CAG Kichere, kwanini uwaite wastaafu Mizigo wakati hela yao ndio imesimamisha NHIF kabla kuingia viwavi jeshi kukopeshana?

CAG Kichere, kwanini uwaite wastaafu Mizigo wakati hela yao ndio imesimamisha NHIF kabla kuingia viwavi jeshi kukopeshana?

mgt software

JF-Expert Member
Joined
Nov 1, 2010
Posts
13,778
Reaction score
7,145
Kwako kichele CAG

Nimeshangazwa na kusikitishwa na pendekezo la CAG Kichere kuwa wastaafu wanauwekea mzigo mfuko wa Bima ya Afya (NHIF) kwa kuendelea kupokea huduma za mfuko huo huku wakiwa hawachangii. Nimesikitika kwa sababu Kichere na genge lake wanajua tatizo linalousibu mfuko limetokea wapi. Kufanya anavyofanya CAG ni sawa na mtu kujificha kwenye shamba la karanga.

Serikali yetu ilivyo ya ajabu inaweza kununua ushauri wake na kesho sheria ikarekebishwa na wastaafu wakaondolewa kwenye mafao. Likitokea hilo wala msishangae wabunge wetu watalipitisha kama wanavyofanya kwa sheria zote kandamizi wanazoendelea kupitisha na Rais atayawekea sahihi kesh yake.

Kichere nimemshangaa sana kwa sababu nchini Morishasi kila mzee analipwa pensheni na anayefikisha miaka 100 pensheni yake inakuwa kubwa zaidi. Iweje CAG na genge lake wapendekeze wazee kunyimwa huduma ili wafe haraka au anashrikiana na wenye kikokotoo chao wastaafu waondoke mapema 67% yao ibakie kwenye mfuko?

Natamani marekebisho haya nayo yafanyike kabla ya uchaguzi ujao labda Mapambazuko yatawafikia wadanganyika wote.
 
Kwako kichele CAG

Nimeshangazwa na kusikitishwa na pendekezo la CAG Kichere kuwa wastaafu wanauwekea mzigo mfuko wa Bima ya Afya (NHIF) kwa kuendelea kupokea huduma za mfuko huo huku wakiwa hawachangii. Nimesikitika kwa sababu Kichere na genge lake wanajua tatizo linalousibu mfuko limetokea wapi. Kufanya anavyofanya CAG ni sawa na mtu kujificha kwenye shamba la karanga.

Serikali yetu ilivyo ya ajabu inaweza kununua ushauri wake na kesho sheria ikarekebishwa na wastaafu wakaondolewa kwenye mafao. Likitokea hilo wala msishangae wabunge wetu watalipitisha kama wanavyofanya kwa sheria zote kandamizi wanazoendelea kupitisha na Rais atayawekea sahihi kesh yake.

Kichere nimemshangaa sana kwa sababu nchini Morishasi kila mzee analipwa pensheni na anayefikisha miaka 100 pensheni yake inakuwa kubwa zaidi. Iweje CAG na genge lake wapendekeze wazee kunyimwa huduma ili wafe haraka au anashrikiana na wenye kikokotoo chao wastaafu waondoke mapema 67% yao ibakie kwenye mfuko?

Natamani marekebisho haya nayo yafanyike kabla ya uchaguzi ujao labda Mapambazuko yatawafikia wadanganyika wote.
HUYU CAG naye anambwembwe za kisiasa wala hana akili ya kusaidia taifa, anaishi kama makonda tu kuangalia tumbo lake, wee watu wamechangia more than 20years halafu leo unampuuza , pesa inakopwa na serikali hairudishwi badala ya kuelkeza nguvu huko unatoa kashfa kwa waliukuza mfuko kuwa ni mzigo, jiangalie wee jamaa
 
Siasa tu ,badala kutumia Elimu yake kumsaidia jamii ndiyo kwanza Yupoyupo tu
 
Hapo amezingua big time, ameanza kuishiwa. Anaacha kuwaumbua wake wa viongozu wastaafu anahangaika na watu wa kawaida
 
Back
Top Bottom