Sio tu wa vijijini!Naam ujinga wa Watanzania na hasa walio vijijini na ambao hawana fursa ya mtandao ndio mtaji mkubwa wa CCM.
Watu wa vijijini wengi na baadhi ya walio mijini ambao hawana mtandao hawapati taarifa sahihi kwa wakati na wakati mwingine hupata taarifa za uongo au kilaghai zilizochujwa na vyombo vingi vya habari ili kuonesha wema wa serikali na CCM ili kuwadanganya wao waone Serikali na CCM wanafanya vyema na kisha wawachague.
CCM huzunguka vijijini kuwadanganya wananchi wa huko kuwa wakiwachagua vyama pinzani kutakuwa na vita mara hawatapelekewa maendeleo, wanatumia ujinga wao wa kutokuwa na taarifa sahihi kuwalisha taarifa za uongo zenye manufaa na wao.
Wananchi wote inabidi tujitahidi kwa ambao tuna ndugu vijijini tuweze kuwafumbua macho ndugu zetu waache kulaghaiwa na CCM.
Mimi juzi hii baada ya uteuzi na mabadiliko yaliyofanywa na Rais Chongolo akiingia tena ulingoni.
Nikiwa Mkoani nikaongea na jamaa yangu nikimtania vipi sijakusijia kwenye teuzi za juzi!
Ikiwa ni siku ya Tatu yake ananiambia mbona Sina Habari yoyote ile!Ile!! Ukweli tu hana simu ya kuweza kuingia mtandaoni hivyo wenginwa waTanzania hawapati Habari motomoto na hasa kauli za wapigania haki na Katiba mpya na wengine wanaijua CCM zaidi hasa wanapohitaji huduma za Serikali mtaa na kuliwa kichwa bila kujua uhuru na haki zao.
Balozi mwenyewe wa nyumba kumi na kakibanda njaa kaweka bendera hapo kwa mlango suruali chanika hapo nyuma bado hajitambui kavaa kofia ya Kijani imezeeka mbaya.
Ni majanga.