Bwawa la Mwalimu Nyerere na athari kwa vijiji vilivyopo bondeni mwa bwawa hilo

Bwawa la Mwalimu Nyerere na athari kwa vijiji vilivyopo bondeni mwa bwawa hilo

Juzi niliona katika taarifa ya habari ya ITV wananchi wa vijiji mbalimbali bondeni mwa Bwawa la Mwalimu Nyerere wakihaha kuokoa maisha yao baada ya kuzingirwa na maji ya mto Rufiji. Hii inatokana na kujaa kwa bwawa hivyo kulazimisha kufungulia maji kutoka bwawani.

Pia tumekwisha fahamishwa kuwa mtambo mmoja kati ya tisa ya kuzalisha umeme bwawani hapo umewashwa na kuzalisha MW 235. Kwa hiyo bado mitambo nane ambayo baada ya kukamilika kufungwa itawashwa na bwawa kuanza kuzalisha MW 2115. Hakika ni jambo jema sana.

Wasiwasi ni kuwa kama kuwashwa kwa mtambo mmoja tu kumesambaratisha wanavijiji na kuanza kuhama makazi yao, hali itakuwa vipi pale mitambo yote tisa itakapowashwa? Je, vijiji vilivyopo bondeni mwa Bwawa vitaendelea kuwepo? Je, wananchi wamekwisha taarifiwa lo lote kuhusu hali ya baadaye ya makazi na mashamba yao?

Ikumbukwe kuwa mitambo yote itakapokuwa inafanya kazi hakutakuwa na kupungua maji tena kwa kuwa maji yatafunguliwa kwa kiwango kile kile mwaka mzima.
hizo ni athari za kawaida kwenye miradi mikubwa kama huu 🐒

na bahati nzuri dosari, kasoro, hatari na athari zinazoendelea kujionyesha zinadhibitika, zinarekebishika, zinaepukika na zaidi sana zinazuilika; na kwahivyo hakuna haja ya kuwa na wasiwasi 🐒

pongezi sana kwa Rais, Comrade Dr SSH, kiongozi wetu, ambae sote tunampenda sana, kwa kusimamia kikamilifu ukamilishwaji wa mradi huu muhimu sana, kwa maslahi mapana ya Taifa na Watanzania wote 🐒
 
Iko hivi, maji "yaliyofunguliwa" hayatumiki kuzungusha huo mtambo bali yanatoka huru ili kupunguza ujazo bwawani, yanayopita kwenye huo mtambo uliowashwa yanaendelea na safari ya kawaida mtoni kama njia zake zilivyowekwa, hivyo wakiwasha mitambo yote tisa maji hayatafunguliwa kupunguza ujazo bali yatapita kwenye turbines zote na kuendelea na safari ya baharini kama kawaida

Sent from my ZTE T1002 using JamiiForums mobile app

Maji yaliyofunguliwa kutokana na bwawa kujaa na yale yaliyofunguliwa kwenye mlango wa turbine moja, mwishowe ni lazima yanaingia kwenye mkondo mmoja wa maji.

Swali ambalo ni muhimu la kujiuliza, je, milango yote 9 ikifunguliwa kwaajili ya kuzungusha turbines zote, unaamini milango yote 9 kwa pamoja itatoa maji pungufu kuliko overflow iliyoruhusiwa kutoka? Kama milango yote ikifunguliwa, itatoa maji mengi zaidi kuliko overflow iliyoruhusiwa, tarajia madhara makubwa zaidi ya haya ya sasa. Hali hii ya sasa ni wake up call kwa wahusika. Na siyo jambo la ajabu. Mara nyingi miradi mipya, pamoja na jitihada zote za tahadhari, ikifika kwenye uhalisia, aghalabu hutakosa kukumbana na mambo ambayo hayakutarajiwa, yanayotakiwa kufanyiwa kazi.
 
Je, wametafutiwa makazi mbadala? Wameandaliwa maeneo ya kufanyia shughuli zao za kiuchumi kufidia maeneo watakayoyapoteza.

Kama hayo yote yalikwishafanyika, kwa nini bado wapo kwenye maeneo hayp hatarishi kwa maisha yao na shighuli zao za kouchumi?
Wacha nikuunganishe na waziri mwenye dhamana!
 
Duh! Mnyalu unajiaibisha kweli. Ina maana huelewi kabisa mabwawa ya kuzalishia umeme yanavyofanya kazi?

Haya, ngoja nikupeleke taratibu na shule hii ya darasa la nne:

Ili kuwa na maji mengi ya kutosha kuzalishia umeme kwa muda mrefu, mabwawa makubwa huwa yanajengwa, mara nyingi kwa kuzuia mito inayotiririsha maji. Hiyo huwa inafanyika kwa kuzuia mkondo wa maji wa asili.

Wakati wa uzalishaji umeme, milango ya bwawa huwa inafunguliwa. Ukifunguliwa mlango mmoja, maji yatakayotoka yatakuwa kiasi fulani. Na huko yanakoelekea wahusika wataona. Ukifungua mlango wa pili, na wa tatu, maji yanayotoka yatazidi kuongezeka huko yanakoenda, na kama tahadhari hazikuwekwa sawasawa, yanaweza kutokea mafuriko yanayozidi hata ya mvua, na kusababisha maafa makubwa. Hata ikitokea kwa bahati mbaya kingo za bwawa zikavunjika, ni balaa kubwa, kama yanakoelekea maji kuna makazi ya watu au wanyama wa porini au viumbe vingine.
Kwahiyo Arab Contractor wameelekeza milango ya mitambo kwenye makazi ya Watu?
 
Taarifa ya habari ya Ijumaa usiku kutoka Tanesco ni kuwa umwagaji wa maji utaendelea hadi mwezi Mei tarehe 15 hivyo wananchi wametahadharishwa kuwa wahame kabisa kutoka bondeni.
 
Juzi niliona katika taarifa ya habari ya ITV wananchi wa vijiji mbalimbali bondeni mwa Bwawa la Mwalimu Nyerere wakihaha kuokoa maisha yao baada ya kuzingirwa na maji ya mto Rufiji. Hii inatokana na kujaa kwa bwawa hivyo kulazimisha kufungulia maji kutoka bwawani.

Pia tumekwisha fahamishwa kuwa mtambo mmoja kati ya tisa ya kuzalisha umeme bwawani hapo umewashwa na kuzalisha MW 235. Kwa hiyo bado mitambo nane ambayo baada ya kukamilika kufungwa itawashwa na bwawa kuanza kuzalisha MW 2115. Hakika ni jambo jema sana.

Wasiwasi ni kuwa kama kuwashwa kwa mtambo mmoja tu kumesambaratisha wanavijiji na kuanza kuhama makazi yao, hali itakuwa vipi pale mitambo yote tisa itakapowashwa? Je, vijiji vilivyopo bondeni mwa Bwawa vitaendelea kuwepo? Je, wananchi wamekwisha taarifiwa lo lote kuhusu hali ya baadaye ya makazi na mashamba yao?

Ikumbukwe kuwa mitambo yote itakapokuwa inafanya kazi hakutakuwa na kupungua maji tena kwa kuwa maji yatafunguliwa kwa kiwango kile kile mwaka mzima.
Umeeleza vzr ila watu hawakuelewi. Cha kushangaza ni kwamba tahadhari imetolewa wakati maji yameshafunguliwa ili hali ilitakiwa kutolewa kabla. Jambo lingine tuliambiwa bwawa litasaidia kupunguza mafuriko mbona sasa lenyewe ndio linaleta mafuriko?
 
Taarifa imetolewa kwamba maji yamefunguliwa kwa Sababu mitambo mingine bado haijawashwa

Very simple 😂
System ya Hydro Electric Power ni nguvu ya maji ndio inatumika kuzungusha hizo motors kwahio kunakuwa na catchment area kubwa ili maji yote katika safari zake za kushuka / kutembea yapite kwenye hizo mashine ili kuzalisha umeme kwahio yakishapita / zalisha huo umeme yanaendelea na safari zake...

Na kama ili kuzalisha umeme zinahitajika pipa kumi basi hizo pipa kumi lazima ziwe zinapita katika sehemu husika continously....

The only way nyingine ya kufanya badala ya hii kuwa generator pekee inaweza pia ikawa battery - wakati matumizi madogo ule umeme wa ziada unatumika kuyarudisha juu baadhi ya maji (labda pipa moja) ili umeme ukihitajika mwingi hilo pipa moja na nyingine zile tano ziweze kuendelea kupita na kuzalisha umeme


NB: (unless kama haya maji yanayoleta tafrani ni yale ambayo yameoverflow hence kwenda mkondo mwingine tofauti na ule ambao yatakuwa yanapita kuendelea na safari zake) and if that is the case itakuwa ni uzembe katika ujenzi
 
Umeeleza vzr ila watu hawakuelewi. Cha kushangaza ni kwamba tahadhari imetolewa wakati maji yameshafunguliwa ili hali ilitakiwa kutolewa kabla. Jambo lingine tuliambiwa bwawa litasaidia kupunguza mafuriko mbona sasa lenyewe ndio linaleta mafuriko?

Lisingefunguliwa mafuriko yangetokea?
 
K
Kila mtambo unahitaji kiasi fulani cha maji ili ufanye kazi. Kwa sasa wamefungulia maji kwa mtambo mmoja na tayari mashamba ya wanavijiji yamefurika na watu kuhama makazi yao. Kwa hiyo maji yataendelea kuongezeka kadri mitambo inavyowashwa.
Kwa nivyoelewa mimi, Kwanza bwawa ni shimo la kukusanyia maji maji toka kwenye mto/mito,
Kwahiyo likichimbwa haliruhusu maji kuendea na safari yake.

Hivyo bwawa la mwalimu nyerere, kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha, limajaa mpaka kiasi kinachohitajika na bado maji, yanazidi kuingia, hivyo inalazimika kuyapunguza kwa kuafungulia.

Na wala hayafunguliwi kwa sababu mtambo unafanya kazi.
 
Juzi niliona katika taarifa ya habari ya ITV wananchi wa vijiji mbalimbali bondeni mwa Bwawa la Mwalimu Nyerere wakihaha kuokoa maisha yao baada ya kuzingirwa na maji ya mto Rufiji. Hii inatokana na kujaa kwa bwawa hivyo kulazimisha kufungulia maji kutoka bwawani.

Pia tumekwisha fahamishwa kuwa mtambo mmoja kati ya tisa ya kuzalisha umeme bwawani hapo umewashwa na kuzalisha MW 235. Kwa hiyo bado mitambo nane ambayo baada ya kukamilika kufungwa itawashwa na bwawa kuanza kuzalisha MW 2115. Hakika ni jambo jema sana.

Wasiwasi ni kuwa kama kuwashwa kwa mtambo mmoja tu kumesambaratisha wanavijiji na kuanza kuhama makazi yao, hali itakuwa vipi pale mitambo yote tisa itakapowashwa? Je, vijiji vilivyopo bondeni mwa Bwawa vitaendelea kuwepo? Je, wananchi wamekwisha taarifiwa lo lote kuhusu hali ya baadaye ya makazi na mashamba yao?

Ikumbukwe kuwa mitambo yote itakapokuwa inafanya kazi hakutakuwa na kupungua maji tena kwa kuwa maji yatafunguliwa kwa kiwango kile kile mwaka mzima.
Elimu ilitolewa kabla ya kuanza kazi ya ujenzi. Watu ni wabishi tu kama vile wa bonde la msimbazi . Acha wakione watakimbia
 
Mkuu wa wilaya ya Rufiji Bw. Edward Gowele amewataka watu wote walio bondeni mwa Bwawa la Mwalimu Nyerere kuhama haraka kwa kuwa sasa Tanesco wamelazimika kufungulia milango 4 baada ya bwawa kuzidiwa na maji. Maji yanayotiririka baada ya kufunguliwa ni kama mita za ujazo 7500 kwa sekunde.
 
Back
Top Bottom