CAF Yaitaja simba kuwa klabu namba 5 kwa utajiri barani afrika

CAF Yaitaja simba kuwa klabu namba 5 kwa utajiri barani afrika

Duh..azama hii ambayo inashindwa kulipa mishahara ya Hadhi kwa wachezaji wake?? Hii ambayo siku hizi haina match allowance? Au ipi hiyo?
Uwekezaji wa Azam fc hakuna team ya bongo iaugusa,Hata kama hayo mengine yapo
 
Mnaosema Arsenal, Bayern & co. hazina viwanja naomba niwaeleweshe.

Kwa suala la Inter Milan ni kweli wanatumia uwanja wa Manispaa ya Milano (San Siro/Guisseppe Meaza)

Lakini kwa vilabu kama Arsenal, Bayern München, Juventus Turin, Atlanta United, Stoke City, Brighton & Have Albion, Newcastle United, Vfl Wolfsburg and Co. Wanauza STADIUM NAME RIGHTS kwa companies mbalimbali.
Arsenal na Fly Emirates walishirikiana kujenga kiwanja yani Arsenal Stadium lakini sharti la mshirika na mikataba waliyowekeana na Arsenal Plc. Ni Fly Emirates ku-hold Stadium name rights mpaka pale gharama walizotumia zitaporudi na ilianza effectively 2006 hadi 2014 deni lilikwisha. (Ikumbukwe pia walilipia gharama za Kits/Jersey sponsor from 2006 hadi 2016) 2015 Emirates alilipa pesa kununua Stadium name rights zamu hii ikuchukia name rights kwa 7 years pia akachukua Kits/Jersey kwa mara nyingine.

Viwanja vingine kampuni mbalimbali zilijenga na nyingine kununua jina la uwanja.
Bayern München - Allianz
Juventus Turin - Allianz (Ulikuwa ikiitwa Juventus Stadium, 2016 Allianz walichukua name rights)
Atlanta United - Mercedes-Benz Arena (Mercedes-Benz walishirikiana kujenga na Atlanta Insurance, Atlanta City na Atlanta United)
Vfl Wolfsburg - VolksWagen (Naming rights)
Stoke City - bet365 (Naming rights, kabla ya hapo Britannia walikuwa ndio wamechukua rights)
Brighton & Hove Albion (AMEX alirekebisha na kuchukua naming rights)
Newcastle United (SportDirec ya Mike Ashley mmiliki, ilichukua naming rights bila mkataba hadi leo Newcastle inasema haikuuza jina la uwanja bali mmiliki hakuelewa mkataba) na vilabu vingine vingi.

Ni sawa leo hii Metl Group (Mo) ajenge uwanja kwa makubaliano na Simba lakini uitwe Metl Stadium kwa kipindi cha miaka 5 baada ya mkataba aanze kurupia 265M kwa mwaka kuendelea kuitwa Metl Stadium.
 
Hata uwanja wa mazoezi haina pia ofisi mbovu mbona mnajidanganya sana Watanzania!!
 
Hata uwanja wa mazoezi haina pia ofisi mbovu mbona mnajidanganya sana Watanzania!!
 
Fake news
Hawajui how to calculate the clubs worthiness hao ….ngoja tuwaache..kama walivyo
 
Mie mshabiki wa simba lakini sishabikii upuuzi. Huo utajiri wa simba upon kwenye nini?. Simba INA kitega uchumi kipi zaidi ya lile jengo LA kariakoo ambalo thamani yake haizidi mil 500?. Tuache ushabiki maandazi. Angalau Singida United wanamilili Mashamba ya Alizeti. Kwa umri wa simba, ilipaswa imiliki mabasi ya mwendokasi, boti za kwenda zenji wanda vya vifaa vya michezo, Msimbazi centre, mabasi ya mikoani mfano Simba luxury coach, chuo kikuu cha michezo( Simba University of Sports and Games),_Shule na hospitali. Simba international school and Simba Medical centre.
Ni kweli ndugu kushabikia upuuzi hapana ! Simba ya Tano ! Mh basi hizi Timu nyingine zikoje FC lUPOPo,VITA ,eL MEREKH,Timu za Libya ,Tunisia,Algeria,Nigeria,Cameruni au Angola .haya ni matango porui
 
Hiyo ya kuwa klabu tajiri namba 5, nakataa kwa kipi hasa mpaka klabu yangu kipenzi iwe namba 5, zaidi ya kighorofa cha kariakoo na ule uwanja wetu usiokamilika hata kwa asilimia 25, kuna vilabu vimewekeza kichizi, ila nimeiona hii kuwa simba ni klabu bora namba 30 kwa bara la afrika.
mrs_omog28-20190223-0001.jpeg


Sent using my nokia ya tochi
 
Back
Top Bottom