Uchaguzi 2020 CCM Maji ya shingo Temeke, mgombea wao wa ubunge hafahamiki popote, Sina Manzi wa CHADEMA ang'ara

Uchaguzi 2020 CCM Maji ya shingo Temeke, mgombea wao wa ubunge hafahamiki popote, Sina Manzi wa CHADEMA ang'ara

Ikiwa kumesalia mwezi mmoja tu kufanyika kwa uchaguzi mkuu, hali ya CCM kwenye jimbo la Temeke ni dhoofuli hali, Mgombea wake aliyeshindwa kura za maoni na Abbas Mtemvu aitwaye Dorothy Kilave hawezi kushinda uchaguzi kwa vile hajulikani na wapiga kura wala hajulikani hata anakoishi, hana ushawishi wala hana hata uwezo wa kupiga kampeni.

Taarifa zingine zinaonyesha kwamba makundi na makovu ya kura za maoni ndio yaliyomteketeza, wapambe wa Mtemvu ambao ni 75% ya wanaccm wote wa jimbo hilo wamejiapiza kutomchagua mama huyo mjane aliyefiwa na mumewe miaka michache iliyopita kwa madai kwamba mama huyo ni chaguo la Makao Makuu na wao hawahusiki naye, hatima yake iko mikononi mwa Tume kwenye uchakachuaji.

Bali njia ni nyeupe kwa Mgombea ubunge wa CHADEMA.

View attachment 1584725

Ambaye duru zinaonyesha kwamba ni mtoto halisi wa Temeke mwenye vinasaba vya Mtoni kwa Azizi Ally na Yombo Buza , maeneo yanayoaminika kuwa na wakazi wengi mno na wapiga kura , huku umaarufu wa Chama chake cha Chadema , chama kinachohubiri maendeleo ya watu na uhuru ukimbeba .
Hata Hadija Said Mwago huenda akashinda jimbo la Mbagala.
 
Kuna vitu huwa watu mnazungumza sijui kwa kutumia nini.
Hivi unajua huyo hadija mwago hawezi kupata kura hata robo ya atazopata chaurembo?
Swali lingine kwako, unajua huyo hadija hajaonekana kwenye kampeni ana wiki kadhaa sasa?
Hata Hadija Said Mwago huenda akashinda jimbo la Mbagala.
 
Kunipuuza ni uamuzi wako, ila kukwambia ukweli ni jukumu langu.
Hakuna tunayemuongopea, kuishinda ccm kwenye hayo majimbo haiwezekani tena. Mimi sio shabiki bali ni mwanachama, ninajua kusema la ukweli na kukanusha uongo.
Nakupa mfano; nilikuta sehemu ccm wanasema watashinda bunda na tarime vijijini, nikawaambia mnajiongopea, hiyo ni ndoto na hamtaweza, ghafla wakaanza kuniambia nimetumwa.
Wewe mbona nishakudharau bado tu huelewi ?
 
Kuna vitu huwa watu mnazungumza sijui kwa kutumia nini.
Hivi unajua huyo hadija mwago hawezi kupata kura hata robo ya atazopata chaurembo?
Swali lingine kwako, unajua huyo hadija hajaonekana kwenye kampeni ana wiki kadhaa sasa?
Mimi nimekutana nae kwenye kampeni za mtaa kwa mtaa
 
Wewe umeshaanza kampeni ?
kyela leo hii
FB_IMG_1601408600749.jpg
FB_IMG_1601408590953.jpg
 
Usimuongopee mtu aisee, pili kinachomcost hadija mwago ni kushindwa kwenye kura za maoni alafu jina lake likarudishwa.
Hadija mwago alipitwa mbali sana kwenye kura za maoni, ila hii inaweza isiwe sababu kubwa sana ya yeye kushindwa. Sababu ni kuwa hajui kufanya siasa, pili nguvu ambayo anayopewa ni ndogo sana na hivyo watu hawamjui kabisa.
Chaurembo ameanza kuutafuta ubunge tokea 2015, na ametumia nafasi yake ya umeya kujijenga kwelikweli mbagala, na ni mtu mjanja sana. Asikuongopee mtu, hakuna anayeweza kumshinda chaurembo mbagala
Mimi nimekutana nae kwenye kampeni za mtaa kwa mtaa
 
Alafu ukishanidharau? Wewe ndio utakuwa wa kwanza kuja kulialia hapa kuwa kura zimeibiwa sababu ya ujinga wako kichwani bila kuelewa huko majimboni nini kinaendelea.
Ungeuliza kwanza nini kinaendelea huko alafu ndio uje ulete humu
Wewe mbona nishakudharau bado tu huelewi ?
 
Usimuongopee mtu aisee, pili kinachomcost hadija mwago ni kushindwa kwenye kura za maoni alafu jina lake likarudishwa.
Hadija mwago alipitwa mbali sana kwenye kura za maoni, ila hii inaweza isiwe sababu kubwa sana ya yeye kushindwa. Sababu ni kuwa hajui kufanya siasa, pili nguvu ambayo anayopewa ni ndogo sana na hivyo watu hawamjui kabisa.
Chaurembo ameanza kuutafuta ubunge tokea 2015, na ametumia nafasi yake ya umeya kujijenga kwelikweli mbagala, na ni mtu mjanja sana. Asikuongopee mtu, hakuna anayeweza kumshinda chaurembo mbagala
Hadija alishinda kura za maoni nachoweza kukubaliana na wewe ni hilo la uzoefu kwenye siasa.

Ndiyo maana hata mimi nimetumia neno "huenda"

Anyway tusubiri matokeo ya uchaguzi ila kwa Temeke hili jimbo ccm mnalipoteza.
 
Hadija alishinda kura za maoni nachoweza kukubaliana na wewe ni hilo la uzoefu kwenye siasa.

Ndiyo maana hata mimi nimetumia neno "huenda"

Anyway tusubiri matokeo ya uchaguzi ila kwa Temeke hili jimbo ccm mnalipoteza.
Nadhani hufahamu na kama unafahamu basi unafanya makusudi.
Aliyeshinda kura za maoni mbagala alikuwa ni Sudai, ila jina lilikatwa makao makuu na kuletwa hadija mwago
 
Nadhani hufahamu na kama unafahamu basi unafanya makusudi.
Aliyeshinda kura za maoni mbagala alikuwa ni Sudai, ila jina lilikatwa makao makuu na kuletwa hadija mwago
Chadema itakusababishia kisukari safari hii
 
Back
Top Bottom