CCM: Kamati ya siasa ya CCM mkoa wa Kilimanjaro kagueni ujenzi wa geti jipya la Chuo cha Polisi Moshi, kabla Rais hajalifungua tar 17.9.2024

Weka picha tuone unachoongea tulinganishe ukweli wako na uongo wangu.
 
Weka picha! Kazi mliyonayo ni kumtuma Rais wetu kufungua miradi ambayo haijakamilika,akishafungua hamkamikishi Tena.
Kila siku ni kumsababishia Samia short na ajali ya kisiasa kupitia miradi mibovu
 
kwan jukumu la ukaguzi wa kiradi ni jukumu la kamati ya siasa ya mkoa?

Sasa mawaziri wenye dhamana husika watafanya nini?

Igp anafanya nini kama kamati ya siasa ndo itafanya hayooo. Anyway hebu tupe somo mleta mada inawezekana kunachakujifunza hapa

Anyway inawezekana mimi ndo sijui?
 
Miradi yote inayotekelezwa na serikali ndani ya Mkoa ,ni kazi ya kamati ya siasa ya mkoa kukagua miradi hiyo,na mkuu wa mkoa ni mjumbe wa kamati hiyo.

Sasa ninashangaa,mkuu wa mkoa hajui Wala hajakagua mradi huo,Rais anakuja kuufungua na eneo sio rafiki kimazingira vumbi kibso, mitaro ya maji ya mvua hakuna, hakuna maji safi na salama, mawe , uchafu,hakuna ukokwa, ni aibu tupu
 
Kama ndivyo wanawajibu wa kukumbushwa wajibu wao kama chama
 
Kwanza, mwenyekiti wa mtaa anatosha kufungua hilo geti.

Pili, Kwanini CCM kwani polisi ni ya CCM?
Soma katiba ya JMT utaelewa Serikali imeundwa/inamilikiwa na Chama Gani...na Irani inayotekelezwa kwa sasa ni ya Chama Gani...pia tafuta maana halisi ya slogan ya KIDUMU CHAMA TAWALA
 
Soma katiba ya JMT utaelewa Serikali imeundwa/inamilikiwa na Chama Gani...na Irani inayotekelezwa kwa sasa ni ya Chama Gani...pia tafuta maana halisi ya slogan ya KIDUMU CHAMA TAWALA
Hata kama ndio kumtoa raisi huko aliko aje kugungua geti 😀😀
 
Kwa nini isiwe Kamati ya Ulinzi ya Mkoa na iwe kamati ya siasa ya CCM ya mkoa.
 
 
Waziri Mh. Hamad Masayuni, badili uelekeo,wakati unakwenda kuingia, chuo cha polisi Moshi,kufungua mkutano,ingilia kwenye geti,jipya ujionee malalamiko haya
Kumuita kiongozi wa chini,na mwenyekiti wa chama Taifa,kuja kufungua geti Hilo ni aibu.

Wafanye marekebisho ya haraka, kutengeneza mitaro ya maji ya mvua, usafi, kumwaga maji kuondoa vumbi, waoteshe ukoka na miti, wafunge maji ya bomba , waokote mauchafu na mawe yaliyozagaa huko, nyaya zimesambaa chini hazijulikabi ni za umeme, wajenge choo cha watumishi watakao hudumia hilo getini, na mwisho kabla Rais ajafungua mradi huo, asomewe taarifa ya gharama ta mradi( value for money ionekane.)
 
Hata kama ndio kumtoa raisi huko aliko aje kugungua geti 😀😀
Sasa Hilo ni jambo la nini ni kipaumbele chao...namna wanavyopanga ratiba zao na kutumia muda wao, ni vigumu kwa watu Baki kama mimi kutambua.
 
Mradi huu,usipokaguliwa,Kuna Kila dalili Rais akasomewa taarifa ngumu,naye akawatangazia watanganyika kuambiwa ujenzi wa geti umegharimu 2.6 billion, wakati geti Hilo limeshikana na bara bara mbovu,inayoelekea hospital ya Rufaa ya Kanda ya KCMC, ambayo matengenezo yake ni 2.6 billion umbali WA KMS 2.6, na wanasema hawana fedha.

Fedha za geti zimetokea wapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…