CCM kumeguka iwapo Polepole atafukuzwa uanachama na huu ndio mwanya wa upinzani kupata nguvu 2025

Tatizo lowasa kashfa ya Richmond ilimchafua angekuwa msafi lowasa chadema mngeongoza
Hakuna cha kashfa, watanzania wanajali unadhani kuhusu hilo? Tanzania hawana sababu ya kukupenda wala kukuchukia ndiyo maana na ufisadi wote bado CCM iko madarakani
 
Kuna mambo yanachekesha wapinzani wenyewe akina zitto, cheyo na lipumba tupilia mbali nguvu za kivyama hao hata nguvu za kiume hawana
Kuchukua $ naona bado hawa hawako serious

Ccm kwenye vita wanaunganaa wanakupiga

Ova
 
Ninavuojua njaa za mswahili akipewa hata bajaj ataendelea kusema NDIO MZEE
 
Mnamjaza ujinga BWANA KOBE.
 
Naamini Magufuli hajawahi kushinda urais
Lakini alikuwa ndiyo rais wetu
Kwa hilo tu tukiacha haya mengine hakuna sababu ya kuwazia kwamba chadema itasumbua ccm

2025 zito anaenda kupewa wabunge kadhaa ili awe chama kikuu cha upinzani
Chadema hapewi hata diwani mmoja

Chadema wanalegalega wakidhani kwamba wamewatisha ccm labda wataenda kuwaonea huruma huko kwenye uchaguzi ujao
Ukweli ni kwamba muda walio nao chadema ndiyo huu kama watashindwa kuforce katiba mpya na tume huru wasije wakajisumbua kuingia kwenye uchaguzi

Katiba ilibidi iwe ndiyo habari
inayoongelewa kila mahali kwa sasa
Kila kona utakayokuwepo lazima usikie habari ya katiba na wananchi wangezidi kusikia na kuelewa kuhusu katiba

Vitu kupanda bei ovyo ilikuwa ni nafasi nzuri sana ya kuongea na wananchi masikini kuhusu katiba na wangeelewa tu chadema wamerelax wanaongea kiuwepesi tu huku siku zinaenda


Kipindi ambacho lowasa anagombea na kushindwa kama angeita watu kuandamana watu wangeandamana na majibu yangepatika lakini alikaa kimya na watu wasijue nini kilimpata au nini kilitokea hapa katikati

kwa kipindi kile raia waliamua
Baada ya kuchoka uongozi wa ccm na haswa Kikwete lakini pia Lowasa alivyotoka ccm na kuingia chadema iliwavutia wengi zaidi baada ya kuona kama u snitch aliofanyiwa huko ccm kwao

Kwanini watanzania kwa sasa hawawezi kuandamana
Watu wanashindwa kuandamana kutokana na uwoga
Enzi ya Kikwete demokrasia ilikuwa juu sana nchi hii japo alikuwa na mapungufu yake mengi mengine lakini tulikuwa na demokrasia kwa kiwango kikubwa sana
Ndiyo maana nasema Lowasa angetaka angeandamanisha watu kwa kuwa watu hawakuwa na uwoga hakukuwa na vitisho kiwango hichi cha leo
Enzi ya Magufuli udikteta vitisho vingi ambavyo ni halisi sana yani ukicheza na moto unaungua kwelikweli wananchi wameingia uwoga Lisu amekuja yuko tayari kuingiza watu barabarani lakini watu wamejawa uwoga kutokana na vitisho vya uongozi wa Magufuli
Chadema wana jukumu la kuelimisha raia kuhusu haya mambo na kuwaondoa hofu
Tofauti na hapo hamna kitu
 
Waache wang'atane
 
Polepole ni mnafiki na alishachafuka,labda akaanzishe chama cha kuokota mibuyu kwao Dodoma na sio cha siasa.
Kipindi kile anashiba hakuyaona hayo.
 
Polepole hana nguvu wala mtandao mkubwa kama mzee Lowasa, wengi wanamuona kama mhamiaji tu. Hana madhara hata akifukuzwa
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] yaani Polepole ndo aigawe CCM seriously? Hakuna mwana ccm mjinga kiasi hicho eti aondoke ccm kisa kiroboto.
 

Hawaijui CCM. Wakaisome vizuri historia yake na hata historia ya wazazi wake(TANU na Afro)
 
Mi ni CCM hila tujitafakari sana hatuta tawala milele maana kuna vitu vya msingi tuviweke sawa, kukomoana hakuleti tija Nchi ni yetu sote,watoto wa Baba na Mama mmoja.Kwa nini Watu hawana Uhuru wa kujieleza na kutoa maoni?

Sent from my TECNO B1g using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…