CCM: Kamati ya siasa ya CCM mkoa wa Kilimanjaro kagueni ujenzi wa geti jipya la Chuo cha Polisi Moshi, kabla Rais hajalifungua tar 17.9.2024

CCM: Kamati ya siasa ya CCM mkoa wa Kilimanjaro kagueni ujenzi wa geti jipya la Chuo cha Polisi Moshi, kabla Rais hajalifungua tar 17.9.2024

Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Kilimanjaro inapaswa kukagua mradi wa ujenzi wa geti jipya la kuingia chuo cha polisi Moshi, na kujiridhisha kabla ya Rais na Mwenyekiti wa CCM Taifa hawajafika kuufungua. Hadi sasa, vyombo vya ndani vimefanya uchambuzi wa eneo hilo, lakini mradi huo haujakamilika. Usafi wa mazingira haupo katika kiwango kinachotakiwa, mitaro ya maji ya mvua bado haijajengwa, na kuna vumbi kubwa sana.

Aidha, ukuta wa mradi haujakamilika, na eneo hilo
halina huduma za maji wala umeme. Kuweka wazi, mradi unafunguliwa kwa kigezo gani ikiwa mazingira ni mabaya kiasi hiki?

Pia, thamani ya mradi kulingana na fedha zilizotumika haionekani kuwa sawa. Mandhari na mazingira ya eneo hili ni aibu kabisa.

Soma pia: IGP: Barabara za kuingia ndani ya Chuo cha Polisi Moshi Kilimanjaro,wajawazito wanashindwa kwenda kujifungulia zahanati ya chuo barabara ni mbovu.

Ni muhimu kutafakari hatua hizi kwa sababu kuna hatari ya kumjaribu Mheshimiwa Rais badala ya kumheshimu. Hali hii inaweza kupelekea aibu kubwa kwa chama na serikali.

Ni vyema kuchukua hatua za haraka ili kuhakikisha mradi huu unafikia viwango vinavyotakiwa kabla ya ufunguzi rasmi.
Kwani kamati hiyo ndio inatoa ithibatii
Wee Jeshi linautaratibu wake!
Hivyo acha kuropokaaa

Jeshi linautaratibu ushawai kusikia mkuu wa wilaya ameenda kwenye kambi yoyote
 
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe.Nurdin Hassan Babu akiwa na Kamati ya Siasa ya Mkoa leo septemba 23,2024 wamefanya ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi kupitia miradi ya Maendeleo wamekagua ujenzi wa barabara ya bomang'ombe - Sanya juu yenye urefu wa kilomita 25 iliyopo katika halmashauri ya wilaya ya Siha na kuwataka wananchi kutunza miundombinu hiyo kwa ajili ya manufaa jamii nzima.

View: https://www.instagram.com/p/DARKobwtCVi/?igsh=ODFud25uMDB0bXdm
 
Back
Top Bottom