Uchaguzi 2020 CCM kuzindua kampeni Jumamosi, Agosti 29, 2020 uwanja wa Jamhuri, Dodoma

Uchaguzi 2020 CCM kuzindua kampeni Jumamosi, Agosti 29, 2020 uwanja wa Jamhuri, Dodoma

Richard

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2006
Posts
15,692
Reaction score
23,038
CCM inazindua rasmi kampeni za uchaguzi ujao siku ya Jumamosi katika viwanja vya jamhuri mjini Dodoma.

Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr. John Magufuli anatarajiwa kutikisa kitovu hicho cha nchi mji wa Dodoma na vitongoji vyake kwa hotuba yake ilopangwa maalum kwa siku hiyo.

Katibu wa CCM wa mkoa wa Dodoma bi Pili Mbanga amethibitisha habari uzinduzi wa kampeni hiyo na kusisitiza kwamba uzinduzi huo utakuwa ni wa aina yake.

Uzinduzi wa Jumamosi utakuwa ni wa mara ya kwanza kwa CCM kuanzisha kampeni ndani ya makao makuu ya Chama Cha mapinduzi na makao makuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa mujibu wa tume ya Uchaguzi NEC uzinduzi wa kampeni kiufundi ulianza tarehe 26 August 2020, hivyo wagombea wote walopitishwa kugombea nafasi mbalimbali ikiwemo nafasi ya uraisi wa JMT wanaruhusa ya moja kwa moja kuanza kampeni.

Vyombo mbalimbali vya habari vimealikwa kuhudhuria uzinduz huo na kuuonyesha moja kwa moja kutoka Dodoma.

Televisheni au "Telly" ya Taifa TBC inatarajiwa kurusha matangazo ya uzinduzi huo yatakayoonekana nchi nzima, moja kwa moja yaani "Live" kutoka mjini Dodoma.

CCM mwaka huu inaingia katika kampeni bila kutegemea sana migogoro ya wapinzani ambayo iliwanufaisha kwa kiasi kikubwa kwenye uchaguzi wa mwaka 2015.

Mpaka sasa ni jambo lisilo ubishi kwamba CCM inajiamini kwa aina ya serikali ilounda ambayo imejikita katika kutekeleza kwa vitendo miradi mingi ya maendeleo ambayo haihitaji mtu kuitafuta bali yote yaonekana wazi.

Miundombinu mbalimbali kama madaraja na maboresho na ujenzi wa reli mpya, mradi wa umeme vijijini na kufikiwa kwa malengo ya ukusanyaji kodi ni miongozi mwa sera za CCM ambazo iliziahidi ingezitekeleza na imefanya hivyo.

Wananchi wa Tanzania hivi sasa wanasubiri kumsikia Rais John Magufuli atazungumzia masuala yepi siku ya Jumamosi huku akiomba kuendelea na miaka mingine mitano ya kuiongoza Tanzania.

Ni siku ya Jumamosi tarehe 20, August 2020 ndio itakayotoa khasa makusudio ya CCM kutaka tena kuongoza nchi hii kupitia kampeni zake zitakazoichukua kuzunguka tena katika mikoa mbalimbali.
 
Umefoka mpaka ukajisahau na kuanza kumpigia kampeni Meko! Aya ya 9 na ya 10 hazikupaswa kuwepo kwenye habari yako!

Sishani kama nimepiga kampeni.

Nimeelezea kinachotarajiwa kushindanishwa.
 
Huna tofauti na kina YEHODAYA jingalao Barbarosa Simiyu Yetu Pascal Mayalla na Lumumba FC wengine!

Huna heshima ya kujiita mchambuzi huru zaidi ya kuwa kada wa CCM

Tatizo ni hilo, ninyi hamtaki mawazo ya aina tofauti na ya kwenu, hata kama anaetoa maoni hayo si wa kutoka Lumumba.

Ni kama sasa hivi hakuna ambae atasema kitu na Tundu Lissu akamsikiliza, hata Mbowe ameamua kukaa kimya.

Mkubali au mkatae, mkakati wenu unafeli vibaya.
 
Mimi najiamini bado ni mchambuzi huru.

Maendeleo hayana vyama.

Kwa hiki kinachoendelea, maneno yangu kuwa ccm sio chama cha siasa bali ni kikundi cha dola kilichojivika koti la chama cha siasa yanazidi kupata nguvu. Kwa sasa ccm haiko madarakani kwa ridhaa ya umma, bali inatumia madaraka ya rais kushurutisha kukaa madarakani.

Hata mtumie nguvu kubwa kiasi gani, na kulazimisha kutumia vyombo vyote vya habari, kama hukubaliki haukubaliki tu. Hii inaitwa kuvuta riziki kwa kamba.
 
Vipi yale malori mliyo omba kubeba watu mmesha pata? Wafanya biashara mlio walazimisha wawachangie mme pata kuasi gani?
Maana bila hivyo hampati watu mtajikuta mko na mgombea tu.

Issue tv msituambie maana hatuziangalii tena. Tumehamia mitandaoni.
 
Meko ni kama vile anaomba kazi ya waziri wa miundombinu, hagusii kuboresha maisha ya watu.
 
Kwa hiyo kampeini zitafunguliwa na Magufuli mwenyewe, siyo Kikwete wala Mwinyi. Tulizowea kampeini zinazinduliwa na rais mstaafu mmojawapo.
 
Kwa hiyo kampeini zitafunguliwa na Magufuli mwenyewe, siyo Kikwete wala Mwinyi. Tulizowea kampeini zinazinduliwa na rais mstaafu mmojawapo.
Yohana anataka ujiko yeye mwenyewe. Hao wengine wataalikwa ili kuonyesha mshikamano.....!!
 
Yohana anataka ujiko yeye mwenyewe. Hao wengine wataalikwa ili kuonyesha mshikamano.....!!
Nadhani hilo ni kosa kimkakati; kampeini inatakiwa ifunguliwe na kufungwa mtu tofauti na mgombea. Kwa mfano wakati wa uzinduzi, angefungua kampeini mtu maarufu asiyekuwa kwenye siasa sasa hivi kama Kikwete au Mwinyi, kabla mgombea mwenyewe hajaanza kujitangaza. Halafu wakati wa ufungujadi, mgombea anatoa summary ya mipango ya serikali yake akichaguliwa, na baadaye kufungwa na mtu maarufu kama Kikwete au Mwinyi.

Hiyo ni kwa CHEDAM pia, inatakiwa ifunguliwe na kufungwa na mtu maarufu asiyekuwa kwenye siasa sasa hivi ingawa hawana wengi wa namna hiyo, hivyo itakuwa ni jukumu la Mbowe tu
 
utawala wa Magufuli umeharabu kbs demokrasia ya nchi yetu, ni kama vile vyama vingine vya siasa haviruhusiwi kuwepo...so sad!.
 
Acha kuonyesha UJUHA WEWE! Mawazo tofauti ya kuruhusu udhalimu na udhalilishaji kama huu wa huyo yesu fake? Utajitoa UFAHAMU hadi lini?


Tatizo ni hilo, ninyi hamtaki mawazo ya aina tofauti na ya kwenu, hata kama anaetoa maoni hayo si wa kutoka Lumumba.

Ni kama sasa hivi hakuna ambae atasema kitu na Tundu Lissu akamsikiliza, hata Mbowe ameamua kukaa kimya.

Mkubali au mkatae, mkakati wenu unafeli vibaya.
 
Nadhani hilo ni kosa kimkakati; kampeini inatakiwa ifunguliwe na kufungwa mtu tofauti na mgombea. Kwa mfano wakati wa uzinduzi, angefungua kampeini mtu maarufu asiyekuwa kwenye siasa sasa hivi kama Kikwete au Mwinyi, kabla mgombea mwenyewe hajaanza kujitangaza. Halafu wakati wa ufungujadi, mgombea anatoa summary ya mipango ya serikali yake akichaguliwa, na baadaye kufungwa na mtu maarufu kama Kikwete au Mwinyi.

Hiyo ni kwa CHEDAM pia, inatakiwa ifunguliwe na kufungwa na mtu maarufu asiyekuwa kwenye siasa sasa hivi ingawa hawana wengi wa namna hiyo, hivyo itakuwa ni jukumu la Mbowe tu
Wafanye hivyo au wasifanye watashinda tu. Ni sawa na ule usemi anaoambiwa jogoo kua "uwike usiwike kutakucha". Hilo kosa la kimkakati lingekua na athari kama kungekua na uwanja sawa na nia ya dhati ya kushindanisha sera na atakayeshinda kwa haki ndio anatangazwa
 
Back
Top Bottom