Bwana Ndugai anahitaji msaada wa haraka wa saikolojia

Bwana Ndugai anahitaji msaada wa haraka wa saikolojia

Malisa too low for you kumuita Halima Mdee..Mzee Mdee..

Wewe Malisa kuna wengi tunakuheshimu

Unaweza kuandika hoja bila kuingia kwenye matusi ya mitandaoni...

Halima hata kama sasa kawa adui
Ana mchango wake na heshima yake..kama mwanamke na kama binadamu kwanza..

Msisahau mlivyomtukana Zitto kipindi kile
Leo ni mshirika wa upinzani hadi Tundu Lissu kaenda kumpigia kampeni jimboni kwake..

Kuna maisha baada ya siasa
Kumuita Halima Mzee Halima ni matusi? Au ni kejeli? Acha hizo mkuu, mzee ni heshima hata wewe twaweza kuita mzee The Boss
 
Kaandika Bibi Happy
MBOWE NI NANI?
Kwa hiyo Mbowe ni Kamati kuu ya CHADEMA? Au Mbowe aishurutishe kamati kuu?

Ngoja kwanza....
Kwamba Mdee alivunjika akiwa anazungumza na Mbowe? Au Bulaya ALIPIGWA na Mbowe hadi akazimia? Au Matiko alilazwa kisa alifumwa na Mbowe? Yaani MBOWE ni nani jamani hata hakamatiki akipiga hawa wanawake?

Kwamba Nusrat aliwekwa mahabusu na Mbowe sio? Kwamba Mbowe alimweka huko ili afie magereza? Wow! Kwamba Mbowe ANAMILIKI magereza, mahakama na wanasheria wote? Wow!

Sasa mkuu, mbona sijaelewa? Kwamba wabunge hawa wapewe nafasi kwa kuwa MBOWE amewanyanyasa? Kwamba ofisi ya BUNGE inawatambua kwa kuwa ndiyo ILIYOAMUA wapewe nafasi hizo?

Kama kweli wabunge hawa HAWAKUJITEUA na walitokana na uteuzi RASMI toka CHADEMA, je, haimaanishi kwamba CHADEMA ILIWAJALI? Kwa nini CHADEMA iwape nafasi halafu IWAFUKUZE uwanachama?

Je, kauli zako hizi zinathibitisha kuwa hawa wabunge HAWAKUTEULIWA na CHADEMA?
Nani aliyemtoa NUSRAT mahabusu? Kama ni CHADEMA ILIMTOA ILI AKAAPE, kwa nini huoni hili ni jambo jema? Kama CHADEMA walimtoa huko mahabusu, unataka kusema CHADEMA ndio wana nguvu ya kumtoa mahabusu yeyote wanayetaka? Hii inaleta picha gani kwa huu mhimili mkuu wa serikali?

Kwamba ALIYEMTOA Nusrat ili akaapishwe, alikuwa ANAMWEPUSHA na unyanyasaji ambao MBOWE aliufanya?

Basi, ni NANI huyo ALIYEMTOA AKAAPE ILI ASIFIE MAGEREZA kama alivyotaka Mbowe ?

Bado najiuliza, MBOWE NI NANI KATIKA NCHI HII? Spika anamlalamikia tu, hata hamfanyi kitu.

Aliyeelewa anieleweshe...
Its so confusing.
Job ndugai ameunajisi mhimili wa bunge, bunge limekuwa sawa na ng'ombe aliyeasiwa
 
Mimi hizo sababu zako zote natofautiana ila la msingi ni kwamba ndugai atajidhalilisha kama ataruhusu wabunge wasiokua na chama bungeni. Wanachohitajika kufanya chadema ni kulifahamisha bunge rasmi kuhusu kuwatimua chama hao wabunge wao. Tena chadema waweke wazi kwa wananchi kuhusu hatua hiyo kisha tuone kama ndugai hatawatimua kina halima bungeni. Isije kua janja na hila za mbowe na mnyima kuvunga na kufanya propagandakwa kumbe taarifa rasmi kwa ndugai hawajatoa wala hawatatoa.
Hili neno, barua iende kotekote, na wauthibitishie umma wa watanzania, maana nchi hii yawezekana, wanatuchezea COMEDY! 😀

Everyday is Saturday................................😎
 
Ni kweli bro msaada unahitajika lakini kwa taarifa za wataalam wa matibabu ya lile gonjwa sugu ni kwamba ikifikia "stage" ARV zikishazidiwa nguvu (stage ya moto inaitwa) mgonjwa anaanza kubwabwaja kila kimjiacho kinywani na mara nyingi anakuwa ni mtu wa hasira kali an visilani...tumsamehe tu kwani tayari watanzania wengi tunajitambua na kikubwa zaidi tunaelewa ila za watawala wa sasa
Kwa nini kukubali kukaa na Spika mgonjwa ambaye kumbe hata afya ya akili imeathirika kwa miaka mitano mizima kama vile nchi haina watu makini?
Watu wa CCM hata wao wanaathirika kuwa na Spika mgonjwa! Nao waliseme hili kwa faida ya taifa sio kunyamaza kwa vile anawakomoa Chadema. Kesho tukinyimwa msaada kwa sababu ya bunge bovu jee ni maumivu kwa Chadema pekee?
Tupaze sauti wote kwa pamoja NDUGAI JIUZULU ILI UTIBIWE, WEWE NI MGONJWA
 
Bwana Ndugai anahitaji msaada wa haraka wa saikolojia.

Malisa GJ

Mosi; Huu uchungu anaouonesha Ndugai sio wa Mzee Halima na wenzake kupigwa, ni uchungu wa kupoteza yale matrilioni ya wafadhili. Ameshaona dalili zote kwamba hata akiwalinda akina Mzee Halima na wenzake waendelee kuwa wabunge, wafadhili wanaweza kugomea kutoa yale matrilioni.

Pili; Mzee Halima na wenzake hawakupigwa kwa ajili ya Mbowe. Walipigwa kwa sababu ya kutetea haki zao. Walipotolewa Segerea askari magereza waliwapiga kama vibaka kwa sababu tu walienda kupokelewa na wafuasi wao. Mashinji alipokelewa na msafara wa wafuasi wa CCM wakiongozwa na Chakubanga lakini hakupigwa. Double standards. Kama kweli Ndugai ana uchungu angewakemea wale askari waliofanya unyama ule sio Mbowe.

Tatu; Mzee Halima na wenzake hawajafukuzwa bila kusikilizwa. Walipewa haki ya kusikilizwa (audi alteram partem) lakini wakakataa kuitumia. Waliitwa kwa maandishi kwenye kamati kuu ili wasikilizwe wakagoma. Sasa Bwana Ndugai alitaka chama kifanyeje? Hata mahakamani mtuhumiwa akikataa kujitetea bila sababu za msingi, mahakama hulazimika kuamua kwa kusikikiza upande mmoja.

Nne; Maamuzi ya Chadema hayakufanywa na Mbowe. Yalifanywa na Kamati kuu ambayo ina wajumbe zaidi ya 40. Ni ujinga kuamini wajumbe wote hawakua na sauti isipokua Mbowe peke yake. Ndugai elewa kwamba Mbowe sio kamati kuu ya Chadema.

Tano; kumbe Ndugai anajua Mzee Halima na mwenzake walipigwa hadi wakazimia pamoja na kuvunjwa mikono na askari magereza? Unyama huu aliwahi kuulaani popote? Aliwahi kumuita Kamishna Mkuu wa Magereza kwenye kamati za bunge ajieleze kwanini Askari wake walifanya unyama ule tena kwa wabunge wanawake? Au aliona ni sawa tu kwa sababu walikua Chadema. Leo wamefurushwa ndio anasikia uchungu.

Huu utaratibu wa mtu kuonewa lakini unakaa kimya kwa sababu sio wa chama chako sio ubinadamu kabisa. Ningemuona Ndugai ana hoja kama angekemea tukio lilipotokea. Sasa Mzee Halima ameshapona na kusahau ndio Ndugai anasikia uchungu leo? Haina tofauti na mkeo kulia kwa uchungu na kukuomba msamaha kwa sababu ya vita vya majimaji eti babu yake alishirikiana na wakoloni kuwapiga wazawa. Wendawazimu.!
Nalia Sana maana wengi hawajuwi Ila hii nidalili mbaya kuwahi tokea. Maana yote yametokea yameweka serikali yangu ktk Sura mbaya ya haki za kibinadam na utawala wa Sheria.
 
Kuna nchi ina spika bogus kama huyu? hivi na hao wanaotoa trilioni 2 ni wajinga kama spika?

Ukimsikiliza Ndugai ni kama anafanya hivyo ili kuwakomoa cdm, na anashindana na watu wa mitandaoni wanaompa ukweli mchungu. Kwa ujumla serikali hii inafanya kazi kushindana na cdm, na kuwakomoa watu wa mitandaoni mpaka wanageuka vituko.
 
Malisa too low for you kumuita Halima Mdee..Mzee Mdee..

Wewe Malisa kuna wengi tunakuheshimu

Unaweza kuandika hoja bila kuingia kwenye matusi ya mitandaoni...

Halima hata kama sasa kawa adui
Ana mchango wake na heshima yake..kama mwanamke na kama binadamu kwanza..

Msisahau mlivyomtukana Zitto kipindi kile
Leo ni mshirika wa upinzani hadi Tundu Lissu kaenda kumpigia kampeni jimboni kwake..

Kuna maisha baada ya siasa
Kumuhurumia msaliti kwasababu yoyote ile ni kujitafutia laana.
 
Kweli chadema ina watu wajinga sana!

Yani Malisa nae kajiunga na kigogo kumuita Halima mzee?

Historia inaonesha kwamba pale chadema kila mtu huwa anasurubiwa kwa wakati wake kulingana na nyakati!

Zitto pamoja na kupigana hadi jasho la damu lakini lilipokuja suala la maslahi ya Mbowe alikiona cha moto

Slaa pamoja na kuvunjika hadi mikono akipigania chadema lakini lilipokuja suala la maslahi ya Mbowe alikiona cha moto.

Sasa hivi ni zamu ya Mdee!

Huyu Malisa ni kidagaa tu pale chadema, ningekuwa mimi ningejikalia kimya tu bila kumkejeli Halima.
 
Malisa too low for you kumuita Halima Mdee..Mzee Mdee..

Wewe Malisa kuna wengi tunakuheshimu

Unaweza kuandika hoja bila kuingia kwenye matusi ya mitandaoni...

Halima hata kama sasa kawa adui
Ana mchango wake na heshima yake..kama mwanamke na kama binadamu kwanza..

Msisahau mlivyomtukana Zitto kipindi kile
Leo ni mshirika wa upinzani hadi Tundu Lissu kaenda kumpigia kampeni jimboni kwake..

Kuna maisha baada ya siasa
Kabisa mkuu!

Malisa ni kidagaa tu pale chadema ila anajitia kimbelembele.
 
Mi namuonaga Ndungai kama mwanasesere tu, hana jipya. Kuwepo kwa wabunge wa Chadema kwa sasa kunawasaidia CCM kuliko unavyowasaidia chadema, bora wakose hizo ruzuku. Wajue kuwa demokrasia ina gharama. apambane na chama chake huko aachane na chadema.
 
Kuna jambo moja kati ya mawili mheshimiwa wetu huyu inapaswa ayafafanue.
Mosi; aseme kama anakataa hawa 19 kufutwa uanachama wa CHADEMA;ama
Aseme kuwa hawa 19 wataendelea na ubunge wao japokuwa wamefutiwa uanachama huko walikokuwa.
Namaliza kwa swali kuwa, hivi inawezekana katiba yetu sio andishi tena bali ya matamshi tu?
 
Mimi hizo sababu zako zote natofautiana ila la msingi ni kwamba ndugai atajidhalilisha kama ataruhusu wabunge wasiokua na chama bungeni. Wanachohitajika kufanya chadema ni kulifahamisha bunge rasmi kuhusu kuwatimua chama hao wabunge wao. Tena chadema waweke wazi kwa wananchi kuhusu hatua hiyo kisha tuone kama ndugai hatawatimua kina halima bungeni. Isije kua janja na hila za mbowe na mnyima kuvunga na kufanya propagandakwa kumbe taarifa rasmi kwa ndugai hawajatoa wala hawatatoa.
Ila wee jamaa nawe huna tofauti na ndugai watu wamefukuzwa na chama na kamati kuu imetoa maamuzi bado unasema janja ya mbowe na mnyika?
 
Back
Top Bottom