Uchaguzi 2020 CCM haina uwezo wa kumuondoa mgombea yeyote kwa sababu ya kutoa rushwa, labda iwe kwa sababu nyingine

Uchaguzi 2020 CCM haina uwezo wa kumuondoa mgombea yeyote kwa sababu ya kutoa rushwa, labda iwe kwa sababu nyingine

Anayeengua watoa rushwa ni Polepole au vikao vyenye jukumu la kufanya uteuzi..maneno mengiii unaongelea mtu badala ya issues, watu hubadilika..ni mjinga tu ndio anaweza kuamini watu akidhani hawawezi kubadilika..asiyebadilika ni Mungu pekee! ukijua hilo Polepole wa 2013 na wa 2020 hawalingani na hilo halishangazi wala siyo issue..
Issue hapa ni UKIGEUGEU wa Bwana Polepole ndio unamnyima sifa za kupambana na wala rushwa ndani ya chama cha mapinduzi.

Msimamo wake mkali akiwa mjumbe waTume ya katiba iliokuwa inaongozwa na Jaji Warioba ni mtu tofauti tokea apate UDC na baadae Ukatibu mwenezi wa CCM katika awamu hii ya 5.
 
Mimi nasubiria kuona yule mama wa mbeya M. M
atachukuliwa hatua gani baada ya clip yake kusambaaa

Ova
kumbuka ilishindikana kwa Mnyeti kule Arumeru licha ya kubambwa live.

unaweza kujikuta unasubiri hadi siku ya kiama!
 
Kawaida kwenye siasa hata chadema walisema lowasa Ni fisadi hawezi kusafishika ajabu hao hao Cha Domo na Wana Sacco's wakamsafisha na barabara wakazideki na ticket ya kugombea uraisi wakampa Sasa wewe ukisema unamshangaa pole pole Mimi naishangaa Sacco's nzima ya mtaa wa ufipa
 
Kawaida kwenye siasa hata chadema walisema lowasa Ni fisadi hawezi kusafishika ajabu hao hao Cha Domo na Wana Sacco's wakamsafisha na barabara wakazideki na ticket ya kugombea uraisi wakampa Sasa wewe ukisema unamshangaa pole pole Mimi naishangaa Sacco's nzima ya mtaa wa ufipa
Jikite kwenye mada
 
Huu ndio ukweli wa wazi kabisa , kwamba kauli za polepole kwamba waliotoa rushwa watafundishwa adabu zichukuliwe kama porojo za kunogesha mazungumzo yake tu , haina ukweli wowote na hata kwa cheo alichonacho hana mamlaka ya kumuengua mtu kwa tuhuma zozote ( soma majukumu wa kati mwenezi wa ccm )

Kingine ni kwamba Polepole si mtu wa kuaminika na wala hajawahi kuaminika , kwa mfano akiwa mjumbe wa Tume ya Katiba mpya chini ya Mzee Warioba alitamka hadharani na kupigia kampeni kuondolewa kwa cheo cha Wakuu Wa Wilaya , kwa hoja kwamba Wakurugenzi wanatosha kusimamia majukumu Wilayani , akaungwa mkono karibu na kila mwenye akili nchi nzima , lakini cha kushangaza alikubali kuteuliwa na kuapishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo kwenye awamu ya 5 !

Pia kwenye tume hiyo hiyo alisema na kurekodiwa kwamba Tume huru ni lazima na akaiponda ccm na kuiambia wazi kwamba ikiwa uchaguzi ukiwa huru na haki basi ijiandae kukabidhi Ikulu , lakini yeye kwa sasa ni miongoni mwa watu wachache sana ndani ya ccm wanaopinga kabisa Katiba Mpya ( nitaambatanisha ushahidi wa video )

Ili kukuhakikishia kwamba Polepole si lolote ndani ya ccm ni kurudi kwa Lowassa ndani ya ccm , Kwa kumbukumbu ya wanajf na wengine wageni Kwenye awamu ya 5 Polepole ndio kiongozi aliyemtukana Lowassa labda kuliko wengine , kwa kutuaminisha kwamba huyu mtu ni fisadi wa kutisha , lakini siku ya kurudi Lowassa aliufyata na hajatukana tena hadi leo , huyu angekuwa na msimamo basi angeondoka ccm siku ileile.

Kwa ufupi ni kwamba Polepole wala ccm hakuna mwenye uwezo wa kupinga rushwa , taarifa zinadokeza kwamba hata Takukuru kuwarejesha waliodaiwa kutoa rushwa ccm ni matakwa ya ccm yenyewe baada ya kutathmini hali ya mambo , uliona wapi watuhumiwa wakapelekwa kwa aliyewatuhumu ili awachukulie hatua badala ya Mahakamani ? ni vigumu mno kwa ccm kuwaengua wagombea kwa tuhuma za rushwa , ikifanya hivyo basi itaengua wote na Wapinzani watapita bila kupingwa , kwa mfano kwenye jimbo la kyela wagombea karibu wote walitoa rushwa , kuanzia pikipiki , cash iliyofikia hadi laki 3 kwa mtu mmoja na pombe , hivi kwenye jimbo kama hili unamuengua nani na unamuacha nani ?

Itaendelea......
tuhuma za rushwa ni Anayeengua watoa rushwa ni Polepole au vikao vyenye jukumu la kufanya uteuzi..maneno mengiii unaongelea mtu badala ya issues, watu hubadilika..ni mjinga tu ndio anaweza kuamini watu akidhani hawawezi kubadilika..asiyebadilika ni Mungu pekee! ukijua hilo Polepole wa 2013 na wa 2020 hawalingani na hilo halishangazi wala siyo issue..
Issue hapa ni UKIGEUGEU wa Bwana Polepole ndio unamnyima sifa za kupambana na wala rushwa ndani ya chama cha mapinduzi.

Msimamo wake mkali akiwa mjumbe waTume ya katiba iliokuwa inaongozwa na Jaji Warioba ni mtu tofauti tokea apate UDC na baadae Ukatibu mwenezi wa CCM katika awamu hii ya 5.
Wewe na akili zako timamu unaweza shangaa mtu kuwa kigeu geu..acha Polepole hata mzazi wako akigeuka juu ya alichosema mwanzo wewe unaona hyo ndio ajenda...ukiwa na akili ya hvyo hutakaa ufanikiwe, lkn nimeuliza kwani Polepole ndiye anaengua watu? Ukipata jibu la hili swali issue ya Polepole kasema nini, lini na wapi haviwezi kukusumbua..leo yupo CCM kesho hayupo, usipoteze muda kumfikiria mtu badala ya issues!
 
tuhuma za rushwa ni Anayeengua watoa rushwa ni Polepole au vikao vyenye jukumu la kufanya uteuzi..maneno mengiii unaongelea mtu badala ya issues, watu hubadilika..ni mjinga tu ndio anaweza kuamini watu akidhani hawawezi kubadilika..asiyebadilika ni Mungu pekee! ukijua hilo Polepole wa 2013 na wa 2020 hawalingani na hilo halishangazi wala siyo issue..
Wewe na akili zako timamu unaweza shangaa mtu kuwa kigeu geu..acha Polepole hata mzazi wako akigeuka juu ya alichosema mwanzo wewe unaona hyo ndio ajenda...ukiwa na akili ya hvyo hutakaa ufanikiwe, lkn nimeuliza kwani Polepole ndiye anaengua watu? Ukipata jibu la hili swali issue ya Polepole kasema nini, lini na wapi haviwezi kukusumbua..leo yupo CCM kesho hayupo, usipoteze muda kumfikiria mtu badala ya issues!
Lo hivi wewe akili zako ziko sawa?
Kama ni siasa your still underdog and in very wrong path. Sitashangaa kama ukiwa wa mwanzo kufutwa kazi.
 
Kumuongezea miaka 10 ni kuvunja katiba ya nchi , tambua hilo
Havunji katiba wala hata gusa katiba
Ila kwa chama ndio kitaona hakuna mgombea mwingine bado kina mwamini Dkt. Aendelee 10 tena ili akamilishe miradi mikubwa ya kimkakati na kujenga uchumi wa nchi kuifanya kuwa kama ulaya.
 
Huu ndio ukweli wa wazi kabisa, kwamba kauli za polepole kwamba waliotoa rushwa watafundishwa adabu zichukuliwe kama porojo za kunogesha mazungumzo yake tu, hazina ukweli wowote na hata kwa cheo alichonacho hana mamlaka ya kumuengua mtu yeyote kwa tuhuma zozote (soma majukumu wa kati mwenezi wa CCM)

Kingine ni kwamba Polepole si mtu wa kuaminika na wala hajawahi kuaminika, kwa mfano akiwa mjumbe wa Tume ya Katiba mpya chini ya Mzee Warioba alitamka hadharani na kupigia kampeni kuondolewa kwa cheo cha Wakuu Wa Wilaya, kwa hoja kwamba wakurugenzi wanatosha kusimamia majukumu Wilayani, akaungwa mkono karibu na kila mwenye akili nchi nzima, lakini cha kushangaza alikubali kuteuliwa na kuapishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo kwenye awamu ya 5!

Pia kwenye tume hiyo hiyo alisema na kurekodiwa kwamba Tume huru ni lazima na akaiponda ccm na kuiambia wazi kwamba ikiwa uchaguzi ukiwa huru na haki basi ijiandae kukabidhi Ikulu , lakini yeye kwa sasa ni miongoni mwa watu wachache sana ndani ya ccm wanaopinga kabisa Katiba Mpya ( nitaambatanisha ushahidi wa video )

Ili kukuhakikishia kwamba Polepole si lolote ndani ya CCM ni kurudi kwa Lowassa ndani ya CCM, Kwa kumbukumbu ya wanajf na wengine wageni , Kwenye awamu ya 5 Polepole ndio kiongozi wa CCM aliyemtukana zaidi Lowassa labda kuliko wengine wote , kwa kutuaminisha kwamba huyu mtu ni fisadi wa kutisha , lakini siku ya kurudi Lowassa aliufyata na hajatukana tena hadi leo , huyu angekuwa na msimamo basi angeondoka ccm siku ileile.

Kwa ufupi ni kwamba Polepole wala CCM hakuna mwenye uwezo wa kupinga rushwa , taarifa zinadokeza kwamba hata Takukuru kuwarejesha waliodaiwa kutoa rushwa CCM ni matakwa ya ccm yenyewe baada ya kutathmini hali ya mambo , uliona wapi watuhumiwa wakapelekwa kwa aliyewatuhumu ili awachukulie hatua badala ya Mahakamani ? ni vigumu mno kwa CCM kuwaengua wagombea kwa tuhuma za rushwa , ikifanya hivyo basi itaengua wote na Wapinzani watapita bila kupingwa , kwa mfano kwenye jimbo la kyela wagombea karibu wote walitoa rushwa , kuanzia pikipiki , cash iliyofikia hadi laki 3 kwa mtu mmoja na pombe , hivi kwenye jimbo kama hili unamuengua nani na unamuacha nani ?

Itaendelea......
Niliona mahali mtu ana maradhi tambuka. Ndiyo hayo?
 
Huu ndio ukweli wa wazi kabisa, kwamba kauli za polepole kwamba waliotoa rushwa watafundishwa adabu zichukuliwe kama porojo za kunogesha mazungumzo yake tu, hazina ukweli wowote na hata kwa cheo alichonacho hana mamlaka ya kumuengua mtu yeyote kwa tuhuma zozote (soma majukumu wa katibu mwenezi wa CCM)

Kingine ni kwamba Polepole si mtu wa kuaminika na wala hajawahi kuaminika, kwa mfano akiwa mjumbe wa Tume ya Katiba mpya chini ya Mzee Warioba alitamka hadharani na kupigia kampeni kuondolewa kwa cheo cha Wakuu Wa Wilaya, kwa hoja kwamba wakurugenzi wanatosha kusimamia majukumu Wilayani, akaungwa mkono karibu na kila mwenye akili nchi nzima, lakini cha kushangaza alikubali kuteuliwa na kuapishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo kwenye awamu ya 5!

Pia kwenye tume hiyo hiyo alisema na kurekodiwa kwamba Tume huru ni lazima na akaiponda ccm na kuiambia wazi kwamba ikiwa uchaguzi ukiwa huru na haki basi ijiandae kukabidhi Ikulu , lakini yeye kwa sasa ni miongoni mwa watu wachache sana ndani ya ccm wanaopinga kabisa Katiba Mpya ( nitaambatanisha ushahidi wa video )

Ili kukuhakikishia kwamba Polepole si lolote ndani ya CCM ni kurudi kwa Lowassa ndani ya CCM, Kwa kumbukumbu ya wanajf na wengine wageni , Kwenye awamu ya 5 Polepole ndio kiongozi wa CCM aliyemtukana zaidi Lowassa labda kuliko wengine wote , kwa kutuaminisha kwamba huyu mtu ni fisadi wa kutisha , lakini siku ya kurudi Lowassa aliufyata na hajatukana tena hadi leo , huyu angekuwa na msimamo basi angeondoka ccm siku ileile.

Kwa ufupi ni kwamba Polepole wala CCM hakuna mwenye uwezo wa kupinga rushwa , taarifa zinadokeza kwamba hata Takukuru kuwarejesha waliodaiwa kutoa rushwa CCM ni matakwa ya ccm yenyewe baada ya kutathmini hali ya mambo , uliona wapi watuhumiwa wakapelekwa kwa aliyewatuhumu ili awachukulie hatua badala ya Mahakamani ? ni vigumu mno kwa CCM kuwaengua wagombea kwa tuhuma za rushwa , ikifanya hivyo basi itaengua wote na Wapinzani watapita bila kupingwa , kwa mfano kwenye jimbo la kyela wagombea karibu wote walitoa rushwa , kuanzia pikipiki , cash iliyofikia hadi laki 3 kwa mtu mmoja na pombe , hivi kwenye jimbo kama hili unamuengua nani na unamuacha nani ?

Itaendelea......
CCM wote kwa ujumla walitoa Rushwa hakuna ambaye hakutoa Rushwa kama kigezo ni Rushwa basi lazima uchaguzi wa kura za maoni urudiwe upya kabsa waanze moja, huo mchujo umekuwa batili wapo wataonewa kwa kisingizio cha Rushwa wakati ni Tatizo la CCM wote jumla, hakunaga CCM malaika kwa Tanzania wote hununua uongozi kwa namna mbalimbali kikubwa ikiwa ni kwa Rushwa tu.
 
Mimi nasubiria kuona yule mama wa mbeya M. M
atachukuliwa hatua gani baada ya clip yake kusambaaa

Ova
Kamati kuu itamrejesha Mwakyembe kairuki ngeleja makonda na wengineo wengi wafuasi wa kusifia mtukufu kila mara, kamati kuu siyo mungu siyo malaika nao ni wanadamu watakosea mengi mno, baada ya kuchuja majina wataleta manung’uniko mengi sana miongoni mwa watanzania wote
 
Akina Mnyete wameonekana wakirubuni madiwani wa upinzani kwa kiwashawishi cha rushwa wamepewa vyeo halafu aenguliwe mtu kwa rushwa ya aina gani hivi CCM kutoa na kupokea rushwa limekuwa kosa lini tusidanganyane biashara ya kununua wapinzani imeshamiri awamu hii sasa ni rushwa ipi inayokatazwa. Ni bora kunyamaza tu.
Hakuna malaika CCM wote wana madhambi yao, wakitaka watanzania waiamini CCM lazima warudie uchaguzi wa kura za maoni upya kabsa
 
Kamati kuu ya CCM wanajiona wapo sawa lakini na wao wanaposwa kuijtathimini kama wanadamu wajue hawapo sawa pia, report nyingi dhidi ya watia nia kura za maoni ni za kupikwa ama kutengenezwa ama shinikizo na zingine chache ni za kweli kabsa, zile report za kweli hasa za akina makonda, waitara, mnyeti, kibajaji Lusinde, kairuki, Mwakyembe na wenzao utashangaa zinaenda kupuuzwa cha ajabu wataenda kufanyia kazi report ambazo nyingi zimeundwa kwa chuki, wivu, Majungu, fitna nk na hapo ndipo Kamati kuu ya CCM italeta gumzo kubwa nchini kote.
 
Issue hapa ni UKIGEUGEU wa Bwana Polepole ndio unamnyima sifa za kupambana na wala rushwa ndani ya chama cha mapinduzi.

Msimamo wake mkali akiwa mjumbe waTume ya katiba iliokuwa inaongozwa na Jaji Warioba ni mtu tofauti tokea apate UDC na baadae Ukatibu mwenezi wa CCM katika awamu hii ya 5.
Polepole ametumia fursa hii kuvuna toka kwa watia nia wote imekuwa fursa kwake hakuna mjumbe malaika toka kwa Mungu huko CCM, polepole alichimba mikwara akiamini itamsaidia kujinufaisha binafsi.
 
Polepole ametumia fursa hii kuvuna toka kwa watia nia wote imekuwa fursa kwake hakuna mjumbe malaika toka kwa Mungu huko CCM, polepole alichimba mikwara akiamini itamsaidia kujinufaisha binafsi.
Kweli nashindwa kuamini kuwa Polepole and company ni watakatifu.NEVER DO WRONG.
Na hiyo itagharimu chama.
Ikiwa huyo huyo Polepole alinunua wabunge wa upinzani kinyume na taratibu za uchaguzi,ni tu wapinzani wamezembea kuwashitaki CCM,njia walizozitumia sio sawa.
 
Kweli nashindwa kuamini kuwa Polepole and company ni watakatifu.NEVER DO WRONG.
Na hiyo itagharimu chama.
Ikiwa huyo huyo Polepole alinunua wabunge wa upinzani kinyume na taratibu za uchaguzi,ni tu wapinzani wamezembea kuwashitaki CCM,njia walizozitumia sio sawa.
Inakuja mahakama ya umma
 
1597926981719.png


Huu ndio ukweli wa wazi kabisa, kwamba kauli za polepole kwamba waliotoa rushwa watafundishwa adabu zichukuliwe kama porojo za kunogesha mazungumzo yake tu, hazina ukweli wowote na hata kwa cheo alichonacho hana mamlaka ya kumuengua mtu yeyote kwa tuhuma zozote (soma majukumu wa katibu mwenezi wa CCM)

Kingine ni kwamba Polepole si mtu wa kuaminika na wala hajawahi kuaminika, kwa mfano akiwa mjumbe wa Tume ya Katiba mpya chini ya Mzee Warioba alitamka hadharani na kupigia kampeni kuondolewa kwa cheo cha Wakuu Wa Wilaya, kwa hoja kwamba wakurugenzi wanatosha kusimamia majukumu Wilayani, akaungwa mkono karibu na kila mwenye akili nchi nzima, lakini cha kushangaza alikubali kuteuliwa na kuapishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo kwenye awamu ya 5!

Pia kwenye tume hiyo hiyo alisema na kurekodiwa kwamba Tume huru ni lazima na akaiponda ccm na kuiambia wazi kwamba ikiwa uchaguzi ukiwa huru na haki basi ijiandae kukabidhi Ikulu , lakini yeye kwa sasa ni miongoni mwa watu wachache sana ndani ya ccm wanaopinga kabisa Katiba Mpya ( nitaambatanisha ushahidi wa video )

Ili kukuhakikishia kwamba Polepole si lolote ndani ya CCM ni kurudi kwa Lowassa ndani ya CCM, Kwa kumbukumbu ya wanajf na wengine wageni , Kwenye awamu ya 5 Polepole ndio kiongozi wa CCM aliyemtukana zaidi Lowassa labda kuliko wengine wote , kwa kutuaminisha kwamba huyu mtu ni fisadi wa kutisha , lakini siku ya kurudi Lowassa aliufyata na hajatukana tena hadi leo , huyu angekuwa na msimamo basi angeondoka ccm siku ileile.

Kwa ufupi ni kwamba Polepole wala CCM hakuna mwenye uwezo wa kupinga rushwa , taarifa zinadokeza kwamba hata Takukuru kuwarejesha waliodaiwa kutoa rushwa CCM ni matakwa ya ccm yenyewe baada ya kutathmini hali ya mambo , uliona wapi watuhumiwa wakapelekwa kwa aliyewatuhumu ili awachukulie hatua badala ya Mahakamani ? ni vigumu mno kwa CCM kuwaengua wagombea kwa tuhuma za rushwa , ikifanya hivyo basi itaengua wote na Wapinzani watapita bila kupingwa , kwa mfano kwenye jimbo la kyela wagombea karibu wote walitoa rushwa , kuanzia pikipiki , cash iliyofikia hadi laki 3 kwa mtu mmoja na pombe , hivi kwenye jimbo kama hili unamuengua nani na unamuacha nani ?

Itaendelea......
 
Back
Top Bottom