CAF Champions League: Al Ahly vs Yanga 20/04/16

CAF Champions League: Al Ahly vs Yanga 20/04/16

Kwa mara ya kwanza nilikuwa naishabikia yanga bila kujijua, uzalendo ni shida!
Yanga wazembe sana, walianza kujilinda mno kusubiri matuta.
Wamejitahidi ila wameniudhi, waarab walikuwa wanafungika hawa! Tungetoa gundu maana ktk matuta kina kitu kiliniambia yanga angepita. Tooo bad, sekunde ya mwisho?? Dah!
 
Wachawi hawa waarabu, lazima kuna ndumba wanatumiaga.
 
Yanga bana, hivi muda wote mlikaa mnasuburi ushindi?

Ha ha ha!
 
Asante saaana tena sana timu bora Afrika, bonge la timu hatari sana na moto wa kuotea mbali hasa kwa wazee wa kupanda ndege, wazee wa kimataifa.
Hatuongei tu from nowhere, takwamu zipo ee! Sante sana na usiku mnono.
 
Mpira tumecheza, asanteni wote mliotuunga mkono. Tunashuka kwenye mtoano wa kombe la Shirikisho. Safari inaendelea.
kuna namna walibweteka sekunde za hatari kwa kudhani shughuli inakwenda kwenye viazi but its poor marking hadi mtu anapiga free header ndio beki anafika
 
nakosa pumzi ya kutosha,na mwili wa anaekabananae upo vizuri saana..
Yaani wachezaji wetu miili na lishe naona kama tatizo,maana hata fitness haipo vizuri kabisaa.
Halafu kuna kipindi wanajichanganya sana,wanagongana kwenye kukaba,bado tatizo lipo ila ngoja tuangalie dakika tano za mwanzo
Ni sehemu ya mchezo kaka. Ila Yanga wanasitahili sifa tena nyingi. Wamecheza na kuonyesha hata wamisri walikuwa hawana uhakika wa kushinda moja kwa moja.
 
Back
Top Bottom