CAF yamfungia mechi 8 Kocha wa Taifa Stars, huku TFF ikimsimamisha. Aliishutumu Morocco kwa kupanga mechi

Yeye na TFF wamejaza wachezaji wa ligi daraja tatu ulaya ili mradi timu ionekane ina wachezaji kutoka ulaya halafu anaanza kulaumu wengine,nchi hii siasa zinaharibu kila sekta.
Haji anachezea daraja la 5 Ben starke anachezea daraja la 7.

Hata sijui alitumia kigezo gani kuwaita .
 
Tatizo ninaloona ni Taifa Stars kuingiliwa mno na wanasiasa. Kwa mfano siwezi kuelewa kabisa kulikuwa na sababu gani ya Waziri kuwachosha wachezaji masaa mawili kwa nasaha zake..!!!... wachezaji wanatakiwa kula, kufanya mazoezi na kupumzika kwa wakati. Hayo masaa mawili yalikuwa kwenye ratiba ya wachezaji?? Ile kamati ya hamasa ilikuwa ya kazi gani? Wangesema wanalipia mashabiki kindakindaki kwenda kushangilia ningeweza kuelewa. Mtu kama Seven Mosha atamhamasisha nani kwenye football? Siku nyingine tuilinde sana STARS dhidi ya wanasiasa.
 
Ilikuwaje kocha akatoa kauli kama hiyo anamaanisha Morocco walitumia fitna kutufunga ama?
 
Edition zingine waende wachezaji wa ndani tu, hao wa nje hakuna cha maana wanachokiongeza zaidi ya weupe.wa ngozi zao. Ushoga mtupu
 
Ilikuwaje kocha akatoa kauli kama hiyo anamaanisha Morocco walitumia fitna kutufunga ama?
Alisema kabla ya mechi..
na hata Rais wa TFF hakukanusha kivile.. akasema hata hapa bongo Azam ndiyo wana amua muda wa kucheza game.. lakin pia akasema ni kweli ule muda una wa favor wao Morocco..
 
warudi tu tuendeleze gurudumu la maandamano na Chadema waachane na mpira hawauwezi p…mbavu zao 😏
 
Tunafanyaje? Tumtimue.
 
Alisema ameenda kujifunza kwahiyo tayari ameshajifunza.

Mpaka Tff waje watu wenye malengo bila hivyo Tanzania itabaki kichwa cha mwendawazimu Kama alivyosema Mzee Mwinyi.
Mkuu Tff wanakosa gani ? Chama cha mpira ni msimamizi wa mchezo wa mpira , jukumu la kutengeneza wachezaji ni jukumu la vilabu vya mpira, ukiangalia wachezaji wetu ni sawa na Kuku wa kienyeji hawajui kesho yao watakula nini na chakula watakipata wapi, tofauti na kuku wanaofugwa kitaalamu. Mchezaji anacheza Simba lakini haijulikani tokea utoto wake kakelewa Academy ipi.
 
CCM waache kufanya siasa kwenye michezo kama kweli wanataka mafanikio wawekeze kwenye michezo maana viwanja wanavyo kwanini wasianzishe Academy zao kwasababu viwanja wanavyo, kazi yao kukusanya na kuchangishana pesa na kugawana, ukiangalia nchi mfano Senegal, Nigeria kwenye mechi zao unawaona waki Mama na vijana wakishangilia timu zao wakiwa wamevalia sare, siyo sisi Raisi anatoa tiketi za bure kwenda kuishangilia Taifa star ukiangalia uwanja washangiliaji hawapo.
 
Kuna ugomvi wa asili algeria bs mprroco ameuhamishia k2enye soka.....zile.nchi hawapatani kabisaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…