Butiku: Ningejua CCM itaingilia mchakato wa Katiba nisingeshiriki


Mzee Butiku anataka kusema nini hapa mbona simwelewi?

loh!
 
ccm wanawalisha watu sumu, kitu ambacho hakiwezi kutatua tata za muungano. muarubaini wa muungano si mbili wala moja. tuko kwenye mbili matatizo tulo nayo ni mengi.

sasa twende kwenye tatu kama kweli tunapenda muungano. tuloungana nao watanganyika tuwajue na ss ndio tupo, na tunachokiunda kiwe wazi. vifitna na unafiki wa mwanakijiji na wenziwe kwa sasa hazina nafasi
 
Butiku ni mingoni mwa wana Ccm wanache, wanao muishi Mwalimu, wengine ni Dr.Salim na Ibrahim Kaduma!.

Hapa Pasco unamaanisha mbali na Mwl, ni watatu hawa wanaoweza kuikosoa CCM bila kuuma maneno. Sasa je, watatu hawa wataweza 'kuyatingisha maji' yanayoonekana yametuama ndani ya 'beseni' la CCM?

btw, Pasco unaonaje mawazo ya Mzee Jaji Warioba? hayafanani na akina Mzee Butiku, Mzee Dr. Salim na Mzee Kaduma?
 
Anapaswa kujiuzulu ili kuonesha msimamo wake. CCM iachie tume wafanye kile kilicho matakwa ya wengi.
CCM ukiwasusia jambo huwa hawajali, cha msingi ni kukomaa nao hadi mwisho; by the way hawakuwa tayari pia nia ya dhati ya kuandika kabisa mpya hii, ndiyo maana watavutia kwao ili waendelee kutawala.
 
kama ana nia kweli basi awe kama Punda, utampeleka kisimani na kama hataki kunywa hatakunywa na wala hutamlazimisha, tume ndo itakayotoa rasimu kwa kuandika, wao waandike wanayoona ni sahihi na wala CCM hawana uwezo wa kuingia kwenye tume na kuandika wanayotaka akishindwa ajitoe.
 
pamoja na maonyo mazuri ya mzee Butiku, alipaswa kukataa huo ujumbe mapema kwa kuwa anaijua ccm fika. Kujitoa lawama muda huu ni kutughilibu
 
Ccm inadhani tanzania ndo yenyewe, lichama hili litavunja muungano kwa kuwapuuza watanzania!
 
Hakuna kujiuzulu,apambane humohumo hadi tuipate katiba mpya,kujiuzulu ni kumsusia nguruwe shamba la mihogo
 
pamoja na maonyo mazuri ya mzee Butiku, alipaswa kukataa huo ujumbe mapema kwa kuwa anaijua ccm fika. Kujitoa lawama muda huu ni kutughilibu


Huyu Mzee kuna habari ambazo siyo rasmi kua ana kiwanja cha wazi kila sekeseke la viwanja likiibuka na yeye anaibuka sasa sijui kama kuna uhusiano na kauli za safari hii.
 
Aache kupiga Siasa.Kama kweli anamaanisha anachokisema ajiuzulu hata sasa ili kutoa Somo kwa CCM,

Huyu Butiku alikuwa amechoka sana wakati alipoteuliwa kuingia kwenye hiyo tume sidhani kama ana ubavu wa kuweza kujiuzuru kutoka kwenye tume yenye ulaji mnono!!! Hiyo yote ni danganya toto tu.
 
Butiku ni mingoni mwa wana Ccm wanache, wanao muishi Mwalimu, wengine ni Dr.Salim na Ibrahim Kaduma!.
Pasco. Nadhani walimwelewa, na umuhimu wa kuwa watanzania kwanza. Tatizo watu tumejitwika vyama, na wengine hawaiju kabisa maana yake. Ebu fikiri mtu chama chake kina ahadi kwa kila mwanachama kuwa inayosema "nitasema kweli daima, fitina kwangu mwiko'. Ukisema neno ukweli, kwangu ni kuwa uwiano sawia kati ya kile unachokifiri, na kusema ama kukiandika na uhalisia wa jambo unalolijadili. Hebu fikiri mfano wa Mwigulu akijua fika kutakuwa na mkutano wa katiba chini ya chadema, naye anaondoa watu kwenda kuangalia mpira wa mchangani kwa kuwaita simba' kwenye mtandao anasema wanairamba wameikataa CDM, lakini mimi naona ilikuwa fitina tu. Kwa hiyo unaweza kuondoka na neno moja Mwigulu si Mkweli, ni mwongo na mtu wa fitina kinyume na ahadi ya chama chake. Sitaki kusema ile ya rushwa, manake unaweza rushwa toka ghorofani endapo uko huko.
 
Nilitarajia kuona neno kifo, kasema laziama aseme ukwel kabla hajafa! Miccm mingine inawaza kummwakyembe.
 
Butiku ni frustrated individual fulani hivi, bado ana hasira za kupigwa chini na Ben Mkapa alipotaka Uenyekiti wa bodi wa shirka nyeti. Since then amekuwa anti CCM in the name of Mwalimu Nyerere foundation.

Hana jeuri ya kujiuzulu and I can bet on that, kuacha posho ya 400,000 kwa siku Shangingi la ngvu na masurufu kedekede kunataka uzalendo wa hali ya juu na Butiku hana. Alikuwa kachoka uso umejaa michirizi kwa njaa, leo anawaka na kumemeremeta. Si basi kamkuta Kikwete muungwana mambo haya asinge thubutu kuyafanya wakati wa Ben Mkapa.

Hii ningejua kama CCM itaingilia nisingekubali, sasa washaingilia sii ujiuzulu tu kwani kuwa kwenye tume ni kufungwa jela huwezi kutoka kwa hiari yako?

Tumsubiri mwanae mmoja anajifanya Chadema saaaana ilhali wanakula fadhila za CCM atakuja tu kumwaga uharo wake
 
Huyu mzee ni mnafiki tu ,baada ya kuvimbiwa ndio anaanza kubwabwaja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…