bulichekaHaya wamerudishwa Wakurugenzi wamebaki walewale nani atawalindia kura zao?
Kumbeee..bulicheka
Kwenye safari ya mapambano lazima ujue kuwa ni safari ndefu na yenye magumu mengi sana...........
Hiyo ni hatua moja kuelekea kwenye ushindi kamili, hilo suala la kulinda kura waachie mawakala wa vyama na hao wakishindwa, basi Umma wa watanzania upo tayari kuingia barabarani, iwapo itathibitika kuwa kura zimeibiwa kwenye sanduku la kura
Hawa mapungu wa Lumumba wameambiwa na bashiru kujibu hoja mtandaoni basi wanajibu bila kutumia akili. Ujinga mtupu. Akili za kuambiwa changanya na za kwako. Mmekuwa vituko mtandaoni. Kama huna hoja kaa kimya, acha kuandika uharo. Buku 7 zinakuondolea heshima!!!
Mkuu Wangu Akili Wanazo Ila Sisi UVCCM Tuko mchanganyiko.... km ilivyo wengine popote pale....πππWachanganye na zipi ikiwa wao hawana hizo akili!
Hawa mapungu wa Lumumba wameambiwa na bashiru kujibu hoja mtandaoni basi wanajibu bila kutumia akili. Ujinga mtupu. Akili za kuambiwa changanya na za kwako. Mmekuwa vituko mtandaoni. Kama huna hoja kaa kimya, acha kuandika uharo. Buku 7 zinakuondolea heshima!!!
Uchaguzi huru na wa haki ukifanyika CCM itapata kura za wanaukoo walioko madarakaniSiyo siri kuwa hizi njama zilizofanywa na hawa wasimamizi wa majimbo, ambao ni makada waaminifu wa CCM, kuwaengua kihuni wagombea wa vyama vya upinzani, kwa wingi na baadaye Tume ya uchaguzi kuwarejesha, kutakuwa kumewaongezea umaarufu mkubwa hao wagombea wa upinzani
Ni lazima hivi sasa wananchi watakuwa na hamu mno ya kuwasikiliza hao "wahanga" walioenguliwa na hao makada wa CCM na baadaye kurudishwa na Tume ya uchaguzi ya Taifa, kwa ilichokidai kuwa sababu za kuenguliwa kwao hao wagombea wa vyama vya upinzani hayakuwa ya msingi
Hivi unaweza anza jiuliza ni "makosa" gani waliyoyafanya wakati wakijaza fomu hao wagombea wa upinzani hadi waenguliwe kwa maelfu nchi nzima, wakati hakuna hata mgombea hata mmoja wa CCM aliyeunguliwa?
Hivi hawa wagombea wa CCM "waliibia" majibu ya kujaza hizo fomu kwa usahihi wa asilimia 100, hadi waonekane "malaika" na hao wasimamizi wa uchaguzi maDED na wapitishwe kwa asilimia 100?
Hao wasimamizi wa uchaguzi maDED, ambao ni makada wakubwa wa CCM, ndiyo waliopewa jukumu nyeti la kuwa "fair" la kusimamia uchaguzi ulio huru na wa haki.
Hakika kama ni mtihani wameshindwa vibaya na kama siyo bosi wao Jiwe ndiye "aliyewaagiza" kufanya madudu yote haya, wangejikuta wamefukuzwa kazi Mara moja!
Kwa Bahati mbaya walifanya "rewind" ya kile walichofanya kwenye ule uchaguzi uliopita ambao ulivurugika wa serikali za mitaa, ambao "walilazimisha" wagombea wao wa CCM kuwa wameshinda na kutulazimisha kuwa ndiyo viongozi waliochaguliwa na wananchi kwa asilimia 99.9!
Sasa ndiyo tunaweza kuamini maneno yaliyotamkwa na Jiwe kwa wakurugenzi hao nanukuu "wewe Mkurugenzi ninakulipa mshahara mnono, gari la kifahari la kutembelea na nyumba nzuri ya kuishi, halafu nisikie kwenye eneo lako, umemtangaza mpinzani kashinda, ujihesabu kuwa umejifukuzisha kazi" mwisho wa kunukuu
Hivi sasa ndiyo tutatambua hivi vitendo vya hawa makada wa CCM ambao ndiyo wasimamizi wa uchaguzi namna vilvyo "backfire"
Hivi nyinyi maccm mnategemea hizo "cheche" atakazouunguruma nazo Maalim Seif huko Zanzibar baada ya kuenguliwa na baadaye kuejeshwa na Tume vitakuwaje?
Hivi unategemea na huyu "kibonge" Jacob mgombea wa ubunge wa Ubungo, hivyo vigongo atakavyoshuka navyo vitamuweka salama Dkt Mkumbo ambaye aliamini anateleza kiulaini kama vile yuko kule mteremko wa kule Kitonga?
Wahenga walinena kuwa mwisho wa ubaya ni aibu!
Kwa hiyo nyinyi maccm ndiyo mliolikoroga wenyewe, kwa hiyo hivi sasa muwe wapole na kulinywa!
Jitahidini na nyie muwe na makada kama CCM wananchi wamewabaini wachumia tumbo, Chama gani kisichokuwa na wafia chama kila siku mnahama. jitahidini mpate na ninyi makadaHabwabwaji kaongea kweli tupu...viongozi wa tume ni makada wa ccm na ushahidi wa video umo mpaka humu JF
NEC ni mali ya CCM ... hilo mbona liko wazi. Kuanzia Mwenyekiti, Mkurugenzi wa NEC, Macommissioner, Wakurugenzi wote wanateuliuwa na Mwenyekiti wa CCM ......JIBU SWALI KWANZA. KWANI NEC NI MALI YA CCM?
Unafaham uteuzi wa hao watu, nani anapaswa kuwateua hao watu kwa mjibu wakatiba?NEC ni mali ya CCM ... hilo mbona liko wazi. Kuanzia Mwenyekiti, Mkurugenzi wa NEC, Macommissioner, Wakurugenzi wote wanateuliuwa na Mwenyekiti wa CCM ......
Nikweli upinzani umekufa, Hilo linajulikana, usibabaishwe na hizi kelele unazozisikia, wanatimiza wajibu tu mkuu.Hivi nyinyi maccm mbona mnaogopa mno ushindani kwenye uwanja wa mapambano?
Si ndiyo nyinyi mlikuwa mnadai kuwa upinzani hapa nchini umekufa?
Hivi kama upinzani hapa nchini umekufa kama mnavyodai nyinyi wenyewe, hivi mngetumia nguvu yote hii kufanya hizo figisu figisu za kuwaengua kihuni wagombea wetu wa vyama vya upinzani?
We we unayelifaham thibitishaaa.Utakuwa Mbumbumbu sana kama hata hilo jambo dogo kiasi hicho unashindwa kuling'amua