Niliapia sitokuja kuongelea kitu chochote serious humu JF zaidi ya pombe na ngono ila ngoja leo nikushauri kitu sababu nimeona sana mabandiko yako na sijui kwanini yananiangukia
Nimefanya kazi za kuallocate funds kwenye startups kutoka kwenye foundations kadhaa nje na ndani ya nchi. Wengi ni wanasiasa kama wewe(usiishie kusoma hapo, vuta pumzi tuendelee). Wanalenga kutoa first impression kwa maneno mataam lakini biashara zao ni zero. Startups nyingi zinakufa hata kama walipewa funds sababu executives na founders ni wanasiasa tu, wanajua theory ya biashara na maneno mazito ya kutongoza investors ila hawajui kuendesha biashara kutokana, kutumia data, takwimu na saikolojia ili kufanya biashara iwe profitable zaidi.
Siku hizi nikisikia neno startup nataka hadi kutapika. Cheki kuna waghana flani walipata hadi usd 86 million wanajiita DASH ila kampuni limekufa, nenda kwa jirani zako JUMIA wako wapi sasahivi? Startups za hapa Tanzania ndo sitozitaja sababu founders lengo lao ni kupata funds wakanunue brevis wajenge nyumba then wafunge biashara.
Sasa mimi nakuomba kitu kimoja tu. Takwimu za biashara zako katika makundi haya.
1)Zitakazonifanya NIWEKEZE kwenye biashara yako
2)Zitakazonifanya NISIWEKEZE kwenye biashara yako.
Hapo kwenye takwimu nataka zote ambazo unatumia kwenye biashara yako kama vile customer follow ups, leads to client ratio, stock turnover, na statistics zote (kama una utimamu wa biashara utajua namaanisha zipi)
lkn pia ambatanisha financial statements za toka mwaka ulioanza kufanya business hadi mwaka huu.
Nitumie PM na kama nitapenda ninachokiona nina 15million hapa cash imekaa inasubiri kufanyiwa starehe tu, nitawekeza nusu kwenye biashara yako. Ukiona risk kunitumia nambie nikupe calendar yangu uchague siku tuonane ofisini kwangu, nitakua na cash ww uje na hizo data.
Good luck sweetheart.