CCM hawakurupuki kwenye mambo yao na mtu akizingua anafinywa ndani huwezi kuta wanaparuana nje. Hapa ndio CHADEMA mnafeli

Mkuu, ccm ilishajifia zamani sana.
Hicho anachokisema huyo bwana kwamba ccm inafinya watu wake ndani,kimsingi siyo ccm..ni dola. Ukitaka kuamini hilo mfano mdogo tu wa Lowassa alipoweka nia kugombea urais 2015. Wajumbe wote wa NEC na Kamati kuu ya ccm karibu wote walikuwa upande wa Lowassa,..na kama dola isingeingilia na kulazimisha chaguo lao Magufuli awe mgombea wa ccm..,mgombea wa ccm angekuwa Lowassa,na kamwe Mafufuli asingeshinda kwa sababu alikuwa na watu wachache waliomuunga mkono. Na Jakaya alikuwa hana jeuri ya kukiuka maamuzi ya dola na kumbeba rafiki yake.
kimsingi Chadema inashindana na dola,siyo na ccm kivile...kwa vile dola ndo inayoiba kura kwa niaba ya ccm.
Nnachosema hapa ni kwamba ccm haina hata ubavu wa kumchagua mgombea au viongozi wao kwa nguvu ya mkutano mkuu. Wanapangiwa na dola.
Dola pia wanaingilia chaguzi za vyama vya upinzani..wakitaka watu ambao watakuwana ushaiwshi juu yao ndo wawe viongozi. Ikishafika hatua hiyo ndipo unaona hela zinamwagwa kwa baadhi ya wanachama ili wafanye dola inachotaka. Dola inaogopa mtu mwenye msimamo
 
Unazungumzia chama cha kidemokrasia au CHADEMA nyingine tusiyoijua?

Unatamani mambo ya CCM?
 
Kawaida maroboti yayawezi kukurupuka kwani uwezo hayana.Kufinyana kwao sii jambo la kuuliza hata maji hawaachiani,bora ntu atie mfukoni na ahame nayo.
 
Unazungumzia chama cha kidemokrasia au CHADEMA nyingine tusiyoijua?

Unatamani mambo ya CCM?
Muda utasema..

Unadhani CCM wanafanya wanayofanya kwa sababu zipi...?

CCM wamecheza game hizi na sasa ni 30 years baada ya MPD na bado wapo solid strong (by any means offcourse)

CDM wana allow full ropo ropo tutaona kinachoenda kutokea in few days...
Hizi funding za press kila kona kwa excuse ya Democracy zinafurahisha sana....

Imagine Kinana awe na Press, SSH awe na yake, Makatibu wawe na yao, Mwenyekiti wa CCM Mwanza na yake.... Tuseme ni kukua kwa Democracy na chama kinakuwa😂

Protectionism is not a crime.
 
CCM inawaogopesha wanachama wake kwa kutumia dola.
Ndani ya CCM ni nidhamu ya woga, wakishasema Form ya urais ni MOJA sasa wewe jipekeke na tumbo lako useme unaitaka hiyo hiyo moja kama huliwi bichwa.
 
CCM wamecheza game hizi na sasa ni 30 years baada ya MPD na bado wapo solid strong (by any means offcourse)
CCM hawawezi kukaa Upinzani hata Mwaka mmoja ndio maana wanatumia nguvu za Dola kubaki Madarakani siku CCM inaondolewa Madarakani ndio utajua hizi siasa zao zimejaa wanafiki tu wanaoogopa kukatiwa Mlo.

Angalao hata KANU kilikaa Upinzani
 
Nafikiri kuna kitu nitajifunza hapa. I might have been very naive.
 
CHADEMA wengi wanaojiainisha na Lissu wanasema muda wa kujificha nyuma ya pazia umekwisha, kuna wakati demokrasia inataka uwazi.

Hayo mambo ya usiri mwingi ni tabia za ki CCM ambazo zimetufikisha hapa. Wao wanataka uwazi zaidi, kama mbwai mbwai mradi ukweli ujulikane bila maigizo.

Yani ni hivi, ili mtoto azaliwe, mama kupata uchungu wa kuzaa ni kitu sawa tu.

Mama anayetaka kuzaa mtoto hatakiwi kuogopa uchungu wa kuzaa, uchungu wa kuzaa ni sehemu ya kuzaa na kuleta mtoto duniani kuendeleza kizazi.
 
Offcourse with expenses...
Who will pay the cost?
Watanzania bado ni watu illiterate sana kuweka mambo yako wazi (Mabaya) ukategemea wakakupigia kura...

Hakuna sehemu yenye opportunists kama kwenye vyama vya siasa...

Wallpo waliojificha CDM ila kwa ndani kabisa they love CCM at heart....
Ukikosea ukampa kila mtu chance ya kuzungumza (Mabaya) ya Chama, no so long mnakuwa irrelevant..

Mfano issue ya Pesa za Abdul, ni kati ya propaganda ya hovyo kuwahi kuisikia kwa Mwanasiasa wa Caliber ya TL... Hovyo kabisa ..

Kwamba kwenye chama chao wanakula "Rushwa" kutoka CCM is so unfortunate na hiyo sio openness ni wendawazimu...
 
Reactions: Tui
Mkuu,

Kitu muhimu ni ukweli.

Watanzania wakiikataa CHADEMA ya falsafa za Lissu kwa sababu CHADEMA imekuwa wazi na ya ukweli sana, then Tanzanians do not deserve that CHADEMA.

Lissu nimemuheshimu sana kwa kuona rushwa katika chama chake , kupewa yeye mwenyewe rushwa, kuikataa rushwa na kukisema chama chake kuwa watu wengi wameikubali rushwa hiyo.

Huu ndio uongozi tunaoutaka.

Lissu ana ajenda ya kwenda kukisafisha CHADEMA.

Lissu akitaka kuwa rais wa Tanzania na kuniambia anaichukia rushwa, rekodi yake itam support. Aliwahi kupewa rushwa na kuikataa na kusema wazi, katika mazingira magumu sana ambayo hayakuwa rafiki kwake na kwa chama chake.

Rais John F. Kennedy akiwa Senator Kennedy anagombea urais wa Marekani, mwaka 1956 aliandika kitabu kinaitwa "Profiles in Courage". Kitabu hiki kimewataja Wamarekani mashuhuri ambao hawakusita kusema ukweli on principle hata pale ukweli huo ulipopingana na interests zao au za vyama vyao. Hawakuogopa kusema ukweli.

Kitabu cha "Profiles in Courage" kilienda kushinda nishani ya Pulitzer ya biography ya mwaka 1957.

Kama kuna mtu ataandika kitabu cha aina ya "Profiles in Courage" kuhusu Watanzania wenye courage ya kusema ukweli, Tundu Lissu hatakiwi kukosa kwenye kitabu hicho. Muhimu zaidi, Tundu Lissu ameandika historia kwenye mioyo ya Watanzania wengi.

Kama CHADEMA na Watanzania hawatamkubali kwa sababu hawawezi kuupokea ukweli, hilo ni tatizo lao, Tundu Lissu ameshafanya anachotakiwa kufanya upande wake.
 
Mfano issue ya Pesa za Abdul, ni kati ya propaganda ya hovyo kuwahi kuisikia kwa Mwanasiasa wa Caliber ya TL... Hovyo kabisa ..
Issue ya rushwa za Abdul kwa Chadema sio propaganda .

Ukweli unamweka Tundu Lissu huru.
 

Chama cha demokrasia na chama cha waibaji kura na udikteta huwezi kuwalinganisha😂
 
Issue ya rushwa za Abdul sio propaganda .

Ukweli unamweka Tundu Lissu huru.
Mkuu ukweli ni very subjective Topic..

Kwenye siasa hakuna mkweli wala ukweli, kuna muda na wakati....

Usimwamini mwanasiasa hata siku moja.. angalia trend...

Hoja za Rushwa TL anaziibua kipindi anahitaji kugombea Chairmanships ya CDM.

For the solid 20 years TL hakuwahi kuona Rushwa CDM, imeanza leo?

Pesa za Sabodo zilikuwa ni za bure?
 
Kuparuana si ndo democracy yenyewe?
 
Haiwezekani rushwa ndani ya CHADEMA ikawa imeanza miaka 3 tu iliyopita?
Pesa za Sabodo zilikuwa rushwa kivipi??
 
Tena akiwa Makamu Mwenyekiti sio mburula tu wa mitaani.Yupo kwenye kamati kuu ya Chadema kutokea 2009.
Ni miaka 15.Sasa hivi ni opportunist anayejua anachokifanya.Hizo tuhuma za rushwa aliambiwa na viongozi wenzake apeleke kwenye vikao vya Chama.Hajafanya hivyo bali ni mpiga kelele tu kwenye vyombo vya habari.Na kwa sababu hakuna waandishi wa habari makini hakuna anayemuuliza maswali kuhusu tuhuma zake.Amekuwa kama Musiba.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…