitesa congo iliyo kubwa kuliko burundi
Unajidanganya sanaaa mkuu
 
Mtusi mwingine huyu hapa
 
Kichekesho! Kama congo kubwa inanyukwa na rwanda, burundi ni kitu gani kwa rwanda? Kagame anaona burundi ni underdog tu akiamua anaifyagia asubuhi tu
DRC ina jeshi dhaifu kwa sababu iliwekewa vikwazo vya kununua silaha, kwa hiyo ina zana za kijeshi duni sana.
 
Jeshi la Rwanda lina nguvu kuliko la Burundi hata kizana na kibajeti.....
 
DRC ina jeshi dhaifu kwa sababu iliwekewa vikwazo vya kununua silaha, kwa hiyo ina zana za kijeshi duni sana.
Mwanajeshi akose hata nguo, akose viatu, akose mafunzo, usingizie vikwazo? Je, kama unajua umewekewa vikwazo, unatunishaje msuri wakati unajua uwezo wa vita huna? Kama wasi wanapata, serikali inashindwaje! Ina maana waasi wana akili kuzidi serikali sasa.
Nchi wazito wanakula raha ulaya na wapi mari wanajirundikia huko, mwanajeshi analipwa dola 150 au mia mbili, anakaa miezi hadi 6 hajapokea mshahara, hata kibaka akiiba gwanda, anautesa mji mzima kuwa yeye ni mwanajeshi, mtu ana miaka 70 lakini mwanajeshi,hilo jeshi au sungusungu!!! Uongozi ndo una tatizo pahala furani.
 
DRC ina jeshi dhaifu kwa sababu iliwekewa vikwazo vya kununua silaha, kwa hiyo ina zana za kijeshi duni sana.
DRC wanapigana vita vya kipumbavu , hakuna motivation yeyote zaidi ya ukabila, M23 wana kila sababu ni haki na usalama wao
 
Wewe focus ugaidi wako na hamas
 
Hizi chai endelea kuwalisha wenzako wasiojielewa huku, pole
 
Unajifunza ulevi? Hao wasio na uniform ni wanajeshi wa DRC au ni wanamgambo wanaowaunga mkono wanajeshi wa DRC?

Kumbuka kula kabla ya kunywa pombe!
 
Kwa hiyo tuseme Rwanda na Burundi wanapigana vita ya nje
Mmoja angepiga mji mkuu wa mwenzie kiumane
Hawa watoto wanataka washikishwe adabu wote
 
Enjoy uhuru tz,kule kwenu uhuru huu hakuna
MTZ 💯 hapa just FYI, na Kagame aendelee kuwanyoosha wakabila nyie na mawazo yenu ya kijima, mmepeleka sumu zenu Congo ndio maana matatizo hayaishi, na Uber driver Tshesekedi ana IQ ndogo sana kuelewa mchawi wa Congo
 

Tanzania: kufungwa kwa kambi kumecheleweshwa kwa mwaka mmoja​


6 Febuari 2025PCN

Wakimbizi wa Burundi wapata mwaka mwingine kabla ya kambi zao kufungwa. Tangazo hilo lilitolewa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Tanzania inayohusika na wakimbizi baada ya kutembelea kambi mbili kubwa za wakimbizi wa Burundi zilizopo kaskazini-magharibi mwa Tanzania.


HABARI SOS Médias Burundi
Ujumbe wa ngazi ya juu kutoka UNHCR na serikali ya Tanzania ulitembelea kambi za wakimbizi wa Burundi wiki iliyopita.

Ziara hiyo ilifanyika Jumatatu Januari 27 na Jumanne Januari 28 mtawalia katika kambi za Nyarugusu na Nduta zilizopo mkoani Kigoma au kaskazini magharibi mwa nchi.

Kulingana na takwimu za UNHCR kufikia Desemba 31, 2024, nchi hii ina zaidi ya Warundi 104,000. Wengi wao walikimbia mzozo wa 2015 kufuatia mamlaka mengine yenye utata ya hayati Rais Pierre Nkurunziza mwaka huo huo

Wawakilishi wa UNHCR katika wilaya za Kasulu na Kibondo ambako kambi hizi mbili zina makao yake, waliwahakikishia wakimbizi kwamba ifikapo 2025, hali haitakuwa mbaya zaidi.

“Maombi yako yamejibiwa. Tume ya pande tatu iliongeza muda wa zoezi la kuwarejesha nyumbani kwa hiari kwa mwaka mmoja. Baada ya kipindi hiki, tutaweza kupanda gia na pengine kufunga kambi,” walitangaza kwa zamu.

Mkimbizi wa Burundi akiwaandalia watoto wake chakula katika kambi ya Nduta nchini Tanzania (SOS Médias Burundi)

Hii ni moja ya hitimisho la mkutano wa pande tatu kati ya Tanzania, Burundi na UNHCR uliofanyika Bujumbura, mji mkuu wa kiuchumi wa Burundi, mwishoni mwa Desemba 2024.

Mkutano ambao pia ulipendekeza kuwa Burundi ijiandae kupokea wakimbizi wasiopungua elfu tatu kwa mwezi.

Wakimbizi hao wanapumua. Pia walishangilia na walionekana kutopendezwa na kilichofuata, kulingana na ripota wa SOS Médias Burundi.

“Asante Mungu hata hivyo, tunaweza kusherehekea siku hii ya kuzaliwa tena. Tunaendelea kuiomba jumuiya ya kimataifa kufuatilia kwa karibu hali hiyo na kuzishawishi mamlaka za Tanzania ili kuachana na mpango huu mbaya na usio wa kibinadamu wa kufunga kambi hizo,” anajibu kiongozi wa jumuiya hiyo kutoka zone 5 ya kambi ya Nduta.

Sudi Mwakibasi alipumzika…
Katika eneo la zone 10 kwenye kambi ya Nyarugusu na pia zone 5 kwenye kambi ya Nduta ambako wakimbizi wa Burundi walikuwa wamekusanyika, Sudi Mwakibasi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani anayehusika na masuala ya wakimbizi, anayejulikana kwa kauli zake za kiberiti kwa wakimbizi wa Burundi, kwa mara moja, alionyeshwa huruma kama ilivyoonyeshwa na Warundi.

“Anajulikana kwa lugha yake kali. Lakini cha ajabu alijigeuza kuwa mzazi akitoa somo na ushauri jambo ambalo lilionekana si la kawaida kwetu,” anasema mkimbizi kutoka kambi ya Nduta aliyesikiliza hotuba yake.

Wakimbizi wa Burundi wakiwa katika mkutano na mamlaka ya Tanzania katika kambi ya Nyarugusu (SOS Médias Burundi)

Sudi Mwakibasi alipendekeza kwamba wazazi wawasomeshe watoto wao vizuri, wawajengee maadili ya kupenda nchi na kazi huku wakionyesha mifano mizuri.
“Vizazi hivi vijavyo ndivyo vitajenga nchi yako. Epuka kuwahimiza kufanya vitendo vya uhalifu. Na zaidi ya yote msikubali kuwa wanafanya shughuli za kuyumbisha nchi yenu,” alishauri.
Mwaka huu huenda ukawa na shughuli nyingi kulingana na mpango uliozinduliwa na ujumbe huu huko Nyarugusu na Nduta.

“Kutakuwa na ziara nchini Burundi za wakimbizi kutoka Tanzania na wanaorejea kutoka Burundi (nendeni mkaone, mje mseme), mechi za soka kati ya makundi hayo mawili ya Makamba (Burundi) na Kibondo (Tanzania) pamoja na vikao vya uhamasishaji juu ya kurudi kwa hiari,” wajumbe walisisitiza.

Hata kama wazo la kufanya mahojiano ya mtu binafsi ili kubaini nia iliyomsukuma kila mkimbizi kutoroka Burundi bado litaendelea kudumishwa, ujumbe huo haujafichua ni lini zoezi hili litafanyika. Jambo ambalo linawafanya wakimbizi wa Burundi kuamini kuwa Umoja wa Mataifa umeishawishi Tanzania kuwaachia huru wale walioomba hifadhi katika nchi hii kwa mujibu wa Mkataba wa Geneva wa 1951 unaohusiana na ulinzi wa wakimbizi.
Tanzania inasalia kuwa nchi inayohifadhi wakimbizi wengi zaidi wa Burundi katika ukanda huo.
 
Unajua lakini Tshisekedi ni mtoto wa nani? Huu uongozi wa kurithi nao shida.
Then, watu walishaisha mapolini miaka nenda rudi, washakuwa kama wanyama, unaanza kuwaelekeza cha kufanya.
Uongozi wa kurithi si tatizo kwani umetamalaki ukanda huu wote kuanzia Tz, Rwanda, Uganda,...
tunatofautiana kidogo kwenye kurithishana. Mfano angalia yule "mfalme" wa Uganda na kijana wake Muhoozi. Tanzania kuna ufalme wa CCM unaotoa wafalme kila baada ya muda flani, lkn pia na hoa wafalme hupatikana kwa namna ya kujuana kama ndugu kigogo flani, anatoka kambi flani, huyu ni mwenzenu,.......
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…