CCM haikujenga uwanja wa Sokoine Mbeya, iliwapora wananchi. Uwanja urudishwe kwa Halmashauri ya Jiji la Mbeya

CCM haikujenga uwanja wa Sokoine Mbeya, iliwapora wananchi. Uwanja urudishwe kwa Halmashauri ya Jiji la Mbeya

Heci

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2016
Posts
3,591
Reaction score
6,114
Sisi wana Mbeya ni wahanga wa matukio ya kibabe ya kidhalimu yaliyofanywa na yanayoendelea kufanywa na chama hiki mumiani. Miongoni mwa udhalimu huo ni kuporwa kwa uwanja wa wananchi, uwanja wa Sokoine kisha CCM kujimilikisha.

Uwanja wa Sokoine ulijengwa na wananchi wa Mbeya Mjini, kisha ukapewa jina la uwanja wa Mapinduzi, kabla ya mwaka 1984 haujabadilishwa jina na kuitwa uwanja wa Sokoine, baada ya kifo cha waziri mkuu ndugu Edward Moringe Sokoine.

Wananchi walihamasika kujenga uwanja huu kwa nguvu zao wenyewe baada ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kukataa msaada wa kujengewa uwanja wa kisasa na serikali ya China kwa sharti uitwe kwa jina la kiongozi wao, Mao Tse Dong.

Wananchi ndio walichanga fedha zao, walifyatua matofali, na walijitoa kikamilifu kwa moyo mmoja hadi kukamilika kwa uwanja. Mwaka 1992 Augustino Lyatonga Mrema akiwa waziri wa mambo ya ndani alitembelea mkoa wa Mbeya na kuhutubia kwenye uwanja wa Sokoine.

Kipindi hicho ndio vyama vya upinzani vimeruhusiwa kufanya siasa. Akaikuta bendera ya NCCR MAGEUZI inapepea uwanjani hapo, sanjari na bendera bendera ya Taifa huku bendera ya CCM ikiwa haipo kabisa uwanjani hapo.

Mrema kwa hasira akasema hawezi kuhutubia bendera ya chama pinzani ikiwa inapepea. Akaamuru bendera hiyo ishushwe na kuanzia hapo uwanja ni mali ya CCM.

NCCR MAGEUZI ni chama kilichokubalika sana enzi hizo mkoani Mbeya, kiliweza kuibwaga CCM kwenye uchaguzi wa diwani jimbo la Mbeya Mjini chini ya mgombea wake Mwalimu Polisya Sikumbula Mwaisyeje.

Sasa ni wakati sahihi kwa CCM kurejesha kwa wananchi uwanja huo, kwani haujawahi kuwa mali yao na wala CCM haikuwahi kuutolea jasho kwa namna yoyote.

Uwanja wa Sokoine sio mali ya CCM, Mbeya sio mali ya CCM. kataa CCM, kataa dhuluma.
 
Hili ni kweli kabisa, Dkt. TULIA, hakikisha uwanja unarudi jiji, hakikisha Mbeya City haishuki daraja, kinyume cha hapo hutoonekana tena bungeni. Kwanza wana Mbeya hawataki jimbo lao ligawanywe kwa ajili ya maslahi yako binafsi.
 
CCM haina kiwanja chochote wala jengo lolote. Vyote walipora. Kirumba; Ally Hasan Mwnyi makao makuu pale Lumumba nk.

Muda ukifika vyote vitarudi kwa wamiliki halali ambao ni wananchi
 
Mimi toka Jana nalalamika hii CCM imepora mashamba ya wananchi Sae uko uko Mbeya hivi ichi chama kina nini?
 
Sisi wana Mbeya ni wahanga wa matukio ya kibabe ya kidhalimu yaliyofanywa na yanayoendelea kufanywa na chama hiki mumiani. Miongoni mwa udhalimu huo ni kuporwa kwa uwanja wa wananchi, uwanja wa Sokoine kisha CCM
Uwanja wa Sokoine ulijengwa enzi za Chama kimoja, na michango ilipita kwa wana Mbeya wa wilaya zote. Na ukumbuke kuwa wakati huo, Mbeya ilikuwa haijagawanywa kama ilivyo sasa. CCM ndiyo ilisimamia serikali katika utekelezaji wa ule mradi, na chama kilishika hatamu kwelikweli.

Kwahiyo, hata kama CCM itakosa uhalali wa umiliki wa kiwanja cha Sokoine, bado hakiwezi kuwa mali ya Mbeya jiji,kwa sababu hakikujengwa na wana Mbeya jiji peke yao.
 
WWewe
Sisi wana Mbeya ni wahanga wa matukio ya kibabe ya kidhalimu yaliyofanywa na yanayoendelea kufanywa na chama hiki mumiani. Miongoni mwa udhalimu huo ni kuporwa kwa uwanja wa wananchi, uwanja wa Sokoine kisha CCM kujimilikisha.
Wewe mwandishi ulikua Chama gani Cha siasla wakati uwanja wa sokoine unajengwa?Hivi wakati jumuiya ya afrika mashariki inavunjika Mali zake zilirudishwa nchi ganii?
 
una shilingi ngapi hadi muda huu mleta uzi? ndio nyie mnakaa kwenye vijiwe vya retco, sokomatola , panapouzwa magezeti na washona viatu na kupiga stori za kijinga sana , wewe una hakika hati ya ardhi ya eneo hilo inasomaje ,
 
Wananchi Wajenge uwanja mwingine tu
Siyo huo tuu, uwanja wa Sheikh Amri Abeid Kaluta jijini Arusha ulijengwa na askari mstaafu wa Kiingereza Colonel Middleton na baadaye akaukabidhi kwa Arusha Township Counsil lakini haya majizi wame unyakua kwa nguvu.
 
Sisi wana Mbeya ni wahanga wa matukio ya kibabe ya kidhalimu yaliyofanywa na yanayoendelea kufanywa na chama hiki mumiani. Miongoni mwa udhalimu huo ni kuporwa kwa uwanja wa wananchi, uwanja wa Sokoine kisha CCM kujimilikisha.

Uwanja wa Sokoine ulijengwa na wananchi wa Mbeya Mjini, kisha ukapewa jina la uwanja wa Mapinduzi, kabla ya mwaka 1984 haujabadilishwa jina na kuitwa uwanja wa Sokoine, baada ya kifo cha waziri mkuu ndugu Edward Moringe Sokoine.

Wananchi walihamasika kujenga uwanja huu kwa nguvu zao wenyewe baada ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kukataa msaada wa kujengewa uwanja wa kisasa na serikali ya China kwa sharti uitwe kwa jina la kiongozi wao, Mao Tse Dong.

Wananchi ndio walichanga fedha zao, walifyatua matofali, na walijitoa kikamilifu kwa moyo mmoja hadi kukamilika kwa uwanja. Mwaka 1992 Augustino Lyatonga Mrema akiwa waziri wa mambo ya ndani alitembelea mkoa wa Mbeya na kuhutubia kwenye uwanja wa Sokoine.

Kipindi hicho ndio vyama vya upinzani vimeruhusiwa kufanya siasa. Akaikuta bendera ya NCCR MAGEUZI inapepea uwanjani hapo, sanjari na bendera bendera ya Taifa huku bendera ya CCM ikiwa haipo kabisa uwanjani hapo.

Mrema kwa hasira akasema hawezi kuhutubia bendera ya chama pinzani ikiwa inapepea. Akaamuru bendera hiyo ishushwe na kuanzia hapo uwanja ni mali ya CCM.

NCCR MAGEUZI ni chama kilichokubalika sana enzi hizo mkoani Mbeya, kiliweza kuibwaga CCM kwenye uchaguzi wa diwani jimbo la Mbeya Mjini chini ya mgombea wake Mwalimu Polisya Sikumbula Mwaisyeje.

Sasa ni wakati sahihi kwa CCM kurejesha kwa wananchi uwanja huo, kwani haujawahi kuwa mali yao na wala CCM haikuwahi kuutolea jasho kwa namna yoyote.

Uwanja wa Sokoine sio mali ya CCM, Mbeya sio mali ya CCM. kataa CCM, kataa dhuluma.
nenda mahakamani, lakini ujue hiyo halmashauri nayo ni mali ya CCM
 
Sisi wana Mbeya ni wahanga wa matukio ya kibabe ya kidhalimu yaliyofanywa na yanayoendelea kufanywa na chama hiki mumiani. Miongoni mwa udhalimu huo ni kuporwa kwa uwanja wa wananchi, uwanja wa Sokoine kisha CCM kujimilikisha.

Uwanja wa Sokoine ulijengwa na wananchi wa Mbeya Mjini, kisha ukapewa jina la uwanja wa Mapinduzi, kabla ya mwaka 1984 haujabadilishwa jina na kuitwa uwanja wa Sokoine, baada ya kifo cha waziri mkuu ndugu Edward Moringe Sokoine.

Wananchi walihamasika kujenga uwanja huu kwa nguvu zao wenyewe baada ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kukataa msaada wa kujengewa uwanja wa kisasa na serikali ya China kwa sharti uitwe kwa jina la kiongozi wao, Mao Tse Dong.

Wananchi ndio walichanga fedha zao, walifyatua matofali, na walijitoa kikamilifu kwa moyo mmoja hadi kukamilika kwa uwanja. Mwaka 1992 Augustino Lyatonga Mrema akiwa waziri wa mambo ya ndani alitembelea mkoa wa Mbeya na kuhutubia kwenye uwanja wa Sokoine.

Kipindi hicho ndio vyama vya upinzani vimeruhusiwa kufanya siasa. Akaikuta bendera ya NCCR MAGEUZI inapepea uwanjani hapo, sanjari na bendera bendera ya Taifa huku bendera ya CCM ikiwa haipo kabisa uwanjani hapo.

Mrema kwa hasira akasema hawezi kuhutubia bendera ya chama pinzani ikiwa inapepea. Akaamuru bendera hiyo ishushwe na kuanzia hapo uwanja ni mali ya CCM.

NCCR MAGEUZI ni chama kilichokubalika sana enzi hizo mkoani Mbeya, kiliweza kuibwaga CCM kwenye uchaguzi wa diwani jimbo la Mbeya Mjini chini ya mgombea wake Mwalimu Polisya Sikumbula Mwaisyeje.

Sasa ni wakati sahihi kwa CCM kurejesha kwa wananchi uwanja huo, kwani haujawahi kuwa mali yao na wala CCM haikuwahi kuutolea jasho kwa namna yoyote.

Uwanja wa Sokoine sio mali ya CCM, Mbeya sio mali ya CCM. kataa CCM, kataa dhuluma.
Viwanja vyote mikoani havinkujengwa na CCM vilijengwa na wananchi,uwanja wa majimaji songea nakumbuka nilishiriki na watoto wenzangi kubebelea matofali mawili mawili toka mto matarawe yalipokua yanafyatuliwa.

Bibi yangu na wenzie walisomba maji toka mtoni,Babu alikua fundi tulikula biskuti na maharage ya kopo(tuliamimishwa ni vyakula vya jeshini(vitani)

Viwanja vyote virudi halashauri au TFF mikoani kwa matumizi ya wote.
 
Viwanja vyote mikoani havinkujengwa na CCM vilijengwa na wananchi,uwanja wa majimaji songea nakumbuka nilishiriki na watoto wenzangi kubebelea matofali mawili mawili toka mto matarawe yalipokua yanafyatuliwa.

Bibi yangu na wenzie walisomba maji toka mtoni,Babu alikua fundi tulikula biskuti na maharage ya kopo(tuliamimishwa ni vyakula vya jeshini(vitani)

Viwanja vyote virudi halashauri au TFF mikoani kwa matumizi ya wote.
Hii dhuluma inasikitisha
 
Back
Top Bottom