CAG Prof. Assad astaafu, Charles Kichere ateuliwa kuwa CAG mpya

CAG Prof. Assad astaafu, Charles Kichere ateuliwa kuwa CAG mpya

Mkuu hapo subir report ijayo itakavo kuwa safi hapo ndo utajua kuna tofauti kat ya msiba na matanga
Kwa hiyo wewe ulitakaje..embu tupe mawazo yako tukujue unayowaza..ndio baadae utupe tofauti kati ya msiba wako na matanga
 
Charles Kichere kama CAG sasa

- Mwaka wa Fedha 2018/2019 alikuwa Kamishna Mkuu wa TRA
- 2019/2020 alikuwa RAS wa Njombe

Je, atajikagua na kujipa hati safi/chafu na kufuatilia majibu ya maswali yaliyopita kuhusu TRA na Njombe?
Hala kuna tatizo.

1. Wenye uzoefu wamo serikalini.
2. Ukiteua wenye uzoefu walio serikalini, unaweza kuwekewa maswali kuhusu wao kufunika walikopita.

Suluhisho hapo ni kuteua yeyote anayefaa, na kama kuna tuhuma tujenge utamaduni na mfumo wa uwazi kiasi kwamba mtu yeyote anaweza kuwa whistleblower.

Ukitaka kuzuia mtu asiteuliwe CAG kwa sababu alifanya kazi serikalini, utakosa watu wengi sana wenye uzoefu.

Magufuli ana makosa mengi, mengi sana.

Tusimtungie makosa ambayo si yake.

Kufanya hivyo kutazidi kuipa nguvu hoja ya kwamba wanaompinga hawana hoja.
 
Cv yake haijatosha kabisa aisee hajapishana sana na mie mtoto wa mkulima wapo watu wengi wenye elimu uzoefu na weledi mkubwa sana waliofaa kuwa cag huyu sidhani
 
Duh kwahiyo hapo kichere atakuwa na miaka kama kumi hivi mbele kazini mpaka aje kustaafu
 
Ana elimu ya Ku unga unga sana kwenye ofisi ya CAG hatoshi pale panataka kichwa angalau chenye CPA.
 
Kwasababu pale Assad Associates(AA) hua wanasahihisha Booklets sio?

Naona umemchanganya na Palamagamba.
Ndiyo kastaafu miaka yake mitano,Boss hakumuongezea ingawa umri bado unaruhusu. Sasa arudi kusasihisha Booklets.
 
Taarifa ya Ikulu imeeleza kuwa Mdhibiti na Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali Prof.Mussa Assad amemaliza kipindi chake cha miaka mitano kwenye nafasi hiyo. Lakini Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 (ambayo ndio sheria mama) haelezi hicho kinachoitwa "kipindi cha miaka mitano"
_
Katiba inaeleza kuwa CAG atakoma utumishi wake atakapotimiza umri wa miaka 60. Yani akifikisha umri wa miaka 60 anapumzika bila kujalisha ametumikia nafasi hiyo kwa muda gani. Iwe miezi miwili, miaka nane, au miaka kumi.

Ndio maana maCAG wote waliotangulia wameongoza ofisi hiyo kwa vipindi tofauti. Mzee Mohamed Aboud aliongoza kwa miaka 27 tangu 1969 hadi 1996. Thomas Kiama akaongoza kwa miaka 9 tangu 1996 hadi 2005. Ludovick Utouh akaongoza kwa miaka 8 tangu 2006 hadi 2014. Sasa hii kauli ya kusema Assad amemaliza kipindi chake cha "miaka mitano" imetoka wapi?

Matakwa ya kikatiba ni umri wa miaka 60, unless aondolewe kwa kushindwa kutimiza majukumu yake. Na ikitokea hivyo Katiba imeweka utaratibu wa kumuondoa kwa kuunda tume.

Lakini taarifa ya Ikulu inaeleza Assad amemaliza kipindi chake cha miaka mitano. Je hiki kipindi cha miaka mitano Ikulu wamekitoa wapi? Kwenye sheria ipi? Kama ipo sheria hiyo ipo ni batili maana inapingana na katiba.

Na kwa kawaida unapotokea mgogoro kati ya sheria na katiba, basi Katiba ndiyo inayoshika hatamu (When a state law conflicts with a Constitution, then constitution prevails because constitution rules supreme above all state laws).
_
Prof.Assad amezaliwa tar.06 October mwaka 1961. Kwa sasa ana umri wa miaka 58. Atafikisha umri wa miaka 60 October 06 mwaka 2021. Hivyo kwa mujibu wa KATIBA alipaswa kustaafu nafasi yake ya CAG akifikisha umri huo, na si kwa hiki kinachoitwa "miaka mitano". I stand to be corrected.!View attachment 1252811
Nakumbuka Kuna Sheria ilipitishwa 2014 ikiwalenga wakurugenzi wote wa taasisi za umma watahudumu kwa vipindi vya miaka mitano mitano renewable Mara mbili tu means baada ya miaka 10 hawezi kuhudumu tena
 
Kichere angeonyesha msimamo wake kama Assad ingependeza sana,after jiwe hana mamlaka ya kutengua nafasi yake,I wish I were him ningefanya kazi yangu with integrity bila kumsikiliza meko

Sent from my Infinix HOT 4 using JamiiForums mobile app
 
View attachment 1252682

Rais John Magufuli leo Novemba 3 amemteua Charles Kichere kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) akichukua nafasi ya Prof. Mussa Assad

Prof. Assad aliteuliwa na Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete wakati wa utawala wake na kuapishwa Novemba 2014.

WASIFU WA KICHERE:

NAME : Charles Edward Kichere

DATE OF BIRTH : 26th March 1970

LANGUAGES : Fluent in English and Kiswahili in both writing and speaking.

ACADEMIC QUALIFICATIONS

November 2016:Tumain University, Bachelor of Law (LLB).

December 2008: University of Dar es Salaam, Master of Business Administration (MBA – Finance).

June 2004: African Renaissance Centre – Mbabane, Kingdom of Swaziland. Awarded Diploma in Financial Management of Donor Funded Projects.

November 1997: University of Dar Es Salaam Awarded Bachelor of Commerce (B.com – Accounting) Upper Second Class with Honours.

May 1992: Shinyanga Commercial Institute (Shycom) Awarded Advanced Certificate of Secondary Education Examinations – Division 1.

November 1989: Tambaza Secondary School Awarded Certificate of Secondary Education Examinations – Division 1

Charles Edward Kichere was a Njombe Regional Administrative Secretary (RAS) and former Commissioner General at Tanzania Revenue Authority (TRA).

He also worked as Deputy Commissioner General at Tanzania Revenue Authority (TRA),
Head of Finance and Chief Accountant at Tanzania National Roads Agency (TANROADS),
Principal Internal Auditor at Tanzania National Roads Agency (TANROADS),
Internal Auditor at Tanzania National Roads Agency (TANROADS),
Internal Auditor at Unilever Tea Tanzania Limited, and Internal Auditor/Treasurer at Unilever Tea Kenya Limited.

Charles E. Kichere holds Bachelor of Laws (LL.B) from Tumaini University College, Dar es Salaam Tanzania, Masters of Business Administration (MBA) in Finance at University of Dar es Salaam,
Diploma in Financial Management of Donor Funded Projects at Africa Renaissance Centre, Mbabane Swaziland,
Bachelor of Commerce in Accounting (B.Com Accounting) at University of Dar es Salaam.

He is a member of the Credit and Audit Committees.
Mie najiuliza, hakuonekana kutosha TRA, atatosha u-CAG?
Na kwa yale yaliyotokea, ni kama "keshakatwa mkia", atakuwa na ujasiri wa kusimamia misingi ya kazi yake kweli? Au inawezekana mteuzi nae amelizingatia hilo ili kujiondolea 'usumbufu usio wa lazima'?
 
Mambo ya hii nchi ukiyatafakari sana ni kujitia tu presha..mbaya zaidi hata upige kelele vipi kuna watu wamekaa sehemu wanasanifu tu huku wanakuna vitambi na tooth pick mdomoni..
 
Back
Top Bottom