CCM ijitathmini irekebishe madhaifu yake, ijenge umoja iendelee kuongoza Taifa. Hatuna wapinzani nchi hii

CCM ijitathmini irekebishe madhaifu yake, ijenge umoja iendelee kuongoza Taifa. Hatuna wapinzani nchi hii

Umeongea ukweli mtupu mkuu,kifupi hatuna vyama upinzani nchi hii kuna madalali wa kisiasa, mbaya zaidi hawajifunzi kbs wanaona wako sahihi tu

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Tuna chama tawala kinachojitambua. Kipindi cha Kikwete porojo ilikuwa ni umeme wa gas kwani umeme wa maji tatizo ni mabadiliko ya tabia nchi. na hadithi ikawa gas ni muarobaini wa tatizo la nishati nchini. Kaingia Magufuli anasema umeme wa maji ni wa gharama nafuu, ccm wote wanashangilia lakini wamesahau chini ya miaka mitano walisema umeme wa maji tatizo ni mabadiliko ya tabia nchi!

Juzi wakati Magufuli yuko hai anasema hakuna corona kisha anaficha data, chama chake kinamsifia kwa kupambana na Corona, akaagiza mambo ya nyungu mpaka kibanda cha ushirikina kujengwe hospitali kubwa kabisa ya nchi. Viongozi wanaojifanya wasomi wakawa brainwashed akina Kabudi wanakunywa dawa za mitishamba hadharani, akina Jafo wanajifukiza na kujivunia tiba zetu. Chini ya siku 100 baada ya kifo cha Magufuli hakuna anayetaka nyungu, mwendo ni barakoa, kibanda cha ushirikina kikaondolewa hospital ya muhimbili kwa aibu. Hicho ndio chama tawala kinachoonekana kiko sawa! Acha wazungu waendelee kutuita manyani.
 
Friends and Enemies,

From Monopartisim to Multipartism 1992 to 1995,nchi yetu imepitia chaguz kadhaa ambazo tunaweza sema nchi bado ilikua changa kwenye Siasa za vyama vingi,na wakati mwingine tunaweza sema kwamba tumepitia siasa ya aina yetu na ya kipekee kama Taifa ambayo hatuwez jifananisha na nchi yoyote ya kiafrika kwa ujumla,

Mfano mzur wa nchi ya kidemokrasia kwa Afrika ni Ghana,wengine tuna safar ndefu kidogo ila ni muhim kuzid kujenga vyama imara vya upinzan ambavyo vitakuwa tayar kuongoza nchi bila ya kuwa na chembe chembe za ubaraka kutoka nchi za magharibi,

Tuwe wakweli,kuongoza Taifa siyo jambo la kufanya Rehearsal ndug zangu,wapinzan tulionao bado wanatia shaka Sana kuwaamin na kuwapa Dola waongoze,labda kama watashirikishwa kwenye serikali ya mseto lakin kiukweli hawana misimamo yenye kueleweka kias Cha kufikia sisi kuwaamin na kuwapa ridhaa ya kuongoza Dola,

Wakati mwingine tuna piga Kura kuwapa upinzan siyo kwamba tuna amin Wana uwezo huo,Bali ni kukosa matumain na baadhi ya mienendo ya CCM,sasa CCM ikijirekebisha na kuwatumikia watanzania kwa haki na usawa,upinzan huu tulionao hautaweza fananishwa hata kidogo na uongoz wa ccm,

Wapinzani tunawahitaji kwa mustakabali wa Taifa letu lakini wana Kazi ya kufanya kwa miongo kadhaa kupata ukomavu huo wa kuongoza Dola.
Mzee unasubiri MELI airport pole sana
 
Viongoz wenyewe wa upinzan hata ukiwangalia hawaish hiyo demokrasia wanayoihubir,mwangale profesa lipumba,kila siku yeye tuh,mwangale mbowe,kila siku yeye tuh,mwangalie mbatia na kadhalika,why hawatengenez generations za uhakika na kukasim madaraka kwao??
Katika watu wapumbavu hapa JF basi wewe ni mmoja wapo. Juzi juzi Magufuli akiwa anawabatiza waislam kwa moto ulikuwa umepotea na mara chache ulizojitokeza ulikuwa unaangua kilio cha ukandamizaji. Leo hii muislam kashika urais unabadili kauli. Hata mashabiki wa Magufuli walikuwa wamejiona kama watatawala milele na hakujua kabisa mambo yanaweza kubadilika kwa wiki moja. Ona sasa wanavyolia. Na wewe unajidanganya kuwa sasa ni wakati wa waislam. Haya jambo usilojua ni sawa na.......
 
Katika watu wapumbavu hapa JF basi wewe ni mmoja wapo. Juzi juzi Magufuli akiwa anawabatiza waislam kwa moto ulikuwa umepotea na mara chache ulizojitokeza ulikuwa unaangua kilio cha ukandamizaji. Leo hii muislam kashika urais unabadili kauli. Hata mashabiki wa Magufuli walikuwa wamejiona kama watatawala milele na hakujua kabisa mambo yanaweza kubadilika kwa wiki moja. Ona sasa wanavyolia. Na wewe unajidanganya kuwa sasa ni wakati wa waislam. Haya jambo usilojua ni sawa na.......
Huu ni uongo na uchonganishi.

Ni lini hao waislam walibatizwa kwa moto na Magufuli??
 
Katika watu wapumbavu hapa JF basi wewe ni mmoja wapo. Juzi juzi Magufuli akiwa anawabatiza waislam kwa moto ulikuwa umepotea na mara chache ulizojitokeza ulikuwa unaangua kilio cha ukandamizaji. Leo hii muislam kashika urais unabadili kauli. Hata mashabiki wa Magufuli walikuwa wamejiona kama watatawala milele na hakujua kabisa mambo yanaweza kubadilika kwa wiki moja. Ona sasa wanavyolia. Na wewe unajidanganya kuwa sasa ni wakati wa waislam. Haya jambo usilojua ni sawa na.......

Magufuli,hakuwasulubu waislam pekeyake,had christians walisulubiwa,

Had ccm wenyewe walisulubiwa,

Na nyinyi wapinzan mliplay very big role katika kumpa credit Magufuli,

Ni wangap kutoka huko chadema walihama na kuuunga mkono juhud za Magufuli??

Mosses machali,

Msando,Joshua Nassari, Wibroad Slaa,

Vicent Mashinji,Mwita waitara,

The long list kutoka kwenu kwenda kuunga mkono juhud, mnataka tuwaamin kwa lipi??

Bado mna Covid 19,mkiulizwa mnasema ooh wamerubuniwa na CCM...

Too bad,but hao ni zao lenu mjuuee
 
Hii sasa ndio rangi yako halisi , Uislam unautumia kama ngazi tu , tunakushukuru kwa kujianika hadharani
Wala mimi sidhani kitendo cha kubaka system nzima ya uchaguzi wa serikali za mitaa na vitongoji, na pia uchaguzi mkuu ni udhaifu. Ule ni uzandiki, ugaidi, udhulumati, ujeuri, ubabe, ufidhuli, ukatili, uuaji, ushamba, ushenzi, utapeli, uanaharamu, na udikteta wa kiwango cha juu. Kwa kuwa mleta uzi wewe ni mwanaccm, fungua macho. Tuna viongozi wa vijiji na vitongoji ambao hawakuchaguliwa na watu. Hawa wanatakiwa wajiuzulu. Tuna wabunge ambao walitangazwa tu bila kushinda ambapo sasa tuna mawaziri wanaotokana na wabunge hao.

Zaidi sana tuna raisi ambaye ni zao la ubakaji wa demokrasia uliofanywa na tume mbovu ya uchaguzi iliyokuwa chini ya dikteta mwendazake. Mwendazake na makamu wake ni zao la Katiba kuukuu ambayo hata Mwl. Nyerere aliita Katiba ya kidikteta. Hapa ni kujiudhulu tu na sio kurekebisha madhaifu. Tunahitaji Katiba mpya inayotokana na maoni ya Wananchi yaliyokusanywa na Tume ya Jaji Warioba iliyozunguka Tanzania nzima. Baada ya kuipata, uchaguzi mpya wa nafazi zote ufanywe ili tuwe ba viongozi waliopatikana kwa haki na kwa uhalali. Naamini hata Mwenyezi Mungu anataka tuwe ba Katiba mpya.
 
Kwanza kitendo cha kuwa na vyama pinzani vingi tu ni ishara kwamba hata wao kwa wao ni wapinzani baina yao,hivyo hakuna cha maana watakacgofanya zaidi ya kelele
Poleni sana,
Kwa hiyo mwataka 'upinzani' wenu tu akina TLP, CUF, PONA na NCCR ndio uendelee kuwapo. Ili iweje?
 
THE BIG SHOW ,

..kama kuna jambo CCM wanapaswa kujirekebisha au kuachana nalo ni matumizi mabaya ya VYOMBO VYA DOLA.

..kila wanapozidiwa kwa hoja CCM hukimbilia kutumia dola dhidi ya aliyewazidi.

..Mashekhe wa Uamsho walitumiwa vyombo vya dola baada ya CCM kukosa majibu ktk hoja ya haki na nafasi ya ZNZ ktk muungano.

..Wananchi wa kusini walitumiwa askari wawapige kwasababu CCM walishindwa kujibu hoja ya matumizi ya gesi asilia inayochimbwa maeneo ya kusini.

..nitaishia hapa.
 
THE BIG SHOW ,

..kama kuna jambo CCM wanapaswa kujirekebisha au kuachana nalo ni matumizi mabaya ya VYOMBO VYA DOLA.

..kila wanapozidiwa kwa hoja CCM hukimbilia kutumia dola dhidi ya aliyewazidi.

..Mashekhe wa Uamsho walitumiwa vyombo vya dola baada ya CCM kukosa majibu ktk hoja ya haki na nafasi ya ZNZ ktk muungano.

..Wananchi wa kusini walitumiwa askari wawapige kwasababu CCM walishindwa kujibu hoja ya matumizi ya gesi asilia inayochimbwa maeneo ya kusini.

..nitaishia hapa.

Uko sahihi kabisa Mkuu,

Je,kwa upinzan huu wa watu kama chadema ya mbowe,cuf ya lipumba na kadhalika,ambao hawana guts za kuitengeneza succession plan ndan ya vyama vyao,je unadhan hata wakipewa Katiba mpya,watawezaje kukosa hii caliber ambayo CCM wanayo??
 
Magufuli,hakuwasulubu waislam pekeyake,had christians walisulubiwa,

Had ccm wenyewe walisulubiwa,

Na nyinyi wapinzan mliplay very big role katika kumpa credit Magufuli,

Ni wangap kutoka huko chadema walihama na kuuunga mkono juhud za Magufuli??

Mosses machali,

Msando,Joshua Nassari, Wibroad Slaa,

Vicent Mashinji,Mwita waitara,

The long list kutoka kwenu kwenda kuunga mkono juhud, mnataka tuwaamin kwa lipi??

Bado mna Covid 19,mkiulizwa mnasema ooh wamerubuniwa na CCM...

Too bad,but hao ni zao lenu mjuuee
Mimi ni mwanademokrasia nisiye na chama chochote. Kwangu mimi Tanzania bila mfumo mpya wa utawala utakaoziba loopholes zote zilizotufanya tufeli kujitawala na kujiletea maendeleo hakuna kipya. Si wapinzani, si CCM. Wapinzani angalau wananifanya niwaunge mkono kwa sababu wanakiri mfumo tulionao haufai kitu ambacho CCM hawakioni. Ni kweli Magufuli alisulubu kote lakini sehemu nyingine kama baraza la mawaziri na teuzi nyingine hakujali kelele wanazopiga kabisa. Alipunguza hata ile idadi ya zamani waliyokuwa wanalalamikia kuwa ni wachache.
 
Uko sahihi kabisa Mkuu,

Je,kwa upinzan huu wa watu kama chadema ya mbowe,cuf ya lipumba na kadhalika,ambao hawana guts za kuitengeneza succession plan ndan ya vyama vyao,je unadhan hata wakipewa Katiba mpya,watawezaje kukosa hii caliber ambayo CCM wanayo??

..hawataweza kwasababu katiba bora mpya itawabana kabla hata hawajanogewa na asali ya kutawala.

..chama chochote kile kikiongoza kwa katiba hii ya sasa hivi lazima kitakengeuka na kuwa cha kifedhuli kama ilivyo ccm.

..pia mazingira yetu ya kisiasa sio ya HAKI na naamini hali hiyo inapelekea radicalization ya watu wa upinzani.

..mtu anayeonewa au anayejisikia kuwa hatendewi haki hawezi kuwa na lugha nzuri na staha anapozungumza na wale wanaomuonea.

..tatizo la succession planning na wapinzani kutokupata watu wazuri kunatokana MADHILA wanayoyapitia ndugu zetu walioko huko.

..sio rahisi kwa Mtanganyika mwenye elimu nzuri, uzoefu wa kazi, au biashara ya maana, kujiunga na upinzani wakati anaona kila siku wapinzani wanakuwa arrested, wana makesi yasiyokuwa na kichwa wala miguu, wanapigwa marisasi utasema ni magaidi, na jamii haionekani kuwatetea.

..I am sure kuna watu very educated and seasoned in their professions hawakubaliani na ccm, na wangependa kujiunga na upinzani, lakini wanakatishwa tamaa na UNYAMA unaofanywa na CCM dhidi ya upinzani.

..Walioko upinzani hapa Tanzania ni watu ambao wamejitokea kwelikweli na tunao wajibu wa kuwatetea.
 
Viongoz wenyewe wa upinzan hata ukiwangalia hawaish hiyo demokrasia wanayoihubir,mwangale profesa lipumba,kila siku yeye tuh,mwangale mbowe,kila siku yeye tuh,mwangalie mbatia na kadhalika,why hawatengenez generations za uhakika na kukasim madaraka kwao??
Hawana institution wana individuals ambao hawajawahi kukubali kutengeneza susuccession plan...Nchi uwape watu ambao wamejaa uanaharakati badala ya kuja na ideology mbadala?
 
Generation wataandaje sasa?! Kila wakiandaa vijana mnawanunua?! Nani hakumbuki manunuzi ya ajabu ya wanasiasa wa upinzani iliyofanywa na hayati? Wale wenye misimamo thabiti mkawapiga risasi (Lissu), mkawachinja (Mawazo) na kuwapoteza (Beni Sanane). Wafanyeje zaidi?
Long as wana nunulika basi ndiyo huko kushindwa kuwaandaa
 
Nyerere alikaa madarakani miaka 24 na hadi leo anasifiwa ni bonge la kiongozi. Baada ya ile mada yako ya kinafiki ya jana naona umekuja kupima upepo.
Two wrongs don't make a right. Kwa vile Nyerere alikaa madarakani miaka 24 ndio excuse ya kiongozi wa upinzani kukaa madarakani miaka 17? And why Nyerere na sio Mwinyi, Mkapa au Jk?
 
Tunahitaji Katiba mpya inayotokana na maoni ya Wananchi yaliyokusanywa na Tume ya Jaji Warioba iliyozunguka Tanzania nzima. Baada ya kuipata, uchaguzi mpya wa nafazi zote ufanywe
Hivi kweli nyinyi watu mko sawasawa vichwani??

Haya tusubirini katiba mpya na uchaguzi mpya
 
Back
Top Bottom