Bwawa la Mwalimu Nyerere na athari kwa vijiji vilivyopo bondeni mwa bwawa hilo

Bwawa la Mwalimu Nyerere na athari kwa vijiji vilivyopo bondeni mwa bwawa hilo

Haiwezekani kuwa sababu ni kuwashwa mtambo mmoja lazima sababu itakuwa ni mvua chini au juu ya bwawa. Ikiwa maji yamejaa bwawani na mvua zinazidi inabidi wafungulie maji yamwagige na hii athari hata lisingekuwepo bwawa ingekuwepo.
 
Juzi niliona katika taarifa ya habari ya ITV wananchi wa vijiji mbalimbali bondeni mwa Bwawa la Mwalimu Nyerere wakihaha kuokoa maisha yao baada ya kuzingirwa na maji ya mto Rufiji. Hii inatokana na kujaa kwa bwawa hivyo kulazimisha kufungulia maji kutoka bwawani.

Pia tumekwisha fahamishwa kuwa mtambo mmoja kati ya tisa ya kuzalisha umeme bwawani hapo umewashwa na kuzalisha MW 235. Kwa hiyo bado mitambo nane ambayo baada ya kukamilika kufungwa itawashwa na bwawa kuanza kuzalisha MW 2115. Hakika ni jambo jema sana.

Wasiwasi ni kuwa kama kuwashwa kwa mtambo mmoja tu kumesambaratisha wanavijiji na kuanza kuhama makazi yao, hali itakuwa vipi pale mitambo yote tisa itakapowashwa? Je, vijiji vilivyopo bondeni mwa Bwawa vitaendelea kuwepo? Je, wananchi wamekwisha taarifiwa lo lote kuhusu hali ya baadaye ya makazi na mashamba yao?

Ikumbukwe kuwa mitambo yote itakapokuwa inafanya kazi hakutakuwa na kupungua maji tena kwa kuwa maji yatafunguliwa kwa kiwango kile kile mwaka mzima.
Uliza jambo kama hulijui. Kuwashwa kwa mtambo hakuna uhusiano wowote na maji kufurika katika vijiji vilivyopo chini ya Bwawa. Ni kwa Bwawa limejaa na linatishia kuvunja kingo hivyo ni kawaida maji yanapojaa kupita kiasi kufunguliwa kiasi ili yapungue kwa ajili ya usalama wa kingo za bwawa. Hata Mtera na Kidatu maji yakijaa kupita kiasi huwa yanafunguliwa kwa utaratibu ili kunusuru bwawa kupasuka. Hivyo, hayo maji hayatokani na kuwashwa kwa mtambo.
 
Uliza jambo kama hulijui. Kuwashwa kwa mtambo hakuna uhusiano wowote na maji kufurika katika vijiji vilivyopo chini ya Bwawa. Ni kwa Bwawa limejaa na linatishia kuvunja kingo hivyo ni kawaida maji yanapojaa kupita kiasi kufunguliwa kiasi ili yapungue kwa ajili ya usalama wa kingo za bwawa. Hata Mtera na Kidatu maji yakijaa kupita kiasi huwa yanafunguliwa kwa utaratibu ili kunusuru bwawa kupasuka. Hivyo, hayo maji hayatokani na kuwashwa kwa mtambo.
Soma hoja siyo kudandia! Sijasema kuwashwa kwa hicho kinu kimoja kumesababisha mafuriko! Lini ulisikia kufunguliwa kwa Mtera na Kidatu kumesababisha mafuriko?
 
Kama wananchi wanapata athari ni vyema wakawalipa fidia
 
Wajichunge siku lisije poromoka😷 waweke mpango mzuri maana maji huwa yananguvu na ujenzi wetu huwa janja janja nimingi kila miradi watu lazima wapige iyo piga uwa laziiima....
 
Wewe nadhani huelewi hoja! Ili turbines zizunguke unatakiwa ufungulie maji katika mahandaki yake. Maji yakisha zungusha hizo turbines yanaendelea katika mkondo wake na kutumika katika shughuli nyingine. Kwa sasa wamefungulia handaki moja ukichanganya na yaliyofunguliwa kupunguza maji bwawani yamesabisha mafuriko. Hoja ni kuwa kama handaki moja limeleta tafrani, vipi mahandaki yote tisa yakifunguliwa.
Iko hivi, maji "yaliyofunguliwa" hayatumiki kuzungusha huo mtambo bali yanatoka huru ili kupunguza ujazo bwawani, yanayopita kwenye huo mtambo uliowashwa yanaendelea na safari ya kawaida mtoni kama njia zake zilivyowekwa, hivyo wakiwasha mitambo yote tisa maji hayatafunguliwa kupunguza ujazo bali yatapita kwenye turbines zote na kuendelea na safari ya baharini kama kawaida

Sent from my ZTE T1002 using JamiiForums mobile app
 
Najaribu kuwaza uwezo wako wa kuelewa! Maji yamefunguliwa kwa sababu Bwawa limejaa ili kupunguza maji. Lakini pia kuna maji yameelekezwa katika kuendesha mtambo uliowashwa. Hii imesababisha mafuriko bondeni. Sasa hoja hapa ni kuwa je maji yakifunguliwa kuwasha mitambo yote tisa hali ya mafuriko itakuaje?
Maji yaliyofunguliwa ni mengi kuliko maji yatayotumika kusukuma mitambo yote Tisa
 
Hao watakuwa wameshajulishwa kinachoendelea. Kama bado mashirika ya sheria za mazingira yaende kuwasaidia kisheria. Sie tunataka umeme tu.
 
Samahani jamani, kuuliza si ujinga.

Kwa hali iliyopo hivisasa yaonekana maji kusimama ama kupungua mto Rufiji, Ninapotaka kujua kuwa je yatafunguliwa tena?

Samahani mwenye ufahamu sahihi kutoka huko kwenye chanzo cha maji haya (STIGO) naomba anisaidie
 
Kila mtambo unahitaji kiasi fulani cha maji ili ufanye kazi. Kwa sasa wamefungulia maji kwa mtambo mmoja na tayari mashamba ya wanavijiji yamefurika na watu kuhama makazi yao. Kwa hiyo maji yataendelea kuongezeka kadri mitambo inavyowashwa.
Kabla ya kujengwa bwawa maji yalikuwa yanapita wapi? Wakizidiwa na maji tutawahamishia msomera
 
Kuna mshenzi mmoja alisema kujenga bwawa ni upuuzi kwani maji yakujaza bwawa hakuna kutokana na mabadiliko ya tabianchi, mie naona tujenge bwawa la pili liwe kubwa kuliko hilo
 
Ilitakiwa kujengwa bwawa la pili kuvuna maji ya ziada yasiishie yote bahari ya Hindi.

Maji hayo ya bwawa la pili yangetumika kwa kilimo cha kumwagilia na maji kwa huduma za kijamii
 
Tayari walishapewa elimu nzima kuhusu kinachoendelea!

Je, wametafutiwa makazi mbadala? Wameandaliwa maeneo ya kufanyia shughuli zao za kiuchumi kufidia maeneo watakayoyapoteza.

Kama hayo yote yalikwishafanyika, kwa nini bado wapo kwenye maeneo hayo hatarishi kwa maisha yao na shighuli zao za kiuchumi?
 
Juzi niliona katika taarifa ya habari ya ITV wananchi wa vijiji mbalimbali bondeni mwa Bwawa la Mwalimu Nyerere wakihaha kuokoa maisha yao baada ya kuzingirwa na maji ya mto Rufiji. Hii inatokana na kujaa kwa bwawa hivyo kulazimisha kufungulia maji kutoka bwawani.

Pia tumekwisha fahamishwa kuwa mtambo mmoja kati ya tisa ya kuzalisha umeme bwawani hapo umewashwa na kuzalisha MW 235. Kwa hiyo bado mitambo nane ambayo baada ya kukamilika kufungwa itawashwa na bwawa kuanza kuzalisha MW 2115. Hakika ni jambo jema sana.

Wasiwasi ni kuwa kama kuwashwa kwa mtambo mmoja tu kumesambaratisha wanavijiji na kuanza kuhama makazi yao, hali itakuwa vipi pale mitambo yote tisa itakapowashwa? Je, vijiji vilivyopo bondeni mwa Bwawa vitaendelea kuwepo? Je, wananchi wamekwisha taarifiwa lo lote kuhusu hali ya baadaye ya makazi na mashamba yao?

Ikumbukwe kuwa mitambo yote itakapokuwa inafanya kazi hakutakuwa na kupungua maji tena kwa kuwa maji yatafunguliwa kwa kiwango kile kile mwaka mzima.
Tusibiri Lema na Mdude kwanza wanasemaje kuhusu hili jambo
 
Kwanini yaongezeke?
Duh! Mnyalu unajiaibisha kweli. Ina maana huelewi kabisa mabwawa ya kuzalishia umeme yanavyofanya kazi?

Haya, ngoja nikupeleke taratibu na shule hii ya darasa la nne:

Ili kuwa na maji mengi ya kutosha kuzalishia umeme kwa muda mrefu, mabwawa makubwa huwa yanajengwa, mara nyingi kwa kuzuia mito inayotiririsha maji. Hiyo huwa inafanyika kwa kuzuia mkondo wa maji wa asili.

Wakati wa uzalishaji umeme, milango ya bwawa huwa inafunguliwa. Ukifunguliwa mlango mmoja, maji yatakayotoka yatakuwa kiasi fulani. Na huko yanakoelekea wahusika wataona. Ukifungua mlango wa pili, na wa tatu, maji yanayotoka yatazidi kuongezeka huko yanakoenda, na kama tahadhari hazikuwekwa sawasawa, yanaweza kutokea mafuriko yanayozidi hata ya mvua, na kusababisha maafa makubwa. Hata ikitokea kwa bahati mbaya kingo za bwawa zikavunjika, ni balaa kubwa, kama yanakoelekea maji kuna makazi ya watu au wanyama wa porini au viumbe vingine.
 
Back
Top Bottom